Mkopaji aishtaki Akiba Commercial Bank (ACB) kwa upotevu wa hati ya nyumba

Akilipwa hiyo pesa...nimekaa pale..
Alafu nilitaka kushangaa dada kamalizaje deni hilo kirahisi hivyo, kumbe alikopa sehem nyingine....
kiufupi, dada kafirisika
Kwa nini bongo mtu akifuatilia haki yake anaonekana wa ajabu? Yaani bongo ukondoo unaonekana ndo kawaida. Daaahhh.
 
mbuzi kafia kwa muuza bucha.
Kwa kweli.
Ila kusema ukweli taasisi nyingi za bongo haziheshimu kabisa wateja wake. Na ni kwa sababu wanajua kuwa wabongo sisi wengi wetu ni makondoo, hatuna cha kuwafanya. Ukisoma hiyi habari, baada ya kuwa wamepoteza hiyo hati badala ya kumuita bidada na kukaa nae kumueleza ukweli na kumwambia hatua wanazochukua, kumuomba msamaha na kumuomba ushirikiano, wao waliamua kumzungusha weeee, hadi mteja kuwaandikia barua mara mbili, wao hawana habari. Hadi walipotishiwa kushitakiwa ndo wakakurupuka kumuandikia barua na kumwambia kuwa wamepoteza hati yake. Its not fair kabisa kwa kweli. Acha wanyooshwe tuu.
 
Halafu mteja wa nyumba unamrudisha wewe?

Umesoma hoja zake? Unaelewa maana ya damage?
Kaka, Watazania wengi wetu ni makondoo, mtu akifuatilia haki yake mguu kwa mguu kama hivi ndo anaonekana wa ajabu. Ila hizi taasisi nyingi za bongo zinasumbua sana wateja wake, kwa sababu wanajua sisi ni makondoo.
 
Apewe hati yake akalale asigeuze hilo tatizo kuwa mtaji
Na mteja wa nyumba atapewa?
Na usumbufu aliosababishiwa na benki kwa sababu ya kutokua wazi tangu mwanzo na badala yake kumzungusha?
Kuonewa bongo ndo standard kumbe.
 
Kaka, Watazania wengi wetu ni makondoo, mtu akifuatilia haki yake mguu kwa mguu kama hivi ndo anaonekana wa ajabu. Ila hizi taasisi nyingi za bongo zinasumbua sana wateja wake, kwa sababu wanajua sisi ni makondoo.
Mwaka 2016 nililipia kifurushi Dstv kupitia tigo pesa ili nione match zote za world cup, guess what.. ile pesa ilikatwa kwenye akaunti lakini haikwenda Dstv.

Niligundua kuwa hazikwenda baada ya kuwasiliana na Dstv na wao kunitaka niwasiliane na tigo. Nilipiga simu sana tena sana tigo customer care, wanakili pesa kweli imekatwa na wanadai kulikua na hitilafu kwenye mifumo yao.

Kufupisha story ile pesa hadi navyoandika hapa sikuwahi kurudishiwa maana baadae ilibidi nilipe kwa mtandao mwingine huku nikiwasiliana nao, hadi kwenye maduka yao nilifika hakuna msaada zaidi ya itarudishwa baada ya saa 72. Naunga mkono hoja watoa huduma wengi wanapuuzia wateja na kuwadharau.

Ngoja hawa wanyooshwe mahakamani.

NB: audio ya mazungumzo kati yangu na wao ninayo.
 
Sisi ni makondoo mkuu, ndio maana taasisi nyingi zinatupotezea tu, kwa sababu wanajua hatutachukua hatua yoyote. Hebu angalia uwezekano wa kuonana na wakili mzuri kama Kibatala au anaefanana na huyo, umuelezee ishu yako na kumpatia vielelezo ulivyonavyo uone kama ni kesi ambayo inaweza kupelekwa mahakamani, andaa tu hela ya consultation ya mara ya kwanza, malipo mengine mnaelewana na kuingia makubaliano yatakatwa kwenye malipo ya ushindi wa keshi asilimia kadhaa kama mtashinda kesi, na kama mtashindwa pia mnakubaliana utampoza vipi.
 
Wale Wenzangu Waliotaka Kuishtaki Crdb Njia Hiyo Iburuzeni Chap Chap
 

Kibatala? He he
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…