Mkoa wa Kagera ni Mkoa masikini zaidi nchini Tanzania; tutaugeuza kituo cha biashara EAC

Mkoa wa Kagera ni Mkoa masikini zaidi nchini Tanzania; tutaugeuza kituo cha biashara EAC

Kuna haja 50% ya mapato ya kila mkoa yabaki kuunufaisha mkoa husika...

Watu wa kagera sio masikini kiasi hicho, tatizo wanachokichangia kwenye kapu la taifa hakiwafaidishi

Ni kama wakulima wa tumbaku kule tabora...wanachangia kiwango kikubwa kwenye kapu la taifa kwa kilimo cha tumbaku ila mwisho wa siku hata barabara za changarawe hawana na serikali yao imewabandika jina la masikini wa kutupa...

Inasikitisha.
 
Hujaeleza bayana ni kwa namna gani Kagera unaweza kyfanywa kama kituo cha biashara Afrika ya Mashariki.
Utakuwa wa kwanza kupata majibu ya hoja ama mswali yako kutoka kwa mleta mada!!! Maani siku hizi hana utamaduni huo.
 
Mimi sielewi anaposema elimu ni duni katika huu mkoa halafu hapo hapo mkoa unaongoza kwa kutoa wasomi....sasa hao wasomi wanasomea mitini au vip....


Mkoa wa kagera unaonekana maskini kwa sababu population ni kubwa kuliko pato la mkoa....sio kwamba eti hakuna huduma za msingi kama hospital, shule, makazi bora, barabara nk...
Mkoa uwe na bandari tatu kubwa, mipaka functional minne, airport nzr tu, wilaya zote ziwe na lami, umeme upo karibu kila kijiji na bado shule bora kabisa nchini zipo katika mkoa huu
Wilaya tu ya muleb ina watu karibu laki saba....
Ameweka gazeti lake na kutokomea kusikojulikana kimya kimya
 
Mkoa huu una mito mingi mikubwa ya asili na uoto mzuri sana na ardhi yenye rutuba nzuri hususani wilaya ya Kyerwa na Karagwe
Wizara ya kilimo ikitumia vizuri fursa hii hakika kagera inaweza kuongeza pato la taifa kupitia kilimo
nani kakuambia wizara inalima? Wenyeji hawajaona hiyo mito, kwanini wasiitumie. Mi nilichoona huko ni uvivu hakuna kitu kingine. Hayo maeneo wangepata watu km wa kaskazini wape miaka 5 tu uone mabadiliko. Hao watu ni wajuaji wa midomoni, ila ni wavivu wa kufanya kazi. Kagera ni mkoa unaopata mvua nyingi kwa mwaka na uko karibu kabisa na mstari wa ikweta uliopitia hapo Entebe-Uganda kuna ardhi nzuri sana.
 
Economic metrics zinaweza kusema hivyo lakini umaskini wa mikoa yetu hautofautiani ukitoa mikoa michache sana. Kutumia kipimo cha pato la mkoa over population ni yale yale ambayo hata mzee Mkapa aliyakataa.

Mfano mmasai mwenye ng'ombe 5000 kwa vipimo vya uchumi ni maskini! Hivyo zipo njia sahihi za asili kuainisha hali ya uchumi ya mtu mmoja mmoja.

Kuhusu Kagera kwavile ni mkoa ninaotokea, binafsi naona ni mkoa wa kimkakati ambao serikali haijawahi kuwa na lengo la ku tap hizo advantages ambazo mh Zitto amezitaja baadhi.

Mkoa umepakana na nchi nyingi kuliko mkoa wowote sio Tanzania tu bali Afrika mashariki, ni mkoa wenye mvua wakati wote na ardhi kubwa yenye rutuba nzuri.

Ule mkoa ungetumika kama hub ya elimu ya vyuo vya kati hadi university ingekuwa center kwa hata nchi za jirani. Lakini pia kibiashara kama miundombinu ya uwanja wa ndege na reli ikiwa sawa wafanyabiashara wa nchi jirani wangetumia Bukoba kama center badala ya Mwanza.

Kilimo cha kahawa ni kama kimekufa inabidi kipewe nguvu upya maana ndio ilikuwa kimbilio la wananchi wengi maskini.
 
Ni maskini kwa kuwa unachangia pato dogo la taifa kulinganisha na population yake....

Hayo mengine sijui huduma za kijamii nk kagera iko vzr tu...
Huoni anajichanganya kusema mkoa una huduma duni za elimu na wakati huo huo unatoa wasomi wengi...sasa hao wasomi walisomea migombani au vip.....kama sio ukichaa ni nini kuelewa hiv
Inabidi Mh.Zitto ajipambanue na utaalam wake wa uchumi bila kufanya hivvyo atapuuzwa tu.
 
Economic metrics zinaweza kusema hivyo lakini umaskini wa mikoa yetu hautofautiani ukitoa mikoa michache sana. Kutumia kipimo cha pato la mkoa over population ni yale yale ambayo hata mzee Mkapa aliyakataa.

Mfano mmasai mwenye ng'ombe 5000 kwa vipimo vya uchumi ni maskini! Hivyo zipo njia sahihi za asili kuainisha hali ya uchumi ya mtu mmoja mmoja.

Kuhusu Kagera kwavile ni mkoa ninaotokea, binafsi naona ni mkoa wa kimkakati ambao serikali haijawahi kuwa na lengo la ku tap hizo advantages ambazo mh Zitto amezitaja baadhi.

Mkoa umepakana na nchi nyingi kuliko mkoa wowote sio Tanzania tu bali Afrika mashariki, ni mkoa wenye mvua wakati wote na ardhi kubwa yenye rutuba nzuri.

Ule mkoa ungetumika kama hub ya elimu ya vyuo vya kati hadi university ingekuwa center kwa hata nchi za jirani. Lakini pia kibiashara kama miundombinu ya uwanja wa ndege na reli ikiwa sawa wafanyabiashara wa nchi jirani wangetumia Bukoba kama center badala ya Mwanza.

Kilimo cha kahawa ni kama kimekufa inabidi kipewe nguvu upya maana ndio ilikuwa kimbilio la wananchi wengi maskini.
Vyuo vimefunguliwa vitatu ili kuleta chachu ila alipokuja ndugu yenu akavifunga.
 
- 51% ya wakazi wake wanatumia chini ya TZS 1,644 kwa siku ( mstari wa umasikini Tanzania ni TZS 49,320 kwa Mwezi ).

- Pato la Wastani la Mtu wa Kagera ni TZS 1.2M kwa Mwaka. Mtu wa Ruvuma na Iringa ana Pato la Wastani mara 3 zaidi ya mtu wa Kagera.

- Mwaka 1994 Kagera ilishika nafasi ya 12 kati ya Mikoa 21 nchini kwa hali ya Uchumi, Mwaka 2022 inashika nafasi ya 26 kati ya Mikoa 26, yaani Ndio Mkoa masikini zaidi nchini.

Iweje Mkoa wa Kagera uwe masikini zaidi? Ni Mkoa wenye ardhi iliyopandwa kahawa kuliko Mkoa wowote nchini, ni Mkoa wenye utajiri mkubwa wa ardhi na hali ya hewa, ni Mkoa uliokaa kimkakati kijiografia ( unapakana na Nchi nyingi zaidi za Afrika Mashariki kuliko Mkoa mwengine wowote), una rasilimali madini kama Nickel na una wasomi wengi zaidi kuliko mikoa mingi ya Tanzania! Kwanini uwe Mkoa masikini zaidi?

Kuna sababu kadhaa, ikiwa ni pamoja na:

1. Uchumi wa mkoa huo unategemea sana kilimo ambacho kinategemea mvua. Hivyo, ukame au mvua zinazopungua zinaweza kusababisha upungufu wa chakula na mapato kwa wakazi wa mkoa huo. Hii pia inasababishwa na sera zilizopitwa na wakati kuhusu masoko ya mazao ya Kilimo na haswa kahawa kiasi cha wakazi wa Kagera kupeleka kahawa Uganda.

2. Miundombinu ya barabara na reli katika mkoa huo ni duni, hivyo kufanya usafirishaji wa mazao na bidhaa kuwa mgumu na gharama kuwa kubwa. Licha ya kuwa Mkoa huu uliathiriwa sana na vita vya Kagera hapakuwa na mpango Maalumu wa kuhuisha Uchumi wa Kagera baada ya vita na Ndio maana kumekuwa na mdororo wa Uchumi wa Mkoa huu.

3. Elimu na afya ni changamoto kubwa katika mkoa huo. Huduma za afya na elimu zinapatikana kwa kiwango kidogo, hivyo kusababisha wakazi wa mkoa huo kuwa na ugumu wa kupata huduma hizo.

4. Kagera ilipata athari kubwa ya tetemeko la ardhi mwaka 2016 ambapo nyumba nyingi na miundombinu iliharibiwa na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi na uchumi wa mkoa huo.

5. Sera mbovu za Serikali ya CCM ambazo hazizingatii muktadha wa kimaeneo katika shughuli za Uchumi. Kwa Mfano Mfumo wetu wa utawala wa Viongozi ‘kuletwa’ kutoka Juu unaondoa ubunifu na uwajibikaji hivyo mikoa kutotumia fursa zao kwa ukamilifu na kukosekana ushindani wa mikoa kimaendeleo.

Chama cha ACT Wazalendo kinadhamiria kurejesha heshima ya Mkoa wa Kagera kwa kuugeuza kuwa Kituo cha Biashara na Viwanda kwa Nchi za EAC. Vile vile kushawishi Mradi wa Kabanga Nickel kufungamanishwa na shughuli za Uchumi za Watu wa Kagera.
Jamaa usitafute political advantage kwa kutumia mkoa wa Kagera, mengi humo umeandika pumba ungeanza kutatua matatizo ya ndugu zako wanaoishi nyumba za nyasi. Eti Kagera haizalishi chakula, ni lini serikali imepeleka chakula cha msaada huko?? Bwege tafuta sifa kwingine sio Kagera.
 
Ni maskini kwa kuwa unachangia pato dogo la taifa kulinganisha na population yake....

Hayo mengine sijui huduma za kijamii nk kagera iko vzr tu...
Huoni anajichanganya kusema mkoa una huduma duni za elimu na wakati huo huo unatoa wasomi wengi...sasa hao wasomi walisomea migombani au vip.....kama sio ukichaa ni nini kuelewa hiv
Jamaa anatumia GDP per capita ya mwaka 2019/2020 ambayo hata population iliyotumika haikuwa halisi, kama Kagera ni maskini hivo mbona mapato ya halmashauri inafanya vizur kuliko mikoa mingi kwani hayo mapato yanatoka wapi?? Pato la taifa ni kwa sababu hakuna uwekezaji mkubwa kama viwanda vikubwa au madini
 
Back
Top Bottom