Mke wangu anamtesa sana mtoto wa marehemu dada yangu

Mke wangu anamtesa sana mtoto wa marehemu dada yangu

Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni jumamosi na jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani
Fukuza hiyo mbuzi
 
Huyo mtoto utasema anakula gunia kwa siku? Na hapo roho mbaya ipo kwenye msosi hana lolote.!!
Mi napenda watoto na naishi na mtoto mpk wa ex wangu na sijali namtunza km wangu.!!

Sasa ingekuwa huyo mtoto ndio wa mume wake si angemuua kabisaa!!
Huyo mwanamke gaidi mtoto mwenyewe yatima anahitaji upendo wa hali ya juu.
Mi naona huyo mama ni wale watu wa fujo/kupigana yaani ni wale watu wauaji
Kama kimo cha tofali kwa mtoto je kwa mtu mzima mwenzio si ataweza kubebea kisu.
Miaka nane kama kakosea kosa gani ubebe tofali???
Aiseee mi nina wasichana wangu wawili wasaidiz juzi nilitoka safari nikawa nimelala my best food ni maarage nazi ubwabwa
Nimerudi tu niakingia ndani nikawaambia waeke maarage
Wakawasha tv…niko chumbani wakayaunguza kama kau kau afu wako wawili age kama wanalingana 19-18
Aisee niliongea jamani mpaka nilijiskia vibaya nikatamani ningeingia tu ndani na kuendelea na kingine
Baadae wakapika kingine wakaja wakawa wananisemesha kama hakijatokea kitu huku wanaangalia mwamposa
Unajua kwanini they are that comfortable kwa age hiyo
Sababu i cant go physical lakin pia siwaonei lakini pia najua ni watoto…..
Sometimes nawafurahia saa ingine wananiuzi maisha yanaendelea
Hawa ni hawa nilionao
Na ni wakubwa nawachukulia kama watoto basi
Kwanini huyo mama asimvhukulie tu huyo kama mtoto
Basi kama zamani wazazi walikua wanasema ukikua utajionea mwenyewe
 
Wewe utakuwa umemchoka shemeji mpk unatamani likizo ya kurudi 😹😹😹
Hapana sijamchoka lakini kurudishwa nyumbani haiwezi ikawa adhabu kwangu...itakuwa adhabu kwake.
Kwangu ni vacation😅😅😅. Hata nigombane nae vipi atahakikisha sirudi nyumbani yaani yupo radhi asiende kazini anichunge nisiondoke..
Iwe nimemkosea au amenikosea yeye ipo hivyo siku zote.
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni jumamosi na jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani
Huyo Mwanamke hata ww kukuua ni Dakika sifuri
 
Dah yaani
Aisee nina mtoto wa mume wangu anakujaga likizo umr wa miaka 12
Aiseee sionagi baya lake japo wanaokujaga ndo wanasema mtoto mkubwa hivi hajui hata kutoa chombo
Akimaliza kula,naonaga sawa tu maana hata wanangu naenda nao hivyo hivyo
Nasema kama wa kiume hawajui hizo kazi why mdogo hivi kisa wa kike awe anafanya hizo activities
Mi napenda watoto wa kike sana
Wa ndugu zangu natamani kuja kumchukua ni ishi nae kabisa

Aisee mtu anae enda physical kwa mtoto wa miaka nane si ni la pili??
Kwa nini anamkokota namna hiyo??
Dah aiseee
Sawa Dada ila mfundishe kazi huyo mtoto kazi si mateso, hata kama una dada wa kazi amsadie hata kufuta vyombo, wakaao kwangu si kike si wa kiume ni kazi tu
 
Mi naona huyo mama ni wale watu wa fujo/kupigana yaani ni wale watu wauaji
Kama kimo cha tofali kwa mtoto je kwa mtu mzima mwenzio si ataweza kubebea kisu.
Miaka nane kama kakosea kosa gani ubebe tofali???
Aiseee mi nina wasichana wangu wawili wasaidiz juzi nilitoka safari nikawa nimelala my best food ni maarage nazi ubwabwa
Nimerudi tu niakingia ndani nikawaambia waeke maarage
Wakawasha tv…niko chumbani wakayaunguza kama kau kau afu wako wawili age kama wanalingana 19-18
Aisee niliongea jamani mpaka nilijiskia vibaya nikatamani ningeingia tu ndani na kuendelea na kingine
Baadae wakapika kingine wakaja wakawa wananisemesha kama hakijatokea kitu huku wanaangalia mwamposa
Unajua kwanini they are that comfortable kwa age hiyo
Sababu i cant go physical lakin pia siwaonei lakini pia najua ni watoto…..
Sometimes nawafurahia saa ingine wananiuzi maisha yanaendelea
Hawa ni hawa nilionao
Na ni wakubwa nawachukulia kama watoto basi
Kwanini huyo mama asimvhukulie tu huyo kama mtoto
Basi kama zamani wazazi walikua wanasema ukikua utajionea mwenyewe
😂😂😂 umefanya nikumbuke ya home kwangu.!!
Nna vijana wa dukani kuna siku niliwarekodi walichokuwa wanaongea sikutaka tena kuwafatilia nahisi ningekufa na presha.!!
Huku nyumbani ndio usiseme nna kijana wa kiume alimshawishi dada wa kazi akubali wanaume wanaomuita ili awachune wapate pesa.!! Nilipiga hiyo siku, halafu baadae huruma ikanijia nikaanza kumbembeleza.!!

Dada na kina kaka wa dukani nikianza kuongea mpk nachoka, kuna muda nasema au mnaniona mdogo ndiomana mnanidharau?? Au kwa vile sina mume hamnisikilizi?? Ila ndio hivyo nawapenda na jana wote tumeenda kutazama mpira wa Simba na Yanga. Tuko na furaha.!!

Sasa huyo mwenzetu ataweza kuishi na watu wengi ambao sio ndugu zake km sisi??
Mara nyingi hao wa hivyo wachoyo na waficha vyakula, hao km unaenda kusalimia utamuona kanuna.!!
 
Mke mwema hutoka kwa Mungu. Mimi mkewangu anaishi na watoto wa mdogo wangu na aawapenda mpaka sometimes nahisi Mimi Sina mapenzi nao kama yeye. Na siyo kwamba wazazi wao hawapo wapo ila walitengana. Ndo maisha lakini .hapo cha kukushauri Mzee huyo dogo mpeleke boarding school na akifunga likizo mpeleke kwa ndugu Yako mmoja unaemwamini . Atakua mkubwa tu siku hazigandi.
 
Hapana sijamchoka lakini kurudishwa nyumbani haiwezi ikawa adhabu kwangu...itakuwa adhabu kwake.
Kwangu ni vacation😅😅😅. Hata nigombane nae vipi atahakikisha sirudi nyumbani yaani yupo radhi asiende kazini anichunge nisiondoke..
Iwe nimemkosea au amenikosea yeye ipo hivyo siku zote.
Anajua utaenda kusalimia mashem wa zamani kwani yeye mjinga? 🤣🤣🤣
Shem anakupenda na ana wivu analinda mzigo wake.! 😹
 
Be a man.
Chukua uamuzi wa kiume.
Sema na amua kuwa mtoto yeyote ambaye hamkuzaa wawili aondoke ndani ya masaa 24. Usibadili uamuzi.
Mchukue mtoto huyo wa dada mpeleke kwa ndugu utatuma pesa kidogo kila mwezi. Na huyo nguchiro wake aondoke haraka.
Hapo utaiponya ndoa yako na atakuheshimu kuwa wewe ni mwanaume unaweza kuamua jambo mda wowote .
Huyo mke wako ukimlea hivyo ipo siku atakuua hao watoto wenu wakikua.
Be a man
 
Mtoto ahame tuu hakuna namna, familia ni baba, mama na watoto, yeyote zaidi ya hapo ni ndugu tuu mpita njia, akiingia kuishi na familia lazima makubaliano ya dhati yawepo, mmoja akikataa huna haki ya kulazimisha, kumbukeni binadamu ni kama wanyama tuu, ndio maana simba akimkuta jike ana watoto kitu cha kwanza anaua wote anaanza upya, wenzetu wazungu hawana longolongo za wajomba au shangazi ni wao tuu na watoto wao, ila alichofanya ni ukatili lakini nature ndivyo ilivyo hampendi anamuona Kama mvamizi tuu, na haya mambo ni very common kwenye familia nyingi ila hatuongei tuu, kwa issue hii huyo aende kwa bibi au babu ndipo atapata mapenzi ya kweli na umsaidie huko kifedha, Kama hawezi boarding inamhusu ila hapo hakai
 
Wanawake bana, miaka ya mwanzo wa ndoa yangu walikuja ndugu zangu wawili wanasoma chuo kutokea nyumbani kwangu, ikawa kila siku ni mashtaka na kununa. Nikawapangia wale madogo chumba kila mmoja cha kwake maana ni jinsi tofauti.

Alivyojua mimi ndo ninayelipa kodi aka washa tena moto! Hatutakaa tuendelee, bla bla...

Tuende nao tu hivyo...
😂😂😂😂😂 jaman wanachuo wakae hostel
 
Kati ya wewe na mkeo nani mwenye hela zaidi? Wewe ndo unamtesa mtoto kwa kushindwa kutumia madaraka yako kama kichwa cha familia.
 
Back
Top Bottom