Mkulima wa nyanya usitupe nyanya zako zilizo kosa soko fanya hivi kuziongezea thamani

Mkulima wa nyanya usitupe nyanya zako zilizo kosa soko fanya hivi kuziongezea thamani

Huwezi kupata soko la unga wa tomato,bora tomato paste
Mtoa mada ana idea za vitabuni. Hamna mtu atanunua unga wakati fresh tomatoes zipo na kwa bei affordable

Hata hao jamaa nilioeleza hapo kwenye post yangu iliyotangulia walifeli sababu demand ya hiyo powder ni almost nothing

Labda kama unahifadhi kwa matumizi yako tu
 
Viwanda na masoko vipo mkuu shida inakuja wakati wa mavuno uzalishaji unakuwa mkubwa kuliko mahitaji sasa shida inarudi kwa wakulima wanauza kwa kiwango kidogo kilicho baki wanakuwa Hawana pa kupeleka ,hivyo badala ya kudump bidhaa zilizo kosa soko basi ni Bora mkulima afenye hivi hili kuepuka hasara ndio hoja yangu mkuu
Nimekuelewa vizuri Mkuu
 
Mtoa mada ana idea za vitabuni. Hamna mtu atanunua unga wakati fresh tomatoes zipo na kwa bei affordable

Hata hao jamaa nilioeleza hapo kwenye post yangu iliyotangulia walifeli sababu demand ya hiyo powder ni almost nothing

Labda kama unahifadhi kwa matumizi yako tu
Shida ni market promo hakuna,soko always lipo.
Soko haliwezi ishinda idea.
Mimi nataka nianze kuzalisha viazi vya kupikwa then vinakaushwa kwa dar ni ngeni lakini shinyanga,Mwanza tabora ni kitu Cha kawaida
 
Hili ni wazo zuri,swali ni kuwa je ukiuza hiyo Tomatoe powder itanunulika...?
Ni bidhaa mpya kwa wengi, unaweza ukalazimisha soko anza na kwa mama lishe,mahotelini,nk.
Mbona Bakhresa anauza Nazi ya paketi
 
Biashara ni pamoja na kuangalia wenzio wameshindwa wapi ,hao walifeli pengine labda kwenye masoko nadhan ukiwekwa mkakati mzuri unaweza kuvuka mbele zaidi ya waliko inshia wao.
Mtanzania anaangalia Bei nafuu na Sio ubora thus mchina kaijua Siri hii anavuna utajiri Africa
 
Wakulima wengi wa nyanya wanapata hasara kutokana na kuzalisha nyanya ambazo zimezidi mahitaji ya soko au Sababu nyingine ni uhaba wa masoko ,Kiasi kikubwa cha nyanya zinaoza shambani au sokoni ni kwa sababu wakulima wengi hawana/hawajui jinsi ya kuhifadhi nyanya zao

Kwa utafiti wangu usio rasmi nimebaini Wakulima wengi wanapoteza zaidi ya nusu ya nyanya zinazozalishwa.

Hasara kubwa wanaipata Kipindi Cha msimu wa mavuno , nyanya nyingi zinaharibika kwa kusubiri wanunuzi na zingine zinaharibika tu kutokana asili ya zao lenyewe lilivyo(laini) hivyo inawalazimu wakulima wengi kuuza kwa bei ya hasara wengine wanazitupa kabisa kwa kukosa wateja.

Sasa Njia nzuri ya kuzihifadhi na kuongeza thamani nyanya zako zilizoharibika (sio kuoza) na ambazo zimekosa soko ni kuzifanya kuwa unga (tomato powder).

Njia hii ni nyepesi Wala haiitaji gharama kubwa , unachotakiwa kufanya unazikatakata nyanya zako kisha unazianiaka juani, baada ya kukauka utazisaga kwa blenda au kwa kutumia kifaa chochote ilimradi iwe unga

kutengeneza tomatoe powder inasaidia kupunguza upotevu wa nyanya baada ya mavuno lakini pia inasaidia kendelea kutumia nyanya nyakati za uhaba wa nyanya,

hivyo ni wazo Bora pia ukiamua kufanya kibiashara , na uzuri ni kwamba tomato powder ikihifadhiwa vizuri inakaa kwa muda mrefu zaidi ya miezi sita kwahiyo kazi kwako mkulima ulifanye kuwa wazo kamili au ulitume pindi nyanya zikishindwa kutoka sokoni.
View attachment 2734709
screenshot_20230831-183313-png.2734710
kula tano mjomba!!!
 
Mtanzania anaangalia quantity na low price hizo factors zingine ni za masaki huko.
Na market kubwa yenye pesa ipo uswahilini.
 
Ni idea nzuri sana hii.
Matunda yote yanakaushwa hata ikiwemo embe muhimu usafi tu na vikinga nzi tu wakati unaanika.
Tumia solar dry yaani vichanja vyenye ngazi kisha Hilo banda lifunike na wavu wa mbu kuzuia nzi kwa maeneo yasiyo na vumbi.
Zipo mashine za kukaushia matunda kwa sehemu za baridi.
 
Kama ndimu,chungwa,papai,embe nanasi yanakaushwa na unauza powder yake sembuse nyanya.
Ukichukua unga wa embe,papai,nanasi,chungwa nk ukitaka kutumia unauloweka kwenye maji unapata ladha halisi ya tunda husika
 
Shida ni market promo hakuna,soko always lipo.
Soko haliwezi ishinda idea.
Mimi nataka nianze kuzalisha viazi vya kupikwa then vinakaushwa kwa dar ni ngeni lakini shinyanga,Mwanza tabora ni kitu Cha kawaida
Swali ni kua bei yako baada ya kufanya hiyo process yote je inaweza kua chini ya bei ya fresh tomatoes [emoji534]
 
Mtoa mada ana idea za vitabuni. Hamna mtu atanunua unga wakati fresh tomatoes zipo na kwa bei affordable

Hata hao jamaa nilioeleza hapo kwenye post yangu iliyotangulia walifeli sababu demand ya hiyo powder ni almost nothing

Labda kama unahifadhi kwa matumizi yako tu
Biashara asili yake ni idea za vitabuni (mawazo ya watu) huwezi kusema hakuna mtu atakaye nunua tomato powder kwasababu tomatoes fresh zipo na hujawai ku practice Wala kufanya research zaidi kuwaona watu fulani wanefeli tena bila kujua Sababu nini.

Tomato inategeneza products nyingi na zote zina soko lake kwa namna yake kama ingalikuwa kama usemavyo basi hizo bidhaa zisingefanya vizuri sokoni kwasababu tomato fresh zipo kwa wingi.
 
Swali ni kua bei yako baada ya kufanya hiyo process yote je inaweza kua chini ya bei ya fresh tomatoes [emoji534]
Siku zote gharama ya bidhaa inapangwa kulingana na upatikanaji wake, operation cost yake na packaging.

Upatikanaji wa nyanya hasa kwa msimu wa mavuno ni mwepesi na kwa bei rahis, pia package na utengenezaji wake rahis.so sidhani kama bei inaweza kuwa juu sana

Ila kumbuka mkuu hii ni value addition of tomato sasa kitu kikishaongezewa thamani hakiwezi kuwa sawa kama kilivyo awali, hata hizi tomato paste &chill bei zake zipo juu kulinganisha fresh.
 
Kama ndimu,chungwa,papai,embe nanasi yanakaushwa na unauza powder yake sembuse nyanya.
Ukichukua unga wa embe,papai,nanasi,chungwa nk ukitaka kutumia unauloweka kwenye maji unapata ladha halisi ya tunda husika
Kila kitu kilianza kigeni promotion ndio inayotambulisha bidhaa ,yani mtu kwasababu hajawai kutumia au kuona bidhaa fulani basi anaamini hakiwezekani huku kukutatisha watu tamaa
 
Back
Top Bottom