Nope!!!
Me wa mikoani ila naishi Dar,hii town kuoga maji hayachemshwi may be ingekuwa hivyo angefanya wife maana kitu kinachoitwa jiko sijawahi kuwasha nikiwa naye,kufua nguo sijawahi kufua akiwepo labda amesafiri na namshukuru Mungu wife anaijua mipaka yake.
Mkuu umri wako siujui ila kwa vyovyote vile mama yako ni aina ya wale wamama wa 60s so kimalezi huwezi kumfananisha kwa namna yoyote na hawa kina Esther na Mwajuma mnaokutana nao huko mavyuoni wakiwa na smartphone mikononi leo utegemee kuishi naye kama mama yako alivyokuwa anaishi na baba yako,never na ikiwa akilini mwako umejijengea picha hii kwa hawa wanawake wa siku hizi i swear jiandae kuzeeka ukiwa bachelor au ukiwa na familia isiyoelewa kama inaenda mbele au inarudi nyuma.sometimes hata wanaume huwa hatuelewi tunataka nini hasa,maana kizazi hiki wengi wenu mnataka na wake zenu watoke wakatafute kula ya familia sasa najiuliza huyu mke anatakiwa naye awahi kazini,so aamke aandae nguo zake,nguo zako (sitaiweka hii ya kuandaa chai alioakiifanya mama maana vijana siku hizi tume-advance chai tunanywea makazini) kisha mbio akaoge kisha tena akupekee wewe maji bafuni wakati huo wewe umekaa tu...kweli mkuu hii inakuingia akilini?!!
Na itabidi aamke saa 9 ili hayo yote ayafanye kumbuka jana alirudi usiku amechoka akakuandalia kila kitu maji ya kuoga yakiwepo na unyumba usiku ulimuomba akakupa au hakukupa mimi sijui yaani kiufupi hapa inakuwa ni vurugu tu unaishi na mateka,haya uniambie ktk zunguka yako yoote umewahi ona ktk kizazi hiki wa kufanya hayo?usijilishe upepo ndoa ni reality tegemea lolote likiwa baya tafuta namna yakufanya liwe zuri likiwa zuri shukuru maisha yaende.u know,hata wakati sijaowa nilikuwa na mitazamo hii hii ila nilipoingia haraka sana nature ikani-select nikakuta kumbe sivyo nilivyokuwa nawaza,utashangaa nimeowa na miaka 27 tu kijana bado ila ubongo ukakaza ukaelewa mabadiliko yote hatua kwa hatua na sasa nimetulia maisha yanaenda.
Na siku hizi kuna kitu kinaitwa feminist sijui feni nini kimeingia hiki kwa mawazo yenu haya tegeemeni kuteseka sana na hawa wanawake,zama hizi hayupo mwanamke atakubali kuanzia mwaka wa kwanza wa ndoa yenu mpaka wa kumi,yeye aweke mtoto chini akupelekee maji bafuni kisa ni mumewe huku umekaa tu,yaani umejinyooshea miguu usubiri maji yaende bafuni nakwambia hayupo na usitegemee kukutana naye hata ukienda kumuokota huko kijijini ndani ndani ipo siku tu atakutaka ujihudumie mwenyewe na utajihudumia!