Mkuu wa Majeshi aitembelea familia ya Sajent Mohamed Abdala Suleiman aliyefariki DRC

Mkuu wa Majeshi aitembelea familia ya Sajent Mohamed Abdala Suleiman aliyefariki DRC

Asante kwa majibu mazuri!
Sasa,nisaidie nijue,Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo ?

Asante kwa jibu nzuri,ninaomba unieleweshe, Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo?

..majirani zetu wakiwa na amani na maendeleo tunafaidika kwa kuchangamana na kushirikiana nao ktk shughuli za kijamii na kiuchumi.

..kwa mfano, amani iliyoko nchini Kenya imewezesha uwepo wa biashara kubwa kati ya Tanzania na Kenya.

..tunapopeleka askari DRC lengo letu ni kurudisha amani kwa majirani na ndugu zetu ili tuweze kushirikiana kijamii, na kiuchumi, na kupelekea faida kwa pande zote.
 
..Jenerali Jacob Mkunda alipokwenda kutoa pole kwa familia ya marehemu Sajent Mohamed Abdala Suleiman.
===

"Mishoni mwa mwaka uliopita (2024) kikundi cha vijana wenye silaha wakijiita M23 walianza chokochoko na kuharibu kabisa amani ya mashariki mwa nchi ya Kongo. Kwahiyo vita ilitokea mnamo January 23, vijana wetu walipigana katika jukumu la kuwasaidia wenzao wa Kongo kurejesha amani mashariki mwa nchi ya kongo. Kwa bahati mbaya sana katika mapigano hayo tulipoteza vijana wawili katika kikosi cha Tanzania pekee, akiwemo kijana wetu Sajenti Mohamed Abdallah Suleiman. Yupo na mwingine private John ambay yeye anatokea kanda ya Mwanza."- General Jacob Mkunda, CDF Tanzania
Soma pia Askari wawili JWTZ wafariki dunia, wanne wajeruhiwa mashambulizi ya M23 huko Goma, DRC


View: https://www.youtube.com/watch?v=rbFHQBDmQ_o&t=45s

Jeshi zima la jwtz sikuizi halina uweredi wowote wa kusoma alama za nyakati ...nchi ikiwa na rais dhaifu kila kitu kinakuwa cha kipumbavu
 
Faida ni kwamba wanajeshi wanapata kazi maana tangu siku ile walivyomaliza kupigana na Idd Amin hawajawahi kupata kazi hadi wengine waliingia na kustaafu bila kupata kazi
Kama walionekana hawana kazi,kwanini wasiunganishwe na JKT,waingie kwenye kilimo!
Kwanini wasibuni viwanda vyao!
KAZI ni kwenda kupigana TU?
 
Hivi Congo hawana jeshi la kujilinda mpaka kutegemea wanajeshi kutoka nchi nyingine?
Wale wakata viuno na kupaka mikorogo, huwa wanakodisha hadi silaha kwa waasi na vikundi vya uhalifu.

Kuna jamaa humu aliwahi kusimulia aliyoyashuhudia huko mojawapo ni polisi kukutana na wanajeshi wakiwakimbia waasi na silaha wameshatupa, polisi wakawatimua kwa viboko wanajeshi wale warudi wakapambane na waasi😁
 
Kwanini Jeshi haliwapeleki Brigedia Jenerali wengi,kupigana vita, badala yake wanawapeleka masajenti vitani?
Pesa mkuu, na hapo ukirudi salama inabidi umkatie cha juu msimamizi/ mkuu wako aliyefanya zengwe Hadi jina lako likapita! Zinazobaki ukanunue ki Subaru chako used, sio used ya Japan, used ya hapa Tanganyika nyingine ukajenge Ka nyumba Kako, nchi ngumu Sana hii!
 
..majirani zetu wakiwa na amani na maendeleo tunafaidika kwa kuchangamana na kushirikiana nao ktk shughuli za kijamii na kiuchumi.

..kwa mfano, amani iliyoko nchini Kenya imewezesha uwepo wa biashara kubwa kati ya Tanzania na Kenya.

..tunapopeleka askari DRC lengo letu ni kurudisha amani kwa majirani na ndugu zetu ili tuweze kushirikiana kijamii, na kiuchumi, na kupelekea faida kwa pande zote.
Hakuna kurudisha amani hapo issue ni kwamba, Saa100 anamlinda mwenzake na ili likitokea la kutokea kwa Saa100 naye aweze kuja kumlindwa
 
Asante kwa majibu mazuri!
Sasa,nisaidie nijue,Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo ?

Asante kwa jibu nzuri,ninaomba unieleweshe, Tanzania inapata faida Gani ya kupeleka wanajeshi wetu Congo?
huo ni mchango katika umoja wa mataifa (UN), kuchangia kuwepo kwa amani Afrika ya Kati.

Sijui kama unakumbuka mauaji ya Rwanda ya 1994 na athari yake kwa Tanzania? Vita ikitokea nchi moja athari yake inakuwa kwa nchi za jirani pia kwani hupokea wakimbizi kwa wingi.

Rwanda, Burundi, Congo.....
na hapo awali ilikuwa ni nchi zinazogombea uhuru - Mozambique, Zimbabwe, South Africa, Namibia, Angola...
 
huo ni mchango katika umoja wa mataifa (UN), kuchangia kuwepo kwa amani Afrika ya Kati.

Sijui kama unakumbuka mauaji ya Rwanda ya 1994 na athari yake kwa Tanzania? Vita ikitokea nchi moja athari yake inakuwa kwa nchi za jirani pia kwani hupokea wakimbizi kwa wingi.

Rwanda, Burundi, Congo.....
na hapo awali ilikuwa ni nchi zinazogombea uhuru - Mozambique, Zimbabwe, South Africa, Namibia, Angola...
Japan haina wanajeshi na hakuna vita! Amani ni kubwa kuliko.
 
M23 hajawapoteza watu? Hii ni vita , toka miaka na miaka vita yoyote huondoka na maisha ya watu.
So dont talk as if M23 ni special sana, life will be lost ni nature ya vita
Mpaka sasa wamekufa vijana zaidi ya 700 wa RDF, wamezikwa kwenye makabuli ya wanajeshi kimya kimya, baada ya General Kagame kupiga marufuku familia zao kusema chochote, huku akiwaahidi kwamba Their Sacrifice Will Not Be In Vain.

Ni suala la muda tu.
 
huo ni mchango katika umoja wa mataifa (UN), kuchangia kuwepo kwa amani Afrika ya Kati.

Sijui kama unakumbuka mauaji ya Rwanda ya 1994 na athari yake kwa Tanzania? Vita ikitokea nchi moja athari yake inakuwa kwa nchi za jirani pia kwani hupokea wakimbizi kwa wingi.

Rwanda, Burundi, Congo.....
na hapo awali ilikuwa ni nchi zinazogombea uhuru - Mozambique, Zimbabwe, South Africa, Namibia, Angola...
Hili kundi,linaishi kwa kufanya kazi Gani, wanakula wapi? Wana mpango Gani kuhusu maisha Yao?wataoa lini na wataolewa lini?Wameajiriwa wapi? Wamesomea nini? Hili ni janga jingine!
 

Attachments

  • VID-20250305-WA0005.mp4
    7.9 MB
  • IMG-20250305-WA0007.jpg
    IMG-20250305-WA0007.jpg
    137.3 KB · Views: 1
Waiache DRC.


Hayo wameyataka wao wenyewe.

Tumekuwa tukishauri Sana hapa mtandaoni kwamba Wanajeshi wa nchi yetu warudi nyumbani ili waje kuimarisha ulinzi kwenye mipaka ya nchi yetu hii, lakini inavyoonekana Watawala wa nchi hawataki kusikia ushauri wetu huo. Matokeo yake ndio haya sasa.

Maandiko matakatifu yanasema kwamba "Aonywaye Mara nyingi naye hushupaza shingo, huvunjika ghafla na hakuna dawa tena."
(Mithali 29: 1)

Kama ni suala la Kulinda Amani, basi Jeshi linapaswa kupeleka Wanajeshi wake katika nchi za mbali, lakini siyo kwenda kulinda amani katika nchi ambazo ni majirani zetu. Hii ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa nchi. Wanajeshi Wapiganaji wa Vikosi vya Kulinda amani vinapaswa kupelekwa katika nchi za mbali huko Kama vile kwa mfano Pakistan, Lebanon, Mynmar, Haiti, n.k.

All in all, Wanajeshi wetu wanapaswa kupelekwa kwenda kulinda amani katika nchi zingine lakini muda wote kabisa wanapaswa wasimame katika Upande wa HAKI. Wasiende huko ili kwenda kuwatetea au kuungana na Watawala wa huko ambao ni Wadhalimu. Ujumbe wa Kulinda Amani usititumwe ili kwenda kusaidia au kuungana na upande wa Wadhalimu.

Daima Tukumbuke kwamba 'ukiungana na Wadhalimu basi tambua kwamba Wapenda HAKI hawatakuwa upande wako.'
Wewe sio mtanzania, ni mtutsi wa m23 kutoka kigali.
 
Back
Top Bottom