Nyunyu karibu sana. Toka jana nilituma watu wakutafute nikaambiwa umekwenda kule nanihii . . . kunanihiii . . . shughuli muhimu.
Siku nyingine ukisikia kikao muhimu kama hiki jitahidi kuwahi. Na siku hizi kuna Boda Boda so, kuwahi siyo issue ya foleni tena.
Turudi kwenye hoja sasa:
Hili na katiba liko sawa na limekaa vema. Tusaidiane kumtafuta dr. Mvungi atuletee draft tuanze kuipitia hapa.
Hili na Elimu nadhani ni Muhimu ila mpaka sasa hatujaliweka sawa. Kuna moja alisemaa elimu ya msingi iwe hadi kidato cha nne. Je baadaa yaa hapo itakuwa imemwandaa kijana wa Kitanzania kukabiliana na maisha?
wale waliobahatika kuhudhuria Silivan Summit mlimsikia Rais wa Mozambique akiongea kuwa yeye Mpango Mzima wa Elimu ni kujenga Vocational training Centres mapka level ya kata. ameshafanya hivyo kila wilaya sasa. Na akasema vijana wakimaliza wanaingia moja kwa moja katika soko la ajira ya kazi za mikono na uzalishaji.
Tuna shida kwani haapa vijiweni down town nawaona hadi university Graduates na wengine na Masters wakitafuta ajira. Wa diploma na advanced ndo usimseme, tayari nina CV 10 wakiomba niwatafutie ajira nami wala sijawapatia bado kwani hazipo.
Hebu tuelewane katika hili, tunataka nini hasa katika Elimu? Let us be brief and to the point.