Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo anashikiliwa na Polisi, anyimwa dhamana

Asilimia 95 ya watumiaji wa JF wana ID fake. Serikali imeshatangaza kuwa kumiliki ID fake kwenye mitandao ya kijamii ni kosa la jinai. Sasa nyie wenye ID fake kiama kinakuja jiandaeni.

Mimi nipo clean.
Nitakuwa wa kwanza kuamini kuwa wewe ni mwongo
 
JF imetumika kumpigia kampeni Magufuli na kwa hakika ina mchango mkubwa kwenye kwenye sera ya CCM ya "kupinga ufisadi". Nadhani waliomkamata hawata sahau mchango mkubwa wa Max katika kukuza demokrasia na uhuru wa habari ambao bila kuwapo hata Lowassa asingejiuzulu Uwaziri Mkuu.

Free Max.
 
I'D zetu zinawahusu nini serikali badala ya kupambana kuwaletea wananchi maendeleo wanapambana kumnyima uhuru wa watumiaji wa mitandao kutoa maoni yao huu upuuzi kiwango cha lami.
 
Kumbe tanganyika inahitajika kupiganiwa uhuru wake mpya, kwa maana wananchi hawako huru kabisa. ..
 
JF ina rensponsibility kubwa sana, kama vivlivyo vyombo vingine vya Habari, kuna mambo mengi ya uongo na uzushi huletwa humu na kuachwa, ikumbukwe kwamba nchi nyingi kama Kenya, Rwanda, Burundi n.k Vita ililetwa na Vyombo vya Habari kama redio na TV, hivyo JF ina jukumu la kulinda amani ya nchi, kama ni kweli amekamatwa, na kama siyo kweli basi wajifunze na wabadilike, watambue jukumu lao kwenye Jamii!

CEO wa JF asipumbazwe na watu wanaosapoti kwenda kinyume na Serikali hapa, wengi wao wana maisha yao na wala hawaishi TZ, na JF ikifa kesho, au ofisi ya JF kunyimwa kibali cha kufanya kazi TZ hawana cha kupoteza, zaidi ya kuhamia kwenye mtandao mwingine na kuendeleza wanayoyafanya, hivyo angalia maisha yako na familia yako, fanya lililo sahihi na jinsi Serikali inavyokutaka kwani mwisho wa siku Serikali ndiyo yenye nchi, watakushauri wanachama wa JF wanavyotaka lkn Serikali ndiyo wasimamizi wa hii nchi!
MAWAZO YA KIPAYUMBU KABISA HAYA...KINYAA HADI KUSOMA...SIJUI KWANN UNAISHI DUNIANI MPAKA SASA
 
Lawama yooote iwaendee waliotuletea hii serikali. Wana CCM kwa haya yanayotokea Mungu anawaona.

Hongera kwa Mimi Mwanakijiji, Dr. Slaa, Lipumba, nk kwa kampeni zenu ili CCM ishinde ituletee haya yanayoendelea kwa sasa.

[HASHTAG]#BringBackBenSaananeAlive[/HASHTAG]
 
View attachment 445795
Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa ndani, Central Police.

Polisi wanaeleza muda huu kwamba leo atalala ndani hadi kesho atakapofikishwa mahakamani.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

=====================

MKURUGENZI Mtendaji wa Jamii Media na mwanzilishi wa mtandao maarufu wa JamiiForums, anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo kuu cha polisi, Dar es Salaam, kwa madai ya kugomea agizo la muda mrefu la jeshi hilo.

Polisi wamekuwa wakiagiza na kuamuru kupewa taarifa za watumiaji wa JamiiForums bila mafanikio.

Maxence alipigiwa simu leo akiwa ofisini kwake asubuhi akitakiwa kufika kituoni hapo na alitekeleza mwito huo.

Baada ya kufika polisi kati, akiwa ameongozana na mhariri na mwanaharakati wa uhuru wa mawasiliano, Simon Mkina na mwanasheria, Nakazael Tenga, Maxence alinyimwa dhamana ya polisi.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa Maxence atafikishwa makahamani kesho asubuhi kujibu mashitaka ya kuzuia upelelezi wa polisi dhidi ya makosa ya mtandao.

JamiiForums imekuwa na msimamo wa kutotoa habari za wachangiaji wake kwa yeyote, kwani kufanya hivyo ni kuingialia uhuru na faragha ya wateja wake.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006, msingi mkuu wa mtandao wa JamiiForums umekuwa kulinda faragha ya watumiaji wake.

Watumiaji wa mtandao wa JamiiForums wako huru kuweka mijadala, kuanzisha mijadala, kuchangia chochote pasipo kuvunja sheria za nchi au kuhatarisha usalama wa taifa.

Kampuni ya Jamii Media, inayoendesha mitandao ya JamiiForums.com na FikraPevu.com imejijengea heshima na umaarufu kwa muda mrefu kutokana na namna inavyoendesha na kusimamia shughuli zake ambazo kwa kiwango kikubwa ni za kimtandao.

Mtandao wa JamiiForums ni mtandao mkubwa wa Kiswahili kwa Afrika Mashariki na duniani ukiwa na wasomaji wasiopungua Milioni 2.5 kwa mwezi ambapo kwa mwaka 2016, mtandao huu unatimiza rasmi miaka 10 tangu uanzishwe.

Mtandao huu unasifika kwa kutoa fursa ya kipekee kwa watumiaji wake kutoa yaliyo mioyoni mwao huku wengine wakijifunza mbinu kadha wa kadha za kijasiriamali, afya, elimu na hata kuibuka wanasiasa wapya waliofundwa na wanajumuia ya JamiiForums.

Pamoja na kuendelea kutoa huduma hata katika nyakati ngumu, mtandao wa JamiiForums unakumbana mara kwa mara na changamoto nyingi zinazosababisha waanzilishi na waendeshaji wake kuwa katika misukosuko mara kwa mara, hasa na polisi.

Kwa muda mrefu tangu kuanzishwa kwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Jeshi la Polisi limekuwa likiushinikiza mtandao wa JamiiForums (kwa njia ya barua rasmi) kutoa taarifa za baadhi ya wateja wake.

JamiiForums katika kuhakikisha inasimamia usiri wa wateja wake, imekuwa ikihoji shinikizo kutoka Polisi yanazingatia sheria gani na kutaka kujua ni vifungu gani vya sheria ambavyo wadau wa mtandao huo wamevivunja bila kupewa maelezo yanayoridhisha zaidi ya kuelezwa kuwa hatua zaidi zitachukuliwa kama ushirikiano hautatolewa kwa Jeshi la Polisi.

Tayari Jamii Media imefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania (Kesi namba 9 ya mwaka 2016); kutaka Sheria ya Makosa ya Mtandao, kifungu cha 32 na 38 viangaliwe upya kwa kuwa vinapelekea kuvunjwa kwa haki za msingi za watanzania watumiao mitandao ili kulinda maslahi ya umma kwa kuzingatia vifungu 26(2) na 30(3) vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.




Baada ya kufungua kesi hiyo Serikali, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliweka mapingamizi sita ikitaka kesi nzima ifutwe na Jamii Media walipe gharama zilizoingiwa.

Lakini mnamo tarehe 4, Agosti 2016 Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya kuzipitia hoja zilizowasilishwa na Serikali na Wanasheria wa Jamii Media iliamua kuwa mapingamizi yote sita ya Serikali hayana mashiko na hivyo kesi ya msingi itaendelea kusikilizwa.

Maxence Melo anakamatwa huku kukiwa na Kesi hiyo ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari.

Wasije wakamfungia sandarusi na kumtupa baharini
 
Pole Max hivi ana kosa gani na atawajuwa wangapi mtandao ambao una member's toka Dar nzima ni maajabu kweli hivi watawala wanajuwa maana ya kunya maisha watu
 
Maxence Melo awe huru then mengine yafate ...very simple ...
 
Asilimia 95 ya watumiaji wa JF wana ID fake. Serikali imeshatangaza kuwa kumiliki ID fake kwenye mitandao ya kijamii ni kosa la jinai. Sasa nyie wenye ID fake kiama kinakuja jiandaeni.
Mimi nipo clean.

Kama sababu ndo hiyooo wakamkamate na Mack zu....
Maana fb id fake ni mingi.
 
Kuna watu mpaka Leo hawajui kwamba hawana akili .. na ukishapita umri flani basi akili ndo hupati tena hata ufanyeje
 
[emoji116]
 

Attachments

  • IMG_20161213_210921_383.JPG
    IMG_20161213_210921_383.JPG
    73.1 KB · Views: 41
JF imetumika kumpigia kampeni Magufuli na kwa hakika ina mchango mkubwa kwenye kwenye sera ya CCM ya "kupinga ufisadi". Nadhani waliomkamata hawata sahau mchango mkubwa wa Max katika kukuza demokrasia na uhuru wa habari ambao bila kuwapo hata Lowassa asingejiuzulu Uwaziri Mkuu.

Free Max.
Ikifungwa itabidi muhamie huko Facebook na Instagram.
 
Hivi umehakikisha na kujiridhisha kuwa mello kaitwa kwa ajili ya tukio hilo tuu. Hilo tukio lilikuwa posted hapa na Hayo Magazeti yameripoti kanusho la Mahamaka na si zuio la awali la mahakama

Nitafutie gazeti ambalo liliripoti kuwa Mahakama yazuia uchaguzi wa meya. Usilete hayo ambayo yameripoti kanusho nipe lile lililoripoti habari kwa mara ya kwanza.

Nakumbuka that day uchaguzi ulipokuwa unasuasua muda
Ule ule ile barua ilipostiwa JF. Ngoja niusake ule uzi nikuwekee hapa kama bado haujafutwa
sikusema kaitwa kwa tukio hilo,ila nilijiuliza mbona polisi kuna mambo mazito ya forgery hawayafanyii kazi kama hilo tukio la zuio feki la mahakama maana ile ilkuwa ni mockery of democracy na hilo suala limeisha kijuu juu tu as if nothing happened.
 
Watuache, JF ni sehemu pekee ya kutoa nyongo zoote. We ngoja Max akiachia majina lazima kuna watu watapozea ajira zao
 
Iparamasa, Kwani Mello naye umemgeuza dili? Mara eti watafuata wahariri, Ujinga mtupu, badala ya kujadili mambo muhimu yenye mstakabari wa Taifa, unapoteza mda kupost utumbo wa kuku. Mello ni nani ktk Taifa hili? ni mtu wakawaida sana hana madhara yeyote, kakamatwa kama wanavyokamatwa Wahalifu wengine ambao hawataki kutii sheria. Acha atiwe adabu.
Lumumba kwa dharau .... eti unauliza Melo ni nani wakati unamwaga upupu kwenye forum yake.
 
Sasa nimeamini kuwa tumeingia katika kipindi kingine cha ajabu sana katika demokrasia ya nchi hii. Tunaapa kwa katiba lakini tunaishi kwa hisia zetu. Hawa Polisi wanataka taarifa gani kutoka kwa Mello? Wanataka watufahamu? Kifungu cha katiba kinachoruhusu uhuru wa kujieleza kunalindwaje na serikali hii?

Tutafika tu ingawa hatujui tuendako!!!
 
Mh!! Serikali hujui kama inauwezo wa kuifungia facebook isiwe hewani Tanzania?
Hawana uwezo wa kuifunga facebook isiwe Tanzania kwa sababu kwa kufanya hivyo ni kukiuka uhuru wa habari wa kimataifa na adhabu yake ni kutengwa kimataifa ambapo kwa nchi masikini kama Tanzania ambayo haina uwezo wa kutengeneza chochote hata dawa ya malaria ni adhabu mbaya sana!
 
Back
Top Bottom