Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Mwenyekiti.
ninatoka nje kidogo kunusa ugoro maana zogo la humu ndani, hatusikilizani.
ntarudi punde

Ohooo, yamekuwa hayo tena? Hivu ugolo si madawa ya kulevya?
 
Mwenyekiti hebu tuwekee pannel yako ya wanamajumuisho maana unaposema kutakuwa na mjumuisho hapo unaniacha njia panda kwani sijajua nani ni nani ktk mjadala huu

Hahaaa msanii, kuna watu wanakimbia maajukumu hapa, nadhani kwa kuwa hakuna posho. Iko hivi:
Dark City = katibu lakini inaonekana amechomoa
WoS= Mwenyekiti ya Kamati ya kuhusu utawala bora na kama wahujumu wanyongwe au la. Kachomoa na kunipigia kelele eti atanifikisha mahakamani. Alimtumia pia lugha ya matusi mazito ya kawaida na ya nguoni pamoja na kejeli na kashfa.

Habari ndo hiyo, kinachoniweka hapa ni uzalendo tu.

Sasa nasubiri warudi niwaulize kama watafanya hiyo kazi au la.
 
Mwenyekiti naona hiki kikao kilikuwa kilikuwa cha dharura sana, Maana wengine tunavile vikao vya posho na hatuwezi kuvikwepa si mnajua jamani hii desturi ya posho nyingi nyingi? Kwa hiyo hivi vikao visivyo na posho huwa tunapiga chenga , lakini hiki ni KIKAO MUHIMU KULIKO POSHO, Mwenyekiti naomba samahani kwa kuchelewa mkutanoni!

Mimi Hoja yangu ya Msingi iko kwenye TUME YA UCHAGUZI, Uchaguzi unaweza kuwa huru na wa haki kama tume itakuwa chombo huru kisichofungamana na chama chochote, hivyo watendaji wakuu katika tume hii wachaguliwe na vyama vyote vilivyoandikishwa na msajili wa vyama vya siasa, lakini pia hata Msajili wa vyama vya siasa awe anaomba nafasi na kusailiwa na hatimaye kupewa kazi na Mashirika au Taasisi za elimu ya Juu zenye utaalamu na uzoefu wa kudahili wafanyakazi , Na katika hili sitegemei chochote kipya kwenye rufaa ya Dkt. Slaa dhidi ya Mgombea wa CCM.
 

Haaa haaaa haya Mkuu, nimekuelewa!
 
Msanii safi sana . . . huwezi kupata soft copy uzibandike hapa? hatufanyi mchezo na agenda hizi. Tukimaliza tunachapisha na kukabidhi kwa serikali ijayo.

Naomba kuwakilisha.
Ninazifuatilia mkuu, nikipata naziweka sawia hapa jukwaani tuangalie na kupima
Msanii, kwanza karibu tena. Mkuu umetukuna sana kwa pointi zako. Zinatuweka vizuri kuongezea zilizopita hasa suala zima la katiba.

Hili la tano Msanii, unaweza kulitolea ufafanuzi wa kina?
Ninaposema maabara ninalenga kuwa serikali iboreshe maabara za mashule hasa kuanzia shule za msingi, pia kila mkoa kama si wilaya kuwepo na maabara hizi. tusisahau katika majeshi yetu ya ulinzi na polisi waboreshewe maabara pia
Aina za maabara siyo zile za kutest litmus paper bali za majaribiop ya kisayansi, kwa mfano maabara zinazohusu masuala ya electronics na components zake, pia zinazohusu masuala ya fizikia hasa mashine na mitambo ili kuwezesha wavumbuzi kujitokeza na kuleta changamoto za maboresho. Nakumbuka nilipokuwa shule nilimwomba mwalimu wa fizikia nifanye jaribio la kurusha roketi (niliambulia kibano). Maabara za masuala ya arts hasa sisi tunaotumia rangi za kuchorea tunaweza kuvumbua aina ya rangi kutokana na malighafi za hapa nchini hivyo tukaongeza pato la taifa (nakumbuka nilipokuwa najifunza uchoraji sikuweza kupata rangi na matirio nyinginezo, nilitumia majani na maua kupata rangi na manyoya ya wanyama kutengeneza brush), hivyo pamoja na maabara waandaliwe watu wa kuziendesha na kumaintain.
Nimeeleweka?
 

Asante sana Kijana wangu. Hili litazingatiwa.

Ila suala la kinywaji kuwa makini . . . maana tuko katika mkutano, na wewe kila ukishika mic una glass yako . . . unanikumbusha mambo ya John walker . . . . Haaa haaa
 

Swadata! Nimekusoma DC! karibu tena!
 

Kijana kwanza karibu sana renegade katika Mkutano . . . Ila tafadhali tumia lugha ya kistaarabu maana matusi haturuhusu, unaweza ukasababisha TBC wakakata matangazo. Tuko zaidi Kiuzalendo na Kitaifa kuliko mambo ya Chama.

Sasa turudi kwenye hoja, tunakubaliana na wewe 100%. Iliongelewa kuwa katiba iainishe kuwe na tume huru ambayo itawajibika bungeni na si serikalini.

Hili la msajili wa vyama ni jipya na limekaa vizuri. unaweza kulitolea ufafanuzi wa kina ili wadau walielewe kwa uwazi?
 
Kwa kuwa suala la katiba limeonekana kuwa kero ya wengi wa waliohudhuria, ni vema hapo baadae tujadili tunataka katiba ya aina gani ili itakapofika kupiga kura za "Ndio" na "La" kieleweke. Mimi naogopa kutumia sana energy ya ubongo sasa hivi nisiije kuishiwa sukari nikadondoka wakati nachangia mada, swaumu imeshanchanganya!
 

jamani tuache utani, hivi mmepitia points zote toka mwanzo? Aisee mnatisha JF na sijui kama Serikali inajua kuna vichwa hapa.

Mimi nimekuelewa sana na naomba tuliweke hivi: Kwamba serikali inayokuja "Ifanye kila jitihada za kuendeleza Utafiti, sayansi na Technolojia mabyo itachochea kuleta maendeleo ya Nchi"

hapo vipi?
 
Ukibofya hapa http://www.hakielimu.org
utakuta hii meseji inakungoja
We are sorry for inconveniences,
For any details please contact:
HakiElimu
Plot # 739, Mathuradas Street
P. O. Box 79401
Dar es Salaam
Tanzania
Tel: +255 22 2151852/3
Fax: +255 22 2152449
sijui ndo wamefulia?
bado nasaka soft copies za ahadi za ccm 2005
 
Sijamuelewa huyu jamaa ana zungumzia nini, bora unge andika kwa lugha moja kuliko hivi unavyo mix swahili na ki-English, fool!
 

Mkuu, tumekusoma sana na tuko pamoja.

Tunaomba wanaomfahamu Dr. Mvungi (PhD mambo ya katiba) atuwekee soft copy ya ile waliyoiandaa ili tuanze kuichambua hapa. tupate kazi ya kufanya.
 
hapo sawa!
 
Sijamuelewa huyu jamaa ana zungumzia nini, bora unge andika kwa lugha moja kuliko hivi unavyo mix swahili na ki-English, fool!

Mnganyizi; kwanza karibu kikaoni, haalafu lete hiyo Mic kwanza.

Tumesema maadili hayaruhusu lugha ya matusi. tuko live TBC au unataka wakate matangazo?

Sasa turudi kwenye hoja yako, nani hujamuelewa?

Wana JF tafadhali tusichakachue lugha. Tutumie kiswahili tu, lugha yetu ya taifa.
 
Mkuu Superman
Nimefanikiwa kwa ombi lako kusaka kwenye net na kukuta hii kitu itakayotuongoza kuchambua ahadi za Kikwete 2005. Nimeweka ilani kwanza kama walivyoiweka wenyewe kisha nasaka ahadi ambazo hazikuwekwa kwenye ilani
 
Ndg M/Kiti,Ktb, na wajumbe wote mlikoko kwa kikoa hiki napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa michango yenu kwa dhati, bila kupoteza muda nina yangu machache kwa kuanzia tu kwa leo hii.


  1. Katiba ya nchi ile ndio ya kwanza kufanyiwa marekebisho
  2. Baaada ya kuundwa katiba ya nchi kuwepo na mustakabali wa nchi hii ni katika kusimamia kila sector za serikali na umma katka uwajibikaji wao katika nchii.
  3. Elimu- kuwepo na mustakabali wa nchi ndipo kutaisimamia mfumo mpya wa elimu kama wenzangu waliotangulia wakiitaji mfumo mpya wa elimu na itatuondolea ile hali ya kila waziri aingiapo wizara hiyo na kujiwekea mfumo wake wa kuiongoza wizara kwa kuifanya kama sarakasi
  4. Afya
  5. Miundombinu na mawasiliano
  6. Viwanda

 

Msanii,

Kuna wengine wanapinga kwa sasa na hasa hasa kwa nchi masikini kujiingiza kwenye tafiti za ugunduzi zaidi (sisemi wasifanye) ila wanadhani (hata mimi naamini hivyo) kwamba kuna level ya hali ya juu ya ugunduzi umeshafanyika na uko kwenye public domain. Kwa hiyo sisi tunatakiwa kujielekeza kwenye technology zaidi ili kutumia hivyo vitu kutegengeza products kwa ajili ya matumizi yetu na kwa kukuza uchumi wetu. Kwa mfano, Cuba wanazalisha zaidi chanjo nyingi (na hasa hasa zile chanjo muhimu za watoto kwa mpango wa EPI) kwa sababu wametumia elimu iliyokwishafanyiwa kazi na kuweka nguvu kwenye uzalishaji. Kwa sasa ni chanzo muhimu cha chanjo hizo kwa shirika la afya duniani (WHO). Pia nasi tunaweza kuangalia mahali pa kuziba pengo, mfano, chanjo ya kipindupindu au products za kifizikia zinazohimili joto la hapa kwetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…