Mke wako wako asikuzidi jina, nyumba yako itambulike kwa baba au mzee fulani na sio kwa mama au bibi fulani

Mke wako wako asikuzidi jina, nyumba yako itambulike kwa baba au mzee fulani na sio kwa mama au bibi fulani

MKE WAKO WAKO ASIKUZIDI JINA, NYUMBA YAKO ITAMBULIKE KWA BABA AU MZEE FULANI NA SIÔ KWA MAMA AU BIBI FULANI.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Moja ya dalili kuwa Mwanaume umefeli ni Nyumba yako kutambulika Hapo mtaani Kwa jina la Mkeo.
Utasikia pale Kwa Mama Taikon, au Kwa Bibi Zeituni,
Nyumbani Kwa Mama Richard.

My friend ikifikia sehemu àmbayo NI yako alafu inatajwa Kwa Jina la Mkeo Jua kûna sehemu muhimu na nyeti umeshindwa kama Mwanaume na kama Baba.

Úkiwa kama Mwanaume muwajibikaji na unayejua majukumu yako jina Lako NI Moja ya Jambo nyeti kulilinda na kulikuza.

Siô Sifa nzuri Nyumba yako iitwe Kwa Jina la Mwanamke NI kwamba wewe Huna lolote. Wewe siô kichwa, wewe sio mtawala yàani upoupo.

NI Sawasawa na úwe Rais WA nchi hii alafu nchi jirani na Huko kimataifa Waiite nchi yako Kwa Jina la Makamu wako au Waziri Mkuu. Hiyo kiutawala Moja Kwa moja inaashiria kuwa Rais Hana chake Hapo.

Nyumba yako iitwe Kwa majina yako au ûkoo wenu.
Kwa Mzee Magufuli,
Kwa Mzee Kikwete,
Kwa Mzee Taikon
Kwa Mzee Mwinyi n.k.

Hata familia yako itambulishwe Kwa Jina laki au ubini wako.
Siô familia ya Mama au Bibi Fulani nop. Hiyo siô dalili nzuri kiutawala.

NI dalili ya kuwa haukuwa active enzi za ujana wako.

Moja ya mambo àmbayo Mungu alimuahidi Ibrahim ni kukuza jina lake na alilikuza. Hata Watoto na wajukuu wake Miaka nenda rudi huitwa Watoto na kizazi cha Ibrahim.
Pia hujulikana kama Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.

Au Mungu wa mababu zetu.
Kitendo cha kukubali Mkeo au Mwanamke akuzidi kete ni kuruhusu Miaka ijayo aitwe Mungu wa Bibi zetu Jambo ambalo kiutawala hasa WA kiroho halipo.

Familia ambazo mama amebeba jina huwaga hazinaga kizazi kirefu Katika mafanikio.

Jina Lako lina thamani. Thamani hiyo lazima Uilinde.
Kiasi kwamba Siku ukiwa haupo Watoto na wajukuu zako wajivunie jina Lako.

Hata Mwanamke hujivunia kuitwa jina la Mwanaume mwenye heshima na legacy Kwa Wakati wake.
Mwanamke Hawezi kubali kubadili jina la ûkoo wake na kuitwa jina Lako kama hajivunii wewe, kama anakuona hujielewi.

Anakuona wewe sio shujaa,

Wanawake wanapenda Wanaume mashujaa, Malegend.
Mwanamke unaweza kukosa Pesa lakini Kama Unajina lenye heshima anaweza kukubali kuishi na wéwe na Kutumia.

Àndiko Hili nimeliandika nikilenga kukuhamasisha kijana upambane, onyesha wewe NI Nani hasa, onyesha wewe NI Mwanaume àmbaye Mwanamke yeyote atajivunia wewe.
Usiwe legelege, jina Lako litadharauliwa. Hakuna atakayeliheshimu jina Lako.
Na kama jina Lako haliheshimiwi Basi hata Mkeo na Watoto na kizazi chako hakitaheshimiwa.

Chochote unachofanya kifanye Kwa weledi na Ñguvu zako zote kuhakikisha unajenga heshima.
Hata kama unashona Viatu, Shona Kwa kiwango cha juu, kwako pataitwa Kwa Fulani mshona Viatu mashuhuri. Hiyo NI heshima kûbwa kuliko kuzubaa zubaa.

Wewe ni Mwanaume hakikisha jina Lako unalilinda na kulipa thamani ili Mungu alikuze na watu wakuheshimu.

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Tatizo ninaloliona kwa ujumbe wa andiko hili ni kuwako hofu au shaka ya uanamme. Kwamba kuna wasiwasi wa uanamme wa mwanamme kutoonekana au kuthaminiwa.

Kwa hali hiyo, ujumbe wa hapa naona una lengo la kutengeneza stress kwa wanamme na migogoro, labda kwa makusudi au bahati mbaya.

Suala la kuulinda uanamme wako ni kitu kilicho ndani yako na wala huwa hakitegemei sauti za nje wala aina yoyote ya misukumo ya nje. Wewe ni mwanamme nawe ukijijua hivyo inatosha.

Ova
 
Ngoja nifanye uchunguzi hapa tulipopanga familia nane panajulikana kwa mama au baba nani.
Utapewa jina la Mama fulani...Wababa ni nadra sana....

Sasa mimi nyumbani hata ukiwa unamuelekeza Boda....anakuambia pale kwa wale watoto wale😅inabidi tu tuwatumie wao zaidi...
 
Issue ni interaction je mwanaume una muda wakufanyia shughuli zako nyumbani Kwa muda mwingi kama mwanamke mpaka ujulikana?Ni kawaida mama Fulani ukakuta anafamika mtaani mpaka na watoto lakini baba Fulani ukaambiwa hawamjui?ukitaka maarufu kwako labda ufungue biashara na uisimamie mwenyewe hapo mtaani Tena bila kumhusisha mkeo ndio unaweza pata umaarufu.Ila kama ndio wale wa kuonekana Kwa maneti sahau i
 
"NI Sawasawa na úwe Rais WA nchi hii alafu nchi jirani na Huko kimataifa Waiite nchi yako Kwa Jina la Makamu wako au Waziri Mkuu. Hiyo kiutawala Moja Kwa moja inaashiria kuwa Rais Hana chake Hapo."

kwa hiyo Rais wa israel amefeli kwa mgongo wa Netanyahu
 
Tatizo ninaloliona kwa ujumbe wa 3andiko hili ni kuwako hofu au shaka ya uanamme. Kwamba kuna wasiwasi wa uanamme wa mwanamme kutoonekana au kuthaminiwa.

Mwanaume kuwa active.

Kwa hali hiyo, ujumbe wa hapa naona una lengo la kutengeneza stress kwa wanamme na migogoro, labda kwa makusudi au bahati mbaya.
Ujûmbe Hapa unalenga Wanaume tuendelee kushikilia wajibu na majukumu yetu. Tuwe strong, tupambane, tuwe hodari na mashujaa automatically Majina yetu yataleta heshima kwèñye familia na jamii Kwa ujumla.

Suala la kuulinda uanamme wako ni kitu kilicho ndani yako na wala huwa hakitegemei sauti za nje wala aina yoyote ya misukumo ya nje. Wewe ni mwanamme nawe ukijijua hivyo inatosha.

Ova

Uanaume upo ndàni na nje ya Mwanaume Husika

Jina ni Moja ya nembo ya Mwanaume.
Ndîo maana Watoto wengi wanaitwa Majina ya Mwanaume na siô Mwanamke.
Jina NI tukufu, Umiliki, na ufahari.

HUwezi kumtaja Mwanaume ukapuuzia jina lake. Jina ñdilo identity na ulinzi wa kizazi Siku àmbayo Mwanaume hatakuwepo.

Mungu anapombariki Mtu(Mwanaume )hubariki mambo yafuatayo;
1. Jina lake
2. Uzao wake.
3. KAZI yake
4. mji na Taífa lake.

Vijana lazima wawe Strong kuhakikisha hayo yanafanyika.

Unapozungumzia Mji Unazungumzia ufalme.

Mke anaweza Kutumia majina ya Mumewe na pasiharibike kitu. Mfano Kwa Maria Nyerere, Moja Kwa Moja Watu WANAJUA hiyo ni milki ya Nyerere.
 
Back
Top Bottom