Mkurugenzi wa Bandari alikuwa sikio la kufa lisilosikia dawa

Mkurugenzi wa Bandari alikuwa sikio la kufa lisilosikia dawa

80% ya mishemishe za dar ziko bandarini, na panapo token changes za kisiasa lazima usikie milio ya mbwakoko
 
Hahahahahahahah vita ya uchumi ni ngumu sana hasa rushwa ya hela ndefu inapoingia kwenye muvi😂😂😂
Mie nakubaliana na prof wajackoya, turuhusu uvutaji bangi na kunyonga mafisadi, JPm angewanyonga Hawa wapiga dili angekuwa hai hadileo
 
Ila tukubali, TZ tumezidi kupeana vyeo kwa kujuana na siasa nyingi. Nafasi kubwa kama hizi za mashirika ya umma, tungekuwa tunazitangaza ndani na nje ya nchi. mchakato unafanywa na reputable companies. Ofisi ya Rais inapelekewa majina matatu au manne kwa ajili ya vetting. Anayeteuliwa anapewa mkataba wa miaka miwili, renewable subject to performance.

Kwa sasa almost wote wanateuliwa based wanamjua nani na maslahi binafsi. I can bet my wallet, hata huyu aliyechukuwa nafasi ya Eric Hamiss pale TPA inawezekana mama hajui hata utendaji wake. Kaletewa jina……so it goes!

lazima tubadilishe mindsets. Haiwezekani nafasi kama Tanroads, ATC, TPA, TRA, NSSF, among many others…..watu wanapeana vyeo kwa mapenzi ya kisiasa na urafiki Na kwa Siri kubwa…Lazima tutakwama tuu. Kuna wa Tanzania wanaweza kuleta matokeo chanya wakipewa nafasi. Bahati mbaya hawamjui mtu huko juu. Tangazeni hizi nafasi watu wenye sifa waombe.

tunapoongelea kujenga mifumo/institutions ndo vitu kama hivi. Nchi yetu ni kubwa sana lazima tuwe na utaratibu transparent na credible kupata watendaji wa nafasi nyeti kwenye taasisi zetu.

vinginevyo tutazidi kutafutana uchawi.
 
Bila kuunda upya TISS, PCCB, TanPol na TPA yenyewe,kamwe tusitegemee bandari kuinufaisha nchi.
Sawa.....

Lakini mindset ya mtanzania akishaajiriwa,akawa mkubwa fulani,ana cheo fulani yeye kitu cha kwanza anawaza kuwa tajiri...
Atapigaaa tu
Sasa hapo ni namna gani ya kuindoa hali hii

Ova
 
Rais alipomteua Eric Hamissi April 2021 alimweleza ufisadi wa Bandarini akamuagiza achukue hatua!

Mwezi Disemba 2021 Rais alivunja Bodi ya TPA akatoa nasaha tena za ufisadi pale! Watu wanachezea mfumo, mizigo inaonekana imelipiwa getini kumbe imepita free na nchi inakosa kodi! Akamwambia tena Mkurugenzi awaondoe watendaji wanaofanya hivyo na akitaka list atampatia yeye!

Sasa uvumilivu umemshinda Rais, kamuondoa Mkurugenzi mwenyewe!

Hii ishu ya bandari unailewa sana upo makini nayo. Au mzee Karamagi wewe
 
Yaani bandari hii inataka kila sehemu iwe inajitegemea peke yake na bosi wake
Naona Bandari ni mzigo mkubwa kuiongoza maana ina ingiza mabilioni na kuna wakubwa wamo kwenye kula hapo na bidhaa ama zao au shared au ni marafiki wakubwa na wanaoingiza mizigo na wanawabeba

Bandari ina mambo haswa na hakuna wa kuiweza hata ukijifanya unajuwa utanyooshwa uwe kama wao penda usipende utacheza ngoma yao
Ndio hapo utaambiwa huna kazi kumbe umebanwa mahali
Uwezo wa Eric ulikuwa mdogo… achana na blah blah za kusikia
 
Uwezo wa Eric ulikuwa mdogo… achana na blah blah za kusikia

Niliyoyaandika hayahusiani na uwezo wake mkubwa au mdogo
Kwani kujifunza ni aibu?
Kwanini wasitume watu wanaangalia bandari za wenzetu zinavyoendeshwa?
Najua wengi huwa wanapinga hili na kujiona wanajua zaidi
Tangu tumekuwa na bandari tumenufaikaje
Kama sio wizi tu
 
Kama mzalendo ukisoma mkataba wa ujenzi wa bandari ya bagamoyo ni vigumu kusaini labda ujitoe muhanga.
 
Mbona wengine wanasema Eric atakumbukwa kwa uzalendo wa hali ya juu
Hakutaka kubinafsisha bandari

Tatizo tumebaki radio mbao tunajazana uongo humu mitandaoni
 
Mbona wengine wanasema Eric atakumbukwa kwa uzalendo wa hali ya juu
Hakutaka kubinafsisha bandari

Tatizo tumebaki radio mbao tunajazana uongo humu mitandaoni
Watamkumbuka kwa kuongezeka kilo kila wiki.
 
Rais alipomteua Eric Hamissi April 2021 alimweleza ufisadi wa Bandarini akamuagiza achukue hatua!

Mwezi Disemba 2021 Rais alivunja Bodi ya TPA akatoa nasaha tena za ufisadi pale! Watu wanachezea mfumo, mizigo inaonekana imelipiwa getini kumbe imepita free na nchi inakosa kodi! Akamwambia tena Mkurugenzi awaondoe watendaji wanaofanya hivyo na akitaka list atampatia yeye!

Sasa uvumilivu umemshinda Rais, kamuondoa Mkurugenzi mwenyewe!
Okay
 
Back
Top Bottom