Mkeo ni wa kundi gani kati ya haya?

Mkeo ni wa kundi gani kati ya haya?

Mkuu, sawa nimekuelewa, ila hapo kwa wazazi wangu umekosea.

Mimi mama yangu (76-80 age) bado anamtngea maji mzee na anamkaribisha chakula. Siawahi kuona mzee anajipakulia chakula wala kujitengea maji ya kuoga.

Sio kwa wazaz wangu tu, hata mabroo zangu wote Ni hivo.

Mnawaendekeza wake zenu dadeki

Mzee kuowa haimaanishi kwamba utaanza kuishi kifalme,liweke hili akilini mwako ngoja siku uowe kisha umtake mkeo mwaka wa kwanza mpaka wa 5 akufanyie aliyokuwa akikufanyia mkiwa mwaka wa 1 uone kama hujaanza safari kwa mshenga kulalamika nyumbani hakukaliki.

Kingine...usije uka-copy maisha anayoishi mwenzako kwenye ndoa yake ukataka uyapachike kwenye ndoa yako mapema sana utavuruga mipango yako,ishi kile kitakachokupa amani.vipi kama akawa anakufanyia yote hayo ila akawa anapika chakula kibovu,watoto kulala bila kuoga au kula na nyumba kutofanyiwa usafi utajisikiaje?na haya ukimuuliza atakwambia anafanya hivyo ili kukimbizana na kasi yako.

Pia huwa sioni logical kusubiri eti utengewe maji ya kuoga na mkeo,kweli hiki ni kitu cha kusubiri?
 
Japo ni single mom,na sijamuoa,lakini naishi nae huku nchi za watu.

Namba moja inamstahiki
 
Mzee kuowa haimaanishi kwamba utaanza kuishi kifalme,liweke hili akilini mwako ngoja siku uowe kisha umtake mkeo mwaka wa kwanza mpaka wa 5 akufanyie aliyokuwa akikufanyia mkiwa mwaka wa 1 uone kama hujaanza safari kwa mshenga kulalamika nyumbani hakukaliki.

Kingine...usije uka-copy maisha anayoishi mwenzako kwenye ndoa yake ukataka uyapachike kwenye ndoa yako mapema sana utavuruga mipango yako,ishi kile kitakachokupa amani.vipi kama akawa anakufanyia yote hayo ila akawa anapika chakula kibovu,watoto kulala bila kuoga au kula na nyumba kutofanyiwa usafi utajisikiaje?na haya ukimuuliza atakwambia anafanya hivyo ili kukimbizana na kasi yako.

Pia huwa sioni logical kusubiri eti utengewe maji ya kuoga na mkeo,kweli hiki ni kitu cha kusubiri?
Pole Sana mkuu
 
.....................Sikuwahi kuchunguza sana kuhusu mabadiliko niliyokuja kuyaona miaka michache baada ya ndoa but nachokumbuka mwanzo ama akini-ectia ama ni mabadiliko tu yalitokea ila alikuwa smart sana kwenye maamuzi na uelewa (sisemi kwamba sasa hivi hayupo smart) ila amenifanya nizidi kuishi nae kwa akili sana.

Nachoweza kusema na kwa experience yangu ndani ya ndoa miaka 8 sasa ni kwamba kadiri mnavyoongeza familia ndivyo na tabia za mkeo zinavyoanza kubadilika,(haijalishi ni understanding au non-understanding)hakuna siku atakutukana ila baadhi ya huduma ulizokuwa ukipewa zamani bila kuuliza itakubidi wewe mwenyewe uanze kujifanyia na wala usithubutu kuuliza omba uwe na hekima ya kujua mapema maana ya mabadiliko hayo lah hukujua utaitumbukiza ndoa kwenye vurugu,personally miaka ya mwanzo akinitengea maji ya kuoga,kuninyooshea nguo,kunipakulia chakula nikirudi home anapokea kama mkononi nina kimfuko au bag atakuja kupokea ila baada ya kupata mtoto wa kwanza hiyo ya kuwekewa maji ya kuoga na kuandaliwa nguo zilikufa nikabaki na favor mbili,kupokewa mzigo mwenyewe nilikataa nikaona kama utumwa sasa tuna watoto wawili hii ya kupakuliwa chakula muda wowote naona itakufa.

Obviously malalamiko mengi ya wanaume kwenye ndoa hutokana na huduma fulani kukatwa ghafla na majibu yasiyotegemewa kutoka kwa wake zao pale wanapouliza sababu,nilichogundua;anakuwa busy zaidi na watoto so hawezi kuacha kumlisha mtoto akakuandalie wewe maji ya kuoga,hawezi kuacha kumnyonyesha mtoto au kumuandaa mtoto awahi school bus akakunyooshee nguo also hawezi kuacha kumuogesha mtoto akakupakulie chakula mezani sasa ukiwa macho juu juu utataka kuhoji “inakuwaje zamani ukifanya hiki na hiki mbona sasa hivi hunifanyii” jibu utakalopewa hapo ndo litakaloamua hatma ya ndoa yenu,binafsi nachoshukuru niliweza ku-match na mabadiliko haya mapema na nachowashauri mnaotaka kuingia kwenye ndoa jueni mke siyo kwa ajili ya kukuhudumia wewe kwa kila kitu wanaopaswa kuhudumiwa kwa kila kitu na yeye wewe pia ukishiriki ni watoto wenu mtakaowazaa.

Well.....vurugu zipo na ieleweke tukubali au tukatae wanawake % kubwa wanafanana akili awe amesoma au hakusoma hakuna mwanamke anayekataa au anayekubali kosa kizembe,ni “kuishi nao kwa akili tu” ukiijua sentence hii na ukakubali ikuongoze kwenye arguments na mkeo ndoa utaiona tamu tofauti na hapo ni pigo.
Mke hakupakulii chakula,hakuwekei maji ya kuoga,hakupasii nguo na umeamua kuchukulia simple tu.

Unafeli bro kweli kuna kipindi wake zetu wanabanwa na kazi sikatai lakini kwa hili hapana aisee..

Mimi nipo tiari nimsaidie kudek au kufua lakini sio kujipakulia chakula au kujipelekea maji bafuni et kisa watoto...ata hao watoto ipo siku watakushangaa haki! Labda ungesema siku moja moja unajisikiaga kufanya ivyo lakini Kama ni kila siku basi wewe bado ni single uliechangamka.
 
Mkuu nahisi tunashea mke mmoja au labda ni twin wake
Namba mbili wapo wengi balaaa


Nilivyooa ndo nikathibitisha ukweli wa kuwa mwanamke hakosei ukitaka Vita na mkeo wewe mwambie kakosea sehemu flani...

Wife bwana chochote unachomwambia ameteleza ujue lazima atakirudisha kwako mpk saivi imebidi uwe utani tu


Mke maji ya kunywa ulikumbuka kuchemsha? mtu mwenyewe hata nikichemsha hunywi.[emoji3][emoji3]

Nimerudi zangu home saa 7mchana badala ya saa 9/10 niliyozoea kurudi.Mke chakula tyr?Mke :Bado,mtu mwenyewe wewe hutabiriki unarud sa ngap nilichelewa kidogo kupika.

Mke umesahau kumpigia mama ulisema utaongea nae leo?wewe huyo hujanikumbusha...[emoji38][emoji38][emoji38]

Mimi:mke punguza sauti ya TV Kuna kazi inachanganya nahitaji umakini kdg,wewe hata ukiwa free hupendi niangalie movies za kikorea...

Mke chumvi leo imezidi kdg wewe huyo unakuja kunipigisha story wakati napika [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Nimeamka zangu asubuh najiandaa kwenda kwenye mishe nikaanzisha story mke umeamka tyr?mbona mapema?Wewe huyo unazunguka zunguka chumbani mpk usingizi umekata

Juzi kadondosha grass ya maji mi nikageuka tu nikamuangalia nikampa pole nikasikia wewe huyo unaniangalia sanaaaaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Maskini hata hajui keshazoea mi saivi akiboronga namwambia sio kosa lako mi Mimi huyo nimesababisha,anachekaaaa balaaa[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Mke hakupakulii chakula,hakuwekei maji ya kuoga,hakupasii nguo na umeamua kuchukulia simple tu.

Unafeli bro kweli kuna kipindi wake zetu wanabanwa na kazi sikatai lakini kwa hili hapana aisee..

Mimi nipo tiari nimsaidie kudek au kufua lakini sio kujipakulia chakula au kujipelekea maji bafuni et kisa watoto...ata hao watoto ipo siku watakushangaa haki! Labda ungesema siku moja moja unajisikiaga kufanya ivyo lakini Kama ni kila siku basi wewe bado ni single uliechangamka.
Mkuu kwani kupelekewa maji wewe umekupatia maana gani? Muda huo unaomsaidia kudeki si bora ujipelekee hayo maji?
 
.............Yah mkuu nilichoandika wala sijakosea ila sijasema hanitengei chakula mezani au hanikaribishi na hata asiponikaribisha unadhani kwenye ndoa ni kitu cha kufuatilia hiki,utafuatilia mangapi na utahoji mangapi?kama amepika vizuri chakula na umekikuta mezani kimekamilika kuna haja gani tena kuulizana mbona hujanikaribisha?na huko kuhoji hoji sana vitu vidogo vidogo ndiko mnapokuta mmezusha vurugu zisizo na kichwa wala miguu unless uniambie unatafuta sababu za kumuacha maana maisha ya ndoa ni continuous viapo ni kuishi milele na kuvumiliana.

Falsafa yangu nayoiishi ktk ndoa yangu ni “sikuowa mke aje kunitumikia” bali kuwa msaidizi wangu pamoja na kuendeleza kizazi changu,nimesema mwanzo akifanya yote hayo ila family ilipoongezeka hayo hanifanyii na nilielewa wala sijawhi kuhoji niliona tu mwenyewe siku za weekend nikiwa home hiyo battle ya watoto humo ndani hakukaliki na kama mimi kukaa na watoto nusu saa tu siwezi yeye anakaa nao kutwa nzima itakuwaje?maana hawaelekezeki kirahisi.iko hivi;nina watoto mmoja 6 aged na mwengine mwaka 1/10,muda ninaoingia home kutoka job ni saa 20:00 usiku nikifika namkuta wife amemsimamia huyu mkubwa ili ale akalale kesho aamkie shule (bahati mbaya ni mtundu mno) akiachiwa upenyo ale mwenyewe chakula utakikuta kwenye basin la vyombo vichafu hakijaguswa hata kidogo.niambie wewe kama baba,utamwambia mkeo aache kumsimamia mtoto akakuandalie maji ya kuoga?je kabla hujamuowa hukuwa unaoga wewe,aliyekuwa anakuandalia maji ni nani?

Baada ya hapo aje kwa huyu mdogo naye amuogeshe kisha aanze kumpa chakula na huyu akiwa analishwa anataka azunguke nyumba nzima hatulii sehemu moja,muda huo ndo nimeshaoga na mimi nipo dinning nataka kula na pale mezani zana zote wezeshi za mimi kuendelea zipo unataka kuniambia nisijipakulie chakula nile ila niite kwa sauti ya mamlaka “wewe mwanamke njoo unipakulie chakula”,well ataweza kutii but vipi mtoto akipaliwa chakula kule aliko umeshafikiria hasara zake?au kuniandalia nguo asubuhi,huo muda wa kufanya hivyo sasa hana tena muda huo anautumia kwa mtoto ili awahi shule yani nilichoandika pale juu ni kitu nakiishi na nimekishuhudia na mke wangu kuweka house girl hataki nilihoji akanipa sababu zake,ukweli hazikuwa na mashiko ila ikabidi nielewe kiutu uzima maana mama mwenye nyumba ameshasema ning'ang'anizane naye kwa faida gani?na naridhika na maisha tunayoishi!

Maisha ya ndoa siyo bongo movie yanataka hekima na busara ukitaka kuamini kama baba na mama yako wapo pamoja mpaka sasa chunguza je bado mama anampelekea mzee maji bafuni?zile ni longolongo tu za uchanga wa penzi wala usizizingatie sana life likishakolea mbona utajikuta upo ndani ya ndoa ila unaishi as if upo kwenye u-bachelor na ukiwa mwelewa hakuna siku utapishana hovyo kauli na mkeo.
We jamaa unaonekana umetokea Pwani. Me nimeishi na Mshua na Maza toka nakua naona maza lazma aamke abandike maji ya kuoga alfajiri...

Ataandaa chai asubuhi mzee akitoka kuoga anavaa nguo zishapigwa pasi siku nyingi kisha anaenda mezani for breakfast. Mie nnje nishafagia na kuosha gari na ilikuwa kama utamaduni wetu. Mshua akirudi akapaki namshushia bag lake la ofisini napeleka chumbani kwake.

Kufua maza anafua nguo sox ananiachia mimi namsaidia. Akiwepo beki 3 anawasha jiko anabandika maji ila ni agizo la bi mkubwa. Kupika cha mshua bi mkubwa anapika mwenyewe. Mshua akiwa kazini madhe anasafisha room kwao. Sometimes ananiomba namsaidia kusafisha akiwa anaumwa au amechoka.

Sasa nikija kuoa mke asiwe kama ambavyo nimekuwa nikiona mazingira ya home au akashindwa ku cope na chores zake lazma tutashindwana tu. Japo mke sio mtumwa ila nimekuzwa kuwa Dominant! Ndio utamaduni wetu ulivyo na hakuna kitu mzee alikuwa anamaindi kama kunikuta jikoni nasaidia kazi 🤣🤣🤣
 
Mzee kuowa haimaanishi kwamba utaanza kuishi kifalme,liweke hili akilini mwako ngoja siku uowe kisha umtake mkeo mwaka wa kwanza mpaka wa 5 akufanyie aliyokuwa akikufanyia mkiwa mwaka wa 1 uone kama hujaanza safari kwa mshenga kulalamika nyumbani hakukaliki.

Kingine...usije uka-copy maisha anayoishi mwenzako kwenye ndoa yake ukataka uyapachike kwenye ndoa yako mapema sana utavuruga mipango yako,ishi kile kitakachokupa amani.vipi kama akawa anakufanyia yote hayo ila akawa anapika chakula kibovu,watoto kulala bila kuoga au kula na nyumba kutofanyiwa usafi utajisikiaje?na haya ukimuuliza atakwambia anafanya hivyo ili kukimbizana na kasi yako.

Pia huwa sioni logical kusubiri eti utengewe maji ya kuoga na mkeo,kweli hiki ni kitu cha kusubiri?
Sio kila mtu ana heater mkuu, wengine mpaka yapangwe mafiga 🤣🤣🤣🤣
 
We jamaa unaonekana umetokea Pwani. Me nimeishi na Mshua na Maza toka nakua naona maza lazma aamke abandike maji ya kuoga alfajiri...

Ataandaa chai asubuhi mzee akitoka kuoga anavaa nguo zishapigwa pasi siku nyingi kisha anaenda mezani for breakfast. Mie nnje nishafagia na kuosha gari na ilikuwa kama utamaduni wetu. Mshua akirudi akapaki namshushia bag lake la ofisini napeleka chumbani kwake.

Kufua maza anafua nguo sox ananiachia mimi namsaidia. Akiwepo beki 3 anawasha jiko anabandika maji ila ni agizo la bi mkubwa. Kupika cha mshua bi mkubwa anapika mwenyewe. Mshua akiwa kazini madhe anasafisha room kwao. Sometimes ananiomba namsaidia kusafisha akiwa anaumwa au amechoka.

Sasa nikija kuoa mke asiwe kama ambavyo nimekuwa nikiona mazingira ya home au akashindwa ku cope na chores zake lazma tutashindwana tu. Japo mke sio mtumwa ila nimekuzwa kuwa Dominant! Ndio utamaduni wetu ulivyo na hakuna kitu mzee alikuwa anamaindi kama kunikuta jikoni nasaidia kazi [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mke alifundishwa kwao, ukaoa kwa taratibu zote za kimila na kidini lazima awe na tabia hz ,huyu ndio Mke hasa wa kuita Mke

Nampenda Mke wangu hizi Sifa anazo ingawa wa kisasa
 
We jamaa unaonekana umetokea Pwani. Me nimeishi na Mshua na Maza toka nakua naona maza lazma aamke abandike maji ya kuoga alfajiri...

Ataandaa chai asubuhi mzee akitoka kuoga anavaa nguo zishapigwa pasi siku nyingi kisha anaenda mezani for breakfast. Mie nnje nishafagia na kuosha gari na ilikuwa kama utamaduni wetu. Mshua akirudi akapaki namshushia bag lake la ofisini napeleka chumbani kwake.

Kufua maza anafua nguo sox ananiachia mimi namsaidia. Akiwepo beki 3 anawasha jiko anabandika maji ila ni agizo la bi mkubwa. Kupika cha mshua bi mkubwa anapika mwenyewe. Mshua akiwa kazini madhe anasafisha room kwao. Sometimes ananiomba namsaidia kusafisha akiwa anaumwa au amechoka.

Sasa nikija kuoa mke asiwe kama ambavyo nimekuwa nikiona mazingira ya home au akashindwa ku cope na chores zake lazma tutashindwana tu. Japo mke sio mtumwa ila nimekuzwa kuwa Dominant! Ndio utamaduni wetu ulivyo na hakuna kitu mzee alikuwa anamaindi kama kunikuta jikoni nasaidia kazi 🤣🤣🤣
Mwanaume akifanyiwa hivi anakabidhi hadi pumbu, limbwata liko mikononi mwetu wanawake hatujui tu, nadhani nimemrithi bi mkubwa wako
 
Mwanaume akifanyiwa hivi anakabidhi hadi pumbu, limbwata liko mikononi mwetu wanawake hatujui tu, nadhani nimemrithi bi mkubwa wako
Hahahah sasa je na ndio michepuko inapopenyea hapo, ila wanawake wengi wajinga hawaelewi hili! Mwanaume anatakiwa apewe treatment special bana. Hata diet yake ni special!

Make a man feel like a man then umemaliza kazi wewe utapendwa hadi siku yako ya mwisho. Sema unachotaka hata dunia utapewa.

Sasa unakuta mke dharau, eti anajibu kwani we hauna mikono ama? That never works on me! Sana sana ntakuzabua nionekane katili.

In Addition ndoa inakaribia ku approach 40 years. Treatment is still the same sasa ambao wanahisi kuwa treated like a man ni kuwafanya utumwa na kunaisha watoto wakizaliwa waangalie walipoteleza.
 
Mkuu kwani kupelekewa maji wewe umekupatia maana gani? Muda huo unaomsaidia kudeki si bora ujipelekee hayo maji?
Mkuu Mimi sikatai wanaume kuwasaidia wake zetu kazi lakini pale inapokua ni lazima huifanye basi tofauti yako na mkeo ni kua karibu nae tu mean hujajitenga na ubachela.
 
Back
Top Bottom