Mke wa Mwandishi wa Habari Azory Gwanda Kutembelewa na Kaimu balozi wa Marekani

Mke wa Mwandishi wa Habari Azory Gwanda Kutembelewa na Kaimu balozi wa Marekani

Japo inasikitisha but she is not very special compared to many Tanzanian women suffering in our country ambao hawatembelewi hata na mjumbe wa nyumba 10. Kuna ambao hata mlo wa siku hawauoni, sembuse mama Azory?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mauwaji kupoteza watu kuteka watu kumiminia watu marisasi ujue kuna watu hawapendi wala kushabikia.
Bad precedence (omen), binadamu sio mzoga wa mbwa eti umetupwa basi!!
Tukae tujiulize taifa linaelekea wapi??
Hadi wageni wanatushangaa!!
 
watasema huyu mama anaingilia mambo yetu ya ndani..atuache.
 
Tunawaita mabeberu lakini wakiamua kukumaliza wanakumaliza kweli kweli. Ukienda Zimbabwe ndiyo utajua uwezo wa hawa mabeberu. Wakikuwekea vikwazo vya uchumi sijui utakimbilia wapi.
 
Lazima amuone muhanga wa Kibaraka wao, hivi huyu balozi amekumbuka kuwatembelea pia Wanawake wa wale Watendaji wa Vijiji na Kata waliokuwa wanauliwa huko Rufiji kwa kutobolewa macho??
Anyway sooon tutamuona anaenda lwa Mama Kabendera nadhan inaweza kuwa New year au wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Waandishi.
All in all Kaburu hajawahi kufanya zuri lolote pasipo kufaidika nalo, waelevu wataelewa.
 
kama mtoto wa Azory akakua akajituma akajikuta JKT mara JW mamaake akamwambia babaako alitekwa na wasiojulikana!!unafikiri atakula kichwa cha nan?
 
Mzungu Hana urafiki na ngozi nyeusi usijidanganye.....she went to visit her for hidden purpose


Sent from my iPhone using JamiiForums
Ukweli mtupu na mchungu.
Wazungu hawajawahi na hawatakaa wawe wazuri kwa mtu mweusi. Ukiona mzungu anakusifia na anajipendekeza kwako kuna kitu nyuma yake.
 
Kaimu Balozi ukimwangalia usoni kuna ujumbe munene unasomeka
Ameogopa Amemuonea huruma sana huyu mama Ameumia sana
Majibu tutayapata siku za usoni
** Journalist Kabendera yupo BBC News leo
Acha tuzidi kuchanga karata karibu tunaokota galasa


Karibu au ndio tuna garasa sasa hivi
 
Masikini sijui ametoa ombi gani kwao. Ningelikuwa mimi ningeliwaomba waibane serikali iseme ilimuweka wapi. Waishinikize kuishitaki mahakama za kimataifa kama sheria inaruhusu preferably ICC maana kuna.mtu anayewatuma wasiojulikana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni walewale waliofanya shambulio la atomiki huko Japan na kusababisha madhara makubwa.

Ni walewale Walioichafua Libya, wakasababisha raia wa taifa hilo kuwa masikini.

Ndio haohao walioitembelea familia ya ndugu yetu Azory Gwanda ambaye hajulikani alipo. Mungu amsaidie arudi salama Inshaallah.

Kitendo cha balozi huyo kufanya ziara kwa familia ya ndugu yetu mpendwa kimetusikitisha sana.

Bila shaka, balozi huyo anatumia machungu ya ndugu yetu kisiasa. Tunajiuliza huruma hiyo ametoa wapi?

Ingelikua ana ubinaadamu angeishauri serikali yake iache kufanya mauaji ya watoto wadogo huko Yemen.

Angeishauri Marekani iache kutengeneza makundi ya kigaidi, maradhi ya ebola na udumavu. Kwakweli angekua na huruma, angejiuzulu.

Tunamshauri balozi huyo akatembelee ndugu wa waandishi wa Marekani ambao waume zao wamepotezwa na Trump.

Waache kumtumia ndugu yetu kama silaha ya kutupiga nayo wenyewe. Mataifa mengi walianza hivihivi wakaishia kufanya uvamizi wa kijeshi.
 
Mbona viongozi wetu malaika wasio na madoa wenye huruma na watu wao ambao hawakutengeneza bomu la nyuklia wala kuichafua Libya hawajawahi wala hawafikirii kwenda kumtembelea mjane huyu mkuu?
 
Back
Top Bottom