wakusoma21
Member
- Nov 16, 2019
- 29
- 78
Niende moja kwa moja kwenye mada. Ni miaka minne toka nimemuweka ndani zamani alikua mtiifu tuu vizuri ila kuanzia mwaka huuu mwanzoni nimeanza kuona dalili ambazo sio nzuri. Kwanza nilishawai kuikagua simu yake kwenye call zake nikakuta anampigia Sana ex wake yaaan unakuta amempigia wameongea ata zaidi ya dakika kumi nikamuuliza akajibu tuu ni stori walikua wanapiga aliniuzi Sana nikataka kumfukuza arudi kwao aliomba msamaha na nikiangalia nina mtoto mdogo nikaona isiwetabu nikafunika kombe . Juzi juzi hapa anapigiwa simu na namba ngeni sauti ya mwanaume anajing'ang'ata tuuuu anadanganya tu unakuja kugundua ni mtu wanatongozana anadai anamtongoza tuuuu. Pia unamtuma labla aende dukani unakuta mtu anakaaa kabisa yaaan anasema mbali yaaan nimeumia Sana mke niliye muoa anakaaa kutumwa na Mimi. Ni mengi Sana huyu mwanamke anachangamoto Jana amenizilia simu na kutoa laini ya simu baada ya Mimi kumuomba simu niingie mtandaoni maana mm natumia kisimu kidogo. Naombeni ushauri jaman maana nahis kuchanganyiwa.