Mkuu wa Majeshi aitembelea familia ya Sajent Mohamed Abdala Suleiman aliyefariki DRC

Mkuu wa Majeshi aitembelea familia ya Sajent Mohamed Abdala Suleiman aliyefariki DRC

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
..Jenerali Jacob Mkunda alipokwenda kutoa pole kwa familia ya marehemu Sajent Mohamed Abdala Suleiman.
===

"Mishoni mwa mwaka uliopita (2024) kikundi cha vijana wenye silaha wakijiita M23 walianza chokochoko na kuharibu kabisa amani ya mashariki mwa nchi ya Kongo. Kwahiyo vita ilitokea mnamo January 23, vijana wetu walipigana katika jukumu la kuwasaidia wenzao wa Kongo kurejesha amani mashariki mwa nchi ya kongo. Kwa bahati mbaya sana katika mapigano hayo tulipoteza vijana wawili katika kikosi cha Tanzania pekee, akiwemo kijana wetu Sajenti Mohamed Abdallah Suleiman. Yupo na mwingine private John ambay yeye anatokea kanda ya Mwanza."- General Jacob Mkunda, CDF Tanzania

Soma pia Askari wawili JWTZ wafariki dunia, wanne wajeruhiwa mashambulizi ya M23 huko Goma, DRC

 
Wanajeshi waliofia Congo ni wangapi?
Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo ?
 
Wanajeshi waliofia Congo ni wangapi?
Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo ?

..kulingana na maelezo ya Mkuu wa Majeshi wamefariki askari wawili.

..askari mmoja ni huyo anayetokea Zanzibar, na mwingine anatokea Mwanza.
 
..kulingana na maelezo ya Mkuu wa Majeshi wamefariki askari wawili.

..askari mmoja ni huyo anayetokea Zanzibar, na mwingine anatokea Mwanza.
Asante kwa majibu mazuri!
Sasa,nisaidie nijue,Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo ?
..kulingana na maelezo ya Mkuu wa Majeshi wamefariki askari wawili.

..askari mmoja ni huyo anayetokea Zanzibar, na mwingine anatokea Mwanza.
Asante kwa jibu nzuri,ninaomba unieleweshe, Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo?
 
..Jenerali Jacob Mkunda alipokwenda kutoa pole kwa familia ya marehemu Sajent Mohamed Abdala Suleiman.
===

"Mishoni mwa mwaka uliopita (2024) kikundi cha vijana wenye silaha wakijiita M23 walianza chokochoko na kuharibu kabisa amani ya mashariki mwa nchi ya Kongo. Kwahiyo vita ilitokea mnamo January 23, vijana wetu walipigana katika jukumu la kuwasaidia wenzao wa Kongo kurejesha amani mashariki mwa nchi ya kongo. Kwa bahati mbaya sana katika mapigano hayo tulipoteza vijana wawili katika kikosi cha Tanzania pekee, akiwemo kijana wetu Sajenti Mohamed Abdallah Suleiman. Yupo na mwingine private John ambay yeye anatokea kanda ya Mwanza."- General Jacob Mkunda, CDF Tanzania


View: https://www.youtube.com/watch?v=rbFHQBDmQ_o&t=45s


M23 hawacheki na kima wanakomboa nchi yao yeyote atakaepeleka pua anakula chuma
Waiache DRC.


Hayo wameyataka wao wenyewe.

Tumekuwa tukishauri Sana hapa mtandaoni kwamba Wanajeshi wa nchi yetu warudi nyumbani ili waje kuimarisha ulinzi kwenye mipaka ya nchi yetu hii, lakini inavyoonekana Watawala wa nchi hawataki kusikia ushauri wetu huo. Matokeo yake ndio haya sasa.

Maandiko matakatifu yanasema kwamba "Aonywaye Mara nyingi naye hushupaza shingo, huvunjika ghafla na hakuna dawa tena."
(Mithali 29: 1)

Kama ni suala la Kulinda Amani, basi Jeshi linapaswa kupeleka Wanajeshi wake katika nchi za mbali, lakini siyo kwenda kulinda amani katika nchi ambazo ni majirani zetu. Hii ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa nchi. Wanajeshi Wapiganaji wa Vikosi vya Kulinda amani vinapaswa kupelekwa katika nchi za mbali huko Kama vile kwa mfano Pakistan, Lebanon, Mynmar, Haiti, n.k.

All in all, Wanajeshi wetu wanapaswa kupelekwa kwenda kulinda amani katika nchi zingine lakini muda wote kabisa wanapaswa wasimame katika Upande wa HAKI. Wasiende huko ili kwenda kuwatetea au kuungana na Watawala wa huko ambao ni Wadhalimu. Ujumbe wa Kulinda Amani usititumwe ili kwenda kusaidia au kuungana na upande wa Wadhalimu.

Daima Tukumbuke kwamba 'ukiungana na Wadhalimu basi tambua kwamba Wapenda HAKI hawatakuwa upande wako.'
 
M23 hawacheki na kima wanakomboa nchi yao yeyote atakaepeleka pua anakula chuma
Mkuu umekosa uzalendo. Kumbuka huyu ni kijana wetu kaiwakilisha nchi yetu. Asante Jenerali Joseph Nkunda kwa kuitembelea na kuwafariji familia ya kijana wetu.

Nawachukia sana M23
 
Hivi Congo hawana jeshi la kujilinda mpaka kutegemea wanajeshi kutoka nchi nyingine?
 
M23 hawacheki na kima wanakomboa nchi yao yeyote atakaepeleka pua anakula chuma
Mkuu umekosa uzalendo. Kumbuka huyu ni kijana wetu kaiwakilisha nchi yetu. Asante Jenerali Joseph Nkunda kwa kuitembelea na kuwafariji familia ya kijana wetu.

Nawachukia sana M23
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba kiuhalisia majanga haya yalikuwa yanaepukika
 
Back
Top Bottom