Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Mwanamke tajiri hana roho ya kimaskini, kinachosumbuwa hapo ni umaskini wa roho tu.

Kumbe hata wanawake huwa wanatangulia kufa pia na kumuacha mume na Watoto.
Inafikirisha sana , ila tutafika tumechoka sana
 
Mapenzi ya mbali kwa dalili hizo inaonyesha kabisa kuna jamaa anamkaza, ukiandika jina lake ndio mwanzo wa kukuchinjia baalini, wewe fanya hivi hapo hakuna ndoa hapo ni kuliana tyming, endeleza kwako wekeza kwa siri, anza kujiandaa kufukuzwa hapo na kuachwa..
 
Acha kiherehere na ubabe, kiwanja cha mkeo wewe ulitumwa nini kwenda kukijenga? Ulifanya hivo ili baadae uje upate auheni ya kwamba una viwanja viwili vyote ni mali yako kwamba uviandike jina lako kisa tu wewe ni baba wa familia? Muachie mama wa watu kiwanja chake aandike jina lake anavyotaka maana hiyo ni mali yake aliitafuta kwa jasho lake. Wewe si unakiwanja chako kwanini usikinjenge kile? Au unampango wa kumuacha?? UNA UBINAFSI WA VIWANGO VYA PHD mkuu
Tuna watoto wawili Sasa. Mimi sikatai kuandika jina lake. Shida ni kwamba hawezi kuhimili maana baada tu ya kuhamia ameshakuwa kiburi akiandika Majina yake tutasumbuana sana na siko tayari tufarakane kwasababu ya watoto wangu nitampa hizo options mbili nopozotaja asipokubali nitatafuta option ya tatu.
 
Kuburi gani? Wewe sema tu unataka kumkwapua mama wa watu mali yake kupitia neno “ana kiburi”
Tuna watoto wawili Sasa. Mimi sikatai kuandika jina lake. Shida ni kwamba hawezi kuhimili maana baada tu ya kuhamia ameshakuwa kiburi akiandika Majina yake tutasumbuana sana na siko tayari tufarakane kwasababu ya watoto wangu nitampa hizo options mbili nopozotaja asipokubali nitatafuta option ya tatu.
 
Si ndiyo hapo sasa🤝
Kiwanja Acha aandike jina lake,kutaka au kulazimisha na jina lako liwepo si u gentleman ukizingatia alinnunua kiwanja yeye. Kujenga ktk kiwanja chake iwe kama umempa zawadi na isiwe sababu ya wewe kujimilikisha kisa vyumba viwili ulivyosimamisha
 
Habari wadau wa jukwaa hili pendwa,

Naomba nienda moja kwa moja kwenye mada.

Mimi nimeoa na Mungu amenijalia watoto wawili. Nafanya kazi sekta binafsi na mke wangu sasa ni mama wa nyumbani. Mke wangu kabla sijamuoa alikuwa amenunua kiwanja chake makao makuu ya wilaya na mimi pia nilikuwa nimenunua kiwanja changu katika wilaya hiyo hiyo ila kwenye tarafa mojawapo.

Tulipooana tuliamua kuishi wilayani, kipindi hicho mimi nilikuwa sina kazi ila yeye alikuwa na kazi japo si mshahara mkubwa na alikuwa kwenye kata mojawapo katika wilaya hiyo nami nilikuwa nimepanga makao makuu ya wilaya, ambapo yeye ndiyo alinunua kiwanja.

Mwaka mmoja baada ya ndoa nikaajiriwa mkoa mwingine hivyo nikamuacha yeye na mtoto, yeye akiwa bado anafanya kazi.
Nikaanza kujenga msingi kwenye kiwanja changu na sikuendeleza nikaachia kwenye msingi. Baadaye nikapiga msingi kwenye kiwanja chake.

Mwaka moja baadaye yeye akaachishwa kazi pale alipokuwa anafanya kazi, ikabidi niwachukue nikae nao mjini. Lakini nikaona ni gharama sana kupanga mjini na mshahara ni mdogo, nikaamua kuchukua mkono nikaendeleza msingi katika kiwanja chake kwa maamuzi kwamba, niendeleze hata vyumba kadhaa halafu niirudishe familia wilaya wakakae huko, mimi nichukue chumba kimoja kupunguza gharama.

Hili pia lilichangia na mgogoro, nikaona siku moja nitapoteza kazi halafu sina pakukimbilia wakati natafuta kazi nyingine. Nikaanza ujenzi na taratibu zote halmashauri nilifanya kwa jina langu. Nikajenga vyumba viwili nikaweka na umeme nikahamisha familia. Kwa sasa wana miezi kadhaa nakuwa nawatembelea walau kila mwisho wa mwezi.

Kilichonifanya niandike uzi huu ni kwamba mke analeta jeuri kwenye hiyo nyumba, kwa kiasi fulani amebadilika, maana juzi kati tulitofautiana jambo fulani dogo nikagundua kiburi kimempanda sana.

Pili, sasa hivi anapambana hati iwe kwa jina lake. Kwa sasa tuna harakati za kuweka maji anajitahidi ajaze fomu yeye kwa jina lake na pia juzi nililipia hela B con na imewekwa sasa yeye anataka kujiandika kama mwenye nyumba.

Ebu naomba ushauri wenu nimuache ajiandike? Nia yangu mimi ni kulinda ndoa yetu, maana naona yeye kama akipata umiliki atanisumbua na tutasababisha mgogoro utakao wasumbua watoto wetu.

Ebu naombeni ushauri kulingana na uelewa na uzoefu, maana mimi kama baba mwenye nyumba ni wajibu wangu kulinda familia yangu, wakina mama wanadanganyika haraka sana. Natarajia kumpiga marufuku harakati zote kwa mamlaka niliyonayo ila nasubiri ushauri wenu.

Asanteni.

Soma mrejesho wa kisa hiki: Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
Muitie Polisi chap
 
Mwenyewe nimewaza. Huenda mwanaume ana michepuko huko anakoendaga kukaa mwezi, Kwahiyo mama wa watu kasanuka. Isitoshe hata kama huyo mama aliongea maneno mabaya kwamba “najuta kuolewa na wewe”…….. hayo maneno yana maana sana, mtu hawezi tu kuongea ghafla bila kuwepo na mazingira yanayoendana na hayo maneno. PERIOD
Huyo mwanamke mnamuonea bure Mimi naona yupo SAHIHI kwanza kiwanja ni chake hivyo ni haki yake

Pili hatujasikia upande wa mke labda jamaa nae kaanza michepuko

Mkeo yupo sawa dunia ya sasa kila mtu anaangalia maslahi yake hongera kwa kupata mke muelevu
 
Habari wadau wa jukwaa hili pendwa,

Naomba nienda moja kwa moja kwenye mada.

Mimi nimeoa na Mungu amenijalia watoto wawili. Nafanya kazi sekta binafsi na mke wangu sasa ni mama wa nyumbani. Mke wangu kabla sijamuoa alikuwa amenunua kiwanja chake makao makuu ya wilaya na mimi pia nilikuwa nimenunua kiwanja changu katika wilaya hiyo hiyo ila kwenye tarafa mojawapo.

Tulipooana tuliamua kuishi wilayani, kipindi hicho mimi nilikuwa sina kazi ila yeye alikuwa na kazi japo si mshahara mkubwa na alikuwa kwenye kata mojawapo katika wilaya hiyo nami nilikuwa nimepanga makao makuu ya wilaya, ambapo yeye ndiyo alinunua kiwanja.

Mwaka mmoja baada ya ndoa nikaajiriwa mkoa mwingine hivyo nikamuacha yeye na mtoto, yeye akiwa bado anafanya kazi.
Nikaanza kujenga msingi kwenye kiwanja changu na sikuendeleza nikaachia kwenye msingi. Baadaye nikapiga msingi kwenye kiwanja chake.

Mwaka moja baadaye yeye akaachishwa kazi pale alipokuwa anafanya kazi, ikabidi niwachukue nikae nao mjini. Lakini nikaona ni gharama sana kupanga mjini na mshahara ni mdogo, nikaamua kuchukua mkono nikaendeleza msingi katika kiwanja chake kwa maamuzi kwamba, niendeleze hata vyumba kadhaa halafu niirudishe familia wilaya wakakae huko, mimi nichukue chumba kimoja kupunguza gharama.

Hili pia lilichangia na mgogoro, nikaona siku moja nitapoteza kazi halafu sina pakukimbilia wakati natafuta kazi nyingine. Nikaanza ujenzi na taratibu zote halmashauri nilifanya kwa jina langu. Nikajenga vyumba viwili nikaweka na umeme nikahamisha familia. Kwa sasa wana miezi kadhaa nakuwa nawatembelea walau kila mwisho wa mwezi.

Kilichonifanya niandike uzi huu ni kwamba mke analeta jeuri kwenye hiyo nyumba, kwa kiasi fulani amebadilika, maana juzi kati tulitofautiana jambo fulani dogo nikagundua kiburi kimempanda sana.

Pili, sasa hivi anapambana hati iwe kwa jina lake. Kwa sasa tuna harakati za kuweka maji anajitahidi ajaze fomu yeye kwa jina lake na pia juzi nililipia hela B con na imewekwa sasa yeye anataka kujiandika kama mwenye nyumba.

Ebu naomba ushauri wenu nimuache ajiandike? Nia yangu mimi ni kulinda ndoa yetu, maana naona yeye kama akipata umiliki atanisumbua na tutasababisha mgogoro utakao wasumbua watoto wetu.

Ebu naombeni ushauri kulingana na uelewa na uzoefu, maana mimi kama baba mwenye nyumba ni wajibu wangu kulinda familia yangu, wakina mama wanadanganyika haraka sana. Natarajia kumpiga marufuku harakati zote kwa mamlaka niliyonayo ila nasubiri ushauri wenu.

Asanteni.

Soma mrejesho wa kisa hiki: Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
1. Kwa kuwa, umekiri kwamba ninyi ni wanandoa (mmefunga ndoa), na,
2. Kwa kuwa, umekiri pia kwamba mna watoto wenu wa wawili ambao wamezaliwa ndani ya ndoa.
Hivyo Basi, suluhisho sahihi zaidi kuhusiana na hili suala lako ni:-
(I) AIDHA, Ardhi hiyo mnapaswa kuimiliki kwa pamoja nyinyi wote wawili kwa umiliki wa pamoja (Joint Occupation or by means of Occupation in Common.
(a) Mmiliki Ardhi hiyo wote kwa pamoja kwa umiliki wenye maslahi yasiyogawanyika, yaani Joint Tenants (Matrimonial Property).
Majina yenu wote wawili (jina lako na la huyo mwanamke) yawepo kwenye Hati ya Umiliki wa Ardhi, hii itaondoa utata na wasiwasi wa kudhulumiana hiyo Ardhi.
(b) Mmiliki Ardhi hiyo wote kwa pamoja kwa Hisa, yaani Common Occupiers in Shares. Mnaweza mkagawana Hisa za umiliki wa hiyo Ardhi, kila Mwanandoa anaweza akamiliki Ardhi hiyo kwa Hisa ya 50% au vinginevyo kwa kadiri mtakavyokubaliana ninyi wenyewe kwa hiyari yenu.

( ii) AU, Wote wawili, yaani wewe na mkeo mnaweza mkajitoa kwenye suala la Umiliki wa hiyo Ardhi, badala yake Ardhi hiyo muimilikishe kwa Watoto wenu na nyinyi mkabaki kuwa wasimamizi tu wa Ardhi husika (Guardianship) hadi hapo watoto wenu watakapofikia umri wa utu uzima wa miaka 18 au zaidi.

NB: Nimeshauri kulingana na uzoefu wangu binafsi wa kimataifa, yawezekana pengine ushauri wangu unakinzana na matakwa ya Sheria za Tanzania, Sina uhakika kuhusu suala hili lakini.
Lakini sehemu nyingi Sana ambazo nimewahi kuzuru, ushauri Kama huu umesaidia Sana katika kutatua Migogoro Kama huu wa kwako.
Naomba kuwasilisha.
I stand to be corrected!
 
Muandikishe tu kwaajili ya watoto,mbona hakuna shida sema hapo kwa kiburi ndio tabu
Fanya tu umemjengea na wanae huna hasara
 
A man who show affection is not a real man. Pesa nitafute mm afu nikuandike wewe awapi
 
Back
Top Bottom