Mkutano wa CAF wapitisha maombi ya Zanzibar kuwa mwanachama huru

huo muungano wenyewe hawautaki sembuse vitu vidogo vidogo kama hivyo
 
Maumivu huanza taratibu. Haya yameanzia kwenye gozi kama yatafika FIFA homa itapanda. Kimataifa sjdhani kama kuna nchi inaitwa Tanzania Bara. Sasa bandugu mtajiitaje na wengi wenu wanadai hawaijui Tanganyika?
 
Mungu ibariki nchi ya Zanzibar , sasa tunaiomba Tanganyika nayo iirejeshee uhuru wake Zanzibar .
Laiti mngejua kuwa serikali ya muungano, kupitia TFF ikipigania zanzibar kuwa mwanachama wa CAF, na imekuwa ni faraja na wala si vinginevyo.....
 
Na Hayatoo kashindwa urais wa CAF

Safi sana hayatou kushindwa! Toka niko secondary school hadi sasa najukuu yumo tu! Alitaka kuwa Havelange wa Africa! Ila nawapongeza ndugu zetu Wazenji kwa kupata nafasi hii. Ila wapunguze "UBONYEEEEEE" haya mambo si lelemama!
 
Acha ushamba mkuu! Angalia namna UK ilivyo! Wales, England na Scotland vinajitegemea! Soma uelimike sio kukariria mitihani!
Wewe akili yako ni ndogo hivi Muungano wa Great Britain Unafanana na Muungano wa Tanzania au Unaropoka tuu.
 
Game kati ya Zanzibar na SISI, sisi tutajiiita Tanzania Bara kwa unafki wetu!
Inamaana wachezaji wa timu ya taifa ni wabara peke yao? Kama ni hivyo hizo timu zitakapo kutana itakuwa ni muda muafaka watu kuonyesha hisia zao.
 
Great Britain *Uingereza) ni muungano wa Visiwa vya Scotland, Wales na Ireland. Hapa kila kisiwa ni mwanachama wa chama cha Mpira Ulaya; Sasa kuna ubaya gani kwa Zanzibar?
Niwanachama wa fifa pia
 
Kwa hela hizo hizo ambazo Zanzibar wapatapa CAF, watafanya makubwa kuliko Tanganyika.

Hawatakuwa na upumb.avu wa kwenda kupanga ofisi kwa million 400 katikati ya mji huku wakianza ofisi zao!
 
Wewe akili yako ni ndogo hivi Muungano wa Great Britain Unafanana na Muungano wa Tanzania au Unaropoka tuu.
Muungano ni muungano tu! Kwa namna ulivyo kiazi! Huoni kuwa Zanzibar wana !mpaka rais na bendera yao! Wana Bunge na mawaziri! Akili yako umeifukia bar!
 
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limeridhia kuipa uanachama wa kudumu Zanzibar kuanzia hii leo. Ombi hilo limeridhiwa na mkutano mkuu wa CAF unaoendelea mjini Addis Ababa nchini Athiopia. “Ombi la Zanzibar limepita bila kuwekewa pingamizi, Zanzibar sasa ni mwanachama wa 55 wa CAF.” Uliandika ukurasa wa Twitter wa shirikisho hilo. Kwa kupata nafasi hiyo, Zanzibar itakua na fursa ya kushiriki michuano yote inayoandaliwa na CAF, kama vile mataifa ya Afrika (AFCON), fainali za wanawake (AWCON) na fainali za vijana (AFCON U17 na AFCON 20).
 
Hongereni,ila wa FIFA hamtapata kwa sababu Zanzibar siyo nchi - haina dola,haina mipaka nk.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…