Mkataba wa Bandari: Mbunge Aida Khenani akiri kupelekwa Dubai, lakini mpaka wanarudi hakujua walikwenda kufanya nini

Mkataba wa Bandari: Mbunge Aida Khenani akiri kupelekwa Dubai, lakini mpaka wanarudi hakujua walikwenda kufanya nini

Wewe ambae hata bandari hupajui, hata biashara ya usafirishaji huijui unapataje nguvu ya kupinga watu wanaoongelea maslahi ya Taifa?

Ukisema kitu ukiulizwa uthibitisho kuonesha umakini wako jibu unachoulizwa
Ukifikia kujibu namna hii, ni dalili tosha kuwa huna au umeshindwa kujibu hoja.
 
Nami ninashangaa kidogo kwa wewe kuuliza swali kama hilo.

Hivi kweli wewe uliona u'seriousness' wa aina yoyote mule ndani ya Bunge; ukianzia kwa Speaker mwenyewe na hata Mawaziri, akina Nnauye waliochangia?

Hebu jaribu kuwa mkweli wa nafsi yako mwenyewe juu ya hili, badala ya kuhoji umakini wa mbunge, tena aliyepewa fursa tu ya kwenda matembezi nje ya nchi.

Katika hali ya kawaida, hivi kweli pasingekuwepo na maandalizi ya kina sana kwa hao wabunge kabla ya safari yao hiyo?
Kuna mbunge yeyote, aliyeeleza ni kwa namna gani waliandaliwa kabla ya safari yao muhimu kama hii? Walipewa seminar yoyote juu ya watakayotarajia kuyaona katika hiyo safari?
Ngoja tuendelee kushaangaana

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
OKW BOBAN SUNZU unataka atumie lugha ili uelewe kuwa rushwa imetembea? Kwa maelezo yake;

1. Kwa Tanzania, walilipwa posho zao na kila gharama na TPA Kwa pesa ya Tanzania..

2. Huko Dubai, wakalipwa posho zao na DP WORLD wenyewe ambao kimsingi ndiyo mfalme mwenyewe wa Dubai maana ndiye mmiliki wa kampuni hii kwa 100%...

3. Hakuishia hapo, anasema, walilipwa na kampuni hizi mbili "kwa utaratibu wa Bunge". Mpaka hapa unaelewa nini wewe? ....... Complete contradiction!!

Lakini pia, hebu tujiulize hili:

Inawezekana vipi kampuni inayoomba deal la mkataba mnono kama huu iwachukue waidhinishaji wa tenda hiyo mahali kwa tour huku walilipa gharama zote na posho juu?

Tafsiri yake ni nini? Obviously ni RUSHWA HIYO. Ndiyo maana wengine humo ndani ya bunge walikuwa wanazungumza kama vile wameamushwa toka usingizini au kama watu mazuzu vile kuonesha kuwa hawajui lolote kuhusu hilo jambo!!.

Ndugu OKW BOBAN SUNZU, elewa kuwan aliyesemaga kuwa RUSHWA HUPOFUSHA FIKRA ZA WATU HUSUSANI UKIWA KIONGOZI WA UMMA hakukosea. Ushahidi ni huu..

Na sheria ya maadili ya viongozi wa umma hapa Tanzania kwetu inasemaje eti kuhusu hili?
Cc. Lord denning & Co
 
Mtu mwongo hafai hata kuwa mjumbe wa nyumba kumi sembuse ubunge? Wana nkasi mfukuzeni huyo shetani mwongo mchonganishi na adui wa maendeleo yenu na ya inchi
 
Hakika shetani ana trick za ajabu sana anapotaka kutenda au anapotenda uovu wake kwa kuwatumia watu waovu hususani viongozi wenye dhamana kubwa za kuongoza nchi na wananchi wa nchi yetu..

Hebu twende pamoja, soma na sikiliza hii👇👇👇

Mkataba wa DP WORLD ni zaidi ya mkataba tu!

• Kumbe kulikuwa na timu mbili za wabunge. Moja ilienda India (kuzuga tu) na nyingine Dubai (kuliko na mpango mzima wa Rais Samia Suluhu Hassan na Prof. Makame Mnyaa Mbarawa). Aida Khenani yeye akapachikwa kwenye trip hii ya Dubai. Nadhani lengo likiwa ili waovu hawa waje kuwa na hoja kusema "hata CHADEMA walikwenda kule wakiwakilishwa na mbunge wao kuona uzuri wa uwekezaji wa kampuni hii..!!". Aidha bila shaka pia kuwa, ili wamtumie ndani ya bunge kuwa kama shahidi wa upande wa upinzani bunge litakapo - ratify mkataba huu. Kwenda kinyume, Spika Dr Tulia Ackson alionekana kushangaa na kupaniki kikatokea tulichokiona. Mpaka naibu Spika wa Spika ndugu Zungu naye akiwa kama back bencher, alisimama eti kumpa taarifa mbunge huyu!!

• Hauishia hapo, mbunge huyu ndani ya bunge akaendelea kuwashangaza wabunge wa CCM aliposema hakubaliani na mambo haya hadharani ndani ya bunge. Nadhani kimya kimya wakawa wanasonya amekula hela zetu bure huyu. Wakamzonga zonga mpaka akaipata fresh huku Spika Tulia Ackson akiwa amevaa koti la mwanasheria Mkuu wa serikali kujibizana naye, kumtoa hofu😂 na kumshawishi akubaliane na serikali..!

Haya ya Spika Tulia Ackson siku ile kiukweli yalikuwa ni kichekecho na upuuzi wa ajabu sana.. Ama kweli, rushwa hupofusha fikra na ufahamu wa mtu!!

• Walioenda India ripoti yao wala hata haihitajiki kwa sababu wahusika sio wahindi wa India bali ni waarabu wa Dubai ambako kabla huyu anayechaguzwa na kauli ya "nani kama mama" alishatangulia kabla kumalizana na "mfalme" na kuchukua chake mapemaaaa..!

• Hii haina shaka tena kuwa, nyuma ya mkataba huu kati ya DP World & Serikali ya Tanzania kuna rushwa kubwa imetembea kwa viongozi wetu.

• Hata hivyo mimi siamini kabisa kuwa huyu mama anaweza kuwa mbaya na mumiani wa kiwango hiki cha kufikia kuuza kipande cha nchi ya Tanganyika.

Maoni yangu binafsi

Ilisemwa na wahenga, ili nchi yoyote duniani ipate maendeleo ya kweli ya watu wake, lazima mambo haya manne yawepo katika ufanisi wake:

1. Ardhi
2. Watu
3. Siasa safi
4. Uongozi bora

Ukiyatazama hayo mambo na ukimsikiliza huyu mbunge ambaye kwa kweli ukimtazama usoni mwake na kile kitokacho kinywani mwake, hutapata shida kabisa kumwamini.

Ukiachilia mbali uwepo wa ardhi na rasrimali watu, Tanzania tunakabiliwa na tatizo moja kubwa la UKOSEFU WA SIASA SAFI ambayo imezaa tatizo la UKOSEFU WA UONGOZI BORA. Na matokeo yake ni haya tunayoshuhudia leo. Tunaulizanaga, hivi ni kwanini nchi yetu ni masikini hata baada ya miaka zaidi ya 60 ya uhuru? Jibu lake liko wazi sasa... Ukosefu wa uongozi bora wa nchi..!!

Laiti tungekuwa na hayo mambo mawili muhimu zaidi, hiki kinachoendelea sasa kati ya Tanzania na DP World, kisingekuwepo maana tungekuwa na viongozi walio madarakani wenye akili, ufahamu, hekima na busara na kujitambua.

Lakini kwa mkataba huu wa DP WORLD, inadhihirisha wazi sasa kuwa kumbe tuna viongozi wajinga, wasio wazalendo wa taifa lao, waliojaa tamaa ya kujilimbikiza mali kwa rushwa na kuwa tayari kujiuza kwa vipande vya fedha, wabinafsi, wala rushwa na wanaojipenda wenyewe na matumbo yao na hawa kamwe hawajawahi kutupenda sisi wananchi wa Tanzania..!!

Sara yetu wote ni:

Mungu wetu uliye juu mbinguni muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo tutie nguvu tupambane na hawa mumiani wanajiita viongozi wa nchi ya Tanganyika lakini kumbe ni mashetani katika sura za binadamu.. Amina

Rais Samia Suluhu Hassan katukosea sana Watanganyika kwa hili la mkataba wa DP WORLD kumuuzia bandari zetu zote za bahari na maziwa ya Tanganyika huku akiacha za kwao Zanzibar mikononi mwa Wazanzibari!
"Wapinzani walichelewesha sana Maendeleo" alisikika Mwendazake mara nyingi na mwiho 2019 na 2020 akafanya maajabu ambayo hatukuwahi yaona Tanzania.Faida yake ni hii tutunze kumbukumbu vizuri.
 
Hivi mwanasheria
Mkuu wa serikali mbona haongei chochote sindio wajibu wake huu?
Ndugu@nyembela bado hupati picha tu kuwa huko serikalini mambo si shwari, hawaelewani na wengine wameshazila na kusema, "shauri lake, na apambane na hali yake?"

Ushahidi wa kimazingira unatupa picha kuwa, si tu yeye AG bali ofisi yote ya AG haijui lolote kuhusu mkataba huu Kwa maana ya kwamba haijashirikishwa nao wanashangaa tu kama tunavyoshangaa sisi..!

Huu ni uchafu wa Bunge (Tulia Ackson - Spika wa Bunge na baadhi tu ya wabunge) na ofisi ya Rais wa JMT Bi. Samia Suluhu Hassan..!!
 
Hakika shetani ana trick za ajabu sana anapotaka kutenda au anapotenda uovu wake kwa kuwatumia watu waovu hususani viongozi wenye dhamana kubwa za kuongoza nchi na wananchi wa nchi yetu..

Hebu twende pamoja, soma na sikiliza hii👇👇👇

Mkataba wa DP WORLD ni zaidi ya mkataba tu!

• Kumbe kulikuwa na timu mbili za wabunge. Moja ilienda India (kuzuga tu) na nyingine Dubai (kuliko na mpango mzima wa Rais Samia Suluhu Hassan na Prof. Makame Mnyaa Mbarawa). Aida Khenani yeye akapachikwa kwenye trip hii ya Dubai. Nadhani lengo likiwa ili waovu hawa waje kuwa na hoja kusema "hata CHADEMA walikwenda kule wakiwakilishwa na mbunge wao kuona uzuri wa uwekezaji wa kampuni hii..!!". Aidha bila shaka pia kuwa, ili wamtumie ndani ya bunge kuwa kama shahidi wa upande wa upinzani bunge litakapo - ratify mkataba huu. Kwenda kinyume, Spika Dr Tulia Ackson alionekana kushangaa na kupaniki kikatokea tulichokiona. Mpaka naibu Spika wa Spika ndugu Zungu naye akiwa kama back bencher, alisimama eti kumpa taarifa mbunge huyu!!

• Hauishia hapo, mbunge huyu ndani ya bunge akaendelea kuwashangaza wabunge wa CCM aliposema hakubaliani na mambo haya hadharani ndani ya bunge. Nadhani kimya kimya wakawa wanasonya amekula hela zetu bure huyu. Wakamzonga zonga mpaka akaipata fresh huku Spika Tulia Ackson akiwa amevaa koti la mwanasheria Mkuu wa serikali kujibizana naye, kumtoa hofu😂 na kumshawishi akubaliane na serikali..!

Haya ya Spika Tulia Ackson siku ile kiukweli yalikuwa ni kichekecho na upuuzi wa ajabu sana.. Ama kweli, rushwa hupofusha fikra na ufahamu wa mtu!!

• Walioenda India ripoti yao wala hata haihitajiki kwa sababu wahusika sio wahindi wa India bali ni waarabu wa Dubai ambako kabla huyu anayechaguzwa na kauli ya "nani kama mama" alishatangulia kabla kumalizana na "mfalme" na kuchukua chake mapemaaaa..!

• Hii haina shaka tena kuwa, nyuma ya mkataba huu kati ya DP World & Serikali ya Tanzania kuna rushwa kubwa imetembea kwa viongozi wetu.

• Hata hivyo mimi siamini kabisa kuwa huyu mama anaweza kuwa mbaya na mumiani wa kiwango hiki cha kufikia kuuza kipande cha nchi ya Tanganyika.

Maoni yangu binafsi

Ilisemwa na wahenga, ili nchi yoyote duniani ipate maendeleo ya kweli ya watu wake, lazima mambo haya manne yawepo katika ufanisi wake:

1. Ardhi
2. Watu
3. Siasa safi
4. Uongozi bora

Ukiyatazama hayo mambo na ukimsikiliza huyu mbunge ambaye kwa kweli ukimtazama usoni mwake na kile kitokacho kinywani mwake, hutapata shida kabisa kumwamini.

Ukiachilia mbali uwepo wa ardhi na rasrimali watu, Tanzania tunakabiliwa na tatizo moja kubwa la UKOSEFU WA SIASA SAFI ambayo imezaa tatizo la UKOSEFU WA UONGOZI BORA. Na matokeo yake ni haya tunayoshuhudia leo. Tunaulizanaga, hivi ni kwanini nchi yetu ni masikini hata baada ya miaka zaidi ya 60 ya uhuru? Jibu lake liko wazi sasa... Ukosefu wa uongozi bora wa nchi..!!

Laiti tungekuwa na hayo mambo mawili muhimu zaidi, hiki kinachoendelea sasa kati ya Tanzania na DP World, kisingekuwepo maana tungekuwa na viongozi walio madarakani wenye akili, ufahamu, hekima na busara na kujitambua.

Lakini kwa mkataba huu wa DP WORLD, inadhihirisha wazi sasa kuwa kumbe tuna viongozi wajinga, wasio wazalendo wa taifa lao, waliojaa tamaa ya kujilimbikiza mali kwa rushwa na kuwa tayari kujiuza kwa vipande vya fedha, wabinafsi, wala rushwa na wanaojipenda wenyewe na matumbo yao na hawa kamwe hawajawahi kutupenda sisi wananchi wa Tanzania..!!

Sara yetu wote ni:

Mungu wetu uliye juu mbinguni muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo tutie nguvu tupambane na hawa mumiani wanajiita viongozi wa nchi ya Tanganyika lakini kumbe ni mashetani katika sura za binadamu.. Amina

Rais Samia Suluhu Hassan katukosea sana Watanganyika kwa hili la mkataba wa DP WORLD kumuuzia bandari zetu zote za bahari na maziwa ya Tanganyika huku akiacha za kwao Zanzibar mikononi mwa Wazanzibari!
Hivi CHADEMA inawabunge? Anyway kwani Tatizo liko wapi hao wabunge kwenda DUBAI? Hii si roho mbaya hii na choyo
 
Hivi CHADEMA inawabunge? Anyway kwani Tatizo liko wapi hao wabunge kwenda DUBAI? Hii si roho mbaya hii na choyo
Unauliza swali kana kwamba hujasoma ulichokikwoti na kumsikiliza muhusika mwenyewe anayetoa maelezo hayo..

Jifunze kusoma na kuelewa hoja za wengine kabla hujamkwoti mtu. Vinginevyo, utakuwa hujui namna ya kuji - engage kwenye mijadala..

Soma, tazama na sikiliza tena hiyo video mwanzo mpaka mwisho. Kisha njoo na hoja specific ili tujadiliane vizuri..

Asante
 
Ndugu@nyembela bado hupati picha tu kuwa huko serikalini mambo si shwari, hawaelewani na wengine wameshazila na kusema, "shauri lake, na apambane na hali yake?"

Ushahidi wa kimazingira unatupa picha kuwa, si tu yeye AG bali ofisi yote ya AG haijui lolote kuhusu mkataba huu Kwa maana ya kwamba haijashirikishwa nao wanashangaa tu kama tunavyoshangaa sisi..!

Huu ni uchafu wa Bunge (Tulia Ackson - Spika wa Bunge na baadhi tu ya wabunge) na ofisi ya Rais wa JMT Bi. Samia Suluhu Hassan..!!
Acha wavurugane mwakani uchaguzi huwenda Mungu anampango wake
 
Kwa hili ni ajabu sana kuliko ajabu yenyewe..!

Mlienda kufanya nini miezi takribani nane baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuwa ameshasaini MoU na mkataba wenyewe? Kutuzuga siyo?

Kwa hili utetezi wako haufai na hausimami bibie..!
ajabu ya kusafiri nje ya nchi au ajabu ipi?

Mimi siyo mbunge nilikuwa nakueleza tu kuwa hawa wabunge huwa wanapangiwa safari za nje katika nchi mbali mbali, kama mtu amefika huko bila ya kujua malengo basi itakuwa amelala usingizi.
 
ajabu ya kusafiri nje ya nchi au ajabu ipi?

Mimi siyo mbunge nilikuwa nakueleza tu kuwa hawa wabunge huwa wanapangiwa safari za nje katika nchi mbali mbali, kama mtu amefika huko bila ya kujua malengo basi itakuwa amelala usingizi.
Rudi kwenye hoja yako ya awali niliyoikwoti Kisha linganisha na jibu lako hili☝️☝️

Anyway, acha ni - recall. Nilikuuliza hivi

"Kama ni ishu ya kwenda kuona na kujifunza ili waje washauri serikali kabla ya kuingia makubaliano/mkataba, hiyo mantiki ya lengo la safari hiyo ya wabunge iko wapi maana MoU na mkataba wenyewe ulishasainiwa tayari na Rais na watu wake tangu mwaka 2022 na mkataba umeingia bungeni juzi ukiwa signed already?

Umenielewa?

Kama umenielewa, sasa maswali yangu kwako wewe na kwa kadiri ya akili na ufahamu wako, ni haya;

1. Hiyo wewe unaipa tafsiri gani?

2. Bado unadhani tu kuwa hiyo ilikuwa ni safari ya kawaida tu kwa wabunge kwa kuwa ni kawaida yao kusafiri mara kwa mara kwa shughuli za kibunge siyo?

3. Bado huoni tu kuwa ni safari ya kirushwa rushwa waliyopewa ili waje kutumika ku - rubber stamp maamuzi haya ya hovyo na mabaya ya Rais Samia Suluhu Hassan na wenzake dhidi ya Tanganyika na rasrimali zake ambazo ni urithi wao halali walizopewa na Mungu kupitia hiki kinachoitwa mkataba??

4. Je, unajua kuwa hata wabunge wasio wa kamati husika akiwemo huyu Aida Khenani nao walipelekwa? Unadhani ni kwanini?

MWISHO;

Kama bado huelewi tu, basi utabaki hivyo hivyo na maneno yako ya "si ni kawaida tu kwa wabunge kusafiri nje" bila kutumia kichwa na akili yako sawasawa kufikiria nje ya box..

To cut it short, mimi nakuambia safari zingine za wabunge nje ya nchi na hata za ndani ya nchi huwa si za kawaida bali huwa kama rushwa ya ushawishi kuwalainisha wapitishe jambo fulani la serikali ikiwemo hii tunayojadili. Narudia tena wakati mwingine tuwe tunatumia akili vyema kufikiri nje ya boksi kudadisi mambo..!!...
 
Kuna jamaa anaitwa poisonous aliposti kitu pia siku 10 zilizopita. Inafikirisha na kushangaza sana. Anayeweza kusoma asome tafadhali..

Kinachofikirisha sana kwenye hoja ya jamaa huyu aliyiposti humu siku kadhaa nyuma ni;

1. Inawezekana kweli hii kitu ndiyo imetokea humo ndani serikalini. Hii nzuri sana kwa wote wanaotaka mabadiliko maana ni kweli na hakika kuwa, ili kuifyekelea mbali CCM lazima kwanza wapatikane watu toka humohumo watakaokuwa wamechochwa na ujinga na upumbavu kama huu wa Rais Samia Suluhu na DP WORLD wajiunge na harakati...

Na kama kweli hili liko kama alivyolileta poisonous, ujumbe tunaoupata ni kuwa, ufalme wa shetani tayari umeshafitinika, hakuna maelewano na wana CCM walio wengi hawataki huyu mama na Kwa kifupi hawautaki muungano..!!

2. Kwa maoni yangu, japokuwa nyuma ya kundi hili linaweza kuwa lina malengo yake kama ambavyo poisonous anasema, lakini ktk sura nyingine mimi naona uzalendo wa watu hawa wa waliovujisha hii kitu kwa manufaa ya Watanganyika.

Kiufupi mkataba haufai, ni mbaya na Kwa hili Rais Samia Suluhu Hassan hatufai..!!

3. Kwa kuvujishwa Kwa mkataba huu huku TISS wakiwa kimya kumshauri Rais kutoa kauli ya kunyamazisha hii kitu, basi huu ni ushahidi kuwa huyu mama ni jeuri na amedhamiria kutekeleza Nia yake hii ovu dhidi ya Tanganyika huku akilinda maslahi ya Zanzibar nyumbani kwao. Tusikubali..

4. Mwisho poisonous anawalaumu wanaomkosoa Rais Samia Suluhu Hassan na kuupinga mkataba wa DP World juu ya bandari zetu na akasema "wanacheza ngoma wasioijua". Ni wazi poisonous hajui siasa..

Yaani anadhani kama CCM chama kilichomo madarakani serikali yake inafanya madudu na ujinga kama wa mkataba huu wa DP WORLD kiasi cha CCM wao kwa wao kuanza kulaluana na kusalitiana, anategemea CHADEMA au chama kingine kilicho nje ya serikali kianze kufanya kazi wa kuwasuluhisha?

NO WAY BRO!...... Yaani haijalishi wanataka kumpindua Rais wao au kumuua ama vyovyote vile, hiyo kwao ni fursa ya ku - attack na kuwa - weaken zaidi na zaidi..

Kwa sababu Rais Samia anayedhoofishwa na kufanyiwa figisu si ni naye ni CCM vile vile? Hilo genge linalomfanyizia Rais Samia kwani nalo linatoka chama gani eti? Si ni ma - CCM hayo hayo?. Upinzani (CHADEMA) watapambana na yeyote.

Kwa hiyo ndugu poisonous, CHADEMA wanacheza ngoma wanayoijua kuliko unavyoijua wewe!!!
Umejaribu kutoa maoni yako nayaheshimu , lakini kuna jambo la msingi hujaligusia
Kuwa na genge ndani ya Serikali linalofanya uhaini sio jambo la kushabikia, hata mwalimu Nyerere kuna watu walikua wanamfanyia uhaini mpaka ikafikia muda akawaweka detention .

Pili, kuwa mpinzani sio kushabikia serikali iporomoke, bora ushabikie chama kiporomoke kwa maana ya CCM kama wewe ni CHADEMA, lakini Serikali ikiporomoka ama isipoelewana kwa sababu ya uchu wa madaraka wa watu flani , wanaoumia ni ndugu zetu wanaotegemea kutibiwa kwa mkono wa serikali, kusoma kwa mkono wa serikali.


Kuna tofauti kubwa sana kati ya uzalendo wa chama na uzalendo wa nchi, hapa tuko kwenye suala la nchi


Vyama vya upinzani hasa CHADEMA kitendo cha kuwa tayari cheza ngoma yeyote ile ilimradi inadhoofisha nchi sio uzalendo.

Leo hii likitokea taifa la nje linataka kuiondoa madarakani serikali yetu kama URUSI na UKRAINE ilivyo , CHADEMA unataka kusema mko tayari kuungana na taifa hilo imradi serikali ianguke?


Tuwe wazalendo , na tupime madhara ya kucheza ngoma zisizo tuhusu

Lakini umejitahidi ku analyse , kuna maeneo umepatia , except sehemu ya uzalendo kwa nchi
 
OKW BOBAN SUNZU unataka atumie lugha ili uelewe kuwa rushwa imetembea? Kwa maelezo yake;

1. Kwa Tanzania, walilipwa posho zao na kila gharama na TPA Kwa pesa ya Tanzania..

2. Huko Dubai, wakalipwa posho zao na DP WORLD wenyewe ambao kimsingi ndiyo mfalme mwenyewe wa Dubai maana ndiye mmiliki wa kampuni hii kwa 100%...

3. Hakuishia hapo, anasema, walilipwa na kampuni hizi mbili "kwa utaratibu wa Bunge". Mpaka hapa unaelewa nini wewe? ....... Complete contradiction!!

Lakini pia, hebu tujiulize hili:

Inawezekana vipi kampuni inayoomba deal la mkataba mnono kama huu iwachukue waidhinishaji wa tenda hiyo mahali kwa tour huku walilipa gharama zote na posho juu?

Tafsiri yake ni nini? Obviously ni RUSHWA HIYO. Ndiyo maana wengine humo ndani ya bunge walikuwa wanazungumza kama vile wameamushwa toka usingizini au kama watu mazuzu vile kuonesha kuwa hawajui lolote kuhusu hilo jambo!!.

Ndugu OKW BOBAN SUNZU, elewa kuwan aliyesemaga kuwa RUSHWA HUPOFUSHA FIKRA ZA WATU HUSUSANI UKIWA KIONGOZI WA UMMA hakukosea. Ushahidi ni huu..

Na sheria ya maadili ya viongozi wa umma hapa Tanzania kwetu inasemaje eti kuhusu hili?
Kama hayo anayoyasema ni kweli na sikutaka umaarufu kwa nini akuyasemea bungeni na nafasi ya kuyasema aliipata?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom