Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

Uchaguzi 2020 Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC: Watanzania hawataki mtu atakayeuza madini yao kwa wageni nje

Huyo mkurugenzi anajitahidi kumsaidia Oleksanda lakini mwaka huu watajua hawajui...
Lissu sio Lowasa....
 
Mkurugenzi waTume ya uchaguzi hawezi kutusemea watanzania, eti Watanzania hawamtaki mtu atakayeuza madini yetu nje...... alikutana wapi na hao Watanzania?
 
Huyu mkurugenzi arejee kujifunza kazi za Tume
 
Je wito wao kwa Lissu kuwa wanamtaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi.....hii ni sawa na Kesi ya Mbuzi imepelekwa kwa hakimu fisi kujitetea kwa nini asiliwe....
 
Eti watanzania hawataki mtu atakayechuka madini yao na kuyapeleka nje?
Ina maana hayo madini tutaenda kuyachemshia uji?
 
Tunaposema Lissu ni hatari ndio muelewe. Mkurugenzi wa uchaguzi kachanganyikiwa na kuanza kunadi sera kama kichaa. Sasa kama kibaraka hofu yake ni dhahiri namna hii ‘bosi’ wake ana hali gani?

Hii sio aibu, ni fedheha!
Salam zangu zikufikie Nifah.
Yaliyopo katika mioyo ya wahovu yatadhihiri hadharani, Mungu anatudhihirishia yaliyopangwa sirini kupitia Lisu. Wanajitokeza wenyewe waziwazi ili watanzania tujue.

Sent from my TECNO K9 using JamiiForums mobile app
 
Rudia kumsikiliza
Mkurugenzi hajaharibu chochote wala hajasema mumpigie kura nani, jukumu la NEC Ni kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha amani haitoweki kwahiyo lazima watoe tamko.

Wafanyakazi si watanzania pekew katika nchi hii,asigawe madini yetu eti kupandisha mshahara wa wafanyakazi
Ajikite ktk maswala yanayogusa mtanzania wote
 
Kwani huyo mkurugenzi anagombea urais kupitia chama gani? Watanzania tuna masikio, hayo matusi ya Lissu anasikia peke yake tu?
Tunayasikia wengi, ila mwenye mamlaka ya kumchukulia hatua Lissu ni Tume ya uchaguzi
 
Mkurugenzi wa tume ni nyanya,hajui kwamba anapaswa kusimama kama nani 🙄 🙄🙄
 
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!

Amesema watanzania hawataki viongozi watakaochukua madini yao na kwenda kuyauza kwa wageni nje, watanzania wanataka viongozi watakaotetea madini yao

Ameyasema hayo alipokuwa anazungumza kumuandikia barua Tundu Lissu ili kutoa maelezo dhidi ya tuhuma za uongo anazotuhumiwa kuzitoa

Amesema Tundu Lissu amekuwa akitangaza matusi, tuhuma na kudanganya wafanyakazi badala ya kutangaza sera


==
YALIYOZUNGUMZWA KWENYE VIDEO YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NEC

Kwa mamlaka ya kisheria Tume iliyonayo, tayari imemuandikia Barua Mh. Tundu Lissu ya kumuita katika Kamati ya Maadili ya Kitaifa ili aje kutoa maelezo na ushahidi wa kile alichokisema katika mkutano wake huko Musoma.

Kwa mara nyengine tena Tume inawasihi Wagombea wa Vyama vyote kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kulinda amani ya nchi yetu, katika kipindi cha kampeni kilichobaki kwa kujali muda wa kampeni, ratiba za kampeni na kuepuka matusi, sababu unatumia muda mwingi kutangaza matusi badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kutangaza tuhuma badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kuwadanganya Watanzania na wafanyakazi badala ya kutangaza sera.

Watanzania sasa hivi wanataka Afya iliyoimarika, Watanzania sasa hivi wanataka barabara nzuri, Watanzania sasa hivi wanataka miradi ya umeme, Watanzania sasa hivi wanataka elimu bora, Watanzania hawataki bra bra. Watanzania sasa hivi wanataka viongozi ambao watalinda madini yao, sio viongozi watakaokuja kuchukua madini yao na kupeleka kwa wageni nje.
Hii ni ajabu kwakweli, hivi mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi kazi yake si kutangaza mshindi tu?
Habari za mgombea kuwaambia hivi au vile wananchi ye zinamuhusu nini?
Anaposema watanzania wanahitaji hiki na kile yeye anatupangia wananchi wote mil 56? Huu ni ujuha wa wazi watanzania, hii inaonesha kabisa malengo hasi ya tume dhidi ya upinzani.
Huu wote ni ushahidi wa wazi wa upendeleo wa chama fulani. Hakuna wanasheria, taasisi za kisheria kukemea Haya mambo ya ukandamizaji wa upinzani na double standards zinazooneshwa na hii tume?
Naona mazingira ya machafuko yanatengenezwa na kuna watu wataitwa The Hugue
 
Wewe ukiisapoti ccm inatosha si lazma tuisapot wote
Zero kabisa, yani mnatetea mtu anaetaka kuweka rehani ardhi yetu? Unajidai upo deep kumbe umejaza manyoya tu kichwani. Mkiona hamuwezi kuisapoti CCM bora mkae kimya kuliko kutetea uovu.
 
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, amesema watanzania wanataka Afya iliyoimarika, barabara nzuri, miradi ya umeme, elimu bora hawataki blah! Blah!

Amesema watanzania hawataki viongozi watakaochukua madini yao na kwenda kuyauza kwa wageni nje, watanzania wanataka viongozi watakaotetea madini yao

Ameyasema hayo alipokuwa anazungumza kumuandikia barua Tundu Lissu ili kutoa maelezo dhidi ya tuhuma za uongo anazotuhumiwa kuzitoa

Amesema Tundu Lissu amekuwa akitangaza matusi, tuhuma na kudanganya wafanyakazi badala ya kutangaza sera


==
YALIYOZUNGUMZWA KWENYE VIDEO YA MKURUGENZI WA UCHAGUZI NEC

Kwa mamlaka ya kisheria Tume iliyonayo, tayari imemuandikia Barua Mh. Tundu Lissu ya kumuita katika Kamati ya Maadili ya Kitaifa ili aje kutoa maelezo na ushahidi wa kile alichokisema katika mkutano wake huko Musoma.

Kwa mara nyengine tena Tume inawasihi Wagombea wa Vyama vyote kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi ili kulinda amani ya nchi yetu, katika kipindi cha kampeni kilichobaki kwa kujali muda wa kampeni, ratiba za kampeni na kuepuka matusi, sababu unatumia muda mwingi kutangaza matusi badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kutangaza tuhuma badala ya kutangaza sera, unatumia muda mwingi kuwadanganya Watanzania na wafanyakazi badala ya kutangaza sera.

Watanzania sasa hivi wanataka Afya iliyoimarika, Watanzania sasa hivi wanataka barabara nzuri, Watanzania sasa hivi wanataka miradi ya umeme, Watanzania sasa hivi wanataka elimu bora, Watanzania hawataki bra bra. Watanzania sasa hivi wanataka viongozi ambao watalinda madini yao, sio viongozi watakaokuja kuchukua madini yao na kupeleka kwa wageni nje.
Huo ni uchoyo , na wao wakigoma kuwauzia silaha mtajilindaje, hapo mtu mpaka chupi kavaa kutoka nje alafu analeta nyee nyee , hadi pedi ni kutooka nje, umaskini shida kweli, mtu anafikiria kwa kutumia sehemu ya kukalia badala ya medula oblongata
 
Mkurugenzi anawasemea watanzania...
Nani kasema watanzania wanataka hayo anayosema?

Kama vp na yeye achukue fom agombee
 
Tume FUTUHI hii
 

Attachments

  • Tume Huru.jpg
    Tume Huru.jpg
    20.4 KB · Views: 1
Lisu and Zitto/Maalim waitidh press conference kutoa msimamo juu ya kauli ya Mahela. And let the world take note.. ICC, UNSC, UN, EU etc Mwanahabari Huru
Huyu mkurugenzi mkuu wa NEC anaitisha vyombo vya habari na kusema eti watanzania wanataka mtu atakayelinda madini yao, atakayewajengea vituo vya afya, atakayewajengea mabarabara, atakayewaletea umeme. Kwani haya yanaihusu NEC?...
 
Back
Top Bottom