Tetesi: MKT wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Kuanza Ziara ya Ulaya na US Kupitia Dubai 28/08/2016? !.

Tetesi: MKT wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Kuanza Ziara ya Ulaya na US Kupitia Dubai 28/08/2016? !.

Anapiga mapushapu ya nini kama hajaribiwi, umewahi sikia wapi mtu mstarabua akapiga mipushapu mbele ya kadamunasi Lol!
Mkuu huo ustaarabu unaotaka wewe yeye hana na ameshatangaza kweupe kila mtu amemsikia kuwa yeye HAJARIBIWI sasa Mjaribu ili ukione kilicho mtoa Kanga Manyoya
 
Wanabodi,

Naomba kuanza uzi huu kwa ku declare my interest kuwa Mimi Pasco wa JF, naunga mkono maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima na siku ya siku, nitajitokeza kushiriki na nitatoa wito wale wote wenye mapenzi mema na taifa hili, tujitokeze kwa wingi! .

Niko kwenye kijiwe fulani hapa mjini kati, jijini Dar es Salaam, nikainasa ndogondogo kuwa wakati chama cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema, kiko kwenye maandalizi ya maandamano na mikutano nchi nzima kuhamasisha UKUTA, siku ya Tarehe 1 September 2016, habari ambazo hazijathibitishwa, zimeeleza kuwa, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mhe. Freeman Aikaeli Mbowe, yuko kwenye maandalizi ya mwisho mwisho kuanza ziara binafsi ya Ulaya na Marekani kupitia Dubai. Ziara hiyo umeelezwa kuwa pia itahusisha matibabu, uchunguzi wa afya na mapumziko mafupi mjini Dubai. Mtoaji wa taarifa hiyo isiyothibitishwa, imesema ziara hiyo ni binafsi, ya kifamilia na ya kibiashara.

Mtoa habari huyu alijitambulisha rasmi kama mkereketwa wa Chadema, na kutaja majina yake, lakini kufuatia habari hizi bado hazijathibitishwa rasmi na uongozi wa Chadema, naomba nisilitaje jina la mtoa habari wangu chini ya kinga ya kihabari iitwayo "the confidentiality of the source " mpaka habari hizi zitakapothibitishwa au kukanushwa.

Kufuatia source wa habari hii sio a trusted source ndio maana habari hii ina lebo ya tetesi, ikiishatibitishwa, neno tetesi litaondolewa! . Sii mara moja wala mbili kwa tetesi mbali mbali kushuka jf na baadae zikathibitishwa au kukanushwa! .

Hii sii mara ya kwanza kwa kiongozi Mkuu wa Chadema kuanzisha maandamano lakini siku ya siku haongozi harakati hizo na badala yake huwa safarini kikazi au kibinafsi hivyo kuwaachia wengine waliopo.

Lengo la kuileta habari hii humu jf hata kabla haijathibitishwa ili ile jf spirit ya "be the first to know! ".

Ikitokea ikathibitika habari hii sii ya kweli bali ni uzushi tuu, nitamuomba mode, asiufute uzi huu bali aufunge tuu kusubiria hiyo tarehe 1 September tuthibitishe this time around, Mwenyekiti atakuwepo kuongoza maandamano.

Lengo la kuomba uzi usifutwe bali ufungwe tuu, ni kufuatia posibility ya Chadema kuikanusha taarifa hii kuwa sii kweli lakini siku ya siku ikaelezwa Mwenyekiti amepata safari ya dharura.

Pasco.
Inawezekana Pasco siku hizi ushageuka kuwa muongo ila kwakuwa ni tetesi sitakuhukumu; labda niseme hili moja tu kwamba atakayetoka barabarani siku hiyo ni kwa hasara yake na familia yake. Upinzani wetu huu wa uchumia tumbo sio wa kuupa uhai wako au kiungo cha mwili wako; yet siasa ni mchezo mchafu ukiamua kuucheza lazima ujue utachafuka na kwa maana hiyo sijui kelele ni za nini kama uongozi unawamwagia tope, si hata wao wangekuwa madarakani wangeleta michezo michafu kuliko hata hiyo wanayoilalamikia? Hebu tuwape kijimda walioko madarakani wafanye klle walichoahidi wakishindwa si kila mtu atajua tu wameshindwa? na hapo si watageukia upinzani kwa point bila mashinikizo? wakati wote muda/wakati ni mwalimu mzuri
 
Tuambie basi hicho kibali cha kusafiri nchi za nje Mbowe alikiomba lini kwa Mungu wa Ikulu na lini kibali hicho kilitolewa!?
Kamanda hao waliotoa kibali ndio waliopenyeza habari hizo,na ndio maana serikali inajiamini kwa tambo zoote inajua wapi pa kuanzia
 
@WanaJamvi,

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe.Freeman Mbowe hana mpango wowote wa kufanya safari nje ya nchi siku za hivi karibuni

Katika Hotuba yake ya Leo kwa vyombo vya habari hapa Arusha ameeleza kuwa atakua mstari wa mbele kwenye mapambano kama ilivyo siku zote.
 
Kwa nini mtapigwa safari hii tena badly?

1. Mahakama kuu imetupilia mbali kesi yenu ya kudai haki ya kuandamana. Hivyo zuio la IJP ni sahihi hadi sasa.

2. Mahakama imewashauri kisheria kuwa, rufaa ikatwe na kuelekezwa kwa bosi wa IJP Mangu ambaye ni Lameck Mchemba Mwigulu ambaye ameishindilia juzi akiwa mtwara kuwa zuio hilo bado ni valid.

Sasa, mna grounds zipi za kulianzisha 1st Sep, 2016?

Mtapigwa tu, maana hakuna namna.
 
Interesting......
1471714400587.jpg
1471714406877.jpg

Nitaandamana tuu no matter what!
 
@WanaJamvi,

Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe.Freeman Mbowe hana mpango wowote wa kufanya safari nje ya nchi siku za hivi karibuni

Katika Hotuba yake ya Leo kwa vyombo vya habari hapa Arusha ameeleza kuwa atakua mstari wa mbele kwenye mapambano kama ilivyo siku zote.
Hivi una kichaa?Huu ndio uthibitisho kuwa hatosafiri?
 
Back
Top Bottom