KERO Mkurugenzi Manispaa ya Moshi awalazimisha watumishi kufyeka na kusafisha makaburi ya Karanga siku za mapumziko

KERO Mkurugenzi Manispaa ya Moshi awalazimisha watumishi kufyeka na kusafisha makaburi ya Karanga siku za mapumziko

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kichwa hapo juu cha husika, huyu Mkurugenzi tangu Jumamosi iliyopita aliwaamuru watumishi hasa walimu kuchukua mafyekeo na majembe kwa amri na vitisho kwenda kusafisha makaburi siku ambayo si ya kazi.

Leo tena Ijumaa ametoa vitisho kupitia kwa Walimu Wakuu kuwa asijekwenda kusafisha makaburi kesho tarehe moja asubuhi na mapema akiwa na jembe au fyekeo asimlaumu mtu kwa kitakacho mkuta. Sasa sisi kama watumishi tunahoji je hii ni haki? Manyanyaso haya yataisha lini kwetu?

Je, tusipoenda na ukizingatia ni siku ambayo si ya kazi hatua zitakazochukuliwa dhidi yetu si ni maonezi?

Kodi zao zinafanya kazi gani?
 
Hiyo yote Kwa sababu Walimu hamna vitega uchumi vya kuingizia kipato mbali na mshahara ila mkiwanavyo hata ukiambiwa Leo kazi basi unaendelea na maisha Yako mtu pekee wa kumuogopa ni mungu mgawa riziki msiende kama kwel mnajielewa
 
Tumesafisha jumamosi iliyopita akasema tumefika wachache anataka turudie jumamosi ya kesho pia mkuu. Je? Hata kama ni jumamosi ya usafi ni utaratibu watumishi kwenda kusafisha makaburi bila kujali nauli tunapata wapi? Yaani ni amri saa 12 ufike bila kujali umbali unaotokea hii ni haki kweli?
Nyie ndiyo mnawaendekeza watu wa aina hiyo. Tatizo nako hamjuwi haki zenu na utaratibu za kazi. Kusafisha makaburi wapi na wapi na kazi yako. Mgomeeni asiwapelekeshe kama ni mwanamke wapeleke mke wake na watoto wake wakasafishe na kama ni mwanamke ampeleke muwe na watoto wake wakafanye hiyo kazi.
 
Tumesafisha jumamosi iliyopita akasema tumefika wachache anataka turudie jumamosi ya kesho pia mkuu. Je? Hata kama ni jumamosi ya usafi ni utaratibu watumishi kwenda kusafisha makaburi bila kujali nauli tunapata wapi? Yaani ni amri saa 12 ufike bila kujali umbali unaotokea hii ni haki kweli?
Na yeye huwa anashiriki au ni nyie walimu tu?
 
Kichwa hapo juu cha husika, huyu Mkurugenzi tangu Jumamosi iliyopita aliwaamuru watumishi hasa walimu kuchukua mafyekeo na majembe kwa amri na vitisho kwenda kusafisha makaburi siku ambayo si ya kazi.

Leo tena Ijumaa ametoa vitisho kupitia kwa Walimu Wakuu kuwa asijekwenda kusafisha makaburi kesho tarehe moja asubuhi na mapema akiwa na jembe au fyekeo asimlaumu mtu kwa kitakacho mkuta. Sasa sisi kama watumishi tunahoji je hii ni haki? Manyanyaso haya yataisha lini kwetu?

Je, tusipoenda na ukizingatia ni siku ambayo si ya kazi hatua zitakazochukuliwa dhidi yetu si ni maonezi?

Watumishi wote.....sio waalimu Peke yao. Soma vizuri tangazo acha mihemko
 
Watanzania tunanyanyaswa sana hapo angerafuta hela yeyote atafute watu wakafanye huo usafi yeye kaamua kuvamia Walimu mbona watumishi wapo wengi si angevamia kada nyingine aone majibu yake...
 
daah amakweli tamisemi kuna miungu watu. unamwamrisha mbaba au mmama wa watu akakwae makaburi ya watu hata hawajui tena wikendi? na si ajabu yeye hajawahi hata kukwaa kaburi la mzazi wake.
 
Nyie ndiyo mnawaendekeza watu wa aina hiyo. Tatizo nako hamjuwi haki zenu na utaratibu za kazi. Kusafisha makaburi wapi na wapi na kazi yako. Mgomeeni asiwapelekeshe kama ni mwanamke wapeleke mke wake na watoto wake wakasafishe na kama ni mwanamke ampeleke muwe na watoto wake wakafanye hiyo kazi.
Kwa mtumishi kugomea elekezo la anayepitisha barua zako ni changamoto kubwa sana.Huyo ni afisa nidhamu wako hivyo ataamuru usumbuliwe,usimamishwe,uundiwe kamati nk,mpaka uje kuonekana ulionewa umeshateseka sana na familia yako.Na ngazi za juu zina mambo mengi mpaka zije kutetea jambo lako miaka imeenda,umepigika na kudhalilika ipasavyo;na kwa ufinyu wa muda wanaweza kukutoa mhanga ili maisha yawe rahisi.Hivyo inabidi akili itulie na zaidi ujishushe na kupotezea ili mambo yaende.
 
Kichwa hapo juu cha husika, huyu Mkurugenzi tangu Jumamosi iliyopita aliwaamuru watumishi hasa walimu kuchukua mafyekeo na majembe kwa amri na vitisho kwenda kusafisha makaburi siku ambayo si ya kazi.

Leo tena Ijumaa ametoa vitisho kupitia kwa Walimu Wakuu kuwa asijekwenda kusafisha makaburi kesho tarehe moja asubuhi na mapema akiwa na jembe au fyekeo asimlaumu mtu kwa kitakacho mkuta. Sasa sisi kama watumishi tunahoji je hii ni haki? Manyanyaso haya yataisha lini kwetu?

Je, tusipoenda na ukizingatia ni siku ambayo si ya kazi hatua zitakazochukuliwa dhidi yetu si ni maonezi?

Hivi Mkurugenzi mzima anashindwa kuomba Magereza wafungwa wafanye huo usafi?

Na kuna wenye vifungo vya nje hizo ndio kazi wanapaswa kuzifanya.

Majitu ya ccm bure kabisa.
 
Kiongozi hana mamlaka yoyote ya kumtuma mwananchi au mtumishi wa umma kazi zilizo nje ya wajibu wake professionally let alone legitimately. Inavyoonekana huko mliko ni kijijini na huyo kiongozi ni mshamba na uncivilized savage anayedhani uongozi wa democracy unampa nguvu za kifalme za kuamua chochote. Na kwa bahati nzuri amekutana na washamba, waoga, wasiotambua haki wala wajibu wao.

Huyo mpuuzi asiyekuwa na akili angekutana na mimi angeacha huo upuuzi mara na asingenifanya chochote. Damn, ningeinjoy hilo kesi!

Embu acheni uoga nyie walimu na mjikusanye mu-question hako ka-modern day savage barbarian kuhusu credibility na legitimacy ya hilo agizo lake la kimbavu na relation yake na kazi, haki na wajibu wenu.

Akileta ubishi na nyie leteni ubishi, sababu technically hana chochote cha kuwafanya zaidi ya kuwatisha tu sababu anajua nyie ni waoga msiojitambua.
 
Kwa mtumishi kugomea elekezo la anayepitisha barua zako ni changamoto kubwa sana.Huyo ni afisa nidhamu wako hivyo ataamuru usumbuliwe,usimamishwe,uundiwe kamati nk,mpaka uje kuonekana ulionewa umeshateseka sana na familia yako.Na ngazi za juu zina mambo mengi mpaka zije kutetea jambo lako miaka imeenda,umepigika na kudhalilika ipasavyo;na kwa ufinyu wa muda wanaweza kukutoa mhanga ili maisha yawe rahisi.Hivyo inabidi akili itulie na zaidi ujishushe na kupotezea ili mambo yaende.
Hii ndio maana ya uoga.
 
Back
Top Bottom