Mke wangu anamtesa sana mtoto wa marehemu dada yangu

Mke wangu anamtesa sana mtoto wa marehemu dada yangu

Wanawake tuna ubinafsi ule wa kuzaliwa nao sema kuna wengine maisha yanafunika hiyo roho, wengine ndo kama hivyo wanajiweka hadharani km mkeo,

Hatokaa ampende huyo mtoto hata ufanye nini, kwanza ndo itamuongezea mateso, cha kufanya kata misaada uliyokuwa ukimpa kwa ndg zake, funga kamera upate ushahidi wa manyanyaso yake kwa huyo mtoto, mpeleke kwenye vyombo vya sheria, huyo ni kiburi pambana nae kijeuri jeuri ukilegeza tu huyo mtoto utamkuta maiti siku moja
Hivi mtu unawezaje kuishi na mtu ana roho mbaya????
 
Ongea na mkeo umuulize mtoto ana shida naye gani labda Kama ana muona jeuri na Kama kuna changamoto nyengine muitatue
Na umsisitize awe na upendo kwa huyo mtoto,inawezekana akabadilisha tabia yake
Ila ikishindikana chagua kumpa likizo mke au kumuhamisha mtoto
Upendo hausisitizwi, huyo mwanamke ana roho mbaya tu kwa ndugu wa mumewe . Hapo hakuna mazungumzo ya kurekebisha hiyo shida, options ni mke au mtoto aondolewe hapo nyumbani.
 
Inawezekana sana tu
Kwasababu tabia hazijifichi na hata kama ikijificha utaona tu mtu akiwa ana roho mbaya anakuwa hana upendo na utu na kwa hilo kosa kumfanyia mtoto ni kubwa sana .upendo haubagui hawa wa kwako au sio wako
Huyo mke ana matatizo ya akili makubwa sana kiufupi ameoa kichaa
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni Jumamosi na Jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani

Duh, pole sana mkuu! Akina mama sijui wakoje. Yaani wanataka tulee watoto wao wa ndugu zetu hawapendi hii haiko sawa wanatakiwa wajitafakari sana! Wa kwangu naye alitaka kuleta ujinga huo nikamtolea uvivu. Maana nilikuwa namwona nyumbani kwangu kunakuwa na mafuriko ya ndugu zake na hapo utamuona meno yote nje wakija wa upande wangu hayo meno huyaoni! Nikamkalisha kitako na kuweka msimamo! Nashukuru Mungu alinielewa! Sasa huyu wako mkuu mkumbushe watoto yatima hawateswi, maandiko matakatifu yanasema Mungu naye atalipiza kisasi kwa ajili yao kwa kuwaueni nyie ili watoto wenu nao wawe yatima.
 
mambo ya binadamu baadhi wanaoitwa wanawake yanatia hasira na kukaraisha sana

mkuu cha kufanya mpeleke huyo mtoto boarding school na huko shuleni uwaweke wazi madhila akiyopitia huyo mtoto ili waweze kumrudisha katika hali ya kawaida ya kujiona kama watoto wengine, wakati wa likizo aje kwako muda ambao upo upo home kama hautakuwa na huo muda awe anakaa kwa ndugu zako ambapo una uhakika hatateswa.

hao ndugu wa mwanamke wote fukuza warudi kwao, na yeye akitaka kuondoka mwambie aondoke.

nimeshuhudia mtoto anatoka namba moja darasan mpaka wa mwishoni mwishoni huko kisa kunyanyaswa na kubaguliwa baada ya wazazi wake kufariki.
Kumpeleka boarding ni kukwepa majukumu,mke anatakiwa arudishwe kwao pamoja na watoto wa ndugu zake. Akae kwao hata mwaka mzima mpaka akili zimrudi na ikiwezekana iwe ni talaka mazima. Mwanaume hatakiwi kui-entertain upuuzi,huyo mama hana tofauti na wale wanajeshi wabakaji.
 
Yaani mwanamke muuaji huyo bado uko nae. Na haitaishia hapo,hiyo kuna siku atakufanyia wewe mwenyewe kitu cha hatari. Na mke anaesemaga naona umenichoka bora nirudi kwetu. Huyo ni mzuri sana,hapo hapo ni kumwambia aende. Na usigeuke nyuma,wala kumfikiria.

Kama bado unaona ubaki nae huyo mwanamke ni bora huyo mtoto umpeleke boarding
 
Wanawake bwana hapo ukimzidi ujanja anaweza hata kukuwekea sumu.
 
kaka mkeo ana tatizo la akili, haya mambo sio ya miaka hii kabisa
 
Duh hii ndo shida ya kumpenda zaidi mwanqmke kuliko anavyokupenda yeye mkuu.Kwa sie wengine hilo haliwezi kutokea sababu mwanamke ndiye anayehaha kukupalilia ili tu usimteme hivyo ukileta ndugu atampambania kumuonyesha upendo sababu ataamini huyo ndo mtetezi wake.

BTW Mkuu japo hauna mke hapo hebu jiformat tena.Usihangaike umpeleke wapi mtoto huyo ni damu yako pure aishi kwako kwa sharti moja kubwa kwa mkeo kuwa achague kuishi kwa upendo na huyo mtoto au akaishi kwa upendo kwao na ndugu zake.


Kamwe usikubali ampe mtoto majuto sababu hakupenda kuishi bila mama na ukifanyacho kumlea kina malipo makubwa kwake,marehemu Dada yako,familia yako na kubwa kuliko vyote kwa Mwenyezi MUNGU.


SIMAMA IMARA BRO hili halikupaswa hata kuombea ushauri humu.
 
Ningekuwa mimi ningesema afanye haraka kujiandaa nimsindikize.
Kuna mambo ya kubembeleza.
Huyo atakuwa anakuchapa kwa fimbo hiyohiyo, maana anajua akisema nitaondoka unanywea.
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni Jumamosi na Jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto kumuacha hapa, nahisi atampiga Yani

Ipo siku kilio hicho atakilipia na yeye
 
Sijui kwanini wanawake wa hivyo wanapata wanaume wa aina yenu wapole...Mimi ningekuwa nimemvunja mguu kama alivomganyia mtoto wa dada,Tena marehemu. Aisee ningeua, kwanza kwa hulka yangu hata asingewaza kufanya hivo.

Mtoe hapo nyumbani uyo mwanamke ibilisi, mtoto miaka nane unampiga na tofali!!!? Nimejisikia vibaya sana
 
Kama mjuavyo sisi wanaume mara nyingi ni kuamka asubuhi na mapema na kuondoka, na kurudi ni usiku, muda ambao Mimi nashinda nyumbani ni Jumamosi na Jumapili.

Usiku wa kuamkia Jana alhamis mtoto wa marehemu dada yangu alianza kulia sana chumbani, akalia sana mpaka ikabidi niamke niende chumbani kwao Ili nione Kuna nini, nilivyo fika nilimkuta kakaa chini huku wenzie wamelala, nikamwuliza Kuna nini? Akanijibu mguu unamuuma sana, ikabidi niuangalie mguu, aisee nilijikuta nalia na Mimi, mguu ulikuwa umevimba sana, nikamwuliza ilikuwaje? Akaniambia mke wangu alimpiga na kipande Cha tofali.

Pale pale nikaenda kumwamusha mke wangu kumwuliza hiki alicho fanya, akawa amekataa na kuanza kumfokea mtoto eti anataka kutugombanisha, Nikasema sawa, ila kwanini mguu unafikia hatua hii ina maana alikuwa hamuoni? Akawa amezidisha hasira eti natafuta sababu kama nime mchoka niseme arudi kwao, nikaona maneno yasiwe mengi ikabidi nimpakie mtoto kwenye gari nikampeleka hospital usiku ule ule, iligundulika kuwa mfupa wa mbele wa mguu uliachia kidogo akafungwa P.O.P.

Nilivyo rudi nyumbani asubuhi Jana hiyo asubuhi ilibidi nishinde nyumbani, ikabidi nifanye upelelezi mana Kuna vitu niliiona haviko sawa, ndo mpangaji wangu mmoja akaniambia kama Kuna sehemu naweza kumpeleka huyu mtoto Bora nimpeleke vinginevyo itatokea hatari kubwa, mtoto anateswa mno na mara nyingi shuleni haendi, na siku alivyo mpiga na tofari alikuwa amemtuma vitafunwa asubuhi akachelewa kurudi, tofari alimpiga mbele ya wapangaji siku tatu nyuma, na siku zote hizo hakwenda shule.

Nawaza mtoto nimpeleke wapi, marehemu dada yangu baada ya kufariki 2022 tuligawana watoto sisi ndugu zake, hili tukio limefanya nimkumbuke marehemu dada yangu aliye fariki Kwa maumivu makubwa ya kansa akiwa mikononi mwangu, nawaza Bora kuachana na mke wangu kuliko kuacha mtoto wa dada ateseke ntakuwa nimemkosea dada.

Mke wangu alimchukua mtoto wa kaka yake anaishi hapa na anaelekea kumaliza form 4 Kwa Gharama zangu, ila mtoto wa upande wangu kashindwa kumlea Kwa miaka miwili tu,hii ni sawa kweli?

Halafu baada ya mtoto kuniambia kuwa yeye ndo alimpiga, muda wote saivi ni kumuangalia Kwa jicho Kali sana na kumwambia eti ametumwa aje kutugombanisha, mtoto wa miaka 8 anawezaje kutugombanisha?

Sikuwahi kumfikiria mke wangu kuwa anaweza fanya hiki alicho fanya kutokana na mambo ninayo wafanyia ndugu zake, na ndiyo maana huyu mtoto nilimleta hapa Kwa kuamini atamsimamia kama mwanae na kama anavyo wasimamia watoto wetu wawili.

Mpaka naogopa kwenda kazini na huyu mtoto ku
Aisee pole sana, huyo mkeo ni utafikiri hajaingia leba?. Cha kufanya mpeleke huyo mtoto shule ya boarding awe anarudi likizo tu, na then mwambie atoe ndugu zake ajue pa kuwapeleka pia, iwe pasu kwa pasu. Mke usimuache , utaacha wanapi?, Mana Kila binadamu ana mapungufu yake, unaweza kutana na bomu zaidi ya Hilo. Hila tu unatakiwa kuishi naye kwa akili mandhari umeshamjua tabia yake halisi, huyo hatoweza kukaa na ndugu yako yeyote yule.
 
Aisee pole sana, huyo mkeo ni utafikiri hajaingia leba?. Cha kufanya mpeleke huyo mtoto shule ya boarding awe anarudi likizo tu, na then mwambie atoe ndugu zake ajue pa kuwapeleka pia, iwe pasu kwa pasu. Mke usimuache , utaacha wanapi?, Mana Kila binadamu ana mapungufu yake, unaweza kutana na bomu zaidi ya Hilo. Hila tu unatakiwa kuishi naye kwa akili mandhari umeshamjua tabia yake halisi, huyo hatoweza kukaa na ndugu yako yeyote yule.
Akirudi likizo si ndio atampa sumu kabisa.
Vitafunwa vimesababisha apasuliwe mguu, na tumeambiwa shule haendi ili awe mtumwa hapo nyumbani.
Bahati mbaya jamaa kaoa shetani maana hata yeye anatetemeshwa.

Nilishawahi kupiga kofi mke wangu miaka 27 iliyopita mpaka hivi leo analikumbuka.
 
Mnaoa wehu ndio tatizo halafu mnapenda hasa
Hata afanye nini utakalia kulia lia vijiweni ukirudi home kama sio wewe
Ngoja akupe sumu tu
Huyo mtoto ana dhambi gani wewe ushindwe kumlinda kama sio wehu na wewe pamoja na upofu wa mapenzi

Mpeleke polisi huyo kama huwezi ustawi wa jamii wapo
Yote ukigoma basi weka namba tuchangie boarding school fees zake
 
Mwanaume unatakiwa kua na authority kwako, mi siwezi kukaa na mwanamke eti kitu kidogo anatishia aende kwao, ungemuacha aende huko na usimfate mpaka arudi mwenyewe, la sivyo ashajua udhaifu wako, Kila mkigombana atakua anatishia kwenda kwao


Kuhusu huyo mtoto, kama Kuna ndugu mwingine anaweza kukaa nae basi fanya mpango huo wewe ugharamikie Kila kitu kwa makubaliano kabisa, kuanzia mavazi,elimu,chakula,matibabu etc... Mtoto kukaa sehemu anaponyanyaswa huathirika physiological.... Mnamletea shida tu za badae huyo mtoto



Hilo lishemeji ulilitoa wapi?
Ushauri huu asipoufanyia kazi basi atakuwa tayari mjomba wake afe kwa mateso anayopata kwa mke wake
 
Back
Top Bottom