Kuna jamaa anaitwa
poisonous aliposti kitu pia siku 10 zilizopita. Inafikirisha na kushangaza sana. Anayeweza kusoma asome tafadhali..
Kwenye Siasa , " Hakuna kinachotokea kwa bahati mbaya " everything is planned . Think about this , Soko la kariakoo wafanya biashara wameandamana, mkataba wa bandari umuvujishwa kwa mbwembwe na tayari kila kona kuna watu wamepangwa kuushambulia , ghafla mkataba hauongelewi maada inageuka kua...
Kinachofikirisha sana kwenye hoja ya jamaa huyu aliyiposti humu siku kadhaa nyuma ni;
1. Inawezekana kweli hii kitu ndiyo imetokea humo ndani serikalini. Hii nzuri sana kwa wote wanaotaka mabadiliko maana ni kweli na hakika kuwa, ili kuifyekelea mbali CCM lazima kwanza wapatikane watu toka humohumo watakaokuwa wamechochwa na ujinga na upumbavu kama huu wa Rais Samia Suluhu na DP WORLD wajiunge na harakati...
Na kama kweli hili liko kama alivyolileta
poisonous, ujumbe tunaoupata ni kuwa, ufalme wa shetani tayari umeshafitinika, hakuna maelewano na wana CCM walio wengi hawataki huyu mama na Kwa kifupi hawautaki muungano..!!
2. Kwa maoni yangu, japokuwa nyuma ya kundi hili linaweza kuwa lina malengo yake kama ambavyo
poisonous anasema, lakini ktk sura nyingine mimi naona uzalendo wa watu hawa wa waliovujisha hii kitu kwa manufaa ya Watanganyika.
Kiufupi mkataba haufai, ni mbaya na Kwa hili Rais Samia Suluhu Hassan hatufai..!!
3. Kwa kuvujishwa Kwa mkataba huu huku TISS wakiwa kimya kumshauri Rais kutoa kauli ya kunyamazisha hii kitu, basi huu ni ushahidi kuwa huyu mama ni jeuri na amedhamiria kutekeleza Nia yake hii ovu dhidi ya Tanganyika huku akilinda maslahi ya Zanzibar nyumbani kwao. Tusikubali..
4. Mwisho
poisonous anawalaumu wanaomkosoa Rais Samia Suluhu Hassan na kuupinga mkataba wa DP World juu ya bandari zetu na akasema "wanacheza ngoma wasioijua". Ni wazi
poisonous hajui siasa..
Yaani anadhani kama CCM chama kilichomo madarakani serikali yake inafanya madudu na ujinga kama wa mkataba huu wa DP WORLD kiasi cha CCM wao kwa wao kuanza kulaluana na kusalitiana, anategemea CHADEMA au chama kingine kilicho nje ya serikali kianze kufanya kazi wa kuwasuluhisha?
NO WAY BRO!...... Yaani haijalishi wanataka kumpindua Rais wao au kumuua ama vyovyote vile, hiyo kwao ni fursa ya ku - attack na kuwa - weaken zaidi na zaidi..
Kwa sababu Rais Samia anayedhoofishwa na kufanyiwa figisu si ni naye ni CCM vile vile? Hilo genge linalomfanyizia Rais Samia kwani nalo linatoka chama gani eti? Si ni ma - CCM hayo hayo?. Upinzani (CHADEMA) watapambana na yeyote.
Kwa hiyo ndugu
poisonous, CHADEMA wanacheza ngoma wanayoijua kuliko unavyoijua wewe!!!