Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Kuna uzi humu ulisema wazi na ushahidi kuwa Makamu wa rais amejiuzulu.

Kuna uzi humu ulipost barua ya ikulu ikionyesha nembo ya ikulu na sahihi ya msemaji wa ikulu ikielezea kutenguliwa kwa mrisho gambo. Huo sio uchochezi ? Au uchochezi kwako ni mpaka watu washike bunduki
Mbona hata facebook yaliandikwa hayo au kwakua hawawez kulipata server la fb
 
kwani hizo taarifa si wanazipata tu hadi wakamsumbue huyo CEO wa Jf? wangetakiwa kujiunga na Jf kisha wakaanza kusoma thread tu ingewasaidia ,mbona mimi napata taarifa zote ,alafu kingine sidhani kama kukamatwa kwa mkuu Maxence kuna husiana na kuminya uhuru wa maoni na kutoa taarifa kama watu wanavyoanza kujishuku humu ndani
 
Mbona commenti chache maana wanaopinga Uhuru wa Habari jukwaa lao kubwa ni hili hili, njooni na hapa mseme huyu anajisikia sana kuliko kukaa kimya. Ni vyema watu wakapewa Uhuru wa Habari kulingana na katiba ya nchi inavyotaka na si vingine.
 
Tofautisha kukosoa na kuleta habari za uchochezi.
Ingekuwa ni kukosoa JF ingekuwa imeshafungiwa muda mrefu sana. Lakini kwa kuwa kuna haki ya mtu kujieleza au freedom of speech ndio maana ipo mpaka leo.

Wanaotafutwa hapa ni wale wachochezi ambao ndio wamemponza maxence mello watu ambao ni chadema na kosa kubwa ni kuitumia JF kama Propaganda tool yao kueneza uchochezi.

Kama utakumbuka vizuri taarifa za kujiuzulu
Makamu wa rais zililetwa humu na pia ni humu humu JF ilitolewa taarifa ikiw na nembo ya ikulu
Pamoja na Sahihi ya msemaji wa ikulu
Ikielezea juu ya kutenguliwa kwa mrisho Gambo.

Hakuna nchi yoyote itakayovumilia uchochezi kama huo na hao ndio haswa wanaotafutwa na serikali Kwasababu aliyefoji amefanya kosa la jinai na anatakiwa afikishwe kwenye vyombo vya sheria na hao waovu ndio mello
Anawalinda.
acha uongo taarifa za makamu wa raisi kujiuzulu hazikuanzia humu zilikuwepo instagram kabla ya jf tena zilipostiwa na mange kimambi
 
Je,wanaweza kukufahamu vipi ili hali tunatumia ID fake? Naomba kujuzwa
 
JF ina rensponsibility kubwa sana, kama vivlivyo vyombo vingine vya Habari, kuna mambo mengi ya uongo na uzushi huletwa humu na kuachwa, ikumbukwe kwamba nchi nyingi kama Kenya, Rwanda, Burundi n.k Vita ililetwa na Vyombo vya Habari kama redio na TV, hivyo JF ina jukumu la kulinda amani ya nchi, kama ni kweli amekamatwa, na kama siyo kweli basi wajifunze na wabadilike, watambue jukumu lao kwenye Jamii!

CEO wa JF asipumbazwe na watu wanaosapoti kwenda kinyume na Serikali hapa, wengi wao wana maisha yao na wala hawaishi TZ, na JF ikifa kesho, au ofisi ya JF kunyimwa kibali cha kufanya kazi TZ hawana cha kupoteza, zaidi ya kuhamia kwenye mtandao mwingine na kuendeleza wanayoyafanya, hivyo angalia maisha yako na familia yako, fanya lililo sahihi na jinsi Serikali inavyokutaka kwani mwisho wa siku Serikali ndiyo yenye nchi, watakushauri wanachama wa JF wanavyotaka lkn Serikali ndiyo wasimamizi wa hii nchi!
Ndugu yangu hivyo ni vitisho. Hakuna vita iliyoletwa na vyombo vya habari, Rwanda chanzo cha vita ni Kutungua na kumuua Rais wa wakati huo Habyarimana; Kenya chanzo cha mapigano ni wizi wa kura na siyo vyombo vya habari kama unavyotaka kuaminisha umma. Angalia Burundi..... kwa nini Nkurunzinza kang'ang'ania madaraka?? Si ndo mwanzo wa kuleta vita na vurugu??? hapo utalaumu vyombo vya habari??? Popote penye haki huwezi kuona vita.
 
Weep not,child
Weep not,my darling
With these kisses let me remove your tears,
The ravening clouds shall no long be victorious,
They shall not long posses the sky,they devour the stars only on apparition.
By Walt Whitman.
Ngugi wa Thiongo alinukuu ubeti mmoja nakukipa jina kitabu chake cha
*WEEP NOT CHILD*
Ujumbe kuntu.
 
It is ok kwamba kwasasa jf inatikisa sii tz tuu bali dunia nzima, watawala matumbo joto! Kumbuka dogo hana kosa bali anatetea uhuru wangu na wako! Je sisi tunaotetewa tukae mimya? Nooo.
 
Siku hizi taarifa za wateja mtu analazimisha kuzipata, inanikumbusha kesi Kampuni Apple na Polisi wa Marekani.
 
JF ina rensponsibility kubwa sana, kama vivlivyo vyombo vingine vya Habari, kuna mambo mengi ya uongo na uzushi huletwa humu na kuachwa, ikumbukwe kwamba nchi nyingi kama Kenya, Rwanda, Burundi n.k Vita ililetwa na Vyombo vya Habari kama redio na TV, hivyo JF ina jukumu la kulinda amani ya nchi, kama ni kweli amekamatwa, na kama siyo kweli basi wajifunze na wabadilike, watambue jukumu lao kwenye Jamii!

CEO wa JF asipumbazwe na watu wanaosapoti kwenda kinyume na Serikali hapa, wengi wao wana maisha yao na wala hawaishi TZ, na JF ikifa kesho, au ofisi ya JF kunyimwa kibali cha kufanya kazi TZ hawana cha kupoteza, zaidi ya kuhamia kwenye mtandao mwingine na kuendeleza wanayoyafanya, hivyo angalia maisha yako na familia yako, fanya lililo sahihi na jinsi Serikali inavyokutaka kwani mwisho wa siku Serikali ndiyo yenye nchi, watakushauri wanachama wa JF wanavyotaka lkn Serikali ndiyo wasimamizi wa hii nchi!

ccm siku zote
 
Humu sio pakujiachia siku hizi zama zimebadilika..! pole Max kwa magumu unayopitia..
 
Kwa hyo tubakie jukwaa la mapenzi tu siasa na habari, hoja mchanganyiko bye bye babangu alisema watz hawapendi kuambiwa ukweli
 
Nje ya tz tunachekwa sana! Unajua wanasemaje? Ni kazi kwelikweli kumtetea mtz. Kwani hajui hata wanaomtetea na wanaomtafuna!
 
Back
Top Bottom