Mkutano wa Kikatiba tu ndiyo utaandika Katiba Mpya

Mkutano wa Kikatiba tu ndiyo utaandika Katiba Mpya

Hatuwaamini watawala
ban.maswali.jpg


Ansbert Ngurumo​

amka2.gif
MTANI mmoja wa Rais Jakaya Kikwete ameniambia hivi: "Sasa naamini kwamba waliosema Kikwete ni chaguo la Mungu walikuwa sahihi. Maana kwa jinsi hii, Mungu aliipenda Tanzania hata akamtuma JK agombee na kushinda urais, ili kila Mtanzania atambue kuwa wakati wa mabadiliko makubwa umewadia."
Maana kama si Kikwete, Watanzania wengi wangeendelea kuamini kwamba Tanzania bila CCM haiwezekani. Sasa wanajua kuwa inawezekana. Na ndiyo Tanzania wanayoitaka.
Hata wana CCM wenyewe, katika makundi makundi, na kwa kuzingatia masilahi ya chama au ya makundi yao, wamefika mahali wanaanza kupata ujasiri wa kufikiria na baadaye kusema (ingawa kwa kificho) kwamba CCM bila Kikwete inawezekana.
Wazo hilo limewafikisha katika tamaa ya mabadiliko ya uongozi ndani ya chama. Wanataka kutumia kauli yake mwenyewe kukivua chama gamba ili kiendane na wakati.
Bahati mbaya kwake, baadhi ya wanachama wanadhani gamba zito linalopaswa kuvuliwa ni uenyekiti wa Kikwete. Kama watafanikiwa au la, ni matokeo ya harakati zao. Lakini wanatamani kuwa na CCM isiyoongozwa na Kikwete, kwa sababu wameridhika kwamba, amejitahidi lakini uwezo wake umeishia hapo.
Walio makini zaidi wanaamini kwamba baada ya kukivua chama gamba wanahitaji kukipa moyo mpya. Hawa ni wale wenye akili pana kuliko ya JK mwenyewe – kwamba wakati yeye anadhani kukivua chama gamba ndiko kukijenga, wao wanafikiri tatizo la CCM si gamba tu bali moyo, ambao ndio uhai wa chama.
Hata hivyo, wapo wengi wanaodhani kwamba iwe iwavyo – kwa moyo mpya au gamba jipya – CCM imezeeka na inakaribia kufa.
Kwamba katika miaka 50 kiliyokaa madarakani, moyo mpya na gamba jipya haviwezi kufanya kazi ya maana kama ubongo umezeeka na kuchoka. Wanaweza kupata gamba. Lakini hawana hakika kama watapata moyo au ubongo mpya wa CCM.
Wengine wanakiri kwamba CCM ya Kikwete na Makamba ni ndege inayoshuka kwa kasi ya ajabu. Imeishiwa mafuta. Na kwa kuwa ni ndege ya kizamani, na katika kasi ya anguko linaloikabili, hakuna jinsi ya kuijaza mafuta ikiwa angani. Hawa wamekata tamaa. Wanasubiri ishuke chini – wapone au wafe!
Kuliko wakati mwingine wote, sasa kauli ya Mwalimu Julius Nyerere, imepata tafsiri ya waziwazi. Alisema: "Chama legelege huzaa serikali legelege."
Kwa hiyo wana CCM wanaotamani mabadiliko makubwa ndani ya chama chao wanakiri kwamba mabadiliko hayo hayawezi kuja wakiwa na Kikwete kama mwenyekiti wao.
Wanakula njama apunguziwe madaraka! Lakini tayari Katibu Mkuu, Yusuph Makamba, amesema njama hizo ni uhaini na haziwezekani!
Lililo dhahiri hapa ni kwamba wanachama walio wengi wamekuwa wanaeleza udhaifu wa Rais Kikwete kwa mzunguko, wakijifanya wanamlaumu Makamba.
Wana akili timamu za kutambua kuwa kama tatizo la chama ni Makamba, asili ya tatizo hilo, ambalo ndilo tatizo lenyewe, ni Rais Kikwete aliyemteua.
Wanakiri kwamba Makamba ndiye katibu mkuu anayekidhi viwango vya JK. Vinginevyo, mwenyekiti mwenyewe angekuwa ameshaona udhaifu wa Makamba; au walau angekuwa amesikiliza malalamiko na ushauri wa wanaotaka chama kiwe na mtendaji makini na mweledi.
Lakini hoja kuu kwa wadau wa mabadiliko na maendeleo ni hii. Kama Kikwete angekuwa mahiri na makini; kama angekuwa ameweza kuongoza chama na serikali; kama angekuwa jasiri na mweledi; kelele hizi za mabadiliko zisingekuwapo.
Kwa mantiki hii, udhaifu wake ndiyo chachu ya mabadiliko ya sasa yanayozungumzwa ndani na nje ya CCM. Ni wazi kwamba dhana ya mabadiliko imekuwako tangu awali, na ndiyo imekuwa nguzo ya sera mbadala za vyama vya upinzani, lakini miaka mitano ya udhaifu wa JK imeunganisha hisia za wananchi katika kudai mabadiliko kwa staili ambayo haikuwahi kuonekana kabla.
Hata hoja za mabadiliko ya katiba zimepata kueleweka vema kwa wananchi kwa sababu kuna mifano hai ya kutoa kwa lugha nyepesi. Na ndiyo maana serikali inapaswa kujihadhari na uchakachuaji wa mfumo wa uandaaji wa Katiba mpya.
Maana wananchi hawakubali kuongozwa na katiba iliyochakachuliwa. Wanajua wasichokitaka, na kile wanachokitaka. Serikali inapaswa ijue kuwa inaongozwa na viongozi wasioaminika kwa viwango wanavyofikiria wao.
Hawa hawa wasioaminika, wangepaswa kujenga mazingira ya kuonekana walau kuna jambo moja kubwa wameliweza, au hata kama hawaliwezi, wana nia njema, ambayo itaungwa mkono na kukamilishwa kwa akili na nguvu za wengi.
Wanapaswa wajue kuwa udhaifu wa uongozi ndio unaofanya kila wanalogusa linamong'onyoka, na kila dili wanayofanya inashtukiwa. Ndiyo unaofanya kila kauli wanayotoa inashukiwa.
Kuna wakati iliwahi kusemwa kuwa Watanzania hatuaminiani. Lakini ukweli halisi si kwamba hatuaminiani, bali hatuwaamini watawala wetu. Wamekuwa magamba ambayo, kama ya nyoka, yamezeeka na wakati wa kujivua (au kuyavua) ni sasa.
 
CCM itapungukiwa nini ikiifuta UVCCM?
ban.nasema.jpg


Christopher Nyenyembe​

amka2.gif
MWAKA 2013, Uchaguzi Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) utafanyika ukiwa mbele kwa mwaka mmoja baada ya kufanyika kwa uchaguzi wa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC) na Kamati Kuu (CC).
Uchaguzi huo wa wajumbe wa NEC na CC unaotegemewa kuwa na mabadiliko makubwa ya kimuundo, kisera na hasa kuwa na sura mpya za watendaji wake ili kuweza kukabiliana na msukumo mzito wa kambi ya upinzani.
Lakini ili hayo mabadiliko yanayokusudiwa yaweze kutimia kwa hali ilivyo wimbi la vijana wa CCM, waliozaliwa ndani ya chama hicho, kulelewa na kukua katika maadili ya kichama, tabia na hulka za vijana hao zinaonekana wazi kuwa zimeanza kuwakera walezi wao.
Malumbano yanayoendelea hivi sasa kati ya walezi, waasisi wa CCM na viongozi wastaafu walioweza kujibebea heshima kubwa na utendaji uliotukuka kwenye serikali ya chama hicho dalili za wazi zinaonyesha kuwepo kwa mmomonyoko mkubwa wa kimaadili na huo unaweza kuwa mwanzo au mwisho wa CCM.
Ikumbukwe kuwa UVCCM ni miongoni mwa Jumuiya zilizoundwa na chama hicho kwa lengo la kukijenga na si kukisambaratisha na wala jumuiya hiyo haikuundwa kwa ajili ya kuwapa kiburi vijana hawa ili waweze kutamka maneno ya dharau na kejeli yanayowalenga viongozi wao waandamizi na wastaafu kutoka ndani ya CCM.
Mbali ya kuwepo kwa UVCCM ikumbukwe kuwa jumuiya nyingine zenye mafanikio makubwa ndani ya chama hicho kikongwe ni Jumuiya ya Wazazi ambayo kwa uimara wake imeweza kusimamia vyema sera ya utoaji wa elimu bora kwa vijana kwa maana ya kumiliki shule zilizoweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuwajengea uwezo vijana na kupiga vita ujinga.
Jumuiya ya wazazi kwa umuhimu wake sio tegemezi sana kutokana na miradi yake kadhaa inayoendesha hasa shule kama nilivyoeleza ambazo zimekuwa zikizalisha wasomi vijana kila kukicha na baadhi yao ndio hao walioibukia kwenye umoja wa vijana wa CCM wanaoonekana kung'ara leo kushinda wazazi wao.
Jumuiya nyingine ni ya Wanawake wa CCM(UWT),jumuiya hii imekuwa ikiheshimiwa kwa kiasi kikubwa ndani ya chama na naweza kusema kuwa imekuwa ikifanya kazi kubwa sana ya kuwahamasisha wanawake wa mijini na vijijini ili waweze kukipenda chama chao na kuviponda vingine, ukweli unabaki pale pale kuwa kazi ya jumuiya hiyo huonekana zaidi wakati wa uchaguzi mkuu.
Ni dhahiri kuwa ushindi mkubwa unaopatikana wakati wa uchaguzi mkuu husababishwa na wanawake ambao kwa kuwa na jumuiya yao tangu enzi hizo kumesaidia kwa kiasi kikubwa kuchochea ushindi wa CCM tofauti na hali ilivyo kwenye kundi la vijana, vijana wanahitaji mabadiliko ya haraka na ni wepesi kurubuniwa au kununuliwa tofauti na kina mama.
Kwa mantiki hiyo hili wimbi la mizozo na malumbano yanayojitokeza kati ya UVCCM na makada maarufu wa CCM kunaweza kukiweka salama chama hicho endapo kitachukua maamuzi magumu ya kusema kuwa UVCCM wanapaswa kupigwa chini na chama hicho kikaamua kubaki na jumuiya mbili muhimu.
Inawezekana ushauri ninao utoa utaigusa sana CCM na kuona kuwa itakuwa vigumu kukiendesha chama hicho bila kuwa na umoja wa vijana kumbe mambo sio hivyo ni wazi kuwa ili kurudisha madhumuni na kanuni za kuundwa kwa umoja huo basi vijana wanapaswa kuangaliwa upya.
Kwa mtazamo wa kawaida hawa vijana wanaoendesha malumbano kila kona tena bila kufuata vikao halali vya kichama na ushirikishaji wa wajumbe wote katika maamuzi hawakijengi chama chao wala jumuiya yao kwa kuwa hawana uwezo wa kuwatafutia Watanzania rais wanayemhitaji wao.
Ni vigumu kuamini kuwa vurumai zote hizi zinazosikika, kuandikwa na kurushwa na vyombo vya habari kuwa zina lengo la kumtafuta Rais wa CCM wa mwaka 2015 hizo tunaweza kuziita kuwa ni ndoto za alinacha na hakika umoja huo hauna nguvu,wala tone la chembe ya kumpata rais atakayegombea kwa tiketi ya chama hicho.
Ni wazi kuwa malumbano hayo yanawapumbaza wenyewe kwa wenyewe kwa kuwa wapo watakaokomea mwaka 2013, sharti likiwa ni umri kuwa hawawezi tena kugombea nafasi yoyote katika jumuiya hiyo mwaka huo na harakati zao za kumpigia debe rais wanayemhitaji zitakuwa zimegonga mwamba.
Vijana wanapaswa kujipambanua katika sura tofauti kwa maana kuwepo kwao ndani ya chama hicho lazima kuendane na mabadiliko waliyonayo vijana wengine nje ya chama hicho hasa nikiamini kuwa idadi kubwa ya vijana wanakimbilia kambi ya upinzani na ndio walioweza kuviunga mkono vyama vya siasa (upinzani) na kusababisha matokeo yaliyokuwepo.
Hali hiyo inaonyesha wazi kuwa UVCCM hawakisaidii sana chama chao kupata ushindi isipokuwa wamekuwa wakifanya kazi ya kusimika makundi ya kimtandao na kusababisha viongozi wa CCM wakose ustahimilivu ndani yake kutokana na wimbi la makundi ya kisiasa yanayoasisiwa na vijana tofauti na zilivyo jumuiya mbili zilizopo.
Ndani ya kundi la UVCCM kuna ombwe kubwa la ajira na ili waweze kukidhi matakwa yao ni dhahiri kuwa wanajigawa vipande vipande kwa kuwa wapambe wa baadhi ya makada wa CCM wenye nyadhifa serikalini, wafanyabiashara wakubwa walioamua kuwa wanasiasa na viongozi wastaafu kwa nia ya kupanga safu wanayoitaka ili waweze kupata chochote.
Naamini kutokuelewana kunakoonekana hivi sasa ndani ya umoja huo ni ulaji, hakuna zaidi wamelemazwa kidogo kidogo kupewa posho kwa ajili ya kuwa kampenia viongozi wanaowataka na sasa tabia hiyo imeota mizizi mibaya kiasi kwamba wengine wasiojua ukomo wao wa uongozi kuwa ni mwaka 2013 wanampanga rais wa mwaka 2015.
Dalili hizi na nyingine nyingi ndizo zinazoweza kuifanya CCM iamue au iwe na maamuzi magumu kuhusu kuwepo kwa UVCCM au kufutwa kwa lengo la kubadili mfumo na muundo wa kichama kuliko kuwa na jumuiya pinzani ndani ya chama mama hasa nikiamini kuwa jumuiya za chama si vyama vya siasa, havijasajiliwa na msajili wa vyama vya siasa hizo ni idara tu ndani ya chama.
Kwa kuwa CCM wanakabiliwa na uchaguzi mkuu mwakani basi nawashauri wautumie muda huo kujiangalia upya na sioni kama chama hicho kikongwe kinaweza kupungukiwa kitu kama kitaamua kuwatosa vijana na kuwa na wanachama waadilifu na makini wasiotoka ndani ya jumuiya hiyo kwani mwana CCM ataendelea kuwa hivyo na kuwa kijana ni umri pengine umri wa vijana kichama uongezwe ili kuweza kukidhi matakwa ya watu wazima ndani yake.
Ndiyo maana nasema hivi sioni na sitegemei kama CCM inaweza kutetereka endapo itaamua kutokuwa na jumuiya ya vijana na kama kuna umuhimu huo basi mjipange upya, ukanda na ukabila umeanza kuota mizizi, sisi wa Pwani tunasema hivi, Tabora hivi, Arusha hivi, Tanga hivi mwishowe CCM itakuwa na jumuiya za vijana kimkoa na si kitaifa tena, bora nini?
 
CCM na gombania goli
ban.blank.jpg


Deus Bugaywa​

amka2.gif
BAADHI ya mafarisayo walipomtuhumu Bwana Yesu kwamba anatoa pepo kwa uwezo wa Mkuu wa pepo, yaani Belizebuli, aliwaambia kuwa utawala unaofitinika wenyewe kwa wenyewe hauwezi kusimama.
Alitaka kumaanisha kwamba haiwezekani mamlaka moja ikawa na matokeo yanayokinzana halafu ikaendelea kuwa moja, yaani kuwa na pepo wanaowavuruga watu halafu kuwa na nguvu ya kuwaondoa na kuwafukuzia mbali pepo hao, nguvu hizi haziwezi kukaa pamoja.
Nimelazimika kuanza na mfano huu ili kueleza hali ilivyo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa sasa, tofauti zilizomo ndani ya chama hicho zimekisaidia chama hicho kujenga nyufa ambazo zinasababisha wanachama na viongozi mbali mbali wa chama hicho kufitiniana wao kwa kiwango cha ajabu.
Chama chochote tunaambiwa, ni mkusanyiko wa watu wenye itikadi moja na malengo yanayofanana, wananchi hawa wanaweza kutofautiana kwa namna ya kuyafikia malengo yao na hata jinsi ya utekelezaji wa kile wanachokiamini pamoja.
Lakini cha msingi zaidi ni kutoruhusu tofauti hizo kuwagawa mpaka kwenye malengo ya msingi, ikitokea hivyo chama hicho kinabaki kikundi tu cha watu ambao hata ukiwauliza wanataka nini na kwanini wako pamoja hawawezi kukupatia jibu la uhakika. Chama siyo jina au kusanyiko la watu tu, hivyo ni vitu vya ziada sana, uhai wa chama ni itikadi inayowaunganisha wanachama, ni lazima wawe na kitu muhimu na cha maana kinachowaunganisha, kama wanaungana kwa sababu ya kuungana tu au kwa sababu ya maslahi hiyo ni zaidi ya hatari kwa uhai wa chama hicho.
Ni ukweli ulio wazi kwamba tofauti za wana CCM sasa zimefikia kiwango cha kugusa malengo ya msingi ya chama hicho, na hapa ndipo hatari kwa mustakabali wa chama hicho ilipo.
Wenyewe wanasisitiza kwamba lengo la kuu ni kuchukua dola, inaonekana sasa wametimiza malengo yao na hivyo wanataka kuvuna kutokana na kuwa katika madaraka.
Lakini kumbukumbu zinatuambia kwamba malengo ya msingi ya awali ya CCM ile iliyopotelea tusikokujua, yalikuwa na kumkomboa Mtanzania kutoka katika unyonge uliomfanya kuonewa, kunyanyaswa na kuteswa.
Unyonge wa maradhi, ujinga na umaskini ndiyo yalikuwa malengo ya msingi ya chama hiki hapo awali ambayo kilizaliwa ili kuleta ukombozi huo. Na kwa kuwa wazazi wake TANU na ASP waliasisiwa ndani ya ukoloni, ndiyo maana wakapigania uhuru kwa nguvu zote.
Malengo, hata hivyo hayakuwa uhuru kama uhuru, ilikuwa uhuru upatikane ili tuwe na mamlaka yetu wenyewe ambayo yataweza kutuwezesha kupanga namna ya kujikomboa kutoka katika unyonge wetu kama taifa.
Ndiyo maana baada tu ya uhuru, maadui waliotangazwa walikuwa ni wale wale ambao ndio kiini cha unyonge wetu kama taifa na hao ni ujinga, umaskini na maradhi. Hawa hawakutangazwa kwa bahati mbaya, yalikuwa ni malengo ya msingi ya kuanzishwa kwake.
Ndiyo, maana hata misingi yake ililenga katika kuyatekeleza haya. Usawa wa binadamu ndio ulikuwa msingi wa kwanza ili kuwawezesha watu kuthaminiana wao kwa wao na kuondoa tofauti zao ili waweze kukusanya nguvu zao kwa msingi kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
Kusema kweli daima na fitna mwiko, kutumia cheo kwa manufaa ya umma, kujiendeleza kwa kadri ya uwezo kwa ajili ya manufaa ya jamii nzima, na zaidi sana rushwa kuwa ni mwiko, kutotoa wala kupokea rushwa.
Haya ndiyo yaliyoifanya CCM iwe ilivyokuwa, maadili ya viongozi yalitaka kuwafanya viongozi watambue kwamba wanapokuwa katika dhamana wanakoma kuwa watu binafsi, wanakuwa ni taasisi, na wenye wajibu mkubwa zaidi kwa jamii kuliko watu wengine kwa sababu wameaminiwa na kupewa majukumu ya kuongoza njia.
Hapa kilipo leo CCM kimetupa misingi mingi iliyokianzisha na badala ya vyeo kuwa dhamana sasa ni dili na mitaji ya watu. Ugomvi na mivutano yote tunayoiona, vijana kuwakosea adabu wazee wao, wazee kwa wazee kukoseana adabu hayatokani na kitu kingine chochote isipokuwa uroho na tamaa ya madaraka.
Uongozi katika Tanzania kwa sasa ni moja ya biashara nono na kubwa, zinazolipa bila jasho, kuwa kikaragosi wa kiongozi fulani kunakufanya na wewe unakuwa bosi wa vikaragosi wezako. Ndio maana tunaona watu ambao tulitambua wana akili na uwezo wa kujisimamia ghafla wanakuwa na akili za kushikiwa.
Wanafanya kitu siyo kwa sababu wanaamini katika kitu hicho isipokuwa kwa sababu anayewalipa ndiye anataka, wamejigeuza vinubi ambavyo mpigaji wake analazimika kuimba wimbo changuo la aliyemlipa, na kwa sababu ya njaa na upofu wa tamaa ya ukwasi wa haraka wanaimba hata nyimbo ambazo ni marufuku kwenye jamii yao.
Tunaambiwa wapo baadhi yao ambao wametambua makosa yao ya kuwachafua wenzao na wamejirudi wamekwenda kuomba radhi au wengine wanajuta kwanini walijiingiza huko, lakini hiyo ndiyo kawaida ya majuto huja baada ya mambo kuhaharibika.
Haya yote maana yake ni dalili za kukosa kitu kinachowaunganisha kwa dhati ya itikadi zao, chama kinaonekana sasa hivi ni kundi kubwa la watu lakini ambao wana malengo tofauti sana, na tofauti zake ni kama giza na nuru.
Kundi moja liko tayari kulihariia au hata kudhuru kundi jingine kwa gharama yeyote ili ili mradi lisiwaharibie.
Chama sasa kimeligeuza taifa hili kama mpira wa gombania goli, kila mtu anataka afunge yeye, kwa sababu goli la mtu mwingine yeye halimsaidii hata kama ni mwanachama mwenzake, badala yake linaweza hata likamletea shida kubwa.
Ndiyo maana hakuna uchezaji wa kitimu, hakuna kupeana pasi kwa wachezaji wa timu moja, badala yake wanalambana buti wao kwa wao.
Mpira akiupata winga wa kushoto anamgeukia beki kulia wa timu yake anamlamba chenga na kumchungulia alipo mlinda mlango wake ili atikise nyavu, na akifunga anashagilia kuliko hata timu pinzani.
Huyu beki naye akipata mwanya wa kumdhibiti winga wa timu yake anahakikisha akimchapa buti siyo ya kugugumia tu na maumivu kidogo halafu arudi uwanjani, anamkata buti itakayompeleka nje ya uwanja kwa wiki kadhaa au hata ikibidi ‘kwa msimu' mzima wa ligi.
Hiki ndicho kiwango cha kufitinika kwa wana CCM wa leo, wamekuwa maadui wao kwa wao zaidi kuliko hata walivyo na vyama vingine.
Bila shaka unaweza ukamwita mtabiri, lakini kwa aina ya mtu aliyekiasisi chama na kukilea, Mwalimu Nyerere alijua wazi kwamba chama kimezika misingi iliyokuwa inakifanya kisimame ndio maana aliona dalili za anguko kuu la chama mapema.
Ingawa wenyewe wanafarijiana kwamba migogoro na kutofautiana ni sehemu ya ukomavu wa demokrasia na kwamba migogoro ndani ya chama hicho haijaanza leo, ni kweli hayo yote ni sahihi, lakini kwa hali ilivyo sasa kama hakutatafutwa mbinu mpya inayokwenda na mahitaji ya mazingira ya sasa.
Kwa hali halisi ilivyo ndani ya CCM inahitaji kiongozi jasiri kwa maana halisi ya neno jasiri, kukemea na kuchukua hatua kali ngumu na nzito kukihuisha chama, la sivyo muda si mrefu kitakuwa cha upinzani.
Sipendi kuwapa wana CCM matumaini na faraja za hewani, bila hatua za namna hiyo, hali ya kufitiniana ndani ya chama chao zina kila dalili za kuashiria mwanzo wa mwisho wa chama chao, la waamue kuchukua hatua za haraka na za makusudi kukinusuru.
Mungu ibariki Tanzania.


h.sep3.gif

0754 449 421, drbugaywa@yahoo.com
 
Vijana CCM ni hatari kwa usalama wa nchi
ban.bamdogo.jpg


Innocent Nganyagwa​

amka2.gif
BABA wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema kuwa CCM legelege, itazaa nchi legelege. Huu ulikuwa kama utabiri wake kutokana na yale aliyokuwa anayaona yanatokea ndani ya chama hicho tawala tangu tupate uhuru.
Wapo ambao hawakuamini lakini kwa wenye kufuatilia kwa karibu siasa za Tanzania, wanajua kuwa utabiri huo unatimia hivi sasa.
Hamkani hali si shwari nchini. Kuna matukio ya kutisha kuhusiana na matukio kadhaa na malumbano yanayoendelea ndani ya chama tawala na pia baina ya wapinzani na wanaharakati kwa upande mmoja na serikali pamoja na makundi mengine kwa upande wa pili.
Mpaka sasa haujapatikana aina ya uongozi wenye uwezo wa kukemea na kusikilizwa. Matokeo yake kila mtu amegeuka kuwa msemaji na mrekebishaji wa wale anaodhani kuwa wamepotoka.
Mambo hayo kwa kiasi kikubwa yanalifanya taifa lote linaonekana kuwa limepotoka na hakuna mwenye uwezo wa kushika hatamu na kulipeleka kule kunakostahili.
Taifa linayumbishwa na mambo mengi lakini haya yanayofanywa na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na baadhi ya makada wake, yanaonyesha dhahiri kuwa si tu serikali, bali pia chama hicho tawala sasa kimekosa umadhubuti kwenye uongozi.
CCM imeshindwa kabisa kudhibiti au ikiwezakana kuzima kabisa malumbano yasiyo na tija baina ya UVCCM na baadhi ya makada. Ni moja ya dalili kuwa wale wanaopaswa kukemea ni sehemu ya malumbano hayo.
Na kwa sababu wao ni sehemu ya malumbano hayo, wanaogopa kusema kwani wanaofahamu undani wake wanaweza kuwasuta iwapo watajitokeza hadharani na kukemea upande wowote.
Lakini yanayotokea sasa si ya kuyachekelea tena kwani yanahatarisha usalama wa Tanzania kama taifa. Wapo ambao malumbano haya yalipoanza tuliamua kuangalia bila kutoa ‘hukumu' kwa yanayotokea.
Lengo hasa lilikuwa ni kutaka kujua kiini hasa cha malumbano hayo. Wiki hii inayomalizika, kiini kimewekwa wazi.
Kwa walioisoma taarifa ya UVCCM mkoani Arusha, iliyotolewa baada ya kikao cha kamati ya utekelezaji ya mkoa huo, watakuwa wameshapata mwanga sasa kuwa kumbe kinachogombaniwa hapa ni urais wa 2015.
Jambo baya ambalo limejitokeza kupitia taarifa hiyo ya vijana wa mkoa wa Arusha ni kuwa katika jitihada zao za kutaka kukemea mgawanyiko baina ya wale wanaoshabikia watu mbalimbali wanaoonekana kufaa kuteuliwa na CCM kuwa wagombea baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wake.
Nao wamejitumbukiza kwenye dhambi hiyo ya mgawanyiko, tena wamejiingiza kwa namna ambayo inaonyesha kukemea kwao kulikwua ni unafiki tu.
Kwa kuwa walikuwa wamegubikwa na upofu wa kutetea mgawanyko wa kikanda, wakajikuta wakilumbana na wenzao wa mkoa wa Pwani labda bila kujua kuwa wanachokifanya ni kujiweka uchi kuliko hao wenzao waliodhani kuwa wanawakemea.
Baraza la UVCCM Arusha linasema limesikitishwa na maneno yaliyotolewa na wenzao kuhusu mgombea urais 2015. Wanawaonya wenzao kwa kauli zilizotolewa wakianza kuhubiri siasa ya kibaguzi wa makabila kwa kutoa matamko kwamba Rais 2015 asitoke kanda ya kaskazini.
Lakini wanapaswa kugeuza hili na kujitazama wenyewe. Ninachokiona hapa ni kuwa kwa kuwa wao ni wa kaskazini, basi wanatetea rais atoke kaskazini. Inajidhihirisha hili kwenye tamko lao hilo.
Wameorodhesha historia ya walikotoka marais walioongoza Tanzania. Wanasema rais wa kwanza (Nyerere) alitoka Kanda ya Ziwa; Rais wa pili (Mwinyi) alitoka Kanda ya Pwani; rais wa tatu (Mkapa alitoka kanda ya kusini na rais wa nne wa sasa anatoka Kanda ya Pwani.
Wanahitimisha kuwa kufuata mtiririko huo, ni zamu ya kanda ya kaskazini hivi sasa kutoa rais. Mtirirko huu wa mawazo unaanza kunitia woga.
Hapa ndipo wanapopaswa kujiuliza; kama wanaosema kuwa rais hapaswi kutoka kaskazini wana dhambi ya ubaguzi, kwa nini wale wanaosema kuwa rais anapaswa kutoka kaskazini nao wasiwe na dhambi hiyo hiyo?
Kwenye tamko lao wana mnukuu Mwalimu Nyerere wakisema kuwa alionya dhidi ya kuendekeza migawanyiko ya aina hii.
Lakini nadhani wanaamini kuwa onyo hilo haliwahusu wao kwani wamewanyooshea wengine vidole vya lawama kwa kitendo ambacho na wao wamekifanya bila ya wao kujielekezea kidole cha lawama.
Ukichukulia na uamuazi wa baraza hilo kumsimamisha mmoja wa wajumbe wake kwa sababu ya kumsema vibaya mmoja wa makada maarufu wa chama hicho, kwa ujumla wake, ni dhahiri sasa kuwa yale yaliyokuwa yakizungumzwa kama tetesi kuwa UVCCM si moja tena, yamejidhihirisha.
Wengine tulidhani kuwa baada ya tamko la kiongozi wa UVCCM mkoani Pwani, basi Baraza Kuu la UVCCM lililofanyika Dodoma siku chache baadaye, lingetumika kusawazisha mambo ili kuleta maelewano ndani ya chombo hicho ambacho kihistoria kimetoa mchango mkubwa katika ukombozi na maendeleo ya nchi yetu.
Lakini kilichotokea hapo ni kupanuka kwa migawanyiko na hivi sasa watu wameanza kutafutana roho zao kwani yule aliyesimamishwa Arusha tayari ameshalalamika kuwa maisha yake yapo hatarini kutokana na misimamo yake ndani ya Umoja huo.
Kupingana kwao ndani ya chama chao inaweza kuwa alama ya kukua kwa demokrasia ndani ya chama lakini hoja wanazozitoa zinapingana kabisa na misingi ya demokrasia.
Hoja za kuonyesha kuunga mkono mgawanyiko wa nchi kwa ukanda na masuala ya kutishia maisha ya wengine kwa sababu tu mmetofautiana kimtazamo, si masuala ambayo yanaweza kuelezwa kuwa ni ya kidemokrasia. Hawa wana lao jambo.
Wakati huu ambapo viongozi wakuu w chama tawala wameshindwa kutoa uongozi unaopaswa ili kuipa nchi mwelekeo unaofaa, tulidhani kuwa vijana hawa ndio wangeshika hatamu na kuonmgoza njia.
Lakini wamekuja kututhibitishia kuwa kumbe nao ni sehemu ya kushindwa kwa uongozi wa juu. Mipasuko iliyoanzia juu imeshuka hadi chini kiasi kwamba vijana nao sasa wamegawanyika kila mmoja akitetea kanda yake. Najiuliza katika hali kama hii, mi muda gani umebakia kwa Tanzania kuendelea kuwa moja?
Tunahitaji mabadiliko ya haraka kama tunataka kusalimika.
 
Mzee wa upako usitupumbaze, tuna hoja za kumweleza Kikwete
ban.blank.jpg


Abdul Juma​

amka2.gif
NAWASHUKURU wasomaji wangu wote ambao mliniandikia kunipa maoni yenu kuhusu makala yangu ya juma lililopita yaliyosomeka: "Kuyavumilia haya ni kujiongezea matatizo."
Hakika nimeguswa sana na michango yenu. Na kusema kweli ni vigumu kuandika kila alichokisema mtu, yawezekana nisimalize.
Lakini katika mengi mazuri lipo zuri kupita yote. Naomba kunukuu ujumbe wa msomaji wangu mmoja kutoka wilayani Kahama.
"Kaka wewe ni chemchem ya fikra mpya, hakika unatufungua macho na napendekeza kolamu yako iitwe ‘fikra mpya'," ndivyo ulisomeka ujumbe huo.
Kweli nimehamasika na kufurahishwa jinsi wananchi wamepata mwamko wa kusoma na kusikiliza vyombo vya habari ili kujua mustakabali wa nchi yao.
Hivyo katika utangulizi wangu wa leo, naomba kuwafahamisheni kuwa uwanja wetu huu utajulikana kwa jina jipya la "Fikra mpya". Kweli mawazo yenu ndiyo yatafanikisha fikra hizo.
Mada yangu leo itamhusu mtumishi wa Mungu maarufu kama Mzee wa Upako, ambaye ni mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Anthony Lusekelo.
Sikuwa na mpango wa kumjadili kiongozi huyu wa kiroho ila kauli yake ya karibuni imenisukuma kujitokeza kumpa neno kuwa aache kutupumbaza, kwani tunazo sababu za kumlaumu Rais Jakaya Kikwete.
Sina hakika kama mchungaji anajua kuwa Kikwete si Mungu bali ni binadamu kama sisi ambao tumempa jukumu la kutuongoza, hivyo akishindwa ni lazima tumhoji ilikuwaje?
Mungu hatumjui, maana hatujawahi kumuona bali tunaamini tu kuwa yupo. Tumejikuta tulivyoumbwa na huyo Mungu wala hakuna aliyemfikia na kuomba aumbwe, kwa hivyo hatuwezi kuhoji hilo.
Lakini kwa Rais Kikwete ni tofauti, yeye alijitafakari akahisi anaweza kutuongoza, hivyo kupitia chama chake cha CCM alikuja kutuomba tumchague atimize yale aliyoahidi kufanya.
Sasa kuna kosa gani ikiwa wananchi wanahoji ahadi zao Rais? Mchungaji Lusekelo anataka tuseme tu ameni kama kanisani ilihali tunaona mambo ni magumu?
Kwa kuwa huyu ni mtumishi wa Mungu basi naomba apime kauli zake upya kwa kutumia ‘busara'. Tafsiri ya neno busara ni akili au werevu wa kuweza kufikiria na kuamua kutenda jambo linalofaa.
Kweli tuamini kuwa busara ya mchungaji Lusekelo ni kuwaona Watanzania wakiimba nyimbo na mapambio ya kumsifu Rais Kikwete wakati wakiogelea kwenye dimbwi la kero zisizo na ukomo?
Kwa akili ya kawaida na pengine kwa kumsaidia mchungaji Lusekelo ni kwamba Rais akichaguliwa tunamtegemea atende mazuri, hivyo hatupaswi kumsifia bali kumkumbusha pale ambapo amekosea.
Lakini mwanzoni mwa wiki hii, mchungaji Lusekelo aliibuka kwenye vyombo vya habari akisema eti wanaompinga Rais Kikwete katika utawala wake wapo katika ushindani lakini hawatashinda katika vita hiyo.
Katika kile alichokiita Afya ya Amani, Umoja, Upendo na Uvumilivu, Mchungaji Lisekelo alisema kuwa ili nchi iwe na afya inahitaji matunzo na si kelele za kulaumiana.
Alisema kulaumiana kumeshika kasi tangu Rais Kikwete ashike madaraka kwa miaka mitano lakini mazuri aliyoyafanya hayasemwi bali mabaya ndiyo yanayozungumzwa hata kama yamejificha.
"Unapojenga afya ya kitu chochote ni lazima ujue misingi ya nchi ni lazima tuheshimu na kuwapenda viongozi wetu tuliochagua na kuwapigia kura.
Akaongeza kuwa hata katika maandiko kiongozi anatakiwa aonywe kwa hadhari, heshima na hekima na si kwa makelele.
"Utawala ni mamlaka inayowekwa Mungu lakini inaashiria wazi kuwa tumeanza kuondoka katika misingi hiyo na sasa mtu yeyote anasimama na kumsema Rais Kikwete anavyotaka," alisema Mchungaji Lusekelo.
Akahoji, inakuwaje Rais Kikwete tunayemfahamu aliingia madarakani akiitwa Masia na chaguo la Mungu leo ni adui wa kwanza?
Kwa mahaba yake, anaamini kuwa hali hiyo inatokana na wachache wanaomsaidia rais kuiacha CHADEMA kuwa na nguvu na kuiacha CCM kuwa dhaifu.
"Hivi sasa kukitokea tatizo kama la kutonyesha mvua basi lawama atatupiwa Rais. Nina imani kuwa rais atakayekumbukwa maishani ni Rais Kikwete," alisema Mchungaji Lusekelo.
Hivyo ndivyo anavyoamini kiongozi huyo ambaye hataki tumwambie rais wetu kuwa giza limetuchosha, ufisadi unatukera chukua hatua, bei za bidhaa zimepanda kuliko kipato chetu.
Afya ya amani, upendo, mshikamano anayoihubiri Mchungaji Lusekelo haiwezi kupatikana katika taifa ambalo lina matabaka makubwa mawili ya wenye nacho na wale wasio nacho.
Nakubaliana na Mzee wa Upako kuwa anayo haja ya kutukataza tusimlalamikie Rais matatizo yetu kwa kuwa yeye si sehemu ya matatizo tunayokabiliana nayo.
Yeye hatembei tena kwa daladala akaona uchungu wa kupanda kwa nauli, kipato kinachotokana na kazi yake ni kikubwa kiasi kwamba maumivu ya gharama za mahitaji muhimu hayapati kama sisi.
Lakini kwa upeo wake alionao Mchungaji Lusekelo, sikutegtemea kama anatoa kauli tata kama ile.
Mara anasema kipindi cha Kikwete lawama zimezidi, hatutashinda vita hiyo na eti wasaidizi wa Rais waiacha CHADEMA itanue na CCM imedhoofike.
Hapa ni bora Mzee wa Upako angejitambulisha wazi kuwa ni mwana-CCM maana si dhambi. Kama alikuwa na hoja angepaswa kujihoji ni kwanini alaumiwe Kikwete kati ya marais wanne waliopita?
Kwa kujihoji swali hilo, falsafa yake asingeitumia kututisha kuwa hatutashinda vita ya kumlalamikia Rais Kikwete bali angetutia faraja na hamasa kuwa tumwombee atimize ahadi zake bila kuogopa mafisadi.
Kama kuimarika kwa CHADEMA kunamtisha na kumuuma Mchungaji Lusekelo, inafaa awe shujaa wa kukisaidia chama chake cha CCM kijirudi na kujivua udhaifu ili kirejeshe mvuto kwa wananchi.
'Kioo cha mtu ni mtu' wanasema wahenga. Kumbe sisi tunaoona udhaifu wa Rais Kikwete na kumweleza wazi ni waungwana kuliko unafiki anaotaka tufanye Mchungaji Lusekelo wa kupongeza kila kitu.
Kanisani tunasema ameni kwa kila kitu kwa kuwa ni imani zaidi lakini kama tungepewa mamlaka ya kuhoji,basi sadaka zingehojiwa zaidi. Kwenye siasa hakuna ameni wala ndiyo mzee tena. Tafakari.
 
Madai haya ya udini hayana mashiko
ban.wazo.jpg


Juvenalis Ngowi​

amka2.gif
JUMA lililopita niliandika makala ambapo pamoja na mambo mengine nilikuwa nikiuliza mambo kadhaa kuhusu ziara alizokuwa akizifanya Rais Jakaya Kikwete. Kama kawaida nilipata maoni mbali mbali. Ningekuwa mtu wa ajabu kama ningetarajia watu wote tuwe na maoni yanayofanana.
Dunia haiwezi kusonga mbele kama sote tutakuwa na mtazamo unaofanana katika mambo yote. Hivyo maoni yanayotofautiana na maoni yangu huwa nayapa heshima na uzito unaostahili.
Hata hivyo katika makala iliyopita nilipata maoni kutoka kwa msomaji mmoja ambaye kwa hakika alinishangaza na hata kunishtua. Mtu huyo alinitumia ujumbe ambao mimi sikuona unaendana kabisa na mada niliyokuwa nimeijadili.
Mtu yule alinitumia ujumbe akisema kwamba udini ndio ulisukuma kuandika niliyoandika. Nilipigwa na butwaa. Lakini baada ya kuangalia matukio machache yaliyokuwa yametangulia nilianza kupata picha halisi. Kwamba kuna watu wachache wanaodhani kwamba wakosoaji wa serikali hii wanaikosoa kwa sababu ya dini binafsi ya Rais Kikwete.
Hizi fikra hazina maana yoyote zaidi ya uzushi na propaganda za kisiasa zinazopandikizwa na baadhi ya watu. Nina sababu kadhaa za kushangaa kwa nini kikundi kidogo cha watu wanaotaka kuweka udini katika hoja za kisiasa.
Makala ile ilihoji hivi kumekuwepo na tija gani au matokeo gani chanya kutokana na ziara za Rais Kikwete? Huu ni mfano mmoja. Hivi hili swali lina udini ndani yake? Dini ya Rais inaingiaje hapa? Lakini urais ni taasisi.
Hata kama yalikuwa matakwa binafsi ya Rais Kikwete kufanya ziara zile, bado ni ziara ya kitaasisi kwa maana ya uandaaji na hata utekelezaji.
Haiwezekani ikawa waandaaji na watekelezaji wa ziara hizi za Rais wote wakawa watu wa dini moja. Kwa vyovyote ni mchanganyiko wa watu ambao hatudhani kwamba wameteuliwa kwa vigezo vya dini zao. Tunapohoji umuhimu wa ziara hizi tunawataka wote wanaohusika watuambie manufaa ya ziara hizo na sababu zake.
Hapo kuna udini gani? Hoja dhaifu kabisa. Wapo wachache waliotofautiana na mimi kwa vigezo vingine. Hao naheshimu mawazo yao hata kama sikubaliani nayo. Ukiniambia kwamba ziara hizo zinaleta hamasa ya utendaji, wakati hiyo ni hoja ya kujadili.
Lakini ukinipinga kwa kusema swali langu linasukumwa na udini inabidi tuhoji uzalendo na udini wako!
Kati ya mambo ambayo yanapaswa kuangaliwa kwa uangalifu mkubwa ni mambo yanayogusa imani. Kwa sababu za kisiasa, kuna watu ambao wamefanikiwa kuwateka watu na kutaka kutumia udini ili kufikia malengo ya kisiasa.
Bahati mbaya kuna watu wamemeza propaganda za uongo na sasa udini unaanza kuonekana kama hatari kubwa kwa taifa letu. Kundi dogo sana la watu wamefikia mahali pa kuthubutu kusema kwamba wakosoaji wa serikali ya sasa, wanakosoa kwa sababu ya dini binafsi ya Rais Kikwete. Haya ni mambo ya ajabu sana.
Binafsi nilianza kuandika makala zangu katika gazeti hili tangu lilipoanzishwa. Wakati huo Rais alikuwa ni Benjamin Mkapa. Sikuwahi hata mara moja kuandika makala za kuisifu serikali kiasi kwamba kuna watu ambao nadhani ni mashabiki wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikuwa wakiniuliza ikiwa serikali haijafanya jambo lolote jema.
Hili nalo ni swali la kizushi. Kwani unapokosoa haina maana kwamba hakuna mazuri. Kuna sababu za msingi za kuandika makala za kukosoa serikali badala ya kuisifu. Moja ya sababu hizo ni kwamba serikali inapotekeleza wajibu wake, haistahili kusifiwa kwa kuwa huo ndio wajibu wake.
Serikali kama taasisi inakusanya kodi kutoka kwa wananchi na ina wajibu wa kuzitumia kwa manufaa ya watu. Hivyo sioni mantiki ya kuisifu serikali kwa kujenga barabara, kusambaza maji na kutoa huduma nyingine yoyote ya kijamii kama afya na elimu. Kinyume chake ni kwamba tuna haki ya kuikosoa serikali pale inaposhindwa kutekeleza wajibu wake huku ikikusanya kodi. Katika mazingira haya udini unatokea wapi? Huu ni uchovu wa mawazo.
Maoni ya msomaji wangu huyo kwamba makala zangu zinasukumwa na udini zilinikumbusha makala ya Maswali Magumu ambapo mwandishi Ansbert Ngurumo alihoji ikiwa hao wanazungumzia udini leo wanataka kutuambia kuwa Rais Kikwete alichaguliwa kwa Uislamu wake?
Hili ni swali la msingi sana kuwahoji wale wote wanaodanganya kwamba wakosoaji wa serikali hii wanasukumwa na udini. Rais Kikwete alipata ushindi wa zaidi ya asilimia hamsini katika uchaguzi uliopita. Je, wanataka kutuambia asilimia 62 ya wapiga kura hao walikuwa waislamu? Je, waliobaki ndio dini nyingine?
Hivi ni kweli kabisa mtu anaweza kusema rais amechaguliwa na waislamu peke yao? Jibu sahihi ni kwamba kwa kuangalia idadi ya kura alizopata Kikwete na mgawanyo wa maeneo alikopata kura hizo ni wazi kabisa kwamba rais amechaguliwa na watu wa dini mchanganyiko.
Labda kama watu hawa wanataka kutuambia kwamba matokeo yalitengenezwa. Hivyo ikiwa Rais Kikwete alichaguliwa na watu wa dini tofauti kwa nini leo hii wajitokeze wachache wadhani kwamba kuna dini hazimpendi Rais kwa ajili ya dini yake? Huu ni ukichaa!
Hata hivyo hao wanaodai kwamba serikali sasa inashambuliwa kwa sababu Rais ni Mwislamu pia watakuwa wavivu wa kusoma. Hivi ni kweli Hawakumbuki serikali ya Ben Mkapa ilishambuliwa mara ngapi? Mkapa binafsi amewahi kushutumiwa mara ngapi? Hivi analalamikiwa kwa sababu ya dini yake?
Madai ya ubinafsishaji usio sawa ni kitendo ambacho hakina uhusiano na dini ya mtu.
Vivyo hivyo watu wanapolalamikia ugumu wa maisha hawalalamikii dini ya mtu. Watu tunapohoji migongano ya mtazamo ndani ya serikali moja hatujadili dini ya mtu, tunajadili tukio na madhara yake.
Watu tunapojadili matokeo mabaya ya kidato cha nne hatujadili dini ya mtu. Tunapojadili kuhusu haki za kujieleza na demokrasia kuminywa hatujadili dini ya mtu. Tunajadili mambo ya kitaifa ambayo yatamfaa mtu yeyote bila kujadili dini yake.
Leo hii tukianza kufikiria kila kinachofanyika kinafanywa na mtu wa dini gani huenda hatutafika mbali sana. Itafika mahali watuhumiwa watamkataa hakimu au jaji asiye wa dini yao. hatujafika pabaya sana lakini tunaelekea pabaya.
Idadi ya watu wenye mawazo finyu ya kupinga mambo kwa kuangalia imani ya mtu ni wachache sana na tuna uwezo wa kuwaelimisha watu wetu ili wasinase kwenye mtego wa wanasiasa wasio na haya walio tayari kutumia imani za watu kulinda masilahi yao bila kuangalia hasara tutakayoipata kama taifa kwa ajili ya upuuzi wa kuleta hisia za kidini.
Kama dini fulani ina matatizo ambayo yanaweza kuwa yamesababishwa na historia au mfumo uliokuwepo, kuna haki ya dini kukutana na kujadili kuhusu matatizo husika. Hapo sio udini. Dini zina haki ya kukemea na kuonya. Watanzania wengi wana dini zao na viongozi wa dini wana heshima kubwa katika jamii. Viongozi hao wakionya sio udini. Tuepuke kunaswa na mtego wa udini.
 
UVCCM wanalaumiwa kwa lipi?
ban.nyamaza.jpg


Salehe Mohamed​

amka2.gif
VIONGOZI wa Jumuiya ya Vijana ya Chma Cha Mapinduzi (UVCCM) hivi sasa wanakabiliwa na shutuma kubwa kutoka ndani na nje ya chama chao kwa madai ya utovu wa nidhamu.
Wanaowalaumu vijana hao wanajenga hoja kuwa hawastahili kutoa kauli za kuwadhalilisha viongozi waliostaafu na wale waliomo ndani ya chama chao ambao wamekuwa wakikosoa chama na serikali.
Wajengaji wa hoja hiyo wanasema watoto hao wamefuka mikapa, hawana adabu na wenye kupaswa kuadhibiwa ikiwemo kuifuta Jumuiya hiyo ambayo hivi sasa inadaiwa kuendeshwa kwa masilahi ya watu fulani.
Binafsi sioni sababu ya kulaumiwa kwa vijana hao kwa kuwa kila wanachokifanya ama kimetokana na kutumwa au malezi ya wazazi wao (CCM).
Kwa yoyote mwenye kuitazama CCM kwa takriban miaka 10 sasa atakiri kuwa UVCCM hawajakosea kitu kuwasema wakubwa zao bali walichokiongeza ni ujasiri wa kutoka hadharani.
Tujiulize kama mawaziri wa serikali hiyo waliweza kubishana hadharani tena wengine kwa lugha za kudhalilishana na hawakupewa karipio lolote, kwa nini UVCCM wasifuate mkondo huo?
Tatizo kubwa ninaloliona mimi ni kwamb Watanzania wengi huwa hawapendi kufikiria chanzo cha tatizo fulani bali hutafuta njia za kulitatua
Kutatua tatizo bila kushughulikia lilikoanzia ni kujidanganya, UVCCM walishaona, kulambishwa na kupendezewa na siasa za kuchafua, kutishiana na nyinginezo kutoka kwa wakubwa zao, leo hii watashindwaje kuziendeleza huku wakiwa wameziboresha zaidi?
Nasema UVCCM hakuna walichokikosea hata pale waliposema mgombea wa urais wa chama hicho kwa mwaka 2015 anamjua Rais Kikwete, walikuw sahihi kusema hivi sasa ni zamu ya mikoa ya kaskazini kutoa kiongozi mkuu wa nchi.
Nani kasema walifanya ubaguzi wa eneo, kabila? Kama walifanya kosa si tungemuona au kumsikia Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Mkamba akitoa karipio?
Tumemsikia Makamba akimzungumzia Sumaye, Lowassa na makada wengineo ambao walijaribu kufungua mdomo wao kukielekeza chama nini cha kufanya kulingana na mazingira ya wakati huo.
Hawakukosea, wanajua Mwenyekiti wao wa taifa Rais Jakaya Kikwete, ni mpinga udini, ukabila, u-maeneo, lakini walijua hawezi kusema neno lolote wao wakitamka au kuamua.
Wanamjua mwenyekiti wao ni mkali pale inapoonekana ubaguzi wa dini, maeneo unakiathiri chama hicho na kupendelea kwa wapinzani, lakini ni mpole mambo hayo yanapokinyookea chama chake.
Hawajasahau kuwa mwaka 2005, mwenyekiti wao ‘alibebwa' na viongozi wa dini waliouaminisha umma kuwa yeye ni chaguo la Mungu, waliona pia mwenyekiti wao alivyokuwa mkali mwaka jana baada ya baadhi ya viongozi wa dini kuonekana kukataa ‘kumbeba'
Wanajua mwenyekiti wao na makada wengine walilazimika kutumia madai ya uwepo wa udini kwenye vyama na wagombea fulani ili kuvidhoofisha na kuipa mwanya CCM kuendelea kutawala
Hawa waliona mwaka 2005, Rais Kikwete alipoaambiwa ni chaguo la Mungu, kijana na sifa nyinginezo huku wapinzani wake wakipewa sifa za kuiba mashamba, fedha na wengine kuhusika na mauaji ya viongozi wa zamani.
Walikuwa miongoni mwa watu waliotaka kusikia hatua zilizochukuliwa kwa wale wote walioshiriki kwenye rafu, lakini hakuna adhabu iliyotolewa kwa wahusika, UVCCM walijifunza jambo na sasa wameanza kazi.
UVCCM wanajua utamu wa fedha wanazopewa kuwachafua, kuwakampenia watu fulani, wanajua CCM si moja, hakuna mwenye uwezo wa kuwakemea kwa sababu kila mmoja wanayajua madhambi yake.
Wakubwa wao nao wanayajua wanayoyafanya, hawataki kuwakanya UVCCM kwa hofu ya kufichuwa siri zao, katika mazingira kama haya tunawalaumu kwa lipi vijana hawa wanaochumia matumbo?
Wanaotoa mawazo ya UVCCM ivunjwe, wanajidanganya, kitu hicho hakiwezi kufanyika kwa kuwa vigogo wa chama hicho wamejificha nyuma ya jumuiya hiyo na wanaendesha mambo yao kwa kivuli cha vijana hao.
Katika mazingira kama hayo sioni kosa la UVCCM, ila naona hatari ya kuja kuwa na viongozi wabovu zaidi ambao wametokana na fedha na hila.
Siamini hata kidogo kama mnyukano unaotokea hivi sasa ndani ya jumuiya za CCM utaweza kuwatoa viongozi safi na waadilifu watakaokuwa mstari wa mbele wa kuteta masilahi ya wananchi,
Si tumeshawasikia vijana hawa wakisema kuwa viongozi wa zamani wameshakula na wamevimbiwa, waachie vijana nao wale. Tunawezaje kumpata kiongozi safi kama vijana wanafikiria kula au kumuingiza madarakani mtu mwenye kujali kula yao?
Tusiwalaumu vijana hawa kwa utovu wa nidhamu bali tuwalaumu baba, mama, walezi wao kwa kutokuwa waadilifu kiasi cha tabia zao kuigwa na vijana wao.
Tusidanganyane UVCCM ni kioo cha CCM, kama chama hicho ni kichafu kamwe kioo hakiwezi kuonyesha usafi, kitaonyesha taswira halisi iliyopo.
Njia bora ya kukifanya kioo kionyeshe usafi ni kwa mhusika kuwa msafi na wala si vinginevyo, UVCCM hawajakosea, wasilaumiwe
 
Kikwete anahangaika asipinduke
ban.mchokonozi.jpg


Charles Mulinda​

amka2.gif
KATIKA siku za karibuni, nimekuwa na kawaida ya kukaa kimya kila ninapoona uwezekano wa kuwepo au kutokea jambo kubwa, liwe zuri au baya linalowahusu marafiki zangu wa karibu ambao wote ni watu wakubwa sana katika taifa letu. Kisa! Sitaki ugomvi nao.
Akili yangu ya kichokonozi imenielekeza kuwa heri niwe mnafiki kwa kukaa kimya, nikiyafumbia macho mambo ya kipuuzi kabisa ya rafiki zangu ili niweze kuishi kwa raha mustarehe kuliko kuwa kiherehere mtetezi wa wachokonozi wasiopenda kutumia mbongo zao sawasawa kupembua wapi wanapigwa changa la macho na wapi wanaambiwa ukweli.
Kwa akili zilizokamilika, nimegundua kuwa Watanzania walio wengi ni wachovu wa kufikiri – nawaomba radhi kwa kuwaambia ukweli huu ambao nina uhakika nao kwa asilimia zinazozidi mia moja - Wanaendesha maisha yao kwa kufuata mkumbo.
Wakilishwa maneno leo na wapayukaji kuwa mchokonozi ni fisadi, hawana muda wa kufikiri na kuhoji amefisadi nini na ushahidi wa kumtia hatiani kwa dhambi hiyo uko wapi! Wataamini hivyo mradi aliyesema ni mpayukaji.
Hii ni moja ya sababu za msingi za mimi kuamua kukaa kimya nikifumbua macho mambo ya hovyo ya marafiki zangu kwa sababu wanaotendewa hivyo nao ni wa hovyo. Wanastahili kutendewa hivyo.
Kwa wale nilionao karibu; ninatambua kuwa staili yangu hii si njema, siwatendei haki marafiki zangu hawa kwa kutowaambia ukweli ninaoujua kabla mambo yao hayajaharibika au kuwa mazuri.
Kwa hawa nieleze kuwa nimelazimika kujenga utamaduni huu kwa sababu mara kadhaa hapo awali nilipokuwa nikiwajuza yajayo mbele, walinicheka, kunidharau na hata kufikiria kunishughulikia kwa dhambi ya kuwa mkweli mno kwao.
Sikuona sababu ya kuvuruga uhusiano mzuri wa kidugu nilio nao na marafiki zangu hawa kwa sababu tu ya kuwa kiherehere wa kuropoka kila jambo jema ninaloliona ambalo wao hawataki kulisikia. Na wala sikuona sababu ya kukosa maulaji ambayo wao ndiyo wagawaji kwa sababu ya kuwaudhi wakati ninaowapigania ni mbumbumbu kuliko ‘mzungu wa reli.'
Hata hivyo, urafiki unashinda udugu. Nimeshindwa kuvumilia na roho unaniuma mno ndani kwa ndani kwa jinsi wenzangu hawa wanavyotekeseka kwa kutoujua ukweli wa mateso waliyonayo sasa wakati kila aina ya utukufu wanayo.
Kwa sababu ya huruma niliyonayo kwao, leo baada ya kimya changu cha muda mrefu na hasa baada ya kuona rafiki yangu kipenzi, rais Jakaya Kikwete, anaanza kubinuka akielekea kuanguka kwenye kiti alichokikalia.
Nimeona ni busara kumfikishia ujumbe wangu wa kichokonozi kabla hajafika sakafuni ili kama anaweza atumie mbinu za kiintelenjensia za kichokonozi kukiiunua kiti chake na kukikalia sawasawa bila kujali kama kitakuwa kimeenda upande. Muhimu aweza kukaa na kuonyoosha mgongo.
Nitoe angalizo mapema kwa wasiopenda kusoma au kusikia ukweli kuwa si lazima waamini maandishi yangu haya. Najua wapo kwa sababu hakuna jamii isiyokuwa na vipofu au viziwi. Hawa wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye roho ngumu kuusoma ukweli huu na kuuamini.
Ninafanya hivi kwa sababu leo nitathubutu japo kwa uchache kuandika ukweli ambao unahitaji kuwa na roho ya kiuendawazimu kuusema mbele ya watu wanaotumia akili za wengine kufikiri.
Naanza; taifa letu liko katika kipindi kizuri mno cha kuelekea kwenye mageuzi makubwa ya kiuongozi ambayo hayawezi kuepukika kwa namna yoyote ile au kwa gharama yoyote ile. Na mageuzi haya yamefanikishwa kwa kiwango na mbinu za kiitelenjensia za hali ya juu zilizotumiwa au zinazotumiwa na rafiki yangu sana Rais Kikwete mwenyewe au watu wake wa karibu. Tafadhali mtu asinibishie katika hili.
Vyovyote iwavyo, chama chetu cha maulaji, kiko katika hatua za mwisho za kuendelea kushika hatamu za kuliongoza taifa letu kikiwa katika umoja wake wa sasa. Kinaweza kwa kudra za Mwenyezi Mungu ninayemuamini sana kuendelea kuwepo madarakani iwapo tu kitawaganyika, lakini si vinginevyo.
Nimepata kuandika mara kadhaa kwa lugha laini kabisa katika safu hii miaka michache nyuma kuwajuza Watanzania kuwa mapinduzi ya kweli ndani ya CCM yataletwa na rafiki yangu Rais Kikwete kwa kukiua kabisa chama hicho au kukigawa vipande vipande ambavyo vitakinyima nguvu kiliyonayo kwa sababu kwa aina ya viongozi kilionao sasa kinakosa sifa ya kuendelea kuwa chama tawala.
CCM inayoongozwa na watu wa aina ya Yusuph Makamba, kiongozi asiyeona taabu kukwaruzana na viongozi wenzake wakiwemo wakuu wa dini na anayeamini katika siasa za kizamani za kutafuta ushindi wa chama chake kwa mabavu. John Chiligati, mwanajeshi wa zamani ambaye matamshi yake hupingana na uhalisia wa mambo.
Bila kuwasahau George Huruma Mkuchika, mzee anayezungumza mambo asiyoyajua na kijana wao Tambwe Hizza asiyejua anapaswa kusema nini kwa wakati uliopo, haiwezi kuwa chama tawala katika zama hizi za kizazi cha taifa wa watu wa kuhoji, wanaochambua kila neno kwenye sentensi zinazotolewa na watawala na kutoa maana yake halisi.
Nimetaja kwa uchache sababu za watu hawa kukosa sifa za kuwa viongozi wa CCM katika zama hizi lakini ninazo lundo na kama yupo anayetaka kujua zaidi, akinitaka kufanya hivyo, sitasita.
Lakini inatosha nikieleza kuwa ni hawa na wengineo wengi ndiyo waliokifisha CCM kilipo sasa. Ni hawa wanaosababisha Kikwete aanze kupinduka katika kiti alichokikalia.
Misuguano ya kipuuzi na shutuma wanazorushiana sasa makada wa chama chetu zinachagizwa na watu hawa ambao hawajui kuwa dhamana walizonazo katika chama chetu, matamshi yao yanaweza kuwa njia ya kukipeleka chama shimoni.
Ninaamini Rais Kikwete anajua kuwa watu hao ni tatizo, alikwisha kuambiwa mara nyingi na yeye mwenyewe anaona mwenendo wa chama kikiwa chini ya wasaidizi wake hawa, lakini kwa sababu ya kile ninachokiamini kuwa anataka kife au kigawanyike, amewaacha waendelee kufanya kazi yao mahususi ambayo sasa inaonekana kwa kila mtu.
Ndiyo maana yuko kimya! Akiwaacha vijana wake wampiganie kwa kulinda hadhi ya jina lake dhidi ya wale wote wanaotishia kulichafua.
Tuendelee; wakati huu Rais Kikwete anapotoa matamshi yanayoashiria kuhangaika kujishikiza huku na kule ili asipinduke katika kiti alichokikalia, moyoni hayuko salama. Nafsi yake inajutia uamuzi wa kuwakumbatia wale waliojiita wapambaji wa ufisadi wakati hawana sifa hiyo.
Watu waliojipachika jina hilo na kutenda matendo yanayofanana na jina hilo kinafiki ili wapate nafasi ya kuwa naye karibu na kutumia mwanya huo kumdhoofisha yeye na serikali yake.
Na sababu ya kufanya hivi ni ile ile kuwa hata wao wanautaka ukubwa alionao.
Hapa, kosa kubwa la Rais Kikwete ni kutishwa na kukubali kutishika na mbwembwe za kijivuni za wanasiasa wa aina ya Samuel Sitta, waliofanikiwa kupata wafuasi kibao nyuma yao, ambao kwa mtizamo wangu ni wale wasiotumia akili zao kufikiri sawasawa.
Sitta amefanikiwa kuwarubuni watu hawa kwa silaha ya upambanaji na ufisadi jambo ambalo lilimtisha Kikwete baada ya jinsi Siita anavyoungwa mkono kiasi cha kulazimika kumuingiza katika ufalme wake huku akijua fika hayuko naye.
Sitta, mwanasiasa ambaye mimi binafsi sijapata kumuunga mkono tangu alipochaguliwa kuwa Spika wa Bunge la tisa kwa sababu ambazo hata yeye mwenyewe anazijua, moja kubwa ikiwa ni kama Tanzania ina mafisadi, yeye hawezi kukosa katika orodha yao, ni mmoja wanasiasa wanaoliyumbisha taifa, serikali na rais mwenyewe kwa kiwango cha hali ya juu.
Wala siandiki haya kwa kubahatisha, ninamaanisha ninachokiandika na ninaweza kuyatetea maandishi yangu haya katika mahakama yoyote hapa duniani pasipo kuhitaji wakili. Kwa sababu za kiintelijensia nabaki nayo moyoni kwanza nikivuta pumzi ya muda muafaka wa kuyawasilisha.
Rais Kikwete anapohangaika sasa kuizungumzia Dowans na dada yake Richmond kwa Watanzania kuhusu namna ya kujinasua na zigo la kutolipa zawadi ya mabilioni baada ya serikali yake kushindwa mahakamani, anajua kuwa kwa namna moja au nyingine ni Bunge lililokuwa chini ya Sitta lililosababisha Dowans ikimbilie mahakamani na hatimaye kushinda kesi hiyo.
Ni Bunge la Samuel Sitta, kwa sababu za kishabiki na unazi wa kisiasa liliibebea mbeleko hoja ya Edward Lowassa kuwa mhusika muhimu wa kashfa ya Richmond huku likikubali mambo mengine lililowaaminisha Watanzania kuwa ni machafu zaidi yaliyogunduliwa na kamati yake teule iliyochunguza sakata hilo yawekwe kapuni kwa sababu ya kuilinda serikali yote isianguke.
Kwa maana nyingine ni kwamba, Mchokonozi yeyote anaweza kutafasiri kuwa ilikuwa sawa kwa Bunge la Samuel Sitta kumtosa Lowassa na kumuacha akianguka kivyake lakini si Kikwete. Na hata watuhumiwa wengine wa sakata hilo walipotaka kueleza wanachokijua kuhusu kashfa hiyo, Sitta kwa kofia yake ya uspika alikataa! Kisa kumlinda Kikwete.
Kama hiyo haitoshi, Lowassa hata alipojaribu kueleza anayoyajua kwa upande wake kuhusu mkasa huo katika kituo cha Televisheni ya Taifa nako aligonga mwamba.
Picha iliyojitokeza hapo ni kwamba Lowassa hakupaswa kujitetea na Watanzania wakasikia utetezi wake kwa kuhofia kuwa angeweza kumchafua Kikwete.
Kitu ambacho mimi ninaamini Kikwete hakikuijua ni kuwa Sitta hakumlinda bure, alitegemea ujira wa namna yoyote ile na ama alikuwa na malengo yake. Moja kubwa ni hili la kutambua dhambi za mwenye nyumba na kuzitumia kumgaragaza.
Jambo la pili ambalo hakulijua wakati ule ni kwamba siku zote muosha huoshwa, hivyo wakati Dowans wakidai mabilioni yao na Sitta na wenzake wakitoa kauli kuwa malipo hayo yasifanyike, rais Kikwete anapaswa kujua kuwa bado ana deni la kuzungumza ukweli wa anachokijua kuhusu mkasa huo.
Vinginevyo hata atoke vipi kuhusu Richmond hakuna Mtanzania atakayemuelewa ingawa anaweza kupunguza kidogo jazba za watu waliochoka kimaisha kama atafanikiwa kupigana kuhakikisha malipo hayo hayafanyiki, jambo ambalo kwa hakika hata kwetu sisi ma-bush lawyers haliwezekani.
Ni jambo lisiloingia akilini kwa rais anayesimamia utawala wa sheria, sheria inapoonekana kuuma upande wa watu waliomlinda, anabadilika, anaapa kupigana kuhakikisha kuwa sheria hiyo inapunguza makali yake au inapindishwa. Jambo ambalo nina hakika halitamsaidia.
Kwa faida ya rafiki rais Kikwete nimkumbushe kuwa, niliwahi kumshauri hapo awali kuwa ili ajivue kashfa ya Dowans na dada yake Richmond anapaswa kuilazimisha kamati teule ieleze iliyoyaficha kuhusu serikali yake na yeye mwenyewe binafsi.
Leo naongezea ushauri mwingine mgumu kidogo kuwa ili kupata suluhisho la kudumu la kashfa ya Richmond ni lazima tulipe deni la Dowans, baada ya kulipa tuanze sasa kumtafuta mtu halisi aliyesabasha utata wa Richmond hadi Dowans aliyotupeleka mahakamani na kutushinda.
Kwa Watanzania tulizoea kufunga mikanda iwe nyakati za Idd au Pasaka, bilioni hizo si nyingi kiasi cha kupiga kelele kwa nguvu kubwa eti tusilipe.
Na ili tusipige kelele sana tunapaswa kutambua kuwa wakati tunanunua kilo ya sukari sh 2,000 wakubwa wanaanza kukutana wiki ijayo huko Dodoma kwa vikao vinavyosindikizwa na kahawa nyeusi nzito ya maziwa ambayo sukari ruksa kujimimia na kutengeza chai yenye utamu za asali.
Na wakati bei ya daladala ikizidi kupaa huku bwana Mkulo (Waziri wa Fedha na Uchumi) akiwaambia Watanzania wabebe misalaba yao, mashangingi ya wakubwa yanatumia mafuta ya mabilioni kuwatembeza hapa na pale katika kipindi hiki kigumu cha Watanzania kulala na njaa.
Yeyote atakayefikiria haya kesho ataungana na mimi kumshauri Rais Kikwete aharakishe kuilipa Dowans ili Watanzania wachukie. Ikiwa hivyo, ili kuwapoza atalazimika kuunda tume huru ya kuchunguza mbivu na mbichi za kashfa hiyo ambayo siku inatangaza ripoti yake atakuwa anashangiliwa na kutangazwa kuendelea kuwa rais bila kupingwa itakapofika mwaka 2015.
Itaendelea wiki ijayo.
 
Kikwete anahangaika asipinduke
ban.mchokonozi.jpg


Charles Mulinda​

amka2.gif
KATIKA siku za karibuni, nimekuwa na kawaida ya kukaa kimya kila ninapoona uwezekano wa kuwepo au kutokea jambo kubwa, liwe zuri au baya linalowahusu marafiki zangu wa karibu ambao wote ni watu wakubwa sana katika taifa letu. Kisa! Sitaki ugomvi nao.
Akili yangu ya kichokonozi imenielekeza kuwa heri niwe mnafiki kwa kukaa kimya, nikiyafumbia macho mambo ya kipuuzi kabisa ya rafiki zangu ili niweze kuishi kwa raha mustarehe kuliko kuwa kiherehere mtetezi wa wachokonozi wasiopenda kutumia mbongo zao sawasawa kupembua wapi wanapigwa changa la macho na wapi wanaambiwa ukweli.
Kwa akili zilizokamilika, nimegundua kuwa Watanzania walio wengi ni wachovu wa kufikiri – nawaomba radhi kwa kuwaambia ukweli huu ambao nina uhakika nao kwa asilimia zinazozidi mia moja - Wanaendesha maisha yao kwa kufuata mkumbo.
Wakilishwa maneno leo na wapayukaji kuwa mchokonozi ni fisadi, hawana muda wa kufikiri na kuhoji amefisadi nini na ushahidi wa kumtia hatiani kwa dhambi hiyo uko wapi! Wataamini hivyo mradi aliyesema ni mpayukaji.
Hii ni moja ya sababu za msingi za mimi kuamua kukaa kimya nikifumbua macho mambo ya hovyo ya marafiki zangu kwa sababu wanaotendewa hivyo nao ni wa hovyo. Wanastahili kutendewa hivyo.
Kwa wale nilionao karibu; ninatambua kuwa staili yangu hii si njema, siwatendei haki marafiki zangu hawa kwa kutowaambia ukweli ninaoujua kabla mambo yao hayajaharibika au kuwa mazuri.
Kwa hawa nieleze kuwa nimelazimika kujenga utamaduni huu kwa sababu mara kadhaa hapo awali nilipokuwa nikiwajuza yajayo mbele, walinicheka, kunidharau na hata kufikiria kunishughulikia kwa dhambi ya kuwa mkweli mno kwao.
Sikuona sababu ya kuvuruga uhusiano mzuri wa kidugu nilio nao na marafiki zangu hawa kwa sababu tu ya kuwa kiherehere wa kuropoka kila jambo jema ninaloliona ambalo wao hawataki kulisikia. Na wala sikuona sababu ya kukosa maulaji ambayo wao ndiyo wagawaji kwa sababu ya kuwaudhi wakati ninaowapigania ni mbumbumbu kuliko ‘mzungu wa reli.’
Hata hivyo, urafiki unashinda udugu. Nimeshindwa kuvumilia na roho unaniuma mno ndani kwa ndani kwa jinsi wenzangu hawa wanavyotekeseka kwa kutoujua ukweli wa mateso waliyonayo sasa wakati kila aina ya utukufu wanayo.
Kwa sababu ya huruma niliyonayo kwao, leo baada ya kimya changu cha muda mrefu na hasa baada ya kuona rafiki yangu kipenzi, rais Jakaya Kikwete, anaanza kubinuka akielekea kuanguka kwenye kiti alichokikalia.
Nimeona ni busara kumfikishia ujumbe wangu wa kichokonozi kabla hajafika sakafuni ili kama anaweza atumie mbinu za kiintelenjensia za kichokonozi kukiiunua kiti chake na kukikalia sawasawa bila kujali kama kitakuwa kimeenda upande. Muhimu aweza kukaa na kuonyoosha mgongo.
Nitoe angalizo mapema kwa wasiopenda kusoma au kusikia ukweli kuwa si lazima waamini maandishi yangu haya. Najua wapo kwa sababu hakuna jamii isiyokuwa na vipofu au viziwi. Hawa wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye roho ngumu kuusoma ukweli huu na kuuamini.
Ninafanya hivi kwa sababu leo nitathubutu japo kwa uchache kuandika ukweli ambao unahitaji kuwa na roho ya kiuendawazimu kuusema mbele ya watu wanaotumia akili za wengine kufikiri.
Naanza; taifa letu liko katika kipindi kizuri mno cha kuelekea kwenye mageuzi makubwa ya kiuongozi ambayo hayawezi kuepukika kwa namna yoyote ile au kwa gharama yoyote ile. Na mageuzi haya yamefanikishwa kwa kiwango na mbinu za kiitelenjensia za hali ya juu zilizotumiwa au zinazotumiwa na rafiki yangu sana Rais Kikwete mwenyewe au watu wake wa karibu. Tafadhali mtu asinibishie katika hili.
Vyovyote iwavyo, chama chetu cha maulaji, kiko katika hatua za mwisho za kuendelea kushika hatamu za kuliongoza taifa letu kikiwa katika umoja wake wa sasa. Kinaweza kwa kudra za Mwenyezi Mungu ninayemuamini sana kuendelea kuwepo madarakani iwapo tu kitawaganyika, lakini si vinginevyo.
Nimepata kuandika mara kadhaa kwa lugha laini kabisa katika safu hii miaka michache nyuma kuwajuza Watanzania kuwa mapinduzi ya kweli ndani ya CCM yataletwa na rafiki yangu Rais Kikwete kwa kukiua kabisa chama hicho au kukigawa vipande vipande ambavyo vitakinyima nguvu kiliyonayo kwa sababu kwa aina ya viongozi kilionao sasa kinakosa sifa ya kuendelea kuwa chama tawala.
CCM inayoongozwa na watu wa aina ya Yusuph Makamba, kiongozi asiyeona taabu kukwaruzana na viongozi wenzake wakiwemo wakuu wa dini na anayeamini katika siasa za kizamani za kutafuta ushindi wa chama chake kwa mabavu. John Chiligati, mwanajeshi wa zamani ambaye matamshi yake hupingana na uhalisia wa mambo.
Bila kuwasahau George Huruma Mkuchika, mzee anayezungumza mambo asiyoyajua na kijana wao Tambwe Hizza asiyejua anapaswa kusema nini kwa wakati uliopo, haiwezi kuwa chama tawala katika zama hizi za kizazi cha taifa wa watu wa kuhoji, wanaochambua kila neno kwenye sentensi zinazotolewa na watawala na kutoa maana yake halisi.
Nimetaja kwa uchache sababu za watu hawa kukosa sifa za kuwa viongozi wa CCM katika zama hizi lakini ninazo lundo na kama yupo anayetaka kujua zaidi, akinitaka kufanya hivyo, sitasita.
Lakini inatosha nikieleza kuwa ni hawa na wengineo wengi ndiyo waliokifisha CCM kilipo sasa. Ni hawa wanaosababisha Kikwete aanze kupinduka katika kiti alichokikalia.
Misuguano ya kipuuzi na shutuma wanazorushiana sasa makada wa chama chetu zinachagizwa na watu hawa ambao hawajui kuwa dhamana walizonazo katika chama chetu, matamshi yao yanaweza kuwa njia ya kukipeleka chama shimoni.
Ninaamini Rais Kikwete anajua kuwa watu hao ni tatizo, alikwisha kuambiwa mara nyingi na yeye mwenyewe anaona mwenendo wa chama kikiwa chini ya wasaidizi wake hawa, lakini kwa sababu ya kile ninachokiamini kuwa anataka kife au kigawanyike, amewaacha waendelee kufanya kazi yao mahususi ambayo sasa inaonekana kwa kila mtu.
Ndiyo maana yuko kimya! Akiwaacha vijana wake wampiganie kwa kulinda hadhi ya jina lake dhidi ya wale wote wanaotishia kulichafua.
Tuendelee; wakati huu Rais Kikwete anapotoa matamshi yanayoashiria kuhangaika kujishikiza huku na kule ili asipinduke katika kiti alichokikalia, moyoni hayuko salama. Nafsi yake inajutia uamuzi wa kuwakumbatia wale waliojiita wapambaji wa ufisadi wakati hawana sifa hiyo.
Watu waliojipachika jina hilo na kutenda matendo yanayofanana na jina hilo kinafiki ili wapate nafasi ya kuwa naye karibu na kutumia mwanya huo kumdhoofisha yeye na serikali yake.
Na sababu ya kufanya hivi ni ile ile kuwa hata wao wanautaka ukubwa alionao.
Hapa, kosa kubwa la Rais Kikwete ni kutishwa na kukubali kutishika na mbwembwe za kijivuni za wanasiasa wa aina ya Samuel Sitta, waliofanikiwa kupata wafuasi kibao nyuma yao, ambao kwa mtizamo wangu ni wale wasiotumia akili zao kufikiri sawasawa.
Sitta amefanikiwa kuwarubuni watu hawa kwa silaha ya upambanaji na ufisadi jambo ambalo lilimtisha Kikwete baada ya jinsi Siita anavyoungwa mkono kiasi cha kulazimika kumuingiza katika ufalme wake huku akijua fika hayuko naye.
Sitta, mwanasiasa ambaye mimi binafsi sijapata kumuunga mkono tangu alipochaguliwa kuwa Spika wa Bunge la tisa kwa sababu ambazo hata yeye mwenyewe anazijua, moja kubwa ikiwa ni kama Tanzania ina mafisadi, yeye hawezi kukosa katika orodha yao, ni mmoja wanasiasa wanaoliyumbisha taifa, serikali na rais mwenyewe kwa kiwango cha hali ya juu.
Wala siandiki haya kwa kubahatisha, ninamaanisha ninachokiandika na ninaweza kuyatetea maandishi yangu haya katika mahakama yoyote hapa duniani pasipo kuhitaji wakili. Kwa sababu za kiintelijensia nabaki nayo moyoni kwanza nikivuta pumzi ya muda muafaka wa kuyawasilisha.
Rais Kikwete anapohangaika sasa kuizungumzia Dowans na dada yake Richmond kwa Watanzania kuhusu namna ya kujinasua na zigo la kutolipa zawadi ya mabilioni baada ya serikali yake kushindwa mahakamani, anajua kuwa kwa namna moja au nyingine ni Bunge lililokuwa chini ya Sitta lililosababisha Dowans ikimbilie mahakamani na hatimaye kushinda kesi hiyo.
Ni Bunge la Samuel Sitta, kwa sababu za kishabiki na unazi wa kisiasa liliibebea mbeleko hoja ya Edward Lowassa kuwa mhusika muhimu wa kashfa ya Richmond huku likikubali mambo mengine lililowaaminisha Watanzania kuwa ni machafu zaidi yaliyogunduliwa na kamati yake teule iliyochunguza sakata hilo yawekwe kapuni kwa sababu ya kuilinda serikali yote isianguke.
Kwa maana nyingine ni kwamba, Mchokonozi yeyote anaweza kutafasiri kuwa ilikuwa sawa kwa Bunge la Samuel Sitta kumtosa Lowassa na kumuacha akianguka kivyake lakini si Kikwete. Na hata watuhumiwa wengine wa sakata hilo walipotaka kueleza wanachokijua kuhusu kashfa hiyo, Sitta kwa kofia yake ya uspika alikataa! Kisa kumlinda Kikwete.
Kama hiyo haitoshi, Lowassa hata alipojaribu kueleza anayoyajua kwa upande wake kuhusu mkasa huo katika kituo cha Televisheni ya Taifa nako aligonga mwamba.
Picha iliyojitokeza hapo ni kwamba Lowassa hakupaswa kujitetea na Watanzania wakasikia utetezi wake kwa kuhofia kuwa angeweza kumchafua Kikwete.
Kitu ambacho mimi ninaamini Kikwete hakikuijua ni kuwa Sitta hakumlinda bure, alitegemea ujira wa namna yoyote ile na ama alikuwa na malengo yake. Moja kubwa ni hili la kutambua dhambi za mwenye nyumba na kuzitumia kumgaragaza.
Jambo la pili ambalo hakulijua wakati ule ni kwamba siku zote muosha huoshwa, hivyo wakati Dowans wakidai mabilioni yao na Sitta na wenzake wakitoa kauli kuwa malipo hayo yasifanyike, rais Kikwete anapaswa kujua kuwa bado ana deni la kuzungumza ukweli wa anachokijua kuhusu mkasa huo.
Vinginevyo hata atoke vipi kuhusu Richmond hakuna Mtanzania atakayemuelewa ingawa anaweza kupunguza kidogo jazba za watu waliochoka kimaisha kama atafanikiwa kupigana kuhakikisha malipo hayo hayafanyiki, jambo ambalo kwa hakika hata kwetu sisi ma-bush lawyers haliwezekani.
Ni jambo lisiloingia akilini kwa rais anayesimamia utawala wa sheria, sheria inapoonekana kuuma upande wa watu waliomlinda, anabadilika, anaapa kupigana kuhakikisha kuwa sheria hiyo inapunguza makali yake au inapindishwa. Jambo ambalo nina hakika halitamsaidia.
Kwa faida ya rafiki rais Kikwete nimkumbushe kuwa, niliwahi kumshauri hapo awali kuwa ili ajivue kashfa ya Dowans na dada yake Richmond anapaswa kuilazimisha kamati teule ieleze iliyoyaficha kuhusu serikali yake na yeye mwenyewe binafsi.
Leo naongezea ushauri mwingine mgumu kidogo kuwa ili kupata suluhisho la kudumu la kashfa ya Richmond ni lazima tulipe deni la Dowans, baada ya kulipa tuanze sasa kumtafuta mtu halisi aliyesabasha utata wa Richmond hadi Dowans aliyotupeleka mahakamani na kutushinda.
Kwa Watanzania tulizoea kufunga mikanda iwe nyakati za Idd au Pasaka, bilioni hizo si nyingi kiasi cha kupiga kelele kwa nguvu kubwa eti tusilipe.
Na ili tusipige kelele sana tunapaswa kutambua kuwa wakati tunanunua kilo ya sukari sh 2,000 wakubwa wanaanza kukutana wiki ijayo huko Dodoma kwa vikao vinavyosindikizwa na kahawa nyeusi nzito ya maziwa ambayo sukari ruksa kujimimia na kutengeza chai yenye utamu za asali.
Na wakati bei ya daladala ikizidi kupaa huku bwana Mkulo (Waziri wa Fedha na Uchumi) akiwaambia Watanzania wabebe misalaba yao, mashangingi ya wakubwa yanatumia mafuta ya mabilioni kuwatembeza hapa na pale katika kipindi hiki kigumu cha Watanzania kulala na njaa.
Yeyote atakayefikiria haya kesho ataungana na mimi kumshauri Rais Kikwete aharakishe kuilipa Dowans ili Watanzania wachukie. Ikiwa hivyo, ili kuwapoza atalazimika kuunda tume huru ya kuchunguza mbivu na mbichi za kashfa hiyo ambayo siku inatangaza ripoti yake atakuwa anashangiliwa na kutangazwa kuendelea kuwa rais bila kupingwa itakapofika mwaka 2015.
Itaendelea wiki ijayo.
Ndg Rutta pamoja na wadau wengine, wenye uchungu na nchi yetu ni kwa nini serikali ambayo tumeiajili kazi ya kutawala, kwa maana ya kumanage nchi yetu itutungie katiba ya kututawala!! Hivi mpango wa kuchakachua haujaisha bado??????????? Wanataka kuchakachua hata katiba???????? Kama hawatakuwa tayari kusikia wananchi wanataka nini kwenye katiba mpya, ni bora wanchi tukaingia barabrani kuandamano kudai watuachie tutayarishe katiba ya Taifa letu sio kina Philimon Luhanjo na JK tuliowaajiri kazi kwenye ofisi zetu za Ikulu. Hapo tutawafukuza kazi kama Misri. Serikali itulie yawepo mazingira ya kuundwa katiba mpya hatua kwa hatua. Je kuna mechanism zipi za kukusanya maoni ya wananchi na mahitajio ya wananchi kuunda katiba imara na time frame yake, sio zima moto kwa faida ya Taifa letu la Tanzania tulipendalo!!!!!!!!!! Tutumie kila mbinu ili serikali isiwe ndau mkuu kwenye huu mkakati, maana wanajua madhara ya katiba mpya watapoteza nafasi za ufisadi!!!!!!!!!Na mafisadi watashitakiwa maana Raisi hatakuwa na madaraka ya kusamehe wezi. Mfumo wa mahakama utakuwa independent na law enforcement institutions zitakuwa huru na nguvu ya kuinvestigate na kuprosecute bila kuuliza sijui nani wala kuingiliwa na mtu yeyote.
Serikali isijiingize kabisa kwenye kuandaa katiba mpya.Huandaliwe mswada wa kupinga serikali kujiingiza kwenye mkakati huo, upelekwe bungeni pia, kuondoa uwezekano wa wao kuteka hii shughuli. Tunao wataalamu wa katiba wanasheria, wadau mbali mbali from different sectors and institutions, wenye ujuzi wa kutengeneza katiba bora kwa taifa letu. Mbarikiwe.
 
Muswada wa Katiba, kipimo cha akili, busara kwa wabunge
ban.blank.jpg


Joseph Sabinus​

amka2.gif
TANZANIA ipo katika mfumo wa siasa wa vyama vingi tangu ulipoanza rasmi mwaka 1992 hapa nchini. Huu ni mfumo ulioakisi busara za mwasisi wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanzania.
Tayari ndani ya mfumo huu, vyama mbalimbali vya siasa vimeanzishwa na hata kushiriki katika chaguzi mbalimbali za kuanzia mwaka 1995, 2000, 2005 na wa Oktoba 31, 2010.
Licha ya ushindani na msikemshike wa kampeni kukitoa jasho Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni chama tawala, bado juhudi za vyama vya upinzani kukiondoa madarakani hazijafanikiwa.
Hazijafanikiwa kwani mwaka 1995, CCM ilifanikiwa kumtoa Benjamin Mkapa "aliyesimikwa" kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania . Mwaka 2000, kiti cha urais kikaendelea kukaliwa na Mkapa wa CCM.
Chaguzi za 2005 na 2010 zikampa madaraka Jakaya Mrisho Kikwete wa CCM.
Hata hivyo, kabla na baada ya chaguzi hizo, vyama vya upinzani na Watanzania kwa jumla, vimekuwa vikipaza sauti za kilio juu ya uchakachuaji jkatika mchakato mzima wa uchaguzi kiasi kwamba, kunakuwapo hofu kwamba baadhi ya watu wanapata "uongozi ingawa sio viongozi".
Katika ujumbe wa Kwaresima wa mwaka huu wenye kaulimbiu "ALIYE MKUBWA NA AWE MTUMISHI WENU" (Mt 20:26), maaskofu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), wanakiri kuwapo malalamiko hayo wakisema, "Ni matumaini yetu kuwa wale wanaohusika watachukua hatua kwa ujasiri, ukomavu na busara ili kuhakikisha kwamba dosari zilizojitokeza hazijirudii tena katika chaguzi zijazo."
Wanaongeza, "Kilio cha Watanzania wengi kwamba hawana imani na taasisi zinazosimamia uchaguzi, hakiwezi kuepukwa wala kubezwa kirahisi. Tunatoa wito kwa wahusika wote wasome alama za nyakati kwa hekima, wachukue hatua ili kurudisha imani ya Watanzania kwa taasisi hizo muhimu kwa ujenzi wa demokrasia ya kweli nchini na kudumisha amani na maelewano miongoni mwa Watanzania."
Miongoni mwa mambo yanayoliliwa na Watanzania hata kutaka kuundwa kwa Katiba mpya, ni pamoja na madaraka mengi aliyo nayo rais ikiwa ni pamoja na kuteua viongozi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na kwamba, hali hiyo ‘inaubaka' uhuru wa tume.
Aidha, mfumo wa utendaji wa baadhi ya vyombo, unatia shaka na kuleta kiu zaidi ya mabadiliko ya katiba. Kwa mfano, kwa kawaida, askari au watumishi wa vyombo vya usalama hawapaswi kufungamana na chama chochote cha siasa. Hilo halina ugomvi wala ubishi.
Mgogoro unakuja kwamba, wakuu wa mikoa (RC) na wilaya (DC), ndio wenyeviti wa kamati za ulinzi na usalama wa mikoa na wilaya hizo.
Wakati hali ikiwa hivyo kwamba wakuu hao wa mikoa na wilaya wakiwa ni wanachama na makada wa chama tawala (CCM), wakuu wa polisi wa mikoa (RPC) na wilaya (OCD) ndio makatibu wa kamati hizo za ulinzi na usalama katika mikoa na wilaya zao.
Kwa msingi huo, wakuu wa mikoa (RC) ndio mabosi wa wakuu wa polisi wa mikoa (RPC) huku wakuu wa wilaya (DC) kadhalika wakiwa mabosi wa wakuu wa polisi wa wilaya (OCD).
Hii inamaanisha kwamba, wakati wowote mkuu wa mkoa ambaye ni kada wa CCM akitumia kofia (cheo) ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, anaweza kumwita RPC na kumwagiza kuzuia shughuli za chama kingine cha siasa mathalani maandamano au mkutano kwa kisingizio cha tishio la ukosefu wa amani na utulivu kumbe anafanya hivyo kwa lengo la kukinufaisha chama chake. Mifano ya malalamiko ya namna hiyo ipo mingi.
Mfumo kama huu ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa wakurugenzi wa halmashauri za miji na wilaya kwa kuteuliwa ambao pia ndio wasimamizi wa uchaguzi katika wilaya zao, unazidi kutia "kigugumizi" na kuchochea hitaji la katiba mpya.
Hapo, linaibuka hitaji la katiba mpya; katiba isiyopora mamlaka kwa umma na kuyarundika kwa mtu mmoja; rais. Katiba inayoweza kutamka rasmi kuwa rais wa nchi asiwe na cheo katika chama ili rasilimali za umma, zisitumike "kukinenepesha" chama kimoja (chama cha rais).
Mfano, kumekuwa na malalamiko kuwa mfumo uliopo sasa umekuwa ukitoa mwanya kwa Rais wa Nchi ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, kutumia rasilimali za umma ikiwa ni pamoja na muda, walinzi na mambo mengine wakati akifanya shughuli za chama chake; jambo hili si haki kwa umma ambao si wanachama wa chama hicho.
Watu wanataka katiba inayotoa haki sawa katika uwanja wa siasa kwa watu na vyama vyote na sio katiba ambayo mwenye mpira anakuwa mchezaji, mshika kibendera na mwamuzi wa mchezo na kwamba pale ambapo timu yake inafungwa, eti basi achukue mpira na kuuweka kwapani kama wafanyavyo watoto katika viwanja vya "mchangani".
Inashangaza kuona kwamba licha ya maaskofu kutoa angalizo kwa wahusika kusoma alama za nyakati, bado macho ya wahusika (serikali) "yamevunja mkataba wa kuona" na kuzisoma alama hizo za nyakati.
Bado wanachokifanya, kinakaribisha wazo la mtu kudhani kuwa akili za baadhi ya watendaji nazo zimevunja mkataba wa kufikiri na sasa zimedumaa palepale kama kwamba zimenaswa na ‘superglue'.
Muswada wa mchakato wa kuanzisha katiba mpya unaopelekwa bungeni na serikali umeonesha ‘kuyatapika' matakwa yote ya wananchi.
Muswada huo uliochapishwa na Gazeti la Serikali, toleo No. 1 Vol. 92 la Machi 11, 2011, ni kama vile unafanya ubabe dhidi ya umma kwani wanayoyakataa wananchi, ndiyo yanabarikiwa na kumezwa na muswada huo, wakati yanayotakiwa na umma, ndiyo ‘yametapikwa' na kufungiwa nje ya muswada.
Serikali kupitia Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani ambaye ameandika maudhui na sababu za muswada huo Machi 8,2011, hawana budi kurudi tena mezani na wote waliouandaa muswada huo ambao Chama cha NCCR-Mageuzi kupitia Mwenyekiti wake James Mbatia kimesema umenakiriwa Kenya, ili usiwape Watanzania "nyoka" wakati wao wametaka samaki; wasiombe mkate, wakapewa jiwe na wala wasiombe kitumbua, wakapewa nge.
Serikali ijue kuwa watu wanataka Katiba mpya iliyo makini na sio iliyojaa mzaha, uvivu wa kufikiri, ubaguzi na kejeli kwa watu kama kwamba Watanzania hawana macho wala akili.
Katiba makini itokanayo na matakwa ya umma ni njia makini na ya uhakika ya kuchochea maendeleo ya watu na kudumisha amani.
Inashangaza kuona kwamba katika mazingira ambayo umma umekuwa ukipiga kelele na kulia dhidi ya mamlaka ya kupindukia aliyo nayo rais, ambayo ni kikwazo kwa maendeleo ya umma, serikali inaleta muswada wenye dosari nyingi zaidi.
Inatia shaka kuhusu viwango vya uelewa wa watu. Inatia shaka hata pale muswada unapompa rais mamlaka ya kuunda Tume ya kuongoza mchakato wa katiba bila kuhusisha Bunge na wadau wengine. Muswada unaiweka katiba mfukoni mwa rais na kuitoa mikononi mwa umma.
Muswada huu ni kipimo kizuri cha busara na akili za viongozi wetu kama kweli wanafanya mambo kwa utulivu, umakini, na bila kunakiri na kwa maslahi ya umma au kinyume chake.
Ni muswada unaoonekana kulenga kupima uelewa, busara na umakini wa wabunge. Watanzania wanataka waone Bunge la sasa ni kwa ajili ya Watanzania au ni Watanzania kwa ajili ya Bunge.
Wabunge na viongozi wa serikali! Tanzania itawalilia na hata tone la damu ya Mtanzania litakalomwagika kutokana na mzaha unaofanywa katika katiba inayotarajiwa kuundwa, utakuwa mtaji wa maswali ya vizazi vijavyo kwenu na pengine, mzaha huo unaweza kugeuka kuni au mkaa kuchoma makaburi yenu.
Hili litatokea endapo mtaangamiza maslahi ya taifa na kutanguliza maslahi ya "Uchama" au "Ubinafsi."
Ikumbukwe kuwa, aina yoyote ya spidi au uchakachuaji wa mchakato huo itakayopitishwa muswada huo usio na tija, bali hasara kwa umma, atakuwa inawachimbia kaburi Watanzania kwa kuchochea machafuko ya nchi. Hili hatulitarajii litokee maana wahenga hunena, mwenzio akinyolewa wewe tia maji.
Nasema hivyo kwani damu ya Waafrika inayomwagika kutokana na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ni nyingi na tayari imerutubisha ardhi kiasi cha kutosha na hata wale ndege na wanyama wala nyama kama fisi na mbwa mwitu, wamenenepa kiasi cha kutosha; Waafrika tuseme, "SASA BASI"
Hivi karibuni wakati akifungua warsha ya siku moja kwa waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba alisema, "Silaha hazitengenezwi Afrika lakini zinaingizwa na kuwaangamiza Waafrika kwa wingi kupitia uhalifu na migogoro ya nchi na nchi au wenyewe kwa wenyewe." "Tusiruhusu hali hii iendelee."
Katika hili la katiba, serikali ijue kuwa kama ni "janja ya nyani" tayari imejulikana. Watanzania sasa sio watu kudanganywa hovyo na kuchezewa akili zao kama mwanasesere maana fumbo mfumbie mjinga, mjanja huling'amua.
Ukosefu wa umakini na vitendo cha serikali kuchakachua mchakato huu wa Katiba, kinaonesha kuwa, serikali (Rais Jakaya Kikwete) hakuwa na nia ya dhati ya kuunda katiba mpya, bali amelazimishwa na mabadiliko ya Katiba mpya Zanzibar ili Katiba ya Jamhuri iyatambue mabadiliko ya Zanzibar kama nchi kamili.
Aidha, hili linaonesha kuwa kitendo cha Rais kutangaza kuridhia mabadiliko ya katiba hata kuuita mwaka 2011 kuwa ni mwaka wa katiba, kisha wataalamu wachakachue na kunakili mfumo wa yaliyofanyika Kenya, ni wazi Rais na watendaji wake "walidandia gari kwa mbele" bila kujua mwanzo wala mwisho wa safari; kwamba hawakujua mapana na marefu ya hoja ya Katiba mpya.
Ndiyo maana nasema, muswada wa mchakato wa huu wa kuunda katiba mpya, ni kipimo tosha cha akili na busara za wabunge.
 
JK, kampeni hii ‘itakula’ kwako!
ban.kalamu.jpg


Samson Mwigamba​

amka2.gif
TANZANIA tumeanza kushindanisha watu kwenye kugombea urais tokea mwaka 1995. Kwa lugha nyingine ni katika chaguzi kuu nne (1995, 2000, 2005 na 2010) ambapo tumeshuhudia nchini mwetu mtu akishindana na mtu ama watu katika kugombea urais.
Huko nyuma tulizoea kuona mtu akishindana na kivuli ambapo mpiga kura akitaka kuchagua mtu anatia alama ya vema upande wa NDIYO na kama hamtaki huyo mtu anachagua kivuli kwa kutia alama ya vema upande wa HAPANA. Lakini napenda kusema kwamba katika chaguzi zote zilizotangulia zile za mtu na kivuli na hata zile za mtu na mtu ama watu, hakuna uchaguzi ambao mmoja alifanya faulo kama ule wa mwaka jana 2010.
Kinachonitisha zaidi ni kwamba faulo hizo zilifanywa na mgombea wa chama tawala ambaye pia alikuwa rais hata wakati anagombea.
Najua wasaidizi wa Kikwete watamdanganya kwamba nimemkosea adabu ama kosa lolote ambalo wao wataamua kunipa. Lakini naomba niseme wazi kwamba uchambuzi wangu binafsi unanituma kwamba JK katika uchaguzi wa mwaka jana alicheza faulo nyingi lakini hii moja ambayo nitaijadili kwa kina leo ni faulo mbaya kuliko zote.
Naomba sasa nianze; Mkakati wa kwanza ulikuwa ni kumtambua adui yao mkubwa ambaye walikuja kumwona kwamba ni CHADEMA.
Hilo halina tatizo kabisa kwa maana kila mshindani anapaswa kumfahamu mshindani wake mkubwa kwa jina, uwezo wake, udhaifu wake, na kadhalika ili aweze kupanga vizuri mipango ya kumshinda. Tatizo langu na JK kile anachokifanya baada ya kugundua kwamba adui wao mkubwa ni CHADEMA.
Walianza na mkakati wa kukionyesha kwamba chama kile ni cha kikabila, wananchi wakawapuuza. Kimsingi hiyo ni faulo ambayo tumeizoea. Hata mwaka 1995 ilitumika sana wakati Lyatonga Mrema na NCCR-Mageuzi yake ilipoonekana tishio kubwa kwa chama tawala. Baadaye akasikika JK mwenyewe akidai kwamba watu wasikichague CHADEMA kwa kuwa ni chama cha msimu eti baada ya uchaguzi hawatakiona tena mpaka ufike uchaguzi mwingine. Hilo nalo likadunda maana mwenye macho haambiwi tazama. Watanzania ni mashuhuda wa dhati wa utendaji wa CHADEMA. Lugha nzuri ambayo inaweza kueleweka vema kwa watanzania wa leo ni kuwaambia kwamba CCM ni chama cha msimu, kwamba CCM wanajua sana kuongea vizuri na wananchi wakati wa uchaguzi lakini uchaguzi ukishapita wanatupa kila kitu wanasubiri uchaguzi ujao.
Lakini ni chama gani kimekuwa muda wote na wananchi kikiwapigania dhidi ya dhuruma na manyanyaso wanayoyapata kila kukicha? Ni chama gani kilikuwa na wananchi bega kwa bega mwaka hadi mwaka kuwaeleza ufisadi wote unaofanywa na vigogo mafisadi wanaojijali nafsi kuliko umma? Bila shaka ni CHADEMA. Ndiyo maana wito wa JK kwa wananchi kutoichagua CHADEMA eti kwa kuwa ni chama cha musimu, ulizidi kumgeukia yeye mwenyewe.
Wakaja na faulo ambayo wao waliiona kuwa kali zaidi na walidhani watakuwa wameimaliza CHADEMA na mgombea wake wa urais. Wakasema mgombea urais wa CHADEMA kaiba mke wa mtu.
Ikavuma sana kwenye vyombo vya habari kwa mkakati maalum ulioratibiwa na makada wa CCM. Kuna taarifa kwamba zilikuwa ni juhudi maalum za Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, kumtafuta kwa udi na uvumba aliyewahi kuishi na mwanamke ambaye hivi sasa ni mchumba wa mgombea wa CHADEMA. Taarifa zinazidi kueleza kwamba Makamba alikwenda mbali zaidi kwa kumpa yule bwana pesa na gari na kumwahidi kwamba wao watalipia gharama zote za wanasheria ili mradi tu yule jamaa afungue kesi ya kumshtaki mahakamani mgombea wa chadema. Lengo lilikuwa ni kumwaribia mgombea huyo siha yake mbele ya wananchi ili asichagulike. Ukitaka kulielewa hilo jiulize hiyo kesi imeishia wapi mbona haisikiki tena! Lakini hapo pia wakadunda.
Maana ni faulo ambayo wameitumia mara kadhaa huko nyuma. Mwaka 1995 Lyatonga Mrema akiwa tishio kwao waliwahi kusema kwamba kampa mimba mwanamke na kumtelekeza.
Yule dada akafungua hadi kesi mahakamani na hatimaye baada ya pilipilika za uchaguzi na mgombea wa CCM akatangazwa mshindi kesi imekufa. mwaka 2000 Prof. Lipumba akiwa tishio zaidi kwa Mkapa, ikavumishwa sana kwenye vyombo vya habari kwamba Lipumba hana mke ni aibu nchi kuongozwa na rais asiye na mke.
Mke wa Lipumba akajitokeza hadharani tena mzuri wa sura kuliko wa kwao (wakati huo). Wakafunga domo na kukaa kimya. Kwa hiyo faulo hiyo nayo dhidi ya mgombea wa CHADEMA mwaka jana ikagonga mwamba.
Ndipo mwisho JK akaja na silaha ya maangamizi ambayo kimsingi inamuua hata yeye lakini hakujali ili mradi afanikiwe kwanza kuingia Ikulu. Kutoka kusikojulikana tukashtukia tu JK anakuja na suala la udini.
Tuliposikiliza kwa makini tukagundua kwamba eti kwa sababu Dk. Slaa aliwahi kuwa padri basi mara kanisa katoliki ndo liko nyuma yake mara Wakristo ndo wako nyuma yake, basi tu ili mradi kila aina ya upuuzi ukawa unasemwa ili mradi kutimiza lengo lao.
Ingawa viongozi wa dini walijitahidi kueleza kwa kina kutokuhusika kwao na kampeni za kidini lakini JK hakutaka kulisikia hilo. Akasahau kwamba yeye mwenyewe ndiye amekuwa akilitegemea zaidi Kanisa Katoliki kuliko mtu mwingine yeyote.
Akasahau kwamba alisoma kwenye shule ya misheni na hakuna waziri wakati wa Mkapa ambaye amekuwa karibu na kanisa hilo kuliko yeye.
Ni yeye aliyekuwa anakuwa mgeni rasmi kwenye sherehe nyingi tu za Kanisa Katoliki. Ni yeye aliyekuwa mgeni rasmi kwenye sherehe mojawapo ya kiislamu mwaka 2005 akawaponda waislam na kuwataka wajitahidi kusoma na kuendesha shule nzuri kama Wakristo akiwaambia kuacha kuwasakama Wakristo kwa kuwa bila Wakristo yeye asingepata elimu nzuri aliyonayo eti kwa kuwa tu alisoma shule ya misheni.
Ni baada ya mambo yote hayo ndipo aliyekuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Methodias Kilaini, akasikika akisema Kikwete ni chaguo la Mungu. Nani sasa anayefanya kampeni za kidini. Haikuishia hapo, baada ya uchaguzi mkuu wa 2005 na tukiwa tunajiandaa na uchaguzi mkuu wa 2010, Kikwete akaalikwa tena kwenye mahafali ya chuo kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki. Wakiwa wameambatana tena na Askofu Kilaini na ambaye alisikika tena akisema bado kauli yake ya Kikwete ni chaguo la Mungu inasimama.
Akammwagia sifa kemkemu eti kwa kuleta utaratibu wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kudai eti utaratibu huo ni mzuri sana wa kuwakopesha hata wanafunzi wa vyuo vya binafsi na eti unafaa kuigwa Afrika Mashariki yote. Wakati huo niliandika makala nzima kumkosoa Askofu Kilaini. Nilimweleza kwamba mpango wa kuwakopesha wanafunzi wa elimu ya juu ni ubunifu wa Mkapa na Waziri wake wa Elimu ya Juu wakati huo, Dk. Pius Ng’wandu. Nikamwambia hata wao waliuiga kutoka Kenya kwa mujibu wa maelezo ya Dk. Ng’wandu mwenyewe ndani ya Bunge wakati wa kupitisha muswaada huo mwaka 2005. Nikamwambia kimsingi Kikwete anastahili lawama kali kwenye suala la mikopo ya wanafunzi badala ya kumsifia.
Wakati kina Mkapa wanaanzisha mfumo huo walilenga kumkopesha kila mwanafunzi kwa asilimia mia ya gharama zake za kusoma chuo kikuu ama chuo chochote cha elimu ya juu, kuanzia ada ya masomo, ada nyinginezo zote zinazotozwa na chuo, gharama za kuishi mwanafunzi (malazi na chakula) pamoja na gharama nyinginezo zinazomhusu mwanafunzi kwa mfano vitabu, mafunzo kwa vitendo na utafiti.
Kikwete akadai akiingia yeye ataboresha lakini alipoingia akaleta madaraja kwamba kuna wanaostahili kwa A kwa maana ya kukopeshwa asilimia 100, B ni asilimia 80, C ni asilimia 60 na kadhalika.
Ni katika kipindi cha Kikwete sasa migomo ya elimu ya juu imeongezeka mara 5. Lakini kwa kuwa wakati huo askofu alikuwa upande wa Kikwete haikuwa nongwa.
Kasheshe ikaanzia pale Baraza la Maaskofu lilipotoa waraka kwa waumini wake juu sifa za kiongozi bora ambaye waumini wake wanatakiwa kumchagua.
Niliupitia waraka ule pote na sikuona dini ikiwa mojawapo ya sifa za mtu ambaye baraza la maaskofu lilimpendekeza kwa waumini.
Wala sikuona jina la mtu kiasi kwamba tunaweza kusema hawakusema lakini walimtaja mtu wao kuwa ndiye anafaa. Lakini kuna siri moja katika waraka ule. Maaskofu walisisitiza kwamba umefika wakati ili tulikomboe taifa tuchague viongozi wasio mafisadi. Huo ni ujumbe ambao hata Kikwete mwenyewe ameutamka kinafiki mara nyingi sana kwa wananchi wake. Maneno hayo hayo yalipotamkwa na viongozi wa dini ambao kimsingi si, na hawatakiwi kuwa wanafiki, Kikwete akashtuka.
Akaona waumini watawaelewa na kimsingi watafanyia kazi na wakifanyia kazi waraka ule inakula kwa CCM maana ndiyo iliyojaza mafisadi.
Ndipo faulo ya udini ikaanza kuandaliwa. Ikasemwa kwamba kuna mgombea anafanya kampeni za udini. Eti maaskofu wamewaelekeza waumini wao kumchagua mgombea wa CHADEMA.
Wengi walidhani na hata waasisi wa faulo hiyo walifikiri kwamba baada ya kampeni na uchaguzi kwisha, hiyo faulo itaijiishia yenyewe wala haitakumbukwa. Hawakujua ubaguzi huo Mwalimu alishasema ni sawa na kula nyama ya mtu, ukishaanza utaendelea tu. JK akajikuta baada ya uchaguzi anafanya kazi ya kuwalilia waandishi wa habari eti wasaidie kuondoa makovu ya udini yaliyojitokeza wakati wa kampeni.
Ni sawa na kwamba alikuwa akisema kuwa wakati wa kampeni alianzisha propaganda ya udini ambayo ilibebewa bango sana na vyombo vya habari vilivyokuwa vimejitoa mhanga kuhakikisha anashinda tena urais kwa njia zozote zile.
Sasa ameshinda anawaomba waandishi wa habari wale wale waliokuza propaganda ya udini wasaidie kuiondoa. Kazi ambayo hakujua kwamba hawaiwezi katu!
Kwa ujumla, waumini wa faulo hiyo wamebaki wakiwa na kutu hiyo vichwani mwao na ni vigumu kuiondoa kabisa. Hivi sasa mkakati umeanza kufanywa na viongozi wachache wenye maslahi binafsi katika dini fulani.
Wameanza kutaja kwa majina tena wazi wazi chama fulani na kukihusisha na dini fulani tena wakitoa wito wazi wazi kwa waumini wao na kuwataka eti wasishiriki maandamano ya chama hicho kwa kuwa chama hicho hakitetei maslahi ya dini yao. Haya ninayoyasema ni yale niliyoyasikia mimi mwenyewe kwenye redio moja ya dini hiyo ambayo hurusha matangazo yake kutokea Morogoro.
Nilimsikia kwa masikio yangu kiongozi mmoja akisema wazi wazi kwamba ni dhambi kubwa kwa muumini wa dini yao kushiriki maandamano ya chama (akikitaja kwa jina) ilhali akijua kwamba chama hicho hakitetei haki za dini yao.
Kama angesema maandamano ya chama chochote cha siasa ningemwelewa, lakini kitendo cha kukitaja chama kwa jina huku ikiwa dhahiri kabisa kwamba kuna vyama kadhaa ambavyo vimekuwa vikiitisha maandamano kwa makusudi hayo hayo ya kisiasa lakini havisemi vyama hivyo, ni dhahiri kwamba huyu anavigawa vyama vya kisiasa kidini.
Namuuliza JK, kampeni zetu za uchaguzi zikianza kuwa za kidini itakula kwa nani? JK, kampeni hii itakula kwako!
Acha kabisa masuala ya kutumia udini kushinda uchaguzi ama kubaki madarakani. Vita ya CHADEMA na CCM ni vita ya vyama vya siasa si vita vya ukristo na uislam. Unawakosea sana Watanzania Waislamu na Wakristo kuwaingiza katikati ya vita ya CHADEMA v/s CCM.
Kuna Waislamu tena wengi ndani ya CHADEMA kama ilivyo kwenye CCM na kuna Wakristo wengi ndani ya CCM kama ilivyo ndani ya CHADEMA.
Kuanza kuwagombanisha kwa maslahi yako na yenu ya kisiasa ni dhambi isiyosameheka.
Kama unataka kuipumzisha CCM kutoka madarakani lakini ukaiacha nchi inamwagika damu na wewe mwenyewe umekimbilia uhamishoni Saudia, endelea na mchezo huo!
 
Kanuni za msingi kuelekea Katiba mpya zisivunjwe
ban.kijiji.jpg


M. M. Mwanakijiji​

amka2.gif
SIJUI watu waliokaa chini kuandika muswada wa sheria itakayosimamia mchakato wa kupatikana kwa Katiba Mpya walikuwa ni Watanzania au ni mamluki kutoka nchi nyingine waliolipwa fedha kufanya kazi ya kutuandikia kwa haraka haraka mswada huo.
Kama ni Watanzania wenzetu na hasa kama ni watu ambao wanafuatilia siasa za Tanzania basi sina budi kusema kuwa kina cha matatizo yetu ni kirefu zaidi kuliko tunavyofikiria.
Sitaki kukosoa sana muswada huo kwani umekoselewa vya kutosha lakini kinachoniogopesha ni kuwa hawa watawala wetu bado kabisa hawajaupata ujumbe. Pamoja na juhudi zetu nyingi za kuwaelewesha kwanini tunahitaji Katiba Mpya inaonekana bado haijawaingia kabisa katika mawazo wao uzito wa kile tunachotaka kifanyika.
Nadhani wanafikiri tunachotaka ni mchakato ambao utasababisha uwepo wa Katiba Mpya. Yaani, katika mawazo yao alimradi kutakuwepo na Katiba Mpya basi hilo peke yake ndilo Watanzania wanataka. Na nina uhakika walipokubali kukumbatia wazo hili walifikiri kuwa Watanzania wanataka Katiba Mpya tu ilimradi yaishe.
Wapo watu wengi tu ambao wanazungumzia "Katiba Mpya" kama mwisho wa kile tunachokitaka kwa hiyo alimradi kutakuwepo Katiba Mpya basi madai ya wananchi yatakuwa yamefikiwa. Labda niseme kwa namna nyingine. Mkulima anaposema anahitaji zana za kisasa za kilimo kwa mtu mwingine anaweza akafikiria kuwa anataka tu zana za kisasa za kilimo tena mpya. Sasa mtu akienda huko Uchina au Ujerumani na kununua matrekta makubwa na kumletea mkulima ni kweli tutakuwa tumempatia treka jipya!
Lakini tutakuwa tumempati kile anachohitaji? Ili tujue anachohitaji ni trekta la aina gani ni lazima tujue mazingira yake, na uwezo wake wa kulitumia na upatikanaji wa vipuri vyake n.k.
Ninachosema ni kuwa Watanzania hawaitaji Katiba Mpya kwa ajili ya kusema kuwa "Katiba yetu Mpya"; wanahitaji Katiba Mpya ambayo itawafaa katika mahusiano yao na watawala wao na vile vile itawafaa katika mahusiano yao kati yao na zaidi ya yote itakayoongoza maisha yao yote. Kufikiria kuwa tunataka tuwe na Katiba Mpya ilimradi tunayo au tumeandika kwa maneno tofauti ni kuwachukuliwa Watanzania kwa dharau.
Ni kwa sababu hiyo ninaamini kabisa kama wengine walivyodokeza kwenye kongamano la UDASA na sehemu nyingine muswada wa kusimamia mchakato wa kufikia Katiba Mpya una udhaifu wa kutosha kufanya hata Katiba itakayokuwa kuwa na matatizo. Binafsi napinga mchakato wowote wa kuandika Katiba Mpya ambao hautazingatia kanuni zivuatazo ambazo naamini ni kanuni za msingi kabisa kuweza kufikia Katiba Mpya. Pasipo kuzingatia kanuni hizi mchakato wowote utakuwa ni jaribio la chama tawala na serikali yake kuteka nyara hoja ya Katiba Mpya na baadaye waandike Katiba wanayoitaka wao (CCM na serikali) na siyo Katiba inayowastahili Watanzania.
KANUNI YA 1: Mchakato uhusishe wote kutoa mawazo
Mchakato wa kufikia Katiba Mpya usipoweka msingi ambao utahakikisha wananchi wote wana nafasi sawa ya kuchangia mawazo yao juu ya yale wanayoyataka kwenye Katiba Mpya basi basi utakuwa ni mchakato mbovu. Utaona sijasema "kukusanya maoni". Ninachozungumzia ni kuwa ni jambo moja kutoa maoni na ni jambo jingine kufanya mawazo yako yasikike. Kwa wale tunaokumbuka mchakato wa kurudisha vyama vingi tunakumbuka jinsi kina Marmo walivyopita na "kukusanya maoni".
Japo wenyewe walijivunia kuwa walifanya kazi nzuri ukweli ni kwamba mfumo uliotumiwa ulihakikisha wenye kutoa maoni ni wasomi, wenye sauti na zaidi watu ambao katika maisha yao walikuwa na nafasi fulani za kuweza kusikika.
Hata katika maeneo ambayo wananchi wa kawaida walitoa maoni hakukuwa na mjadala wa kutosha kati ya watu na watu kabla ya kufika kwenye tume ya maoni.
Yaani, kwa masaa machache watu walitakiwa kutoa maoni yao kwenye kikao cha masaa machache kabla hawajaondoka hao wanakamati kwenda mji mwingine "kukusanya maoni". Kama vipepeo tume ya kukusanya maoni iliruka ruka na kupokea mshiko wa nguvu toka serikali ikikusanya maoni na baadaye kutoa ripoti yake. Matokeo yake asilimia 80 ya waliohojiwa walitaka tuendelee kuwa na mfumo wa chama kimoja. Wao wenyewe waliamini ni kwa sababu "CCM inapendwa" lakini hawakutaka kuangalia kuwa wananchi hawakuwa na muda wa kugonganisha mawazo yao ya kutosha.
Mbinu hii ya kukusanya "maoni" kwa mtindo ambao umewekwa kwenye mswada (ambao hauna tofauti na ule wa kina Marmo chini ya Tume ya Nyalali).
Mbinu ya kukusanya maoni hairuhusu mjadala huru wa watu kuweza kushawishiana kubadala maoni. Sasa tukikubali tume ya "maoni" kama ilivyo tujue mapema kabisa kuwa hawa watu watapita, wanakijiji wataitwa, kutakuwa na maelezo ya hapa na pale, maswali yataruhusiwa na wajumbe wataonekana wanaandika andika kwenye makaratasi yao na baadaye kikao kitaisha na watu watarudi makwao wakiwa "wametoa maoni"yao.
Lakini mfumo bora ni ule wa kuhakikisha kuwa watu wote wanahusishwa siyo tu watu wachache wanatoa maoni lakini watu wote wanahusishwa katika mjadala wa Katiba Mpya. Kwa hiyo sheria itakayosimamia mchakato wa kufikia Katiba Mpya ni lazima iweke mfumo mzuri wa kuendesha mjadala kwa watu wengi zaidi KABLA ya kuanza kukusanya Maoni.
Maana yake ni kwamba kabla wananchi hawajaanza kuulizwa kutoa maoni yao ni lazima yawepo mazingira ya kiasi cha juu kabisa (optimal environment) ambapo wananchi watashiriki mjadala wa katiba katika mashule, makanisa, misikiti, maofisini, mitaani, kwenye vyama vya siasa n.k. Kabla ya kuanza kuratibu maoni tufanye mjadala kwanza ambao utahusisha Watanzania katika ngazi zao zote.
KANUNI YA PILI: Mjadala uruhusu kuzungumzwa kwa yote
Hatuwezi kufikia Katiba Mpya inayotokana na wananchi wenyewe na inayowastahili wananchi wenyewe kama hatuwezi kujadili na kuzungumza yote yanayotuhusu kama raia na kama binadamu. Ibara ya 9:2 ya muswada huu ambao umependekezwa kusimamia mchakato unatuambia kuwa tunaweza kuzungumza mambo mengine yote lakini tusije kugusa mambo 10 ya msingi.
Mambo hayo wataalamu wetu waliotuandikia muswada (sijui walikuwa watu wangapi) wametuambia kuwa mambo hayo kumi hatayakiwi kuguswa au kubadilishwa.
Sasa hawa watu sijui nani kawapa uwezo wa kuwaambia wananchi milioni 43 na ushee kuwa wasizungumzia mambo fulani fulani au hata kuyafuta.
Ndugu zangu tunapotaka kuandika Katiba Mpya ni LAZIMA mambo yote yaletwe mezani hakuna "mambo matakatifu yasiyogusika". Katika mjadala wa Katiba Mpya hata mambo ambayo hayako mezani na yamewekwa pembeni ni lazima tuyatafuta na kuyaleta pembeni hata yale ambao labda tulishayatupa inabidi tukayachukue huko na kuyaleta mezani.
Huu ni mjadala wa Katiba Mpya yaani nyaraka kuu itakayosimamia maisha ya Watanzania. Ndiyo maana kwenye nchi nyingine Katiba ina nguvu kuliko maandiko matakatifu na hii si kufuru. Kama maandiko matakatifu tuliletewa na watu na kuambiwa kuwa ni neno la Mungu kwa sababu kuna watu walitokewa na Mungu, malaika au walivuviwa na wakatupatia neno la Mungu na wengi wetu tumejikuta tukiamini.
Hata leo utaona watu wanapigana na kuumizana kwa sababu ya maandiko hayo. Lakini Katiba (kwa maoni ya baadhi ya watu) ni juu ya vitabu hivyo vitukufu! Kwa sababu katiba ni sauti ya watu ambayo ina nguvu kama sauti ya Mungu. Yaani, kama kungekuwa hakuna vitabu vitakatifu vya kutuamulia maisha yetu ya kiroho basi binadamu tungetakiwa kuwa na mfumo fulani wa kujiongoza na mfumo huo ungekuwa ni mtakatifu kwa sababu unatokana na sisi wenyewe.
Vivyo hivyo Katiba. Kuna msemo wa Kilatini kuwa Vox Populi, Vox Dei yaani sauti ya watu (ni) Sauti ya Mungu. Katiba basi inatakiwa kuwa ni nyaraka ambayo inaakisi sauti ya watu kuhusu maisha yao na mfumo wanaotaka uwaongoze na watu hao wakiwa na taarifa sahihi, wakibadilishana mawazo na kushawishiana kwa hoja mbalimbali huweza kufikia kitu kilicho bora zaidi. Sisi binadamu tumepewa uwezo na Mwenyezi Mungu kufikiria na kutambua kitu ambacho hatukitaki hata kama hatuna uhakika wa kile tunachokitaka. Kwa mfano hakuna mwanadamu anayependa kudhulumiwa na mtu mwingine, au anayependa kufanya mtumwa na mtu mwingine. Hii hata hivyo haituzuii kuwadhulumu wengine! Kumbe Katiba ikiruhusu kuzungumzwa kwa yote inatusaidia kuona ni kitu gani hatukitaki na ni kitu gani tunaelekea kukikata au tunajua tunakitaka.
Ni kwa sababu hiyo basi yote LAZIMA yaruhusiwe kuzungumzwa na kujadiliwa. Hivyo sheria yoyote itakayosimamia mchakato wa Katiba ihakikishe kuwa wananchi wanashiriki kutoa mawazo yao kwa kila jambo.
Ili hili lifanikiwe ni lazima kwanza kabisa kufanyia mabadiliko sheria ya Usalama wa Taifa ya 1970 pamoja na Sheria ya Magazeti ya 1976 kwani sheria hizo mbili ni kizuizi kikubwa cha uhuru wa mawazo na maoni kuliko kitu kingine chochote.
Hivyo, katika mjadala huu ni lazima wanaotaka Muungano uvunjwe waruhusiwe kuzungumza mawazo yao bila ya kuogopa kutiwa pingu; wanaotaka muda wa kikomo cha urais uondolewe ili rais aweza kugombea bila kikomo kama wabunge waruhusiwe bila ya kuonekana "si wana demokrasia", wanaotaka Tanzania iwe Ufalme wa Kikwete na tuondokane na mfumo wa urais waruhusiwe kutoa mawazo hayo. Naam, hata kama kuna watu wanataka kuzungumzia kuwa Tanzania iwe na Sharia za Kiislamu au iongozwe kwa Sheria za Kanisa watoe maoni yao vile vile. Tunapozungumzia Katiba Mpya ni lazima tuweke utaratibu utakaoruhusu mawao YOTE kutolewa hata yale ambayo hatuyapendi au yale ambayo yanatugusa vibaya.
Ninaposema YOTE nina maana kusiwepo na watu ambao watasema "hilo halizungumziki". Kwa mfano wakati wapo wanaoweza kutaka tusema kwenye Katiba kuwa Tanzania inamuamini Mungu tujue wapo ambao pia wangependa tutambue haki za mashoga na wapo ambao wanaweza wakataka tutambue kuwa wanawake nao wana haki ya kuolewa na mume zaidi ya mmoja!
Kwa hiyo, tunaporuhusu mjadala wa mambo yote, maana yake ni kuwa tutakapofika wakati hasa wa kuanza kukusanya maoni na hatimaye kuanza mchakato wa kuandika Katiba tutakuwa tumesikia hoja karibu zote zenye kugusa wananchi karibu wote na hasa zile hoja ambazo pasipo mjadala kama huu zisingeweza kutolewa. Matokeo yake ni kuwa baada ya mjadala huru wenye kuhusisha watu wote na wenye kuzungumzia mambo yote basi mawazo yaliyo bora zaidi na yenye kuvutia watu wengi zaidi ndiyo yatakuwa msingi wa Katiba.
KANUNI YA 3: Katiba ni ya wananchi wenyewe
Kanuni hii ya tatu inatokana moja kwa moja na hizo mbili za kwanza. Ukisoma mswada ulioandaliwa na "wataalamu" wetu utaona ni jinsi gani kama nilivyosema awali hawajupata ujumbe. Neno "Rais" linatokea mara 12 katika muswada huo, neno "mwananchi" linatoka mara mbili na moja kati ya hizo ni "asiye-mwananchi) na neno "watu" linatokea mara nne tu. Kwa maneno mengine, hawa watu watu walioandika mswada huu walikuwa wakiongozwa na fikra za kutekeleza na kulinda maslahi ya rais.
Katiba Mpya siyo zao la Rais aliyeko madarakani. Kutokana na hilo mchakato wowote ambao unampa nguvu kubwa Rais (kana kwamba ni mfalme wa Tanzania) ni mchakato mbovu unaohitaji kukataliwa. Walioandika inaonekana ni watu walioamua kufuata njia yenye vikwazo vidogo zaidi (a path of least resistance). Kwa maneno mengine hawakutaka kufikiria zaidi ya namna nyingine ya kufanya kitu hata kama ni bora zaidi na hivyo wakaamua tu kumrundikia rais majukumu mengi na yasiyo na sababu. Kimsingi wanachopendekeza hawa walioandika ni TUME YA RAIS YA KUPITIA KATIBA.
Sasa kama watu wangetaka rais aunde tume tungeomba Rais aunde tume! Hakuna aliyemuomba rais aunde tume na wala hakikuhitajika kibali chake kwenye suala la Katiba Mpya. Katiba Mpya ni zao la Watanzania na hasa ni zao la wanamageuzi nchini. Sasa kuandaa muswada wa kusimamia mchakato huo bila kuwashirikisha wanamageuzi siyo kutendea haki kwa sababu baada ya kuiteka hoja ya "katiba mpya" sasa wameenda mbele zaidi na wameamua kuteka mchakato wa kufikia Katiba Mpya na tukiwakubalia watateka na katiba mpya.
Ninachosema kwa maoni yangu ni kuwa sheria itakayosimamia mchakato wa kufikia Katiba Mpya ni lazima itambue kuwa ni katiba ni lazima itokane na wananchi, kufikiwa kwake ni lazima kuoneshe kuwa ni Katiba ya wananchi na hivyo hata muundo wa mfumo wa kuifikia uwe ni ule wenye kuheshimu hilo.
Pamoja na ukweli wa kanuni hizo hapo juu nina uhakika kuwa mswada huu unaweza kupita ukiwa na mabadiliko machache tu. Ninachojua ni kuwa endapo mswada utapita jinsi ulivyo au ukiwa na mabadiliko machache tu tutakuwa tumerasimisha mchakato wa Katiba Mpya mikononi mwa CCM. Hivyo, huu utakuwa ni utaratibu wa CCM kufikia Katiba Mpya. Yaani, wao ndio wataamua Katiba Iweje na kwa maoni yangu itakuwa ni dhambi kwa dhamira zetu kutoa ushirikiano wowote kwa tume hiyo ya Rais.
Kutokana na hilo ninaamini ni wajibu wa kila anayoengozwa na dhamira ambayo inamsuta kutoa ushirikiano kutofanya hivyo. CCM na serikali yake waendeshe mchakato wao na wafikie kwenye Katiba Mpya wanayoitaka wao. Sisi wengine tutaanza mchakato huru na wawazi zaidi baadaye.
Ushauri mwingine ambao naamini ni bora zaidi ni kuwa kikao cha sasa kifupishwe ili mambo mengine tu yajadiliwe lakini Bunge liurudishe mswada huu kwa serikali na kukusanya maoni bora zaidi (nami nitakuwa tayari kutoa maoni ya mchakato bora ambao utaakisi kanuni hizo hapo juu).
Ila kifanyike kikao maalumu cha Bunge ambacho kwa kuitwa kwake kitakuwa kinaonyesha watawala wetu wanatambua uzito wa tukio lililo mbele yetu.
Binafsi ninaamini watawala wetu bado hawajelewa uzito wa jambo hili. Yaani kuliweka kama sehemu ya kikao cha kawaida ni kutolipa jambo hili uzito wake. Ninaamini suala la Katiba Mpya ni sawasawa na Musa alipofika karibu na kichaka cha moto! Tunataka kufanya jambo takatifu na hivyo tuonyeshe uzito wake. Ninaamini kikao maalumu cha Bunge cha kujadili Muswada wa Sheria ya Kuongoza Mchakato wa Katiba Mpya kiitwe hata kama kitakuwa ni cha siku tatu tu.
Kikao hicho kisiwe sehemu, ya kikao cha kawaida (kama cha sasa) au kile cha Bunge la Bajeti. Kiwe ni kikao maalum.
Na tukifanya hivyo tutatoa muda kwa pande nyingine kutolea maoni sheria hizo na hata kwa upinzani kuja na mapendekezo ya mswada wao ili hatimaye miswada hiyo miwili (au zaidi) iweze kujadiliwa na hatimaye upatikane mswada ulio mzuri zaidi. Kama tulivyokosoa muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na watu walidhani tunawaonea wivu lakini tulikuwa sahihi nina uhakika tuko sahihi wakati huu tena.
Muswada huu ukipitisha kama ulivyo utachangia ujio wa sheria nyingine mbovu zaidi ambao katika dhamira safi baadhi yetu tutashindwa kuitii. Sasa kama tunataka kweli kufikia katiba mpya ni lazima kwanza tubadili fikra. Watawala wasidhani wanatutendea hisani na wananchi tusifikirie tunabembeleza watawala wetu. Ni bora tusubiri miaka mitano tuweze kuleta timu itakayotuongoza kufikia katiba mpya kuliko tuharakishwe ndani ya miaka hii mitano kuongozwa kuelekea kwenye machozi. Katiba mpya itokane na fikra mpya.
Hilo litawezekana vipi wakati bado wapo watu wana fikra za zamani?
 
Kanuni za msingi kuelekea Katiba mpya zisivunjwe
ban.kijiji.jpg


M. M. Mwanakijiji​

amka2.gif
SIJUI watu waliokaa chini kuandika muswada wa sheria itakayosimamia mchakato wa kupatikana kwa Katiba Mpya walikuwa ni Watanzania au ni mamluki kutoka nchi nyingine waliolipwa fedha kufanya kazi ya kutuandikia kwa haraka haraka mswada huo.
Kama ni Watanzania wenzetu na hasa kama ni watu ambao wanafuatilia siasa za Tanzania basi sina budi kusema kuwa kina cha matatizo yetu ni kirefu zaidi kuliko tunavyofikiria.
Sitaki kukosoa sana muswada huo kwani umekoselewa vya kutosha lakini kinachoniogopesha ni kuwa hawa watawala wetu bado kabisa hawajaupata ujumbe. Pamoja na juhudi zetu nyingi za kuwaelewesha kwanini tunahitaji Katiba Mpya inaonekana bado haijawaingia kabisa katika mawazo wao uzito wa kile tunachotaka kifanyika.
Nadhani wanafikiri tunachotaka ni mchakato ambao utasababisha uwepo wa Katiba Mpya. Yaani, katika mawazo yao alimradi kutakuwepo na Katiba Mpya basi hilo peke yake ndilo Watanzania wanataka. Na nina uhakika walipokubali kukumbatia wazo hili walifikiri kuwa Watanzania wanataka Katiba Mpya tu ilimradi yaishe.
Wapo watu wengi tu ambao wanazungumzia “Katiba Mpya” kama mwisho wa kile tunachokitaka kwa hiyo alimradi kutakuwepo Katiba Mpya basi madai ya wananchi yatakuwa yamefikiwa. Labda niseme kwa namna nyingine. Mkulima anaposema anahitaji zana za kisasa za kilimo kwa mtu mwingine anaweza akafikiria kuwa anataka tu zana za kisasa za kilimo tena mpya. Sasa mtu akienda huko Uchina au Ujerumani na kununua matrekta makubwa na kumletea mkulima ni kweli tutakuwa tumempatia treka jipya!
Lakini tutakuwa tumempati kile anachohitaji? Ili tujue anachohitaji ni trekta la aina gani ni lazima tujue mazingira yake, na uwezo wake wa kulitumia na upatikanaji wa vipuri vyake n.k.
Ninachosema ni kuwa Watanzania hawaitaji Katiba Mpya kwa ajili ya kusema kuwa “Katiba yetu Mpya”; wanahitaji Katiba Mpya ambayo itawafaa katika mahusiano yao na watawala wao na vile vile itawafaa katika mahusiano yao kati yao na zaidi ya yote itakayoongoza maisha yao yote. Kufikiria kuwa tunataka tuwe na Katiba Mpya ilimradi tunayo au tumeandika kwa maneno tofauti ni kuwachukuliwa Watanzania kwa dharau.
Ni kwa sababu hiyo ninaamini kabisa kama wengine walivyodokeza kwenye kongamano la UDASA na sehemu nyingine muswada wa kusimamia mchakato wa kufikia Katiba Mpya una udhaifu wa kutosha kufanya hata Katiba itakayokuwa kuwa na matatizo. Binafsi napinga mchakato wowote wa kuandika Katiba Mpya ambao hautazingatia kanuni zivuatazo ambazo naamini ni kanuni za msingi kabisa kuweza kufikia Katiba Mpya. Pasipo kuzingatia kanuni hizi mchakato wowote utakuwa ni jaribio la chama tawala na serikali yake kuteka nyara hoja ya Katiba Mpya na baadaye waandike Katiba wanayoitaka wao (CCM na serikali) na siyo Katiba inayowastahili Watanzania.
KANUNI YA 1: Mchakato uhusishe wote kutoa mawazo
Mchakato wa kufikia Katiba Mpya usipoweka msingi ambao utahakikisha wananchi wote wana nafasi sawa ya kuchangia mawazo yao juu ya yale wanayoyataka kwenye Katiba Mpya basi basi utakuwa ni mchakato mbovu. Utaona sijasema “kukusanya maoni”. Ninachozungumzia ni kuwa ni jambo moja kutoa maoni na ni jambo jingine kufanya mawazo yako yasikike. Kwa wale tunaokumbuka mchakato wa kurudisha vyama vingi tunakumbuka jinsi kina Marmo walivyopita na “kukusanya maoni”.
Japo wenyewe walijivunia kuwa walifanya kazi nzuri ukweli ni kwamba mfumo uliotumiwa ulihakikisha wenye kutoa maoni ni wasomi, wenye sauti na zaidi watu ambao katika maisha yao walikuwa na nafasi fulani za kuweza kusikika.
Hata katika maeneo ambayo wananchi wa kawaida walitoa maoni hakukuwa na mjadala wa kutosha kati ya watu na watu kabla ya kufika kwenye tume ya maoni.
Yaani, kwa masaa machache watu walitakiwa kutoa maoni yao kwenye kikao cha masaa machache kabla hawajaondoka hao wanakamati kwenda mji mwingine “kukusanya maoni”. Kama vipepeo tume ya kukusanya maoni iliruka ruka na kupokea mshiko wa nguvu toka serikali ikikusanya maoni na baadaye kutoa ripoti yake. Matokeo yake asilimia 80 ya waliohojiwa walitaka tuendelee kuwa na mfumo wa chama kimoja. Wao wenyewe waliamini ni kwa sababu “CCM inapendwa” lakini hawakutaka kuangalia kuwa wananchi hawakuwa na muda wa kugonganisha mawazo yao ya kutosha.
Mbinu hii ya kukusanya “maoni” kwa mtindo ambao umewekwa kwenye mswada (ambao hauna tofauti na ule wa kina Marmo chini ya Tume ya Nyalali).
Mbinu ya kukusanya maoni hairuhusu mjadala huru wa watu kuweza kushawishiana kubadala maoni. Sasa tukikubali tume ya “maoni” kama ilivyo tujue mapema kabisa kuwa hawa watu watapita, wanakijiji wataitwa, kutakuwa na maelezo ya hapa na pale, maswali yataruhusiwa na wajumbe wataonekana wanaandika andika kwenye makaratasi yao na baadaye kikao kitaisha na watu watarudi makwao wakiwa “wametoa maoni”yao.
Lakini mfumo bora ni ule wa kuhakikisha kuwa watu wote wanahusishwa siyo tu watu wachache wanatoa maoni lakini watu wote wanahusishwa katika mjadala wa Katiba Mpya. Kwa hiyo sheria itakayosimamia mchakato wa kufikia Katiba Mpya ni lazima iweke mfumo mzuri wa kuendesha mjadala kwa watu wengi zaidi KABLA ya kuanza kukusanya Maoni.
Maana yake ni kwamba kabla wananchi hawajaanza kuulizwa kutoa maoni yao ni lazima yawepo mazingira ya kiasi cha juu kabisa (optimal environment) ambapo wananchi watashiriki mjadala wa katiba katika mashule, makanisa, misikiti, maofisini, mitaani, kwenye vyama vya siasa n.k. Kabla ya kuanza kuratibu maoni tufanye mjadala kwanza ambao utahusisha Watanzania katika ngazi zao zote.
KANUNI YA PILI: Mjadala uruhusu kuzungumzwa kwa yote
Hatuwezi kufikia Katiba Mpya inayotokana na wananchi wenyewe na inayowastahili wananchi wenyewe kama hatuwezi kujadili na kuzungumza yote yanayotuhusu kama raia na kama binadamu. Ibara ya 9:2 ya muswada huu ambao umependekezwa kusimamia mchakato unatuambia kuwa tunaweza kuzungumza mambo mengine yote lakini tusije kugusa mambo 10 ya msingi.
Mambo hayo wataalamu wetu waliotuandikia muswada (sijui walikuwa watu wangapi) wametuambia kuwa mambo hayo kumi hatayakiwi kuguswa au kubadilishwa.
Sasa hawa watu sijui nani kawapa uwezo wa kuwaambia wananchi milioni 43 na ushee kuwa wasizungumzia mambo fulani fulani au hata kuyafuta.
Ndugu zangu tunapotaka kuandika Katiba Mpya ni LAZIMA mambo yote yaletwe mezani hakuna “mambo matakatifu yasiyogusika”. Katika mjadala wa Katiba Mpya hata mambo ambayo hayako mezani na yamewekwa pembeni ni lazima tuyatafuta na kuyaleta pembeni hata yale ambao labda tulishayatupa inabidi tukayachukue huko na kuyaleta mezani.
Huu ni mjadala wa Katiba Mpya yaani nyaraka kuu itakayosimamia maisha ya Watanzania. Ndiyo maana kwenye nchi nyingine Katiba ina nguvu kuliko maandiko matakatifu na hii si kufuru. Kama maandiko matakatifu tuliletewa na watu na kuambiwa kuwa ni neno la Mungu kwa sababu kuna watu walitokewa na Mungu, malaika au walivuviwa na wakatupatia neno la Mungu na wengi wetu tumejikuta tukiamini.
Hata leo utaona watu wanapigana na kuumizana kwa sababu ya maandiko hayo. Lakini Katiba (kwa maoni ya baadhi ya watu) ni juu ya vitabu hivyo vitukufu! Kwa sababu katiba ni sauti ya watu ambayo ina nguvu kama sauti ya Mungu. Yaani, kama kungekuwa hakuna vitabu vitakatifu vya kutuamulia maisha yetu ya kiroho basi binadamu tungetakiwa kuwa na mfumo fulani wa kujiongoza na mfumo huo ungekuwa ni mtakatifu kwa sababu unatokana na sisi wenyewe.
Vivyo hivyo Katiba. Kuna msemo wa Kilatini kuwa Vox Populi, Vox Dei yaani sauti ya watu (ni) Sauti ya Mungu. Katiba basi inatakiwa kuwa ni nyaraka ambayo inaakisi sauti ya watu kuhusu maisha yao na mfumo wanaotaka uwaongoze na watu hao wakiwa na taarifa sahihi, wakibadilishana mawazo na kushawishiana kwa hoja mbalimbali huweza kufikia kitu kilicho bora zaidi. Sisi binadamu tumepewa uwezo na Mwenyezi Mungu kufikiria na kutambua kitu ambacho hatukitaki hata kama hatuna uhakika wa kile tunachokitaka. Kwa mfano hakuna mwanadamu anayependa kudhulumiwa na mtu mwingine, au anayependa kufanya mtumwa na mtu mwingine. Hii hata hivyo haituzuii kuwadhulumu wengine! Kumbe Katiba ikiruhusu kuzungumzwa kwa yote inatusaidia kuona ni kitu gani hatukitaki na ni kitu gani tunaelekea kukikata au tunajua tunakitaka.
Ni kwa sababu hiyo basi yote LAZIMA yaruhusiwe kuzungumzwa na kujadiliwa. Hivyo sheria yoyote itakayosimamia mchakato wa Katiba ihakikishe kuwa wananchi wanashiriki kutoa mawazo yao kwa kila jambo.
Ili hili lifanikiwe ni lazima kwanza kabisa kufanyia mabadiliko sheria ya Usalama wa Taifa ya 1970 pamoja na Sheria ya Magazeti ya 1976 kwani sheria hizo mbili ni kizuizi kikubwa cha uhuru wa mawazo na maoni kuliko kitu kingine chochote.
Hivyo, katika mjadala huu ni lazima wanaotaka Muungano uvunjwe waruhusiwe kuzungumza mawazo yao bila ya kuogopa kutiwa pingu; wanaotaka muda wa kikomo cha urais uondolewe ili rais aweza kugombea bila kikomo kama wabunge waruhusiwe bila ya kuonekana “si wana demokrasia”, wanaotaka Tanzania iwe Ufalme wa Kikwete na tuondokane na mfumo wa urais waruhusiwe kutoa mawazo hayo. Naam, hata kama kuna watu wanataka kuzungumzia kuwa Tanzania iwe na Sharia za Kiislamu au iongozwe kwa Sheria za Kanisa watoe maoni yao vile vile. Tunapozungumzia Katiba Mpya ni lazima tuweke utaratibu utakaoruhusu mawao YOTE kutolewa hata yale ambayo hatuyapendi au yale ambayo yanatugusa vibaya.
Ninaposema YOTE nina maana kusiwepo na watu ambao watasema “hilo halizungumziki”. Kwa mfano wakati wapo wanaoweza kutaka tusema kwenye Katiba kuwa Tanzania inamuamini Mungu tujue wapo ambao pia wangependa tutambue haki za mashoga na wapo ambao wanaweza wakataka tutambue kuwa wanawake nao wana haki ya kuolewa na mume zaidi ya mmoja!
Kwa hiyo, tunaporuhusu mjadala wa mambo yote, maana yake ni kuwa tutakapofika wakati hasa wa kuanza kukusanya maoni na hatimaye kuanza mchakato wa kuandika Katiba tutakuwa tumesikia hoja karibu zote zenye kugusa wananchi karibu wote na hasa zile hoja ambazo pasipo mjadala kama huu zisingeweza kutolewa. Matokeo yake ni kuwa baada ya mjadala huru wenye kuhusisha watu wote na wenye kuzungumzia mambo yote basi mawazo yaliyo bora zaidi na yenye kuvutia watu wengi zaidi ndiyo yatakuwa msingi wa Katiba.
KANUNI YA 3: Katiba ni ya wananchi wenyewe
Kanuni hii ya tatu inatokana moja kwa moja na hizo mbili za kwanza. Ukisoma mswada ulioandaliwa na “wataalamu” wetu utaona ni jinsi gani kama nilivyosema awali hawajupata ujumbe. Neno “Rais” linatokea mara 12 katika muswada huo, neno “mwananchi” linatoka mara mbili na moja kati ya hizo ni “asiye-mwananchi) na neno “watu” linatokea mara nne tu. Kwa maneno mengine, hawa watu watu walioandika mswada huu walikuwa wakiongozwa na fikra za kutekeleza na kulinda maslahi ya rais.
Katiba Mpya siyo zao la Rais aliyeko madarakani. Kutokana na hilo mchakato wowote ambao unampa nguvu kubwa Rais (kana kwamba ni mfalme wa Tanzania) ni mchakato mbovu unaohitaji kukataliwa. Walioandika inaonekana ni watu walioamua kufuata njia yenye vikwazo vidogo zaidi (a path of least resistance). Kwa maneno mengine hawakutaka kufikiria zaidi ya namna nyingine ya kufanya kitu hata kama ni bora zaidi na hivyo wakaamua tu kumrundikia rais majukumu mengi na yasiyo na sababu. Kimsingi wanachopendekeza hawa walioandika ni TUME YA RAIS YA KUPITIA KATIBA.
Sasa kama watu wangetaka rais aunde tume tungeomba Rais aunde tume! Hakuna aliyemuomba rais aunde tume na wala hakikuhitajika kibali chake kwenye suala la Katiba Mpya. Katiba Mpya ni zao la Watanzania na hasa ni zao la wanamageuzi nchini. Sasa kuandaa muswada wa kusimamia mchakato huo bila kuwashirikisha wanamageuzi siyo kutendea haki kwa sababu baada ya kuiteka hoja ya “katiba mpya” sasa wameenda mbele zaidi na wameamua kuteka mchakato wa kufikia Katiba Mpya na tukiwakubalia watateka na katiba mpya.
Ninachosema kwa maoni yangu ni kuwa sheria itakayosimamia mchakato wa kufikia Katiba Mpya ni lazima itambue kuwa ni katiba ni lazima itokane na wananchi, kufikiwa kwake ni lazima kuoneshe kuwa ni Katiba ya wananchi na hivyo hata muundo wa mfumo wa kuifikia uwe ni ule wenye kuheshimu hilo.
Pamoja na ukweli wa kanuni hizo hapo juu nina uhakika kuwa mswada huu unaweza kupita ukiwa na mabadiliko machache tu. Ninachojua ni kuwa endapo mswada utapita jinsi ulivyo au ukiwa na mabadiliko machache tu tutakuwa tumerasimisha mchakato wa Katiba Mpya mikononi mwa CCM. Hivyo, huu utakuwa ni utaratibu wa CCM kufikia Katiba Mpya. Yaani, wao ndio wataamua Katiba Iweje na kwa maoni yangu itakuwa ni dhambi kwa dhamira zetu kutoa ushirikiano wowote kwa tume hiyo ya Rais.
Kutokana na hilo ninaamini ni wajibu wa kila anayoengozwa na dhamira ambayo inamsuta kutoa ushirikiano kutofanya hivyo. CCM na serikali yake waendeshe mchakato wao na wafikie kwenye Katiba Mpya wanayoitaka wao. Sisi wengine tutaanza mchakato huru na wawazi zaidi baadaye.
Ushauri mwingine ambao naamini ni bora zaidi ni kuwa kikao cha sasa kifupishwe ili mambo mengine tu yajadiliwe lakini Bunge liurudishe mswada huu kwa serikali na kukusanya maoni bora zaidi (nami nitakuwa tayari kutoa maoni ya mchakato bora ambao utaakisi kanuni hizo hapo juu).
Ila kifanyike kikao maalumu cha Bunge ambacho kwa kuitwa kwake kitakuwa kinaonyesha watawala wetu wanatambua uzito wa tukio lililo mbele yetu.
Binafsi ninaamini watawala wetu bado hawajelewa uzito wa jambo hili. Yaani kuliweka kama sehemu ya kikao cha kawaida ni kutolipa jambo hili uzito wake. Ninaamini suala la Katiba Mpya ni sawasawa na Musa alipofika karibu na kichaka cha moto! Tunataka kufanya jambo takatifu na hivyo tuonyeshe uzito wake. Ninaamini kikao maalumu cha Bunge cha kujadili Muswada wa Sheria ya Kuongoza Mchakato wa Katiba Mpya kiitwe hata kama kitakuwa ni cha siku tatu tu.
Kikao hicho kisiwe sehemu, ya kikao cha kawaida (kama cha sasa) au kile cha Bunge la Bajeti. Kiwe ni kikao maalum.
Na tukifanya hivyo tutatoa muda kwa pande nyingine kutolea maoni sheria hizo na hata kwa upinzani kuja na mapendekezo ya mswada wao ili hatimaye miswada hiyo miwili (au zaidi) iweze kujadiliwa na hatimaye upatikane mswada ulio mzuri zaidi. Kama tulivyokosoa muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na watu walidhani tunawaonea wivu lakini tulikuwa sahihi nina uhakika tuko sahihi wakati huu tena.
Muswada huu ukipitisha kama ulivyo utachangia ujio wa sheria nyingine mbovu zaidi ambao katika dhamira safi baadhi yetu tutashindwa kuitii. Sasa kama tunataka kweli kufikia katiba mpya ni lazima kwanza tubadili fikra. Watawala wasidhani wanatutendea hisani na wananchi tusifikirie tunabembeleza watawala wetu. Ni bora tusubiri miaka mitano tuweze kuleta timu itakayotuongoza kufikia katiba mpya kuliko tuharakishwe ndani ya miaka hii mitano kuongozwa kuelekea kwenye machozi. Katiba mpya itokane na fikra mpya.
Hilo litawezekana vipi wakati bado wapo watu wana fikra za zamani?
 
Wabunge onyesheni uzalendo wenu kwa taifa

ban_tahariri.jpg

amka2.gif
JANA vikao vya Bunge la 10, mkutano wa tatu vimeanza mjini Dodoma huku mojawapo ya kazi zilizo mbele ya mkutano huo zikiwa ni pamoja na kupitisha muswada wa mchakato wa kuandika Katiba mpya.
Muswada huo utakaopelekwa bungeni na serikali baada ya ombi la hoja binafsi ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, kutupiliwa mbali, tayari umekosolewa na wadau mbalimbali wakiwamo waliohudhuria kongamano la Katiba lililoandaliwa na wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA).
Baadhi ya mambo yaliyokosolewa ni makosa ya lugha kimuundo na kikanuni kama ilivyoainishwa na Mwanasheria maarufu na Mhadhiri wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kigoda cha taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, Profesa Issa Shivji.
Naye Jaji Mkuu mstaafu, Barnabas Samatta, ambaye alikuwa mmoja wa wasemaji katika kongamano hilo alisema kitendo cha mwandishi wa muswada huo kutaka kutoguswa wala kujadiliwa kwa ibara zinazomhusu rais na mamlaka yake pamoja na zile za mahakama, ni kwenda kinyume cha mahitaji na matakwa ya Watanzania wa sasa.
Pengine Jaji Samatta alitoa kauli hiyo kutokana na hisia iliyokuwepo pale kwamba muswada ule unaonekana uliandikwa na mtu mmoja ambaye hakufikiri chochote bali alichofanya ni kunakili muswada wa mabadiliko ya Katiba ya Kenya uliowasilishwa miaka kadhaa iliyopita na kuibua makundi mawili ya chungwa na ndizi, moja likiupinga na jingine likiuunga mkono na hatimaye lile lililokuwa linapinga likashinda.
Makosa mengine ni kumwonyesha rais kama mamlaka ya mwanzo na mwisho, akiwa na mamlaka ya kuteua tume itakayokusanya maoni na hatimaye kutoa ripoti kwake pamoja na hoja za wadau mbalimbali zilizojitokeza.
Sisi wa Tanzania Daima Jumatano kama sehemu ya jamii tunaheshimu maoni yaliyotolewa na washiriki hao wa kongamano ambalo kimsingi ni la wanataaluma tunaowategemea sana katika kuweka mwongozo na mwelekeo sahihi wa taifa letu.
Kwa mantiki hiyo tunaungana na baadhi ya washiriki wa kongamano hilo ambao walitoa wito kwa wabunge wetu kutoupitisha muswada huo unaotarajiwa kuwasilishwa bungeni katika mkutano huo wa Bunge.
Katika hili tunasema hatutarajii kuona wabunge wetu wakiweka mbele masilahi ya vyama vyao, kwa kuwa vyama vitapita lakini taifa litabaki pale pale.
Tunawapa rai wabunge kuonyesha uzalendo wao kwa kuukataa muswada huo wa mchakato wa Katiba mpya ya nchi yetu.
 
Mizania ya siasa, uchumi kwa mlalahoi
ban.blank.jpg


Bakari Mohamed​

amka2.gif
MARA zote mfumo wa uhai wa maisha ya binadamu huongozwa na utashi wa siasa-uchumi.
Hata pale mwanzo binadamu alipoumbwa na kuachwa uwandani kwa mujibu wa kanuni za kimaumbile, aliwajibika kujitafutia riziki yake kwa jasho lake!
Hii ilikuwa, imekuwa na itaendelea kuwa ndiyo njia ya mwenendo wa binadamu hata pale atakapomaliza siku zake za kuishi kwa mujibu wa kanuni zinazotawala maisha ya binadamu.
Kwa kuwa binadamu ni kiumbe wa kijamii na anawajibika kuishi kijamii kama wanajamii wengine wanavyoishi, basi ni wajibu kwa binadamu huyo kufuata sheria, taratibu na kanuni za kimaumbile kwa jinsi ya mwenendo murua wa maisha ya kijamii na ya kibinadamu.
Hata hivyo, kwa sehemu kubwa mwenendo murua wa maisha ya kijamii kwa sehemu kubwa ya wanajamii wa dunia, Tanzania ikiwemo, umeharibiwa na ufisadi (uharibifu) wa mizania ya siasa-uchumi.
Makala hii kwa jinsi ya kifalsafa na kisayansi (uchunguzi na mantiki) yatajaribu kuonyesha jinsi mizania ya siasa-uchumi kwa mlalahoi ilivyovurugika na kuwafanya watu maskini (walalahoi) kuishi maisha ya msoto na yenye dhiki na taabu nyingi za maisha ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Kwa sehemu kubwa, mlalahoi amegeuka mtumwa wa nafsi yake na anatumika kinyume na utashi wake wa uhuru, haki na usawa. Mlalahoi hana jinsi ya kujinasua na kwa jinsi hiyo analazimika kukubali maumivu ya mbinyo wa maisha ya shida na taabu nyingi hata kama kwa shingo upande!
Japokuwa binadamu ameumbwa kwa taabu bado anahitaji maisha ya staha na yenye kuzingatia utashi wake kama mtu. maisha bora kwa kuzingatia chakula bora na cha kutosha, malazi bora na yenye faragha, afya bora na endelevu, huduma bora na endelevu za kijamii, mavazi yenye heshima na sitara kwa rika zote, na siasa inayoendeshwa kwa uhuru, haki na usawa baina ya makundi yote ya kijamii.
Kwa ujumla, maisha ya kiumbe wa kijamii (binadamu) yanahitaji ustaarabu wa utu na heshima inayozingatia utu wake. Huu ndio mwenendo wa ustaarabu juu ya kufikia saada ya maisha ya staha na raha kwa mujibu wa kanuni za kimaumbile.
Mlalahoi, kama anavyotafsiriwa kwa maana ya neno, ni mtu mwenye maisha duni kutokana na kuwa na kipato kidogo. Mlalahoi ni mtu mwenye fursa chache na au zisizoweza kutumiwa kabisa katika kumuongozea tija na saada kwenye mzingo wa maisha yake kama kiumbe wa kijamii.
Kwa ujumla, walalahoi ni wale wote wanaoishi kwa taabu na dhiki za maisha zinazotokana na mbinyo wa ufinyu wa fursa za kiuchumi hali inayosababishwa na mizani ya siasa-uchumi kuzidi upande mmoja.
Hususan, siasa isiyozingatia maslahi ya walalahoi kutumia fursa za kiuchumi kwa maslahi binafsi ya watu wachache kwenye mfumo wa siasa-uchumi.
Inawezekana wasomaji wakadhani ulalahoi ni hali ya kukosa kazi na au hali ya kujishughulisha na kazi (zisizo rasmi) na zenye kipato kidogo na au kisichokidhi haja kiuchumi. La hasha, ulalahoi ni hali ya jumla ambayo mtu (yeyote na wa kada yoyote ile) anaposhindwa kukidhi mahitaji yake muhimu ya kila siku kutokana na uwezo mdogo wa kiuchumi.
Kwa jinsi hiyo, hata wafanyakazi (wa sekta ya umma na au binafsi) wanaolipwa ujira (mishahara) usiyokidhi maisha yao ni walalahoi! Hawa ndio wale wanaominywa na kusubiri mwisho wa mwezi ilhali wamezongwa na madeni huku na huko.
Maisha ya mlalahoi yamegubikwa na tamaa ya kupata kwa bahati nasibu (sadfa) japokuwa ni nadra kufanikiwa. Mlalahoi mara zote haishi kuitesa saikolojia (akili) yake kwa kufikiria mawazo mzunguko yanayomsababishia msongo wa mawazo hatimaye kumtia magonjwa kama shinikizo la juu la damu, tumbo kujaa hewa, na hata vidonda vya tumbo kutokana na fikra mzunguko zisizokuwa na suluhisho!
Mlalahoi anataabika na njaa ya kutaka kushiba kwenye mfumo ambao kwa jinsi yake ataendelea kuota ndoto za maisha bora ilhali siku za uhai wake zikipungua kwa kasi kwa kuzongwa na madeni yasiyolipika!
Mlalahoi hata kama ataonekana na afya (siha) njema ya kiwiliwili. Ieleweke kuwa akili (saikolojia) yake inaumwa maradhi makubwa na yasiyokuwa na tiba (hata kwa kikombe cha Babu wa Loliondo).
Maradhi ya akili ya mlalahoi ni kule kuota ndoto ya maisha bora hata kwa kudanganywa kujengewa "ghorofa angani" kama alivyokuwa akiota Abunuwas (kwenye Hekaya za Abunuwas). Mlalahoi ni mtu aliyekata tamaa ya maisha na hivyo haonekani kujitoa kwenye mzingo wa fikra mzunguko hadi pale atakapopata fikra ya ukombozi na kuipindua akili yake.
Kwa kuwa sehemu muhimu ya maamuzi yanayoweza kumponya mlalahoi juu ya maradhi ya fikra mzunguko na au mawazo mgando yanayomtweza nguvu hata kujiona ni dhalili asiye na jinsi, ni fikra-huru; na kwa kuwa mlalahoi hana budi kuleta mapinduzi ya fikra ili kuondokana na unyonge wake.
Kuna kila sababu kwa mlalahoi kuchukua nafasi yake ya kutumia fursa zinazomzunguka katika kupambana na mazingira yasiyo rafiki kwa mustakabali wa maisha yake na ya jamii yake sawia. Mlalahoi lazima apambane na fikra hasi ili azibadilishe na kuwa fikra chanya katika kujenga mizania sawa ya siasa-uchumi.
Tuchukue kundi kubwa la walalahoi, kama mfano wa kwanza, wakulima maskini wa vijijini. Hili ni kundi kubwa linalokadiriwa kufikia asilimia zaidi ya 75 kwa mujibu wa takwimu zinazokubalika Tanzania.
Wakulima walalahoi wa Tanzania wametelekezwa na wamejitelekeza kwa muda mrefu na wamebaki kuimba nyimbo zilezile za "TANU yajenga nchi" ilhali wachache wamekwisha imomonyoa (kwa pupa na ulafi) keki (tamu) ya taifa!
Wakulima vijijini wamebaki na jembe lilelile la mkono (kiserema) la tangu enzi za ujima! Wakulima wamesahaulika na wamejisahau, hakuna wa kuwatetea japokuwa wanaalikwa kuhudhuria karamu ya "Kilimo Kwanza" ilhali wenye tai shingoni ndiyo waalikwa!
Ana nini mkulima zama hizi? Ni suala linaloweza kuwakera wapanga sera, hata hivyo, ukweli utabaki kuwa wakulima walalahoi (wadogo) ndio waliyotelekezwa na nguvu ya serikali imeelekezwa kwa wakulima wakubwa na wa kati wenye nafasi za mtaji (na elimu ya ujasiriamali) ambao kwa sehemu fulani ndiyo wanaokopesheka na taasisi za fedha na au ndiyo wanaowanyonya wakulima wadogo kwa kuchuuza mazao yao yakiwa shambani kwa kisingizio cha kuwatafutia masoko ya uhakika.Mkulima mlalahoi amebaki shambani ilhali mazao yake yakichuuzwa kwa bei ya ubwete na walanguzi!
Kundi la pili, kama mfano, ni la wafanyakazi wa kada za chini. Kwa ujumla, wafanyakazi wa kada za chini na wale wanaoitwa wafanyakazi vibarua kwenye sekta za umma na binafsi wamekuwa wakisota msoto mbaya mbele ya waajiri wao.
Maisha ya wafanyakazi hawa hutegemea kipato cha mwisho wa mwezi. Hata hivyo, sio mwisho wa mwezi ule unaoweza kumfanya mfanyakazi aweze kumudu maisha ya siku angalau ishirini na tano za mwezi kwa kujikimu kwa mahitaji yake muhimu kama vile chakula, kodi ya pango la nyumba, matibabu, elimu ya watoto wake, na hatimaye kujiwekea akiba.
Kipato cha mfanyakazi malalahoi ni kiduchu ambacho kwa jinsi yoyote hakiwezi kukidhi mahitaji muhimu ya mwezi mzima.
Hapa ndipo mfanyakazi mlalahoi, atake asitake, anapowajibika kuingia kwenye msongo wa kukopa madeni hata kama yenye riba kubwa.
Pamoja na kukopa kwenye taasisi za fedha kama mabenki, wengi wa wafanyakazi walalahoi wa umma na wa binafsi wanakopa kwenye maduka mbalimbali yanayouza bidhaa za mahitaji ya kila siku.
Kwa ujumla, na ukweli usiopingika ni kwamba sehemu kubwa ya wafanyakazi walalahoi wana madeni kwenye maduka hata ya mitaani wanakoishi.
Kwa wale waliobahatika kufanyakazi za kada za juu na kada za kati kwenye taasisi za umma na au za binafsi wanapata walau kiasi cha kumudu maisha ya kifamilia kwa sehemu fulani ya maisha.
Hata hivyo, kwa jinsi ya maisha ya kijamii yalivyosukwa na jinsi wananchi wa Tanzania wanavyoishi kijamaa kuna kila sababu ya kudhani kwamba wale wote wenye nafasi ya mishahara mizuri kiasi wana kila sababu ya kuishi maisha ya kujitolea na au kujikamua ili kusaidia jamii zao katika kugawana umaskini na ulalahoi.
Wengi wa watu wenye mapenzi mema na ya kijamaa (kiukoo na au kifamilia) wanafanyakazi ya ziada katika kusaidia watu wa jamii zao kwa jinsi wanavyoweza.
Pamoja na ukweli huu, kuna hali ya ubinafsi iliyojengeka baina ya watu na jamii zao hali inayofanya sehemu kubwa ya maisha ya wananchi walalahoi kuwa kwenye mashaka makubwa kwa vile wanaonekana kama ni waliyokosa matumizi mazuri ya fursa.
Sehemu ya watu wenye bahati ya kuwa kwenye mduara wa ndani wa maisha bora na yenye raha wanadhani kwamba huo ni ujanja wao na wanasahau kwamba walalahoi wamefanywa hivyo na mfumo usiyozingatia mizania ya uhuru, haki na usawa juu ya siasa-uchumi.
Siasa-uchumi isiyozingatia uwiano wa matumizi ya uhuru, haki na usawa juu ya fursa na rasilimali katika kujenga jamii ya watu waliyo sawa na huru ndiyo iliyofanya kuwepo kwa kundi kubwa la walalahoi na kundi dogo la matajiri wanyonyaji wanaonyonya jasho la walalahoi wengi wa mijini na vijijini.
Haya yalishuhudiwa na mwanafalsafa wa sayansi ya uchumi-jamii, Vilfredo Pareto alipofanya utafiti na kuthibitisha kwamba asilimia 20 ya watu wanamiliki utajiri mkubwa wa asilimia 80 ilhali sehemu kubwa ya watu wanamiliki sehemu ndogo ya utajiri.
Kwa jinsi hii, kama alivyobainisha Vilfredo Pareto (na kuthibitishwa na Lorenzo), ni ukweli kwamba watu wengi wanapogawana sehemu ndogo ya utajiri kuna kila sababu ya kila mmoja miongoni mwa wengi kupata kiduchu, jambo linalosababisha ongezeko la umaskini na watu maskini.
Pengo la kipato (tofauti) baina ya matajiri wachache na maskini wengi ni kubwa sana na hata haliwezi kupunguzwa kwa kuwa matajiri wanatumia nafasi yao katika kuzitumia fursa zote katika kuchuma zaidi na kulimbikiza mali kwa kutumia gharama za walalahoi.
Walalahoi wamekuwa wakinyonywa ilhali matajiri wakitumia nafasi yao katika kuhakikisha kuwa hakuna mtu na au kikundi cha watu wanaoweza kuzuia mfumo wa unyonyaji na uporaji na au kuhodhi utajiri.
Wafanyakazi walalahoi wamekuwa wakipuuzwa madai yao na au hata kuzibwa midomo kwa mbinyo wa sheria na kanuni zinazolinda maslahi ya matajiri badala ya kuwalinda walalahoi.
Vyama vya wafanyakazi vimekuwa vikikosa nguvu kwa utumizi wa rungu la sheria kandamizi hali inayochochea kukata tamaa kwa sehemu kubwa ya jamii ya wafanyakazi katika kudai maslahi bora na yanayokidhi hali halisi ya maisha ya siasa-uchumi kwa kuzingatia mahitaji ya muda.
Kwa jinsi hii, wafanyakazi na wakulima walalahoi wamekalia kuti kavu juu ya mnazi mrefu uliyoparama! Maisha ya kiuchumi ya walalahoi yamewekwa rehani na mfumo mbovu wa siasa-uchumi ambao kwa jinsi yake umepoteza uhalali wa kuwatumikia watu kwa uwiano wa uhuru, haki na usawa.
Hakuna mtu anayetamani kusimamia ukombozi wa walalahoi kwa dhati ya nafsi yake miongoni mwa waliyepewa nafasi ya kuongoza mapambano ya kujenga jamii ya watu waliyo sawa na huru. Kila mmoja na lwake, ubinafsi kayaya umekuwa ndio mwenendo wa kuongoza watu.
Walalahoi wameachwa wahangaike huku na huko katika kutafuta riziki kidogo inayopatikana kwa shida na taabu nyingi ilhali viongozi wenye mamlaka na dhamana ya kuwatumikia wananchi hao wakifanya starehe na kuponda raha na anasa kwa matumizi yasiyoelezeka na hata wengine kudiriki kusema kwamba, "hawajui sababu za umaskini wa wananchi wa Tanzania."
Sikutegemea kama Tanzania, kwa miaka hamsini ya uhuru, ingefikia upeo huu wa uongozi kushindwa kujua sababu za watu wake kuwa maskini! Je, hii ni laana? Au, kwa mtazamo wa kifalsafa tuseme, "aliyeshiba" hamjui mwenye njaa!
Sidhani kama ni muafaka na ni sahihi kwa uongozi makini na unaozingatia uhuru, haki na uadilifu kutumia fursa zote za kuwaondolea shida na taabu watu wake kwa kebehi! Kama walalahoi wa Tanzania wamefikia hatua ya kufanyiwa kebehi ya hali ya juu kwa jinsi hii, sidhani kama kuna dhamira ya dhati na makusudi ya kudadavua tatizo la umaskini linalowakabili wananchi wengi wa Tanzania.
Kwa kuwa hakuna asiyetambua matatizo mengi yanayowakabili wananchi wa Tanzania – mijini na vijijini na kwa kuwa hata viongozi kwa jinsi wanavyoongoza wamesahau wajibu wao wa kuleta hali bora kwa wananchi waliyo wengi maskini.
Ni haki ya kila mwananchi kutumia fursa hiyo katika kuleta mapinduzi ya fikra na kuondokana na unyonge unaotokana na umaskini wa kipato.
Ni wakati wa kutambua wajibu wa kutumia rasilimali pekee ya mnyonge – umoja! Kwa pamoja, walalahoi wanaweza kutumia fursa zilizopo kwa gharama nafuu katika kuleta mapinduzi ya fikra, kama alivyowahi kusema nguli wa reggae, Bob Marley, "jiondoeni (wenyewe) kutoka kwenye utumwa wa kiakili; hakuna (awezaye) kuwaondoa isipokuwa (nyinyi) wenyewe!"
Walalahoi wengi wana akili angavu na wana utambuzi makini na hakuna awezaye kuwazuia wasilete mapinduzi ya fikra na kuchukua uongozi wa kuleta hali bora na mizania ya uhuru, haki na usawa kwenye siasa-uchumi.
Ni wajibu kwa viongozi wa kijamii kuchukua nafasi zao katika kuonyesha njia ili kwa njia hiyo walalahoi wapate msaada katika maisha yao kwa mujibu wa mgawanyo wa haki na wa usawa wa fursa kwa matumizi makini na endelevu ya rasilimali zilizopo.
Kila mmoja kwa nafasi yake ahakikishe anatumia nafasi yake kwa manufaa ya taifa la Tanzania. Kila mmoja akatae ubinafsi kayaya na apige vita ufisadi wa kimfumo na wa ndani ya mfumo katika kuhakikisha jamii inaongozwa kwa misingi ya uhuru, haki na usawa bila ya ubaguzi na upendeleo wa jinsi yoyote.
Tanzania inaweza kufikia malengo ya maendeleo ya karne (Millenium Development Goals – MDGs) kama kila mmoja atatamani kumsaidia mwenzake kwa uhuru, haki na usawa. Mapenzi ya utaifa (uzalendo) na undugu baina ya wananchi ndiyo njia pekee ya kuifanya Tanzania kupata mizania ya haki juu ya siasa-uchumi.


h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa simu: +255 713 593347
Barua pepe: maligwa1968@yahoo.com
 
CCM changeni vyema karata hii
ban.blank.jpg


Ruhazi Ruhazi​

amka2.gif
KIKAO cha Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kinatarajiwa kuanza keshokutwa katika ofisi za makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma.
Nakiona kikao hicho kama turufu ya mwisho wanayoichanga CCM, kwamba wakichemka katika uchangaji wao huo, basi wamekizika chama chao na binafsi nitawashauri warejee vijijini wakalime.
Ni dhahiri kuwa kikao hicho kitakuwa na mvutano na malumbano mazito ambayo kama mchangaji wa karata viongozi wakikosea katika kukiendesha majuto yatawajia muda si mrefu ujao.
Viongozi wa CCM wanalo jukumu la kuzichanga vema karata zao ili wayaweke madume na mizungu upande wao huku wakiwaachia garasa upande wa pili ambao ni wapinzani wao, kinyume na hivyo basi zama zao zitakuwa zimekwisha.
CCM wanayo kazi ya ziada katika kuuzika mpasuko uliojitokeza taratibu baina ya wanachama wake na kuanza kupapaliwa na kurutubishwa na Umoja wa Vijana wa Chama hicho (UVCCM).
Majibizano, kurushiana maneno, kupakana matope kupitia vyombo vya habari, kukinanga chama hadharani ni mambo yaliyoshamiri kwa sasa ndani ya chama hicho.
Mambo haya kwa sasa yamekuwa kama fasheni mpya kwa wana CCM na laiti kama hakutaptikana suluhu katika kikao hicho basi tutasubiri kujionea makubwa yakiibuka katika siku chache zijazo.
Yote hayo yameibuka na yataendelea kuibuka kwa kinachoaminika kuwa ni kuanza kujipanga kwa makundi na watu binafsi kwa ugombea wa urais mwaka 2015, kupitia chama hicho.
UVCCM, imetoa matamko makali yakiwalenga baadhi ya viongozi wenye nyadhifa ndani ya serikali pamoja na wale walio nje ya uongozi kwa sasa lakini bado wana nguvu au heshima ndani ya chama chao.
Vijana hao wa CCM ambao walitarajiwa kuwa viongozi wa chama hicho na pengine taifa siku zijazo, wamewanyooshea vidole Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye, Waziri Mkuu wa kwanza wa awamu ya nne aliyelazimika kujiuzulu Edward Lowassa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.
Kwa ujasiri wa hali ya juu viongozi wa UVCCM, hawakutaka kuuma maneno bali waliwashambulia viongozi hao wakisema wameanza kujijenga kuwania urais wa mwaka 2015 ndiyo maana wanadiriki kukikosoa chama chao hadharani.
Kauli hizi na nyingine zilizotolewa na zinazoendelea kutolewa na viongozi wa UVCCM pamoja na baadhi ya viongozi wa CCM, zinanishawishi kuamini kuwa kikao hiki cha Dodoma kitakuwa sawa na moto ulio katika tanuri.
Ni kikao kinachohitaji hekima na busara ya hali ya juu, kueza kuzika uhasama na kunyoosheana vidole ili kurejesha umoja na mshikamano wa kichama, kinyume na hivyo, tutegemee kuzaliwa kwa uhasama zaidi ndani ya chama.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba, hawa waliotajwa ni wachache kuliko wana CCM halisi ambao kwa sasa wanatizamwa vibaya na UVCCM na pengine wengine kati yao hawatajwi kutokana na sababu maalum.
Sumaye na Lowassa wamekwisha thibitisha kuwa kinachowafanya wasemwe na vijana wa UVCCM ni nafasi ya urais wa awamu ya tano, ambayo itawaniwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Hoja ya viongozi wa UVCCM pamoja na ya viongozi wa CCM kuwataka, Sumaye, Lowassa, Sitta na wengine kuzungumzia masuala ya chama nje ya vikao vya chama ni usaliti.
UVCCM na CCM, wanaona kusemwa nje ya vikao sio kukumbushwa ili kurejea katika mstari bali ni kuchafuliwa na wao wanaamini hawapaswi kuchafuliwa na yeyote yule aliye ndani au nje ya chama hicho.
Binafsi sitaki kujua iwapo ni kweli wana CCM hao wanaoshambuliwa na viongozi wa UVCCM na CCM kwa ujumla wana nia ya kuwania urais 2015 ama la, lakini ambacho kinanikera ni kule kurushiwa maneno makali.
Binadamu yeyote kwa asili, ni kiumbe anayehitaji na kupenda kuheshimiwa na kuthaminiwa na ndiyo maana Sumaye alilazimika kutoka Hanang', mkoani Manyara na kufunga safari hadi Dar es Salaam kuja kuzungumza na vyombo vya habari.
Kujitetea kwake pamoja na kujitetea kwa Lowassa, kunathibitisha hilo na kuonyesha ni jinsi gani walikereka au kuathirika kutokana na kushutumiwa na kulaumiwa huko.
Pamoja na hilo pia kikao hiki kitakuwa na jukumu la kuzungumzia mustakabali wa uongozi wa juu wa chama hicho hususan nafasi mwenyekiti wa Chama baada ya baadhi ya wana CCM kutaka kiti hicho kitenganishwe na kiti cha urais.
Wanaoitetea hoja hiyo wanasema inakuwa vigumu kwa chama kumshauri au kumwajibisha mwenyekiti wake pale anapokwenda upogo kutokana na kofia ya urais ambayo kimamlaka ya nchi ni cheo cha juu mno.
Ni kutokana na hilo, baadhi yao sasa wanadhani umefika muda kofia hizo mbili za uongozi zitenganishwe, kwamba ikitokea chama kimeshinda kiti cha urais, mwenyekiti wake asigombee nafasi ya mwenyekiti wa chama.
Kuna baadhi ya wana CCM wamekuwa wakimnyooshea kidole moja kwa moja Mwenyekiti wao Rais Jakaya Kikwete ‘JK', kwamba kunyamaza kwake kimya baada ya matamko makali kutolewa na UVCCM, kunatokana na yeye kuwa na mkono juu ya hilo.
Wale wenye mtazamo huo nao wanaungana na kuupa nguvu upande unaotaka kushinikiza mabadiliko ndani ya CCM kuweza kutenganisha kofia hizo za uenyekiti na urais.
Hoja yao kubwa ni kuwa mwenyekiti wa anapokuwa na upande anaouegemea atakuwa na urahisi wa kufanikisha azima yake kwa sababu atatumia kofi ya urais na wala sio ile ya kichama.
Hoja ya wana CCM kutoka visiwani kutaka suala la mgombea nafasi ya urais wa chama hicho irejee katika kupokezana kati ya bara na visiwani nalo linaweza kuleleta kizaazaa kingine ndani ya kikao hicho kama litafikishwa na wale wajumbe kutoka visiwani.
Utata wa suala hilo kama litawasilishwa linaweza kutibua kila kitu kutokana na uchache wa wajumbe kutoka Zanzibar, jambo ambalo linaweza kuanzisha malumbano ya hoja ikatokea uamuzi wa hilo kuamuliwa kwa kura.
Wazanzibari hawatakubali kupigiwa kura kwa kuwa wanafahamu fika wakikubali hilo watabwagwa, kutokana na uchache wao lakini ni namnagani watashinikiza, hoja yao tunasubiri kusikia kitakachotokea.
Kitu kimoja kilicho wazi ni kuwa wapinzani wa sera au mfumo wa CCM wa ndani na nje ya nchi wanaombea kikao hicho kizae kutokubaliana na kutoelewana mwanzo hadi mwisho ili yatimie wayatakayo.
Binafsi nawaambia CCM vyovyote iwavyo, cha muhimu kwenu ni kuzichanga vema karata zenu katika kikao hicho kwani kosa moja litawagharimu na kuwapa pigo ambalo hamtalisahau.


h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa simu 0713 - 765757, barua pepe: wiruhinda@yahoo.com
 
Askofu Ruzoka amlima barua Waziri Kombani


*Aonya muswada wa katiba utachochea hasira zaidi
*Ataka taifa lipate muda wa kufaa na chombo huru
*Muswada wawasilishwa bungeni, wazua malumbano


Na Waandishi Wetu

WAKATI Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ikipewa jukumu la kujadili na kukusanya maoni ya wadau kuhusu muswada wa
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Tume ya Haki na Amani inayoongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Tabora, Mhashamu Paulo Ruzoka, imemlima barua Waziri wa Katiba na Sheria Bi. Celina Kombani.

Katika Barua hiyo Askofu Ruzoka ambaye pia ni mwenyekiti wa tume hiyo, alionya kuwa muswada huo utachochea hasira za wananchi.

Barua hiyo ilikuwa na kichwa kichwa cha habari
"Hofu na mashaka ya wananchi kuhusu muswada wa mapendekezo ya kutungwa kwa sheria ya madiliko ya Katiba ya nchi ya mwaka 2011".

Katika barua hiyo Askofu Ruzoka alisema suala hilo linaweza kuchochea hasira ya jamii kwa kutofuata njia inayostahili kwa kuwa mamlaka yote ya kuratibu kazi hiyo yanatoka na kuishia kwa rais.

"Mheshimiwa Waziri...Baada ya kuusoma muswada huu tulishangazwa kuona mchakato wote unaanzia na kuishia kwa Rais na kwamba Chombo Kikuu cha kuratibu mchakato wote ni Tume itakayoteuliwa na Rais ambaye ni Mwenyekiti wa Chama tawala," ilisema sehemu ya baurua hiyo na kuongeza:

"Tunatambua kwamba kilio cha kutaka Katiba mpya kilitokana na utashi mwema na pia hasira njema ya jamii ya Watanzania wakitaka mabadiliko yaliyo na hekima na utu.

Alisema wao kama wapenda amani na utulivu wa nchi wanahofia kwamba maudhui na mwelekeo wa muswada huo ambao uliwasilishwa bungeni na kusomwa mara ya kwanza jana kwa hati ya dharura, havitakidhi mahitaji mazito ya Watanzania.

"Huenda ukachochea hasira ambayo imekwisha jidhihirisha katika jamii yetu.

Tunakuomba ulisimamie zoezi la marekebisho ya katiba kwa hekima sana ukiongoza tafakari jadidi na elimu angavu itakayowezesha zoezi lote kuwa la mazungumzo ya kitaifa kweli kweli huku amani, maelewano na makubaliano vikilindwa katika wakati huu mgumu," alionya Askofu Ruzoka katika barua hiyo.

Aliomba Waziri Kombani kulipatia taifa muda wa kutosha na chombo huru kinachoaminika kuongoza wananchi kufikia makubaliano yatakayojenga msingi imara na kukidhi matarajio.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu akiwa mjini Dodoma, Waziri Kombani alisema hadi muda huo wa jana jioni alikuwa hajapata barua hiyo.

Hata hivyo, aliomba mwandishi wetu kumsomea yaliyomo kwenye barua hiyo na alipoulizwa maoni yake alisema hawezi kuzungumza lolote hadi hapo atakapolipata mezani kwake.

Malumbano bungeni

Wakati huo huo, mjadala huo mzito uliibuka bungeni jana kutokana na tangazo la Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda, kuwa muswada huo uliowasilishwa kwa hati ya dharura utajadiliwa na wadau katika vituo viwili vya Dodoma na Dar es Salaam pekee.

Kutokana na kuwasilishwa bungeni kwa hati ya dharura, Bi. Makinda alisema utaratubu wake utatofautina na ile inayopitia utaratibu wa kawaida.

Alisema kutokana na suala hilo kupendwa na wananchi wengi mijadala itakuwa katika ukumbi wa bunge wa Msekwa mjini Dodoma ambapo Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria itakuwepo huku kituo kingine kikiwa katika ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam.

Mbunge wa Jimbo la Mkanyageni (CUF), Bw. Mohamed Habib Mnyaa, alikuwa wa kwanza kuhoji kutowekwa kwa kituo cha majadiliano ya muswada huo Tanzania visiwani wakati suala la katiba likiwa ni la Muungano.

"Kwa nini Zanzibar napo pasiwepo na kituo cha wadau kukutana na kuujadili muswada huo kama ambavyo mmeona kuna umuhimu wa kuweka vituo Dodoma na Dar es Salaam ili mpate mawazo ya wengi, hamuoni kama hili suala ni la nchi nzima," alihoji Bw. Mnyaa, ambaye aliungwa mkono na Mbunge wa Mji Mkongwe, Bw. Mohamed Ibrahim Sanya.

Akijibu hoja hiyo, Bi. Makinda alisema vituo hivyo vilipangwa kwa kuzingatia mahitaji na kuwaomba kila mmoja atoe maoni yake kwa uwazi ili suala hilo liweze kufikiwa kwa ufanisi mkubwa.

"Kikubwa katika hili jambo watu tuaminiane, tujadili kwa uwazi ili baadaye bunge liamue na kwenye huu muswada watu wasiupotoshe, hii ni hatua ambayo inaangalia ni namna gani tunaingia kwenye hatua ya katiba," alisema Spika Makinda.

Alisema muswada huo uko chini ya hati ya dharura na kwa maana hiyo unatakiwa kuwasilishwa haraka ili michakato mingine iweze kuendelea.

Mvutano wa pili ulihusu muswada huo kuandikwa kwa lugha ya Kiingereza badala ya Kishwahili ambayo ni lugha ya taifa ulimlazimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema kutoa ufafanuzi.

Akijibu hoja hiyo, Jaji Werema alikiri umuhimu wa muswada huo kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili kwa kuwa inafahamika na kusisitiza kuwa umuhimu huo ndio uliosababisha katiba ya sasa kutumia kiswahili.

"Hilo tumelizingatia na katika hayo maeneo kutakuwa na watu ambao wanatoa tafsiri ya muswada huo ili wadau waweze kuuelewa vizuri na hatimaye watoe maoni yao, hivyo sidhani kama kutakuwa na tatizo katika hilo," alisema Jaji Werema.

Kwa upande wake Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, alitaka kusimamishwa kwa mchakato huo ili wabunge wapate fursa ya kwenda majimboni mwao kuzungumza na wananchi kuhusiana na mchakato huo.

"Kama huu muswada hautatoa mwanga vizuri hili jambo halitafikiwa kwa mafanikio, pamoja na kuja na hati ya dharura ingekuwa vyema ukasimamishwa ili wabunge tupate fursa ya kurudi majimboni na kuwaeleza wananchi ambao ndio hasa walengwa," alisema Bw. Zitto.

Hata hivyo, hoja hiyo ilizimwa na Spika Makinda kwa kueleza kuwa mbunge huyo alikuwa ni miongoni mwa wabunge waliotaka muswada huo uwasilishwe haraka na uende na hati ya dharura.

Aliwataka wabunge kushiriki katika majadiliano na wadau yatayoendeshwa na Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala wa Bunge.

Katika hatua nyingine Kikao cha kwanza cha mkutano wa tatu wa bunge la 10 lilianza jana kwa mjadala mkali baada ya wabunge kadhaa kumbana Spika Makinda wakitaka mwongozo wake kuhusu mambo kadhaa.

Baadhi ya mambo hayo ni majibu yaliyotolewa na baadhi ya mawaziri pamoja na hatua wanazoweza kuchukua iwapo Waziri akijibu swali nje ya eneo aliloulizwa na mbunge.

Akitoa mwongozo wake Spika Makinda alitaja njia tatu zinazoweza kutumiwa na mbunge kuwa ni pamoja na kutumia kifungu cha 50 kifungu kidogo cha kwanza, kifungu cha 28 kifungu kidogo cha 8 pamoja na kifungu cha 63 kifungu kidogo cha sita.

Imeandikwa na John Daniel na Grace Michael
 
Mashirika yapinga mapitio ya katiba Send to a friend Wednesday, 06 April 2011 21:56

Exuper Kachenje
WAKATI juzi Serikali iliwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba ambao ulisomwa kwa mara ya kwanza, mashirika manne ya kiraia nchini yamesema kuwa muswada huo umempa rais ,mamlaka makubwa na haufai.

Mashirika yaliyotoa msimamo huo kupitia katika taarifa yao ya opamoja ni Policy Forum, Jukwaa la Katiba, HakiArdhi na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC),.

Katika taarifa hiyo iliyosambazwa katika vyombo vya habari, mashirika hayo yamekosoa maeneo saba ya muswada huo na kutoa mapendekezo matano.Yamesema a muswada huoumempa madaraka zaidi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hautoi ukomo wa muda wa mchakato wa kupata katiba mpya.

"Muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba una mapungufu na haufai, umempa rais mamlaka makubwa mno, hauweki ukomo wa mchakato wa kupata katiba mpya," ilisema sehemu ya taarifa ya mashirika hayo.

Taarifa hiyo ilianisha kasoro za muswada huo kuwa ni pamoja na
kuandikwa kwa lugha ya Kiingereza, bila kuzingatia kuwa asilimia 80 ya Watanzania, wanazungumza na kuelewa Kiswahili.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hali hiyo itawafanya Watanzania wengi, washindwe kushirikji kikamilifu katika kutoa mapendekezo yanayohusu katika mpya.Mashirika hayo yalisema wa vyovyote vile, muswada huo haufai."Ukiangalia jina la muswada huu, haliakisi utungwaji wa katiba mpya bali ni kufanya mabadiliko katiba iliyopo," ilisema taarifa.

Ilieleza kuwa muswada huo hauna malengo mahsusi na kwamba una vifungu vilivyorudiwa na kutoa mfano wa kifungu cha 9, 17 .Hali kadhalika vifungu vya 23(3) na 26 ambavyo vimeelezwa kuwa vina mkanganyiko na makosa zaidi ya arobaini .

Ikizungumzia mamlaka ya rais, taarifa ilisema muswada huo umempa kiongozi huyo mamlaka ya kuunda tume na kuteua wajumbe, kutoa hadidu za rejea kwa tume hiyo, kumteua katibu wa sekretariati ya tume, kupokea taarifa na tathmini na kuunda Bunge maalum la Katiba bila kujali kuwapo kwa Bunge la Muungano na Katiba iliyopo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo muswada huo pia una kasoro kwa kuwa hauelezi ushirikishwaji wa vyombo rasmi vya utungaji katiba na kupendekeza kuwapo kwa vyombo vya mchakato wa kuwa na katiba mpya.

Walivitaja vyombo hivyo kuwa ni pamoja na Tume ya kupokea mapendekezo ya Katiba, Bunge maalum la katiba, Mkutano wa kitaifa wa Katiba, kura ya maoni ya wananchi na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata hivyo, katika mapendekezo yake mashirika hayo yameomba muswada usambazwe kwa wananchi kupitia vyombo vya habari,taasisi za umma,serikali za mitaa ili wananchi waweze kujua maudhui yake.
 
Bunge lawaka moto
• Kamati ya Mrema, Cheyo zaibua ufisadi wa kutisha

na Martin Malera, Dodoma


amka2.gif
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa inayoongozwa na Kamati ya Hesabu za Serikali Kuu na ile ya Mashirika ya Umma, zimeibua ufisadi wa kutisha ulioligeuza taifa kuwa shamba la bibi.
Kamati hizo ambazo zinaongozwa na Augustine Mrema (TLP), John Cheyo (UDP) na Zitto Kabwe (CHADEMA), ziliwasilisha taarifa zake za mwaka wa fedha wa 2008/2009 jana bungeni.
Katika halmashauri za wilaya nchini, ufisadi mkubwa umebainika kuwepo katika ununuzi wa spea za magari kwa kuongeza bei isiyo halisi, bei ya kughushi katika ununuzi wa mafuta, matumizi makubwa kwa ajili ya posho kuliko utekelezaji halisi wa miradi kama ya (TASAF), Mazingira na miradi mingine ya maendeleo.
Akiwasilisha taarifa ya kamati yake, Mrema alisema kwa mujibu wa ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka wa fedha 2008/2009, Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga ilitumia sh milioni 2.9 kwa ajili ya kutengeneza pikipiki ya Kichina, iliyonunuliwa kwa bei ya chini kuliko ile iliyotumika kuitengenezea.
Alisema katika Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro, kamati yake ilibaini kuwa halmashauri ilitumia sh milioni 15 kwa ajili ya kununua spea ya gari (Injector Pump ya Land cruiser had top).
"Lakini tulipofuatilia kwa kupiga simu kwenye duka lililouza spea hiyo, tuliambiwa bei yake ni sh milioni tatu," alisema Mrema na kuwaacha wabunge wakibaki na mshangao.
Mbunge huyo wa Vunjo aliendelea kusema kuwa kuna wilaya nyingine ambayo hata hivyo hakuitaja, waligundua kuwa ilitengewa sh milioni 12 kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa wa ukimwi, lakini kati ya hizo sh milioni kumi zilichakachuliwa na sh milioni mbili tu ndizo zilizowafikia walengwa.
Kwa mujibu wa Mrema, katika kipindi hicho cha mwaka wa fedha, taarifa za CAG zimebaini kuwa mali za sh milioni 111.2 zilitumika kununulia mali za halmashauri mbalimbali, lakini hazikuandikwa kwenye vitabu vya mali za halmashauri husika na sh milioni 158, zilitumika kununulia mafuta ambayo matumizi yake hayajulikani.
Akiendelea kuibua ufisadi katika halmashauri za wilaya katika kipindi cha mwaka wa fedha 2008/2009, Mrema alisema sh milioni 792.9 katika halmashauri 40 nchini, zililipwa kama mishahara hewa kwa watumishi waliokwisha kufariki dunia na wengine kustaafu.
Lakini wakati sh milioni 792.9 zikilipwa kama mishahara hewa, sh bilioni 1.7 za mishahara isiyokuwa na wenyewe haikurejeshwa hazina na kusababisha hasara kubwa kwa taifa.
Huku akisikilizwa kwa makini na wabunge, Mrema alisema kiasi hiki cha mishahara hewa kina uwezo wa kujenga madarasa 113 ya shule za msingi nchini.
"Shilingi bilioni 328.2, zilizotolewa kwa ajili ya shughuli za maendeleo katika halmashauri 132, hazikutumika, sh bilioni 1.9 zilizokusanywa kama mapato ya ndani, katika halmashauri 43, hazikurejeshwa na mawakala kwenye halmashauri husika.
"Katika mwaka huo huo, halmashauri 113, zilikuwa na jumla ya madeni yaliyofikia sh bilioni 35.6, katika mwaka huohuo, vitabu 1,341 vya makusanyo ya mapato mbalimbali, havikupatikana kwa wakaguzi katika halmashauri 50. Kutaja mifano michache tu," alisema Mrema.
Ili kukomesha tabia hiyo, Mrema alisema kamati yake imependekeza mambo kadhaa ikiwemo kamati za Bunge za usimamizi kufuatilia fedha hizo mara zinapotolewa.
Kuhusu mishahara hewa, Mrema alisema waliohusika kwanza wazirejeshe, pia Hazina iache utaratibu wa kutuma pesa kwenye akaunti ya watumishi moja kwa moja bila kupitia kwa waajiri wao.
Cheyo na Kamati ya Hesabu za Serikali
Wakati Mrema akiibua ufisadi katika halmashauri za wilaya nchini, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu, John Cheyo, aliishukia Wizara ya Maliasili na Utalii kwamba kuna makampuni ya kitalii ambayo yamekuwa yakifanya kazi bila leseni, hivyo kuikosesha serikali mapato.
Alisema msako uliofanywa na wizara husika, ulibaini kuwa makampuni 23 yalikuwa yakifanya kazi bila leseni, hivyo kuikosesha serikali mapato.
Aliilipua pia Wizara ya Fedha na Uchumi kwamba Februari 25 mwaka 1999, ilisamehe ushuru wa makampuni ya madini kulipia ushuru wa mafuta ya dola za Marekani 200,000.
Akizungumzia deni la taifa, Cheyo alisema limefikia sh trilioni 6.4 na kwamba linaendelea kukua kwa kasi. Mbali ya deni la taifa, Cheyo pia alisema wizara kadhaa zina mzigo wa madeni, hali ambayo inaweza kuathiri bajeti ijayo.
Akitolea mfano, alisema Wizara ya Miundombinu ilikuwa na madeni ya sh 742,920,080.58 na mihadi iliyofikia sh 178,596,360,000.
Alisema yapo madeni mengine kadhaa ya wizara na idara za serikali kama vile elimu, Jeshi la Polisi, Magereza na Wizara ya Afya na kuongeza kwamba madeni hayo yanatokana na uzembe wa maofisa masuhuli.
"Haya ni madeni ambayo wizara inaenda nayo katika mwaka wa fedha unaofuata. Wasiwasi ni kwamba madeni haya yataathiri bajeti inayofuata kwa kulipia madeni," alisema Cheyo.
Kamati ya Zitto Kabwe
Kwa upande wake, Zitto Kabwe alisema kuwa fedha nyingi za umma zimepotea katika suala la manunuzi ya mali za umma.
Akitolea mfano, Zitto alitaja manunuzi yasiyozingatia sheria ya manunuzi kama yale yaliyofanywa na Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) ambapo sh 102,285,441 zilitumika.
Pia alizungumzia Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) kwamba linapaswa kuwezeshwa kama serikali ilivyokuwa ikifanya lilipokuwa likiendeshwa kwa ubia ambapo ilikuwa ikipata sh milioni 500 kila mwezi.
Tundu Lissu amvaa tena Ngeleja
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, jana alimvaa tena Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, akimtaka ajibu kwa ufasaha majibu ya maswali ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe (CHADEMA), aliyetaka kujua Shirika la Umeme nchini (TANESCO), linapata wapi fedha za kununulia mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya IPTL.
Lissu (CHADEMA) ambaye juzi alitoa kauli bungeni kwamba Waziri Ngeleja ni muongo na kutakiwa kuthibitisha kesho, aliomba mwongozo wa Spika akitaka waziri huyo ajibu maswali ya Zitto kwa ufasaha.
"Mheshimiwa Spika, kanuni zinasema waziri atakuwa na wajibu wa kujibu swali la mbunge kwa ufasaha ndani ya Bunge isipokuwa kwa swali linalohitaji takwimu na vielelezo vingi. Swali la Mbunge (Zitto), halihitaji takwimu za aina hiyo. Naomba ajibu kwa ufasaha," alisema Tundu Lissu.
Akijibu hoja hiyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda, alisema kuwa mwenye uwezo wa kumtaka waziri ajibu swali kwa ufasaha ni Spika na kama mbunge anaona jibu lake halijakamilika, anapaswa kufuata taratibu. Someni kanuni vizuri," alisema.
Awali akijibu swali la msingi la Zitto, Waziri Ngeleja aliliambia Bunge kuwa mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya Kampuni ya IPTL, hutumia sh bilioni 15.62 kwa mwezi kwa ajili ya kugharimia ununuzi wa mafuta mazito ili kuendesha mitambo hiyo.
Waziri Ngeleja, alisema kiasi cha sh bilioni 46.4 au wastani wa sh bilioni 15.62 kila mwezi huitajika kwa ajili ya kugharamia ununuzi wa tani 36,800 za mafuta mazito (HFO) kwa kipindi cha miezi mitatu.
Ngeleja alisema kuanzia Novemba 15 mwaka 2010 hadi Februari 14, 2011 sawa na tani 400 ya mafuta mazito hutumika kwa siku.
Alisema pamoja na hatua zote hizo, hivi sasa kampuni mbili za Oryx na Total ndizo pekee zinazofanya biashara ya mafuta mazito na ndizo zilizoombwa kushiriki katika mchakato wa ununuzi wa mafuta hayo.
Waziri Ngeleja alisema utaratibu unaotumika kupata kampuni za Oryx na Total ni kwa ‘Restricted Tendering' ambapo kampuni za mafuta zilitakiwa kufikisha mafuta katika maghala ya IPTL kuanzia Novemba 2010.
Aidha, alisema katika hali ngumu kama hiyo maamuzi ya serikali yalihitajika kufanyika kwa haraka ili kupunguza ukali wa mgawo wa umeme kwenye mfumo wa gridi ya taifa.
Alisema fedha za kununulia mafuta ya kuendeshea mitambo hiyo ya IPTL hutoka katika mfuko mkuu wa serikali.
Waziri Ngeleja pia alisema serikali bado ina nia ya kuibadili mitambo ya IPTL kutumia gesi, lakini inashindwa kufanya hivyo kutokana na kesi iliyopo mahakamani iliyofunguliwa na IPTL dhidi ya TANESCO.
Hata hivyo majibu hayo yalimfanya mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani kuuliza swali dogo la nyongeza ambapo alihitaji kufahamu fedha hizo za kununulia mafuta hayo mazito zinatoka katika bajeti gani.
Alisema kwa sasa TANESCO iko kwenye mvutano wa kisheria na IPTL na kila siku hulipa sh bilioni 3.6 na kuziingiza kwenye mfuko maalumu na kuna zaidi ya sh bilioni 1.6 zimehifadhiwa humo.
"Ni kweli fedha hizo haziko kwenye bajeti lakini namtaka mbunge aje pale kwenye ofisi zetu tumuonyeshe wapi fedha hizo zinatoka," alisema Ngeleja.
Jibu hilo ndilo lililomfanya Lissu kuomba mwongozo wa Spika kutaka Ngeleja ajibu kwa ufasaha.


h.sep3.gif
 
Urais 2015 wamshtua Mengi


na Hellen Ngoromera


amka2.gif
KELELE za urais wa mwaka 2015 zimeonekana kumshtua Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi, akiwashangaa wanaozungumza kuhusu anayepaswa kuwa rais, akisema kuwa wanapoteza muda na kwamba wanalikosesha taifa mwelekeo.
Mengi aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali ya nchi.
Alisema inasikitisha kuona watu hao wakizungumzia kuhusu suala hilo baada ya kipindi kifupi tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani badala ya kufikiri na kuzungumza kuhusu matatizo yanayoikumba nchi, ukiwamo umaskini na hali ya uchumi.
"Oktoba mwaka jana nchi ilifanya uchaguzi wa viongozi, si mbali tangu tulipofanya uchaguzi huo mkuu, ni juzi tu, lakini kinachonipa shida ni kuwa baada ya kipindi hicho kifupi kupita watu wameanza kuzungumzia kuhusu rais wa 2015.
Inasikitisha kuona hali ya maisha ikiwa ngumu lakini badala yake watu wanazungumza kuhusu nani atakuwa rais wa mwaka 2015. Hii ni dharau kwa wananchi," alisema Mengi.
Kwa mujibu wa Mengi ambaye ni mfanyabiashara maarufu nchini, jambo ambalo wananchi wanatakiwa kulifikiri ni kuainisha sifa za viongozi wanaowataka ziwe vipi na si kuainisha nani anapaswa kuwa rais.
Alisema hali hiyo inasababisha taifa kupoteza mwelekeo, hivyo wananchi hawana budi kujirudi na kuwa taifa imara na kwamba kama taifa halikutamka linamtaka kiongozi wa sifa gani, nchi itaishia mahali pabaya.
Alisema si vibaya kusema rais wa mwaka 2015 awe na sifa gani ili anayetaka kuwania wadhifa huo ajiulize kama anazo sifa hizo na kama hana arudi nyumbani kwake na kufungua mgahawa, bucha au genge na kuuza nyanya au vitunguu.
Alipoulizwa yeye binafsi anamtaka rais mwenye sifa gani, alisema awe mwenye wito na asiyeona kuwa urais ndio mwisho wa kila kitu.
Alitaja sifa nyingine kuwa ni awe mtumishi wa watu ambaye hatakuwa na ubinafsi, mwadilifu ili awe mfano kwa watu anaowaongoza, kwani kama hatakuwa mwadilifu anaowaongoza hawatamwamini.
Aidha, Mengi alizungumzia suala zima la ufisadi akisema watu wengi walitarajia vita hiyo ingeshinda lakini imeendelea kuwa ngumu Tanzania na hata nchi nyingine.
Alisema nchi imekuwa ikielekeza nguvu zake kwa wapokea rushwa na kuwaacha watoa rushwa, hasa wakubwa ambao aliwaita ‘Mafisadi Papa' wakiendelea na harakati zao.
"Hatujaelekeza nguvu za kutosha kwa watoa rushwa wakubwa ‘Mafisadi Papa' kwa sababu wanaweza kuhonga watu 1,000 hadi 2,000.
"Leo unamweka mtu kuwa katibu mkuu wa wizara fulani, kisha akaja fisadi papa na kumuhonga na mwisho wa siku kiongozi yule akafukuzwa na kuletwa mwingine, lakini haitasaidia kwani fisadi papa yule atakwenda tena kwa kiongozi huyo na kumhonga, kuna haja ya watoa rushwa hawa kushughulikiwa kisheria," alisema Mengi.
Kwa mujibu wa Mengi, wote wanaowakumbatia na kuwakubali watoa rushwa wakubwa nao ni sehemu ya rushwa na kwamba wanawasaliti Watanzania maskini.
"Ifike mahali tuseme imetosha, tumechoka na hali hii, Watanzania wenye hali nzuri wajikumbushe wametoka wapi na kila mmoja akumbuke kuwa ametoka wapi na siku moja atarudi kijijini amebebwa," alisema Mengi.
Alisema watoa rushwa hao wakubwa wanajishughulisha na kazi nyingi na kueleza kwamba nyingine zinatisha.
 
Back
Top Bottom