Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!...
Huyu alitakiwa kuwa campaign manager wa chama chake badala ya kuwa referee wa wote.

Tanzania mbona tunakuwa natume ya karne iliyopita?
 
tumeCCM, mwaka huu hapatatosha!
Screenshot_20200927-183350.jpeg
 
Aisee! Hivi ndugu Nkuugenzi(in Sambaaz voice) ni wa kanda maalum ee
 
Hovyo kabisa huyu. Ni kwa mamlaka ipi anawasemea raia? Double standard
 
zero kabisa, yani mnatetea mtu anaetaka kuweka rehani ardhi yetu? Unajidai upo deep kumbe umejaza manyoya tu kichwani. Mkiona hamuwezi kuisapoti CCM bora mkae kimya kuliko kutetea uovu.
Ardhi yetu na madini yetu yalishawekwa rehani na hao hao Ccm. Tena kwa mikataba mibovu ya miaka 100 ambayo haiwezi kuvunjwa. Hata Maghufuli hawezi kuvunja.
 
Wanasheria chukueni taadhari,kuna haja ya Ku-note sehemu flani kwa msaada wa baadae ikibidi. Pia kama kuna mtu mwenye video crip ya huyu bwana kada wa ccm aliye jivika ngozi ya NEC tunaiomba hapa pls.
Zama Twitter, inasambaa sana kule
 
Mkurugenzi hajaharibu chochote wala hajasema mumpigie kura nani, jukumu la NEC Ni kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha amani haitoweki kwahiyo lazima watoe tamko.

Wafanyakazi si watanzania pekew katika nchi hii,asigawe madini yetu eti kupandisha mshahara wa wafanyakazi
Ajikite ktk maswala yanayogusa mtanzania wote
Unampangia Lissu cha kunadi kwa wananchi?
 
Hali ni ngumu ndani ya CCM, Bashiru amepwaya sana na Polepole amepagawa.
Njia iliyobaki imeonekana ni kwa Mkurugenzi wa NEC ambaye bila kujua anatazamwa na Balozi zote na nchi wahisani kuingia kwenye timu ya kampeni ya ccm.

Refa akiamua kuweka filimbi mfukoni na kucheza midfielder njia sahihi ya kufanya ni kumpiga kiatu bila kujali unatengua nyonga au kuvunja mguu.
Kudadeki!
 
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!

Amesema watanzania hawataki viongozi watakaochukua madini yao na kwenda kuyauza kwa wageni nje, watanzania wanataka viongozi watakaotetea madini yao

Ameyasema hayo alipokuwa anazungumza kumuandikia barua Tundu Lissu ili kutoa maelezo dhidi ya tuhuma za uongo anazotuhumiwa kuzitoa

Amesema Tundu Lissu amekuwa akitangaza matusi, tuhuma na kudanganya wafanyakazi badala ya kutangaza sera


==
YALIYOZUNGUMZWA KWENYE VIDEO YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NEC

Kwa mamlaka ya kisheria Tume iliyonayo, tayari imemuandikia Barua Mh. Tundu Lissu ya kumuita katika Kamati ya Maadili ya Kitaifa ili aje kutoa maelezo na ushahidi wa kile alichokisema katika mkutano wake huko Musoma.

Kwa mara nyengine tena Tume inawasihi Wagombea wa Vyama vyote kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kulinda amani ya nchi yetu, katika kipindi cha kampeni kilichobaki kwa kujali muda wa kampeni, ratiba za kampeni na kuepuka matusi, sababu unatumia muda mwingi kutangaza matusi badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kutangaza tuhuma badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kuwadanganya Watanzania na wafanyakazi badala ya kutangaza sera.

Watanzania sasa hivi wanataka Afya iliyoimarika, Watanzania sasa hivi wanataka barabara nzuri, Watanzania sasa hivi wanataka miradi ya umeme, Watanzania sasa hivi wanataka elimu bora, Watanzania hawataki bra bra. Watanzania sasa hivi wanataka viongozi ambao watalinda madini yao, sio viongozi watakaokuja kuchukua madini yao na kupeleka kwa wageni nje.
Kwa maneno yake mwenyewe, huyu ni mkurugenzi wa NEC ama nayexni sehemu ya timu ya kampeni ya CCM? Hawa vikaragosi wa CCM ifike wakati wakutane na hukumu ya umma, ukiwachekea hawa, itakuwa ni sawa kabisa na kuwaachia nyani shamba la mahindi, ni bayana tu kuwa utaambulia mabuwa.

Imefika kipindi sasa wameanza kuvuka mstari wa uvumilivu. Katika kipindi ambacho kampeni zimepamba moto, wanafanya kila hila kumtoa Tundu Lissu kutoka ktk reli.

Wakati jeshi la polisi likionekana wazi likifanya kazi zake kwa weledi na pia likitii matakwa ya umma. CCM ilitegemea kuwa jeshi la polisi lingekuwa upande wa udhalimu wao, na kwa makusudi kukwepa kuwajibika kwa kutokuruhusu mikutano ya wapinzani kwa kutoa visingizio vya sababu zitokanazo na intelejesia na usalama mdogo.

Kimbilio lao kuu ovu na pekee lipo sasa kwa msajili wa vyama na viongozi wa tume ya uchaguzi. Hii taarifa ya kuwaita maDED nchi nzima wala siyo ya kuipuuzia hata kidogo. Pengine kwa kuepuka "physical movements" ambazo zingaliweza kustukiwa.

Kutoka na uwepo wa ICT kuna uwezekano mkubwa wa kufanya mkutano huo kupitia "tele conference" mathalani "Zoom or Skype meetings"
Nia yao ovu imeweza pia kushtukiwa kwa kuwa ndani ya watendaji wa vyombo na usalama wapo wazelendo wa kweli wenye kutimiza wajibu wao kwa weledi, maadili na uadilifu mkubwa.

CCM ni lazima wakumbuke ya kwamba, teknolojia huwa haziongopi. Ukweli wote utawekwa bayana.
 
Jamani maji yamezidi unga,maji yako shingoni ,binafsi imebidi nicheke kwa hiki kioja Cha jamaa wa tume,kwamba sasa hata time waungane na ccm hakuna kitakachobadilika watzn wameshaamua Kama mbwai na iwe mbwai
😆😆😂😂🤣🤣 Kwa kweli nimeamini mwananchi sio wa mchezo mchezo ,seems huyu jamaa Yuko kwenye shinikizo kubwa kwa Nini walipitisha jina la TL ,huwezi kushindana na Mungu kwa vioja hivyo
Basi tufanye ccm huwa wanachimba madini na kugawia wananchi.Aisee watu wamepanic kinoma na bado kadiri tarehe ya uchaguzi tutazika wengi kwa pressure
 
Hayo anayoyaongea ndiyo kazi ya Tume? Mbona anaiweka Tume kwenye nafasi ya hatari sana? Yaani Tume inawalazimisha wagombea kitu cha kuongea? Watanzania wanajua wanachotaka kusikia na kila Chama kina ya kwake ya kujinadi kwa wananchi na Wananchi ndiyo wataamua.

Kwani madini yetu huwa yanauzwa wapi? Tume inahusika vipi na utekelezwaji wa Ilani za vyama? Mbona haijaongea kitu kuhusu aliyejisifu kuwanyima wananchi maendeleo kwa kutomchagua na kuahidi kuendelea kuwanyima kama hawatomchagua?

Mpaka hapo Tume imeshapoteza uhalali wake wa kusimamia uchaguzi huu na naiona kwamba kuwa ndiyo chanzo cha vurugu nchini.
Mwaka huu tutaelewana tu
Kmmk watuletee uhajisi wao hawataamini
 
Dooh, kweli ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauna!
Mkurugenzi si aanzishe chama chake tu.
Asitupangie watanzania tunataka nini.
Sisi wengine tunataka ubwabwa tu, sio Barabara nzuri wala ndege.
 
Back
Top Bottom