matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 7,968
- 19,368
- Thread starter
- #21
Kufunga muhimu mkuu.Muda wa faragha ya mtu na Mungu wake ni siri
Halafu kufunga si lazima.
Tafuta origin bible verse ya lile neno kwa kuomba na kufunga utaona lile neno kufunga limewekewa mabano .
Mabano maana yake ni neno lililoongezwa na mwandishi mwingine baadaye.
Suala la kuomba nakuunga mkono, bila maombi ni sawa na mtu mfu ila hayo maombi lazima yawe ya rohoni (kunena kwa lugha).
Shetani ametumia neno lile lililoongezwa na wahuni kuwaondolea ujasiri wana wa Mungu. Imefika wakati mwana wa Mungu kama hajafunga anashindwa hata kutoa pepo, akiaambiwa kesho tukamwombee mgonjwa au tukapige maombi ya vita mahali basi atakimbilia kufunga.View attachment 2784171
Katika battle kubwakubwa kwenye maandiko walifunga kuanzia watoto, wazazi hadi mifugo.
Ezra na msafara wake, walifunga kupata ulinzi wa kupita kwenye hatari kubwa.
Kando ya mto ahava.
Ester kupindua matokeo ya kufutwa kwa taifa la israel walifunga siku tatu bila kula
Yesu ili aanze mambo makubwa alifunga.
Paulo ili kanisa likue alifunga
Ninawi ili isiangamie walifunga.
Daniel ili watoke utumwani alifunga
Nehemia ili akafanye project ya kuijenga yerusalem alifunga
Yesu alisema kuna ishu ili utoboe ni lazima uchanganye maombi na mfungo