Mke wangu kalipendea nini hili jitu?

Mke wangu kalipendea nini hili jitu?

ivi unaendaje kwa watu unavaa boxer peke yake mwenye nyumba tu havai ivyo who are u, me ningemblast dress properly
 
Nenda naye jino kwa jino.
Anazunguka ndani na boxa wewe zunguka ndani na boxa pikipiki huku umevaa boxa.

Anatembea kifua wazi tembea kitambi wazi huku umekichora six packs na kalamu ya biki au maka peni.

Anasaidia kuosha vyombo wewe unaosha hadi vitakavyotumika kesho yake.

Yote hayo ukifanya na akiendelea kung'ara yeye tu, mwambie "Binamu rudi nyumbani"
 
Kuna makabila binamu wanakulana tu. Tena siku hzi mabinamu hawa si wa kuwaamini. Mpk mama anakutolea mfano kifua cha jamaa. Ina maana amekizimia.
 
Huyo hata ukimfukuza kama wife ameshamuelewa lazima watafutane tu na watimize haja zao
 
Waheshimiwa nina mgeni ambae sasa anaelekea kumaliza wiki akiwa hapa kwangu, ni binamu yangu huwa anaishi mkoani amekuja kwa shughuli zake binafsi, ataondoka atapokamilisha yaliyomleta.

Nimewaandikia kwa sababu, huyu jamaa amenishangaza sana, imagine weekend hii iliyokwisha anashinda na boxer kutwa nzima tena kifua wazi, au kwasababu amevimba kifua anataka tumwone au?

Mke wangu na house girl wanafua nguo Jumamosi asubuhi eti anaenda pale awasaidie kufua, natoka ndani namuuliza wife mbona mgeni anafua nguo, najibiwa kuwa eti ameomba mwenyewe, hii ni sawa kweli?

Yote tisa, kumi ni Jana, inafikia hatua linamkuta wife jikoni anasonga ugali linaomba limsaidie kusonga ugali, mgeni gani wa namna hii?

Wadau nitumie njia gani kulitimua hili jitu hapo nyumbani? Kabla halijaleta madhara maana mdogo wa mke wangu naona kama yuko nalo karibu sana, pia wife kaniuliza kama mimi pia naweza kufanya mazoezi nikawa kama hilo jitu badala ya kitambi, ingawa alinieleza kwa utani huku tukifurahi na kutaniana ila najiuliza kwanini aseme sasa wakati hili jitu lipo?

Linakaa hapo sebuleni kwenye video hadi usiku mwingi likiwa na mdogo wa mke wangu bila kujali maadili.

Jumapili nilienda kwenye Bonanza la timu yetu ya veterans narudi nimekuta nyumba nzima hawapo wameenda beach wote pamoja na huyu jamaa.

Hivi unaendaje ugenini halafu unaanza kuleta ujuaji wa namna hii?

Wadau msaada wa mawazo unatakiwa haraka.

Lipe muda kwanza!
 
Umeumizwa sana.kama Accacia na Tz vs mchanga wa dhahabu.
 
Utakua unampenda au unamla shemeji yako wewe, kwa nini unamuonea wivu? Hapa inaonyesha kabisa jamaa ana interest na mdogo wa mke wako ila wewe unataka ku justify kwa kumpa kesi ya kumtaka mkeo
 
Utakua unampenda au unamla shemeji yako wewe, kwa nini unamuonea wivu? Hapa inaonyesha kabisa jamaa ana interest na mdogo wa mke wako ila wewe unataka ku justify kwa kumpa kesi ya kumtaka mkeo
I guess
 
maisha ndivyo yalivyo familia inahitaji socialisation and charming sio kumfanya mke kama mtumwa wewe unatakiwa ubadilike uwe kama hilo jitu kabla hujalifukuza ili ukilifukuza usiache gap. kuvaa boxer wewe ndo unaliendekeza linunulie kaptura buga
 
Kama mke wako kashaanza kushauri ufanane kwa umbo na hilo jitu, aise karibia unaibiwa hapo.

Kumbuka: Linapokuja swala la mapenzi hutakiwi kumwamini hata baba mzazi. Litimue hilo jitu mkuu.
 
Unamuonea wivu mdogo wake mkeo. Boss wewe ni hatari. Jokes!!

Mimi naona huyo jamaa amepata treatment nzuri sana ambayo labda hajawahi kupata katika maisha yake, mfn mazingira ya hapo home, upendo, vyakula, nidhamu, townlife, kuthaminiwa, uhuru nk. Sasa hivi vitu ni kama vinamfanya arudhishe fadhila, ama niseme kucompensate ili aonekane ni mtu wa faida, ndio maana utamuona ana give back upendo, anatamani afue, apike, aoshe vyombo nk. Hii yote ili asionekane mzigo hapo home na pia aonekane si lelemama. Ni wanaume wa mkoani hua wapo hivyo boss.

Pia nahisi mke wako anakujali sana kukwambia upunguze kitambi uwe kama hilo lijitu, hii ni kwa afya yako, ila kwasababu tayari umeshamchukia lijitu, unaona km vile upo insulted. Kiuhalisia mkeo yupo sahihi sana, jivunie boss kua na mke anaependa ndugu wa kila aina, km mkeo angekua hovyo hayo yote unayoyasema kuhusu hilo lijitu yangefanyika kwa siri mno.
Naweza kukuunga mkono ila anachokodea tu huyu jamaa ni kukaa na boxer hadharan,,ila kila kitu anafanya sababu asionekane hawajibiki
 
Back
Top Bottom