MKASA WA KWELI: Ni bora ubaki na umaskini kuliko utajiri wa pesa za "ndagu" au majini

MKASA WA KWELI: Ni bora ubaki na umaskini kuliko utajiri wa pesa za "ndagu" au majini

INAENDELEA:

Huyu Gado akaendelea kuwa tajiri sana mwenye ukwasi wa kufa mtu, nakumbuka mwaka 2015 alimuita ndugu yangu mmoja hotelini pale Musoma mjini baada ya kuja kusalimia kijijini Hawa walikuwa hawajaonana siku nyingi katika maongezi yao aligusia kwamba kwa mda ule alikuwa na akiba bank kama 400m hivi...

Jamaa akawa anaogolea kwenye ukwasi na pale kijijini akawa anaheshimika sana na akawa tayari amepata watoto wawili na yule mkewe traffic... kitu nilichogundua ukiwa na pesa hata watu wakijua ni za madhara bado watakuheshimu na kukunyekea tu yaani huyu jamaa alikuwa ananyenyekewa pale kijijini utafikiri mfalme.

Kuna mwaka, mama mkwe wa Wasosi ambaye Sasa ni shemeji yake na huyu Gado maana Kaka yake ni yule aliyetolewa kafara akafariki pale kijijini na Mimi Kama kijana nikaenda kushiriki ule msiba, Cha kushangaza Gado sijui alipata wapi Ujasiri akafunga safari kuja msibani.

Pale Msibani alikuwepo mama yake Wasosi pia, wakawa wamepata taarifa za ujio wake huyu mwamba msibani jamaa alipofika na mkewe lile gari tu kuingia yule mama yake Wasosi alipiga ukunga ambao sijawahi uona Aisee huku akilalamika kwa uchungu na kutukana..nanukuu baadhi ya maneno ninayayakumbuka..." Uwiiiiiiiiiii mbwa wewe, Shetani mkubwa umemuua mwanangu Sasa wewe unafurahia na maisha, umeuua mwananangu, kweli umeuua mwananangu au hiyo gari ndio mwanangu" huyu mama alikiwa akiongea haya huku akionekana kuishiwa nguvu.

Wabibi wenzake wakawa wanamtuliza na baadhi ya wazeee lakini hali ya pale Msibani ikawa sio nzuri japo jamaa hakuonekana kujali kabisa..na baada ya kuzika yeye akaondoka.

Mimi nilikuja kuondoka pale kijijini nikaendelea na harakati za kutafuta maisha mikoani, mwaka juzi nikapata habari za huyu mwamba kwamba ameanza kufirisika ..kweli mpaka nakuja Arusha huyu Gado amebaki na Ghorofa moja tu zingine zote ameshauza na hata gari Hana..mke alishamkimbia nadhani hata hii ghorofa itauzwa mda si mrefu sijui alikosea wapi kwenye masharti yake huyu mwamba.

Mishe zimemgomea kabisa, Hana pesa tena.

Kibaya zaidi familia imeshaparanganika baba yao alishafariki.., watoto wote na mama hawaaminiani tena na hata upendo kati yao haupo kabisa yaani wanapitana Kama unavyompita mtu njiani..wanaishi kwa kuviziana sana.

Huyu mkubwa Joseph kwa Sasa ni Dereva Merelani hapo na afadhari amerudi kupatapata vipesa yuko njema kiasi chake kwa Sasa.

Yule mtoto wa Sarah, kwa Sasa ni binti mkubwa yuko vidato kadhaa na anajua kila kitu kuhusu stori ya kifo Cha baba yake...binti ana kisasi sana na Hawa ndugu ndugu zake

kupitia kwa watu na hata Joseph mwenyewe anasema binti amesema hawatambui akiwemo mama yake mzazi Sarah na hajawahi hata kwenda kuwasalimia hata kwenye simu.

Maisha yao yamegeuzwa kuwa Arusha japo kwa Sasa yamekuwa magumu sana wanaona soni kurudi pale kijijini tena na pale Kijijini Kuna miamba mipya iliyofuata nyayo za Gado imeibuka ndio inatawala sasa.

Sarah kachoka sana hadi anatia huruma...



,.........................................................
Hiki kisa ni cha kweli na hakijatokea miaka mingi..Ukiwa unatoka mwanza au Bunda na unaenda Musoma mjini au Tarime shuka hapo sabasaba mbele ya kiabakari na Mazami...hapohapo barabara kuu ya Musoma ulizia kwa mzee Nyanda au uliza mtu yeyote hii stori ukifika sabasaba.

Kwa mlioko mjini unaweza kumuona huyo Kiringo hapo udsm na atakupa huu mkasa uliochukua maisha ya kaka yake.

Poleni kwa uandishi wangu mbovu....

Niko zangu sitimbi now mapumziko naangalia madon wapya walioibuka
Asante kwa story yenye kufundisha Don mtarajiwa, ukweli ni kuwa hakuna short cut kwenye utajiri, utajiri wa haraka huwa una mazonge-mazonge mengi sana.

Vv
 
Asante kwa story yenye kufundisha Don mtarajiwa, ukweli ni kuwa hakuna short cut kwenye utajiri, utajiri wa haraka huwa una mazonge-mazonge mengi sana.

Vv
Acha uoga mkuu
Kuwa mjanjaa upate pesa ohoooo utakufa maskini, shauri yako
 
Story km ya kutunga hivi, speaking of ndago hakuna ukweli wowote ni story tu za vijiweni
Mbona amemtaja mtu ambaye namfahamu na ni jirani yetu hapo maeneo ya UDSM? Mtafute akuthibitishie uongo/ukweli wa story.

Vv
 
Mbona amemtaja mtu ambaye namfahamu na ni jirani yetu hapo maeneo ya UDSM? Mtafute akuthibitishie uongo/ukweli wa story.

Vv
Boss watu wengine ni kubisha tu.. huyo Kiringo hata Mimi namfahamu. Anaitwa John Bosco Kiringo yuko hapo Mlimani ni mkuu wa usalama Nina mawasiliano yake lakini simtafuti leo kwa sababu tutakutana kwenye vikao vya harusi ya mwanae nitamuuliza hili.


Lakini ninachofahamu Mimi kaka yake alikufa na alikuwa ameoa na mke sijui yuko wapi kwa sasa
 
Watu wa humu ni zaidi ya wajuaji aiseee.
Haya naitoa wapi?

Unajua story za kusimuliwa wewe?...A u unataka nikupe majina ya wahusika kabisa

Mkuu muwe mnapunguza ujuaji basi....na mbona nimeshamaliza yote
Na wewe utoe mahali basi,acha wivu
dogo...
 
Silasy kaniuliza swali hili PM

"mtu akimtoa kafara ndg yake akawa tajiri ikagundulika na yeye anaweza akanyang'anywa utajiri wake kiuganga?nimesoma ktk hiyo story mtu huyo pamoja na kugundulika aliua shemeji yake lkn ana guts za ku attend functions zote kijijini bila ya woga wowote"

Mshana Jr tunaomba jibu.
Hili swali ni kubwa kwangu
 
Story za uongo zisizo na evidence yoyote,
Ukiona mtu anapesa jua kaziiitafuta kwa njia flani halali au sio halali ila hakuna kitu kama majini wala ndagu, huo upuuzi ni uongo mtupu na wanaoamini huo ushenzi wote maskini
ndago ni njia isiyo halali pia...acha kujikanyaga
 
Back
Top Bottom