Mke wangu kanipa wakati mgumu

Mke wangu kanipa wakati mgumu

Kwa maisha mliyoishi miaka 30, sioni shida kwenye hizo meseji.

Mawasiliano ya kawaida kabisa hayo, kama hayakupendezi ni vyema kumwambia ayasitishe muendelee kuishi kwa amani.
Nifah,ni kweli uyasemayolakini roho inauma , nakubaliana na wewe , lakini naona kama mahusiano yalikuwapo muda mrefu , nimeacha kazi miaka miwili iliyopita nikaanza kuona dalili za dharau hivi, ndio nikaanza uchunguzi na kukutana na hayo.

Nimepanga kumuuliza kesho.
 
Kama una above 50 msamehe tu, hakuna jipya, wote wanaliwa Kaka. Utakuja kufa bure Kaka yangu.

Pia ukiona mwanaume hana interest hivyo, ujue mkeo anamchuna na hana time naye kabisa.

Wanawake wote wako hivyo hivyo, tunaomba Mungu tu uzima na tusipateagongwa Kaka.
Lakini upendo utsendelea tena ndugu yangu kuishi na mtu wa namna hii,
Kumbuka nimeishi naye miaka yote hiyo kumbe slikuwa na mambo yske,

Nasikia uchungu sana kama ni kweli alikuwa ni malaya, nashindwa hata kuongea naye vizuri,

Kila akiongea naona ni tapeli fulani,

Lakini swali langu lipo palepale , je nimuulize?
 
Kama una above 50 msamehe tu, hakuna jipya, wote wanaliwa Kaka. Utakuja kufa bure Kaka yangu.

Pia ukiona mwanaume hana interest hivyo, ujue mkeo anamchuna na hana time naye kabisa.

Wanawake wote wako hivyo hivyo, tunaomba Mungu tu uzima na tusipateagongwa Kaka.
Uttoh2020, kwa jinsi unaona hizo chart, kwa muono wako , je ni nzuri kwa Mume, au zinatia mashaka
 
Tatizo hapo sioni message yoyote kama ni marafiki wa kawaida tu,

Maana kama ni urafiki , labda ningeona wanazungumzia kitu fulani, lakini naona ni kama mke wangu anataka kitu kwako
Hapo sasa ni kuwa ni marafiki walio zoeana na jamaa anaonekana hana haiba ya kutoka na mke wa mtu.

Ni wanawake wote au niseme wengi wanatabia kama za mkeo.
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, nimeishi na mke wangu zaidi ya miaka 30, lakini nilihisi ana bwana wa pembeni, nikaanza kufanya uchunguzi, kweli nikafuma baadhi ya msg , ambaxo kwa tabia yake kwangu aliyonionesha kwa miaka hiyo tuliyoishi, niliona si kawaida.

Mbaya zaidi hizo msg alizokuwa anatuma kwa huyo bwana( siwezi kumwita hawara kwa sasa) ilikuwa ni kama yeye anataka mahusiano yaendelee, maana mwanaume alikuwa akimjibu kwa mkato tu.

Mke- kwema, kimya
Mume/ baada ya siku tano/- kwema nipo, sawa
Mke- mmm sawa hiyo vipi,
Mume/ safi
Mke — mvua tu

Baada ya wiki
Mume— mzima wewe
Mke—upo poa wewe
Kwema tu, hofu kwako,
Kimya jamani, naona umetupa jongoo na mti wake,
Jua kali tu ee utadhani limeshuka.

Mume, nipo , hujibu SMS zangu!
Mke— saa ngapi tena wewe ndio hujibu.
Mume—- hahahaa upo!

Mke— nipo kuzeeka tu ndio kumepamba moto.

Mume—- aaa baba ajambo

Mke—- yupo tu aliacha na kazi sasa hivi yupo tu nyumbani.,
Mume—/ poa

Mke tena baada ya wiki
Mke —Upo kaka, za uzima!

Mume— poa.

Baada ya kushindwa kuvumilia na kuepusha kuona maajabu zaidi, nimeamua kulileta hili hapa ili mnisaidie, mke wangu bado nampenda, lakini nataka nijue nini kinaendelea,

Swali je nimuulize au nivumilie kidogo.

Watoto tunao wanne na wana maisha yao.
Wanaume kama nyie mtakufa maskini.

After 30yrs of living together ndio unajifanya kumfatilia?

Au umepata kigoli unamtafutia Sababu?

Au ni Stori ya kutunga hii.

Wewe ni Mzee ndugu yangu kua na heshima.
 
I can figure it out uko around 50+, kuna umri ukifika hata mke achepuke it doesn't bother. Vipi watoto wote ua uhakika ni wako?

Anyway, mwambie tu kuwa umejua. Halafu usifanye kitu.
Aisee, inahitaji moyo,
Je nimwambie hilo tu, au inatakiwa nijue zaidi kwa kumuhoji
Ni kama walikuwa na mahusiano ambayo kwa sasa hayako active, japo wakati wowote wanapasha kiporo...ni muhimu umuhoji akupe maelezo yasiyotia shaka kabisa maana ukinyamza sonona itakumaliza.
sawa ushauri mxuri sana, hilo la kupasha kiporo ndio linaniumiza, maana sitamwamini tena, ni maisha bila kuaminiana hayana maana
 
Wanaume kama nyie mtakufa maskini.

After 30yrs of living together ndio unajifanya kumfatilia?

Au umepata kigoli unamtafutia Sababu?

Au ni Stori ya kutunga hii.

Wewe ni Mzee ndugu yangu kua na heshima.
Kufuatilia mke sio kitu rahisi hivyo, nimesema kuna vitu ambavyo sio vya kawaida nimeviona toka kwake ndio nikaamua kufuatilia,

Na kweli nimegundua mambo kama hayo.

Lakini ndugu yangu kwa umri huu , halafu nione vitu kama hivi si ndio kufa mapema huku
 
Huyo mwanamke kwanza kabisa anakudharau.
Badala ya kusema umestaafu, anasema umeacha kazi upo tu nyumbani.
Ni hilo neno ndio ndio limeniudhi sana , kwa nini amwambie nimeacha kazi ni nipo tu nyumbani,
Inaamanisha kuwa kwangu nyumbani ni kama anamfamisha kuwa , hana nafasi vizuri tena kama zamani
 
Samahani ndugu, kwa umri wako unaonekana ni mtu mzima na ulienda jandoni! Hii jamii forum huwa naichukulia ni kama mtaa au kijiji.

Itajengwa hoja kuwa hatufahamiani na tunatumia majina bandia lakini humo kuna watoto, wahuni, wavuta bangi, wanafunzi,watu wazima hovyo,wenye busara na hekima n.k (Ila huwezi kuwajua mpaka atoe majibu)

Swali: Je, upo tayari matatizo yako yote hata ya aibu mtaa mzima au kijiji uyafahamu??

Kwa umri wako umeshindwa kuwatafuta wakongwe wenzako mkakaa kikao na kujadili changamoto inayokukabili kwa utulivu mkubwa??

Hapa naona umewatangazia kijiji au mtaa! Vumilia majibu ya waliopoteza ndoa, waliokosa ajira, walevi, wavuta bangi, vichaa, wanafunzi, watoto, walioachwa n.k!

Nb: Ni mtazamo tu!
😂😂😂😂 umetusahau backbenchers bro
 
20240402_120316.jpg
 
Back
Top Bottom