Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Maharage Chande asema pamoja na kukamilika kwa mradi wa Bwawa la Nyerere, watanzania tutegemee migao zaidi!

Ndugu Mleta madam, kwanza isome vizuri hiyo Article ya nwananchi na sikiliza vizuri alichosema Chande.

Amesema utafiti umefanywa nankuandikwa kwenye majarida, ili kuwe na uchumi wa Viwanda lazima katika kila Jamii 1m wawe na umeme wa 1000MW kutosheleza watu na viwanda.

Sasa hivi tunazalisha 1600MW, Bwana likikamilika litazalisha 2100MW = Approx. MW 3700, haitoshi watu 60m na viwanda.

Tuwe makini sana kutafsiri maneno ya wenzetu .
 
Mbona wapiga Kura washafanya hivyo mara kadhaa.. Wanapiga chini ccm, halafu NEC inawatangaza ccm kuwa washindi.
Huwa hawategemei kura!
Absolutely true.

Ndiyo maana tunataka Katiba mpya, ambayo itaweka muundo mpya wa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi nchini.
 

Swali kwako wewe unayemuelewa Maharage, kwa nini tumeishi miaka 5 kabla ya Maharage na Makamba bila mgao wa umeme wala maji? Huo umeme tuliokuwa tunatumia ulikuwa unatoka wapi? Na kwa nini ghafla tu baada ya Raisi huyu kuletwa mgao wa maji na umeme ukaanza?
 

Tumecoka kusema Rais Samia anahujumiwa, sasa tunamtwika udhaifu yeye mwenyewe. Rais Samia anadanganywa na wanamdharau watendaji wake aliowataua kwa sababu wote kawateua inawezekana kawateua kwa mashinikizo. Yaani mi hata kumuombea sasa nimeshachoka kabisa. Yaani Rais aseme bwawa likikamilika mgao basi ila agent wa economic hitmen aseme mgao utaendelea kuwepo. Yaani inaudhi sana tena sana. Lengo lao ni kuhakikisha Tanzania haivutii wawekezaji kwa kutokuwa na uhakika wa umeme. Kwa sababu kama unajiandaa kuwa na umeme wa uhakika laizma ujigambe ili dunia ijue haitakuwa na tatizo la umeme watu waje wawekeze ila hawa wateule wa rais wao kila siku wanaona sifa kusema eti mgao mgao. Hivi kwa nini kipindi cha Dkt Magufuli umeme ulikuwa haukatiki?? Yaani ingekuwa china walipaswa kuuawa kwa rushwa ila iko siku

 
Sitaki kukiongezea kichwa changu stress zaidi kwa haya matamko na mafafanuzi
 
View attachment 2456456
Tumecoka kusema Rais Samia anahujumiwa, sasa tunamtwika udhaifu yeye mwenyewe. Rais Samia anadanganywa na wanamdharau watendaji wake aliowataua kwa sababu wote kawateua kwa vimemo
Ni Upuuzi kuteketeza 7Trilioni kwenye umeme wa maji halafu ni 2115MW tu.

Kama kweli wana nia nzuri wawekeze kwenye umeme wa nuclear.
 
Ni Upuuzi kuteketeza 7Trilioni kwenye umeme wa maji halafu ni 2115MW tu.

Kama kweli wana nia nzuri wawekeze kwenye umeme wa nuclear.
Tatizo la nchi yetu ni kukosa au kutokuwa na kamati ya maamuzi, tunategemea wanasiasa badala ya watalaamu. Halafu eti unamkuta professor anasifia maamuzi ya mtu ambaye uamuzi wake una shaka kabisa
 
Ni Upuuzi kuteketeza 7Trilioni kwenye umeme wa maji halafu ni 2115MW tu.

Kama kweli wana nia nzuri wawekeze kwenye umeme wa nuclear.

Umeme wa nuclear mpaka wapate ruhusa kwa bosi, uliza AK mpaka Zuma aliondolewa kisa alitaka umeme wa nuclear na mpaka leo bado AK wanahaha na kuhangaika isitoshe kama huu wa maji tu unatushinda kuutumia kwa 100% tutauweza wa nuclear?

Tanzania kuna mgao sababu ya uzembe na incompetence na siyo kukosekana kwa maji, hivyo hata hiyo gesi pia kwa incompetence hii hamna kitu!
 
Ni strategy tu. Tatizo la nchi yetu ni kukabidhi maamuzi ya kitalaamu kwa mtu mmoja anayeitwa Rais. Kipindi cha Mwl Nyerere ilikuwa sawa maana ndiye alikuwa msomi. Ila kwa sasa nchi imebadilika sana, rais anatakiwa awe kama Mkapa au Dkt Magufuli, yaani rais akubali kutumia watalaamu na yeye mwenyewe asome nyaraka na kusoma strategy za nchi au ahakikishe watalaamu wanamuweka wazi bila wogs
 
Umeme wa nuclear ndio wa uhakika ,sema initial cost ndio gharama na inachukua muda kuumaliza ila ukishaufunga ndio ntolee mkataba tosha miaka 100+
 
Kasema kwa uchumi wa viwanda kimahesabu kila watu 1m watahitaji megawatt 1000,so Tanzania 60m tutahitaji 60,000megawatts..Sasa huo uchumi wa viwanda tz uko wapi!?..yeye aliongelea makadirio,muwe mnasoma na kuelewa
 
Ha ha ha ha kwahiyo anamaanisha tokea hii Nchi izaliwe imefanikiwa kuzalisha umeme kwa asilimia 2.5% tu ya mahitaji halisi na bwawa likikamilika itakuwa asilimia 6.3% ya mahitaji.
Jamaa lazima kuna mahali kajichanganya.

Na hizo MW 60k sio za mchezo mchezo.
Nchi za wenzetu zilizoendelea 1 MW inahudumia fully makazi approximately 1000 kwa mwaka sasa sisi hizo MW 60k ni za nini.
 

Dunia inaongozwa na satanist, itoshe tu kusema hivyo, usifikiri kila mtu anapenda maendeleo ya watu wote, kuna watu wanapenda tunavyopata shida ndiyo furaha yao, matazizo mengi na umaskini uliopo ni wa kutengenezwa kwa makusudi kabisa, …
 
Kama vipi zalisha umeme uwauzie Tanesco au kuwa self-sufficient kwa kuwa na chanzo chako cha umeme.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…