Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mrisho Gambo ana kiherehere utafikiri kuku anaetotoa
Tatizo Mkuu wa Mkoa anatoa maagizo kinyume na sheria,taratibu za uendeshaji Jiji.
Naomba unitaji angalao pasna shaka watetezi wa wanyonge wa nchi hii hata watano tu tanguliza hofu ya Mungu kwanza usilete hila za she.twani hapa zitashindwa na kulegea.
K
Kama jiji linafanya mambo yasiyofaa na kulalamikiwa na kusimamiwa na madiwani wenye tamaa na visasi vya kulipiza visasi yeye asiingilie kati sio. Yeye ni mwakilishi wa Raisi katika mkoa. Lawama na vilio vilivyokua hapo stendi ndigo na maeneo mengine aache tu kwa kua jiji linasiamamiwa na chadema. Acha hizo.
Majukumu na wajibu wa Mkuu wa Mkoa ni kupokea mwenge katika mkoa wake na lingine ni kuongoza vikao vya ulinzi na usalama katika mkoa wake na mwisho ni kumpokea Rais anapotembelea Mkoa wake.
Mkuu wa Mkoa anapojiingiza katika shughuli za utendaji wa Jiji ni kuingilia kazi ambazo hazimhusu.
Maagizo yapi na yapi aliyatoa mkuu wa mkoa yalikuwa kinyume na sheria na taratibu za uendeshaji jiji? Au unajiropokea tu?
Katika arguments za mayor ametoa mpaka reference za sheria na kanuni jinsi maamuzi yanavyofanywa na taratibu zake zote. Mpaka Mh. Waziri Simbachawene amesema anachoona yeye zilizotumika kufanya maamuzi ni busara. Na kasema kuwa kama taratibu zilifuatwa ni sawa ukiangalia anakwepa kujibu. Na upande wa pili hakuna anayetoa reference yyoyote ya kisheria au kanuni inayo back huo uamuzi. Halafu hili la posho kwa nini iwe Arusha tu? hizi posho zinalipwa mikoa yote. Basi utoke muongozo wa nchi nzima. Uamuzi unaoongelewa ulifikiwa jiji likiwa chini ya chama kingine nahiyo haikuwa issue naulifuata taratibu zote mpaka kukubaliwa na waziri wa wakati ule. Ila sasa ni haramu. Sheria hutungwa kwa kuanzia katika busara. Mara nyingi kinyume na sheria huwa haina busara. Sheria nyingi za zamani ziliwekwa kufuatia maamuzi ya busara. Naikija busara mpya sheria hubadilishwa. Sijaiona hiyo busara mpya kwenye hili.
hebu kwenda huko na slogan za muflisi wa kisiasa. eti mtetezi wa wanyonge! huku kujipendekeza ni keroooAcha umbea dhidi ya mchapa kazi na mtetezi wa wanyonge Mh Mrisho Gambo. Wananchi wa kawaida tunakuunga mkono mkuu wa mkoa.
Ngoja nikumegeea kiduchu.
Posho za madiwani na staili zao zote zinasimamiwa na nani ?.Ukiweza kunijibu hili swali dogo labda nitaweza kujadiliana na wewe.
hebu kwenda huko na slogan za muflisi wa kisiasa. eti mtetezi wa wanyonge! huku kujipendekeza ni kerooo
Aibu na iwe kwenu kama kukesha kote kule na makelele yote ya kipindi cha uchaguzi mpaka sasa kumbe lengo lilikuwa kulilia posho. Acheni mambo ya ajabu, tafuteni kazi za kudumu na za maana hamtokaa mtake kutoana macho na watu kisa posho. Mnatukwaza ati
Toa reference ya authority ya kauli yako
Majukumu na wajibu wa Mkuu wa Mkoa ni kupokea mwenge katika mkoa wake na lingine ni kuongoza vikao vya ulinzi na usalama katika mkoa wake na mwisho ni kumpokea Rais anapotembelea Mkoa wake.
Mkuu wa Mkoa anapojiingiza katika shughuli za utendaji wa Jiji ni kuingilia kazi ambazo hazimhusu.