Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Muda wa kuanza kutumia VPN sasa naona umefika sio kwa kufatiliana huku
 
View attachment 445705
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.
Tunahitaji busara daima tunapocomments issues
 
Uhuru mbona upo sana. watu tunaruhusiwa kujadili kadri tunavyotaka. kuna watu wanautumia vibaya uhuru huu. kutoa matusi kwa viongozi na hata sisi kwa sisi humu tunatukanana.

Mello, usiwafiche wanaotukana bhana, wapeleke washikishwe adabu, ili jukwaa hili liwe mahali salama pa kujadili mambo ya msingi.
 
View attachment 445705
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

Kama ni hivyo basi kazi ipo!
 
Social media hazina tofauti na print and electronic media. Moja kati ya maadili ya uandishi wa habari ni kuto reveal source of your story hasa story zile ambazo mtoa habari ambaye amekupa habari in confidence. Kwa mwandishi mwenye maadili ya uandishi wa habari yuko tayari kufungwa lakini si kureveal source wake. Ninaamini mahakama itapima hiyo habari ambayo mwandishi amekataa kureveal chanzo kama ni ya kweli, sio classified information wala haihatarishi usalama wa nchi. Tunahamu kubwa kujua ni habari gani ambazo polisi walikuwa wanazitaji kujua source ili tuweke mizania kati ya public interest, state interest na individual interest. Tunasubiri
 
Watu wanatafutwa humu makosa ya kimtandao miaka30 unafia hukohuko
 
Ikosekane, sio kila unalosemwa au kulisikia likufanye ushindwe kutimiza malengo , minadhani JF ifungiwe tu, Facebook , twitter na mitandao yoooote.

Mnatka, tukae kwenye social media tukiongea the same way?!!!! Kwamba tunaipongeza...... Tunampongeza.......... Zombie sie?!!! Yazimwe tu!!!
Kwani hata mkikosoa kuna faida gani? kuna mtu alikosolewa sana humu ila sasa ndiyo anasifiwa bila hata kujua yale aliyokuwa anakosolewa amesahisha vp?
 
Waziri juzi kasema tusiwalaumu polisi wanapotenda makosa....bali tawalaumu wakubwa zao wa naowatuma...akiwemo yeye kwa maana hiyo
 
Magufuli Hoyee...CCM Hoyee! ndo kuisoma namba kwenyewe huko. Hadi wote tubaki tukiimba utukufu kwa JPM!
Naona lawama zote zinaenda kwa Magufuli tu basi pia Kikwete apewe nae sifa zake, maana isemwa kuwa haya mambo hayakuwepo kipindi chake.
 
Back
Top Bottom