much know[emoji879]Sababu ni zile zile tu zinazofahamika.. na almost mikoa mingi ya Tanzania iko ivyo..na sababu zinafanana everywhere
- Inequality or social injustice
- Lack of education
- Poor basic infrastructure
- Selfishness
- Much know
- Poor Government support
****Hivi kuna mhaya mnaweza kukaa mezani mkapanga mipango siriaz ya maisha?Una watu Wana mdomo sana badala ya kufanya kazi.
Maendeleo binfsi huletwa na juhudi ya mtu mwenyewe na sio wanasiasa hasa wa bongoHuo Mkoa Wana diaspora wengi sana, lakini remmittance zote zinaishia Dsm,Mwanza na Arusha, wanaogopa kujenga kwao, ushirikina mwingi, ma nyaruju.
Nilitarajia Mkuu wa Mkoa aanze kampeni ya Kila familia kupanda parachichi, hakuna, michikichi, hakuna, labda aongee na SIDO wajenge mashine kubwa za kukamua chikichi, hakuna, yeye anatukanana na wanasiasa tu.
Natarajia tarehe ijayo SSH amuhoji kuhusu parachichi na chikichi
Komenti ya Hawa akiongea na nyoka EdenMtausema sana huu mkoa. Watanzania mna roho ya kwanini.
Mkoa unatoa wasomi sana lkn mliweuwekea passmark za juu sana. Wahaya walikimbilia mikoa mingine kutafuta elimu. Kuna wahaya Wana majina mpaka ya Kimasai. Wakati wagogo wakirudisha namba za mitihani wao wameshinda hata Kama hawakuandika chochote. Kagera ilikuwa na shule nyingi miaka ya sabini kuliko mikoa mingi lkn walijaa makabila mengine tena wenye passmark kdg. Kisa NYERERE HAKUWAPENDA NA ALISEMA HAKUNA MHAYA KUWA RAIS. Mambo mengi yaliyofanywa tangu nyuma ndiyo yanaonekana leo. Na mpaka sasa bado mnawachukia hawa wahaya. Kama mnakubali kuwa wameelimika na elimu.ni ufunguo wa maisha, kwanini hawa wahaya wasifunguliwe maisha?
Umemaliza kila kitu kwa mlengo chanya bila kuweka dhoruba tunazopitia bila ya kupewa msaada na serikaliBurundi hawana purchasing power kubwa pamoja na kwamba ni mamilioni ya watu. Kagera almost haina cha kuuza Burundi.
Rwanda haina cha kununua kinachozalishwa Kagera zaidi ya kutumika kama transit ya bidhaa.
Mwanza inachukua vitu vingi zaidi ya hizi nchi mbili.
Uganda na Kagera wanafanana kila kitu, Kagera inafanana Uganda kuliko mkoa wowote Tanzania. Ni sawa uitake Songea inunue mahindi ya Rukwa.
Serikali inapiga marufuku kuuzwa mazao nje ya nchi, kahawa inauzwa bei ndogo sana haimshawishi mkulima kuweka juhudi. Vanilla ndio hiyo bei inapanda na kushuka zaidi ya 50% kwa msimu. Bei ya vanilla Uganda huwa ni almost twice ya Kagera, bei ya kahawa Uganda miaka yote inakuwa juu ila jichanganye ukamatwe unaitorosha uone. Border tunayo-share na Uganda ni ndogo na sehemu nyingine hazina makazi hivyo ni rahisi kuilinda tofauti na border mfano na Kenya utailinda uimalize ile? Kwahiyo kufanya smuggling kule ni rahisi.
Kagera iko more than 1000km kutoka bandarini, ni gharama kubwa kusafirisha bidhaa na mazao mengi kutoka kule hayafiki sokoni au yakifika inabidi yafidie higher transport cost na hivyo hayapo competetive kwenye soko. Ukifunga ndizi kuzileta Dar zinaweza iva kabla hujafika.
Na mwisho ni priorities za central government. Sipendelei Federation kwa Afrika maana zinasumbua umoja ila Tanzania hii central government yetu kuna mikoa haina vipaumbele. Bora Kagera tutasingizia iko mbali, Lindi je? Mtwara wanavuna korosho hata serikali kuweka kiwanda kikubwa cha kubangua hawawezi mpaka korosho iende unprocessed kwenye magunia.
Afadhali wewe umeongea kwa hoja. Watu hawajui kwamba Biharamulo na Ngara pia ni sehemu ya Kagera. Pia wengi wao wanatumia kigezo cha stand na soko kuhalalisha umaskini wa Kagera. Wachache waliotembelea vijiji vya Muleba, Kyerwa, Karagwe na Misenyi.Wahaya wanapambana wapate stendi na soko, sawa, lakini hivi havitaondoa gepu ya uchumi wa kahawa, hasa Bukoba mjini.
Wilaya zinazofanya vizuri ni Kyerwa, Kuna kahawa na mifugo, Karagwe, Kuna mifugo na kahawa, Muleba, Kuna uvuvi na kawaha na ufugaji.
Bukoba mjini itaendelea kiwa masikini wa kutupwa.
Kwenye hili uko sahihi lakini wahaya wanaogopa kuhujumiwa na Serikali. Wengi wangependa kuwekeza lakini kahawa tu imehujumiwa mpaka watu wakafyeka mashambaZiwa Victoria upande wa Kagera wameshindwa kutumia vizuri fukwe zao kuweka hotel au beach nzuri za kuvutia wageni na watalii ingawa wana maeneo mazuri.
Uvuvi unafanyika kiwango cha kawaida, Bukoba inatakiwa wapambane wawe na kiwanda cha kuchakata samaki. Wavuvi wengine wanatoka sehemu za Mwanza wanasogea mpaka Bukoba kuvua samaki na dagaa.
Usafiri wa abiria kutoka Bukoba Port kwenda visiwani wanatumia boti ndogo za mbao na nyingine sio salama kulingana na idadi ya abiria. Kwenye meli za mizigo kati ya Uganda na Bukoba zilikuwa zinaleta sabuni na mafuta kutoka kiwanda cha mukwano. Matajiri na diaspora wakiwekeza mji utapanuka kibiashara, kuna wahindi walikuwa Port Bell Uganda na Boti za Earth Wise lengo lao ilikuwa ni kufanya trip za Uganda - Bukoba wakakwama.
Kuna kiwanda Cha samaki kemondo na pia Bukoba mjini.Ziwa Victoria upande wa Kagera wameshindwa kutumia vizuri fukwe zao kuweka hotel au beach nzuri za kuvutia wageni na watalii ingawa wana maeneo mazuri.
Uvuvi unafanyika kiwango cha kawaida, Bukoba inatakiwa wapambane wawe na kiwanda cha kuchakata samaki. Wavuvi wengine wanatoka sehemu za Mwanza wanasogea mpaka Bukoba kuvua samaki na dagaa.
Usafiri wa abiria kutoka Bukoba Port kwenda visiwani wanatumia boti ndogo za mbao na nyingine sio salama kulingana na idadi ya abiria. Kwenye meli za mizigo kati ya Uganda na Bukoba zilikuwa zinaleta sabuni na mafuta kutoka kiwanda cha mukwano. Matajiri na diaspora wakiwekeza mji utapanuka kibiashara, kuna wahindi walikuwa Port Bell Uganda na Boti za Earth Wise lengo lao ilikuwa ni kufanya trip za Uganda - Bukoba wakakwama.
Watanzania hamtaki watu wanaojiamini. Hilo linatukwaza sana. Ona report ya CAG. Wizi mwingi lkn hakuna mtu wa kujiamini hata kuhojiTabia za watu wa Kagera, wajuaji sana, wanajua hadi eti Kiingereza/kizungu kuliko british wenyewe..!! Wahaya ni shida, wabishi kuliko watu wa kigoma, but kiuhalisi kumbe hawajui mambo vizuri, sbb anaejua mambo vizuri hujikamua katika lindi la umaskini.
Dharau kubwa sana kwa wachaga kuwaweka kundi Moja na wahayaKatika watu wasomi na matajiri ni wahaya na wachanga tu.
Umewasahau wanyakyusa wale watu huwezi ingia ofisini usiwakute na ni wapoleKatika watu wasomi na matajiri ni wahaya na wachanga tu.
Bugabo kwao na akina Dio ππππHivi bado soko kuu Bukoba siku ya jumapili linafungwa mchana?π
Bukoba ikifika saa mbili kamji kanakuwa kimyaaa
Mpaka wa Mutukula ni waganda ndio wanaunogesha
Kagera Kuna ardhi nzuri sana, kwa mfano misenji ni π₯tatizo uvivu
Kuna biashara ukianzisha na usipokuwa wa kwao utapata tabu
Stendi ya Bukoba ni aibuu mvua ikinyesha
Mzunguko wa pesa ni mdogo sana Kagera, tuliwahi kuishi Karagwe kwa miezi minne, umaskini tuliokutana NAO ni mkubwa sana.
Q bar sijui bado ipo?
Halmashauri Haina root za hiace....
Wenyeji kuuza ardhi ni wagumu sana
Niliwahi kwenda Bugabo nusura niliwe