Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Kama akiachiwa kwa madai ya insanity kweli basi hiyo itakuwa ni doa kubwa sana kwa Rais na serikali yake kwa jumla. Yaani Rais anaweza kumteua mtu insane kuwa Mkuu wa Mkoa! Au kwa maana nyingine ni kuwa kuna wateule wa Rais ikiwa ni pamoja na Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, na Mabalozi ambao ni insane!

Kichuguu,
Siyo wateule wake tu, bila shaka hata Rais mwenyewe atakuwa insane!!!
 
Nimefurahia maneno ya mwendesha mashtaka "Hakuna aliye juu ya sheria"... was that a message to somebody!!
 
mkurugenzi diptopile mzuzuri mungu amekusame kwa vile vyote ulivotenda na ile bastola ilitoka mfukoni kwake akampiga dereva wa daladala na yeye ni mkuu wa mkoa wa tabora tarifa yake imeshapatikana kwa jk na jk kashamtembelea magerezani nayeye atakata kuwa mkuu wa mkoa wa tabora atabaki apo gerezani mpaka afie uko uko


Manka 7yrs old

MUOMBE MUNGU SAANA
 
Ndugu wa Ditopile wawafanyia fujo tena waandishi

2007-01-30 11:00:10
Na Hellen Mwango na Rosemary Mirondo
Watu wanaodaiwa kuwa ni familia ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri anayekabiliwa na kesi ya mauaji, jana waliendelea kuwaletea fujo waandishi wa habari wanaofuatilia mwenendo wa kesi hiyo.

Watu hao wengi wao wakiwa ni wanawake, walifanya hivyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Hii ni mara ya pili kwa watu hao kuwafanyia vurugu waandishi wa habari mahakamani hapo wakiwa kazini.

Katika tukio la kwanza, mwanamke mmoja alidiriki kuziba kwa kutumia kitambaa cheusi kamera ya mpiga picha wa ITV ili asichukue picha za mshtakiwa Ditopile anayedaiwa kumuua dereva wa daladala.

Na katika tukio la jana, watu kama hao, pia waliwatolea lugha chafu ya matusi huku wakitandaza pande za khanga kuwazuia waandishi wa habari wasipige picha za matukio mbalimbali hasa la mshtakiwa Ditopile mahakamani hapo.

Hali kadhalika, watu hao wakiongozwa na mwanamke mmoja alisikika akijitaja kwa jina la Jamila Jumbe na kujinadi kuwa ni `dada` wa damu wa mshtakiwa na kwamba siyo wa manati wala wa kuunga unga.

Aidha, mbali ya kutoa kashfa na kejeli kwa waandishi wa habari, pia walidai kwamba, wamechoshwa na tabia ya waandishi hao kuendelea kumsakama ndugu yao Ditopile kila anapofikishwa mahakamani hapo kwa kumpiga picha huku wakitambua kwamba anasumbuliwa na kisukari na shinikizo la damu.

Na hata baada ya Ditopile kuingizwa katika chumba cha Mahakama, mwanamke huyo aliyedai kuwa ni dada yake wa damu wa mshtakiwa akiwa pamoja na mwanaume mmoja, waliziba kwa upande wa khanga mpiga picha ili asipige picha yoyote inayohusiana na tukio hilo hadi alipoingia Hakimu Mkuu Mkazi, Bw. Michael Luguru anayesikiliza kesi hiyo.

Baada ya Mahakama kuanza shughuli zake, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Bw. Charles Kenyella, akisaidiana na Mrakibu Msaidizi Bi. Naima Mwanga na Inspekta Msaidizi Bw. Boniface Edwin, alidai kuwa, upelelezi kwa upande wa polisi umekamilika na jalada limewasilishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) kwa hatua.

ACP Kenyella aliongeza kuwa, kwa sasa upande wa mashtaka wanasubiri maelekezo zaidi na ushauri kutoka kwa DPP.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Cuthbert Tenga na Samwel Mapande, ulidai kuwa, umesikia hatua hiyo ya upepelezi wa kesi hiyo kukamilika. Waliiomba mahakama wasipumzike ili kesi hiyo ifikie tamati.
ACP Kenyella alidai kuwa, anaamini kwamba, DPP atalishughulikia shauri hilo.

Katika kesi ya msingi, Ditopile anadaiwa kuwa, Novemba 4, mwaka jana, saa 1:00 usiku, kati ya Barabara ya Bagamoyo na Kawe, jijini Dar es Salaam, alimuua dereva wa daladala, Hassan Mbonde kwa kumpiga risasi.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Februari 12, mwaka huu itakapotajwa tena na mshtakiwa alirudishwa rumande.

SOURCE: Nipashe

Dito is a killer and he will be treated like any other killer.
 
Nimechukua habari hii toka gazeti la Uhuru. Ingefaa kuwekwa kwenye topic yake original, lakini sijaipata. Endelea.....

23 kutoa ushahidi kesi ya Ditopile
Abadilishiwa shitaka, sasa ni kuua bila kukusudia
DPP asema kesi haziendeshwi kama enzi za Pilato
Na Ester Bulaya
MASHAHIDI 23 wanatarajia kutoa ushahidi katika kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuru (58)
Miongoni mwa mashahidi hao ni kondakta wa daladala alilokuwa akiendesha marehemu Hassan Mbonde, abiria waliokuwa wamepanda gari hilo siku ya tukio na waliokuwepo eneo la tukio.
Kulingana na taarifa kwenye faili jipya la kesi lenye namba 13/2007, lililofunguliwa Mahakama Kuu, Januari 31, mwaka huu, mashahidi hao 23 ndiyo waliotoa maelezo wakati wa upelelezi wa kesi hiyo.
Chini ya mashitaka hayo mapya, Ditopile anashitakiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia, ambapo anadaiwa Novemba 4, mwaka jana, saa moja usiku, katika njia panda ya Kawe na Bagamaoyo, Wilaya ya Kinondoni, alimuua bila kukusudia Hassan Mbonde.Mashitaka hayo mapya yanafuatia uamuzi wa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), kubadilisha shitaka la awali la kuua, kutokana na ushahidi uliopo.Kwa mujibu wa DPP, Lawrence Kaduma, msingi wa mashitaka hayo mapya unatokana na ushahidi uliokusanywa kwa watu walioshuhudia tukio hilo.Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kaduma alisema ushahidi unaotolewa wakati wa upelelezi ndiyo unaomfanya abadili shitaka.
Kaduma alisema alifikia uamuzi wa kubadili shitaka kwa kuwa mashahidi wote walitoa ushahidi unaofanana, kwa maelezo kulikuwa na malumbano kati ya Ditopile na dereva na pia Ditopile alitukanwa.
Alisema anashangazwa na baadhi ya watu kuhoji uamuzi wa kubadili shitaka na kwamba hafanyi kazi kwa shinikizo au kusikiliza maneno ya watu, bali anachofuata ni sheria.
Kaduma alisema upelelezi unaonyesha Ditopile alitukanwa na katika hali ya kawaida ya kibinaadamu, hakuna mtu ambaye anapenda kutukanwa hivyo alipandwa na hasira na kupelekea kufanya kosa hilo.
"Unajua watu hawajui sheria, kama angeamka na kutembea na bastola kuanzia asubuhi na kusema lazima auwe hapo sawa. Hiyo moja kwa moja ni shitaka la mauaji, lakini yule siyo 'chizi' atoe bastola na 'kushuti', kulikuwa na majibizano, alitukanwa akapandisha hasira, na kwa misingi ya kisheria hakukusudia kwa sababu hakupanga kufanya hivyo, "alisema Kaduma.
Alisema mashahidi waliotoa maelezo yao ni kondakta wa dalalada alilokuwa akiendesha marehemu, abiria waliokuwemo kwenye daladala hilo na watu wengine waliokuwepo eneo la tukio na kushuhudia vizuri tukio hilo.
Aliendelea kusema kuwa hawafanyi kazi kwa kufuata hisia za watu, kwani kesi zinaendeshwa kwa misingi ya kisheria.
"Hatuwezi kuendesha kesi kama pilato, eti watu wakisema kaua basi iwe hivyo, lazima tufuate sheria na ushahidi na vielelezo husika, Yesu aliuawa bila kosa kwa uoga wa Pilato kwa kuwaridhisha wale watu, sasa sisi hatufanyi hivyo," alisema DPP.
Naye Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Prophir Lyimo, alithibitisha kupokea hati mpya ya mashitaka kutoka kwa DPP na kwamba tayari shauri hilo limeshafunguliwa ingawa bado halijapangiwa jaji na kwamba kinachofuatia ni kusomewa maelezo ya awali katika Mahakama ya Kisutu kabla ya kuhamia rasmi Mahakama Kuu, kuanza kusikilizwa.
"Nimeshapokea jalada la kuua bila kukusudia linalomkabili Ditopile, nadhani tayari makarani watakuwa wamefungua na kuwajulisha Mahakama ya Kisutu, ila bado halijapangiwa jaji, bado kusomewa maelezo ya awali huko Kisutu," alifafanua.
Hata hivyo, upande wa Mahakama ya Kisutu ambapo kesi hiyo ilikuwa inakwenda kwa kutajwa, upande wa mashitaka uliokuwa ukiondozwa na Gurvanus Muhume ulidai hauna taarifa ya kubadilishwa kwa hati ya mashitaka na kumuomba Hakimu Mkazi Mkuu Michael Lugulu kuwapa muda wa wiki moja ili wafuatilie.Hata hivyo, Wakili Ringo Tenga anayemtetea Ditopile, alipinga vikali hoja ya upande wa mashitaka na kudai taarifa hizo ni za kweli, hivyo wiki moja ni muda mrefu na kwamba upande wa mashitaka upewe siku mbili kwa ajili ya kupeleka taarifa sahihi juu ya taarifa hizo.
Hakimu Lugulu alikubaliana na upande wa utetezi na kuwapa upande wa mashitaka siku mbili, hadi keshokutwa, ili kuithibitishia Mahakama yake juu ya shitaka jipya.Katika Mahakama ya Kisutu jana kulikuwa na hali ya utulivu na ulinzi mkali kuliko ilivyokuwa ikitokea mwanzo, ambapo ndugu wa Ditopile walikuwa wamedhibitiwa na polisi huku mshitakiwa huyo akichanganywa na wengine tofauti na zamani, ambapo alikuwa akiletwa peke yake.
Ditopile aliwafanya watu waliokuwapo mahakamani hapo kuangua kicheko baada ya kuvaa kofia kubwa nyeusi iliyokuwa imemziba uso hadi pua yake, kwa kukwepa kupigwa picha. Kofia hiyo ilimfanya atembee kwa taabu kwa kuwa hakuwa akiona vizuri.
Ditopile alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Novemba 6, na kusomewa shitaka la mauaji ya Mbonde kabla ya DPP kubadili shitaka na kuwa la kuua bila ya kukusudia.Kwa sasa mshitakiwa huyo anaweza kuachiwa kwa dhamana kwa kuwa shitaka husika lina dhamana na Mahakama Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kufanya hivyo.

Source: Uhuru Publications, Online Edition, 13/02/2007
 
Niliposema wanasheria wapanguliwe, I had this thing in my mind... ngoja nitafute ile thread nyingine
 
Je ilikuwa ni ajali?
"Ajali haina kinga" waswahili walisema, kale kadaladala kugonga gari la RC yawezekana kuwa ajali (ingeweza kuwa gari la mtu yeyote kwani hiyo ni mashine tu), lakini kitendo cha mtu kuamua kutoka ndani ya gari lake, kujibizana na dereva, kumfuata hadi kwenye gari lake, kuweka kidole kwenye trigger, kulenga mahali pa kichwa na kufyatua huwezi kuita ajali, unless neno "ajali" limepoteza maana yake!!

Je aliua kwa kukusudia?
Jibu langu ni ndiyo. Hakuna mtu anayenyosha bastola iliyo na risasi, na kuweka kidole kwenye trigger huku ameielekeza kwa mtu/watu na baadaye kufyatua, mtu/watu wakafa halafu huyo mtu aseme hakukusudia kuua!! Kama lengo lake ilikuwa ni kumtishia huyo kijana, angefanya kama wanavyofanya mapolisi au hata watu wengine kabla ya kuamua kumlenga mtu kujitetea. Wanafyatua risasi hewani kutishia!!! Unapozidiwa nguvu hapo ndipo unapoua ukitetea maisha yako, and that is a defence.

Je ni mauaji ya kujitetea maisha?
Hilo lingekuwa na ukweli endapo tu, yule kijana angetajwa mahali popote kuwa alibeba silaha (ya aina yoyote) na kumtishia Bw. Mkuu wa Mkoa. Hadi hivi sasa hakuna ushahidi wowote kuwa Hassan alifanya hivyo. Kinachojulikana alipigwa risasi (iwe moja, mbili, au kumi) akiwa ameketi kwenye kiti cha gari huku amefunga vioo!

Je Bunduki inahitajika kuonesha nia ya kosa (mens rea)
La hasha, mazingira peke yake yanatosha kuonesha kama mtu alikusudia kutenda tendo ovu (actus reus) au la. Mtu akikutwa juu ya paa la nyumba ya mtu mwingine huku akiwa ameshikilia gudulia la petroli akimimina, na baadaye kushika kiberiti na kuwasha nyumba hiyo na baadaye akakutwa amesimama pembeni anaangalia huku nyumba inaungua, mkononi amebakia na njiti zilizoungua, na ana harufu ya mafuta na mashahidi wapo waliomuona akifanya hivyo, na ikathibitika kuwa ndani ya nyumba kulikuwa na mtoto wa miaka 4 aliyeuawa kwa moto, polisi hawahitaji guduria la mafuta lililotumika kumwaga mafuta!!!

Je kitendo cha viongozi kwenda kutoa rambirambi ni kuokoa vurugu?
Kwa nje kitendo hicho kinapongezwa, ni cha kibinadamu na ni cha kiungwana. Hata hivyo, ukichunguza kwa karibu utaona kuwa ndani ya kitendo hicho kumejaa unafiki, uzandiki, na wa hali ya juu. Lengo lake ni moja tu nalo kumuonesha mtuhumiwa kuwa anajutia tendo lake (kitu ambacho hakibadilishi uzito au ubaya wa tendo hilo) na kujaribu kwa namna fulani kumuombea msamaha kwa wafiwa. Kitendo cha viongozi kutoa ahadi za kuisaidia familia n.k kina lengo moja tu nalo ni kuwanyamazisha wanafamilia (siyo kuzuia vurugu). Je watu waliokuwa wanalia mwanzoni kuwa famiilia imempoteza mtu pekee ambaye ndiye alikuwa anawasaidia kwa kila inahitaji nini zaidi ya mtu kuwapa uhakika wa chakula na malazi ya hapo baadaye?

Je ni watu wangapi ambao wanafiwa na baba zao, jamaa zao wanaosadia familia zao lakini huo RAis, makamu, meya, mawaziri, n.k wakijipanga msururu kuahidi misaada?

Ukweli ni kuwa, viongozi hawa wote wanafanya wanayofanya si kwa sababu wana uchungu kuwa Mbonde ameuwa kinyama, siyo kwa sababu familia inahitaji msaada sana, siyo kwa sababu hakuna mtu anayeweza kuwasaidia tena.. La hasha!! Viongozi hawa wanafanya wanachofanya kwa sababu anayetuhumiwa kuua ni NANI.

UKWELI NI HUU
Kama muuaji wa Hassan angekuwa Mmachinga fulani, jambazi fulani n.k unadhani viongozi hawa wangepanga foleni kwenda huko Kawe? Je alipouwa yule mwandishi wa habari wa The East African, viongozi wangapi wangazi za juu walienda kutoa pole kule na kuahidi kuisadia familia yake? Sitashangaa kuna viongozi walioenda kutoa pole, sitashangaa kuna mawaziri walioenda kutoa rambirambi kule, ila WANGAPI KATI YA HAO WALIKWENDA WAKIFUATANA NA WAANDISHI WA HABARI NA WAPIGA PICHA?

Kama hamuyaoni mazingaombwe, basi inabidi mkalie ndimu!!!

M. M. Mwanakijiji
 
Tulitabili kuwa mzee atashitakiwa kwa kosa dogo tu. Maskini Mbonde keshafariki na sierkali yetu haijali haki yake kama raia. Uraia wake ulikuwa wa kubabisha.

Yaani Ditopile alitukanwa hivyo akatoa bastola na kuikoki na kumlenga kichwani na kufyatua bila kukusudia. Alikuwa akikusudia nini kumlenga na hiyo bastola kichwani. Watanzania tusiokuwa na ubavu tuatonewa na kupigwa hadi kuuwawa bila utetezi wowote. Miaka ya nyuma kidogo wale jamaa waliomwua marehemu CD Konjesta waliachiwa hivi hivi tu na ofisi ya DPP. Je kweli ofisi ya DPP iko pale kulinda sheria za nchi kweli au inapindisha sheria kulingana na anavyotaka yeye mwenyewe.
 
waungwana hii inaonyesha kuwa kunzia hivisasa si itakuwa sawa tu kama mtu atakutukana jibu lako si kumuwashatu kwa mujibu wa sheria mpya ya kasi mpya na ari mpya?mmmmm,,, lakinilazima uwe mwanamtandao'IGA,,,,
 
Ni sawa DPP kuanza "kutoa ushahidi" kabla ya kesi kuanza?

Mbona inakuwa kama anamtetea mtuhumiwa?

Si angeacha maswali na majibu huko huko mahakamani?
 
Chama Chetu cha Mapinduzi kinajenga Nchi . Baada ya mashitaka kubadilishwa hatapatikana na hatia , then nadhani atarudi kazini kama kawaida na bastola yake atapewa. Kweli DPP mtu akikutukana wewe kazi yako ni kuondoa roho yake kwamba unapandwa na hasira ? Ditto kesha watukana wangapi Duniani jamani hata kweney majukwaa ya kisiasa maana tusi ni tusi lakini hajauliwa ?
 
Nimesoma mahali kuwa huyu mheshimiwa hupelekwa mahakamani kwa "baloon". Ni gari lake binafsi au la Magereza? Ni kwa ajili ya usalama wake au umaarufu wake?
 
Yoyote mwenye akili timamu, ambaye amekuwa anafuatilia mienendo ya kisiasa tanzania kwa muda atakuwa anajua kwamba ditopile hatahukumiwa kifungo. Hilo lilijionyesha toka mwanzo kabisa, mara baada tu ya tukio kwa mionendo na kauli za serikali na viongozi wake, akiwemo raisi.

Sina cha kusema zaidi kuhusu hili, lakini naomba watanzania wenzangu ikiwezekana tufanye hata mfungo, nchi yetu inaelekea pabaya sana. Kama unadhani mauaji ya kongo, rwanda na burundi ndiyo ilikuwa the worst, subiri uone bongo, Mungu apishie mbali, lakini tunavyokwenda hivi, sijui!

Nina mengi sana ya kusema, na nimekuwa nasoma hii forum mara nyingi sana, matter of fact, kila siku, ila nimekuwa najizuia kuandika maoni yangu au hata kuongelea siasa in public, kwa sababu nimegundua siasa siku hizi inaweza kukudhuru (physically, financially etc.) kuliko hata maongezi ya dini.

Kuna threads chache zimekuwa zinanivutia, nitajaribu kutoa maoni yangu machache huko kulingana na topic.
 
Kama watu walimfunga nguza na familia yake Maisha Bila ya kuwa na ushahidi wa kisayansi hata DNA tu, ambayo kwasasa tunayo Nchini Basi ujue wanauwezo wa kufanya lolote,Sasa hili la kuua kwa huyu bwana Linahitaji ushahdi gani kuonyesha kwamba aliua kwa kukusudia?Huwezi kuwa ni professional katika utumiaji wa silaha kama ditopile,ukaitoa ukamuelekezea mtu uliyekaribu naye,sio mguuni kwenye eneo la mwili ambalo unajua ukilipiga risasi halitaleta jereha tu bali litasababisha kifo,Mtu huyo ni kiongozi halafu faili lake la mashitaka linapitia hatua zote kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu,Je ni wangapi wenye mashitaka kama yake faili limepitia ngazi husika kwa kipindi kifupi namna hiyo?Hatujaona watu wakisota magerezani zaidi ya miaka 7-10 wakisubiri mafaili yao yapitie ngazi hizo?Hapa hakuna jipya ni yale tuliyokwishayasema hapo awali na sasa ni zamu kuyatekeleza kwa kuhakikisha mwenzao na Best Man anakuwa huru zaidi,NI nasema anakuwa huru zaidi naamini hata hivi sasa yupo huru,Mahakamani anakuja na saloon safi,ni wangapi wanajau kama yupo kweli gerezani?Hata waandishi hawaandiki yupo wapi au hawatembelei huko gerezani kutupa habari za uwepo wake huko, NA HATA KAMA YUPO HUKO, JE ANAISHI KAMA WASHITAKIWA WENGINE?HAYA NDIYO MATABAKA AMBAYO MZUNGU AKIMUA MUAFRIKA KULE SOUTH WAKATI HUO NI SAWA LAKINI MWAFRIKA HATA AKIJITETEA KWA KUKWEPA KIBANO CHA MZUNGU AMEKUSUDIA KUUUA.LEO TUNAYAONA HAPA KWETU NA TUTAENDELEA KUYAONA ZAID KAMA HATU ZA KUINUSURU NCHI HAZITACHUKULIWA NA USIMAMIZI WA UTAWALA WA KWELI WA SHERIA UKATEKELEZWA..
 
Nimesoma mahali kuwa huyu mheshimiwa hupelekwa mahakamani kwa "baloon". Ni gari lake binafsi au la Magereza? Ni kwa ajili ya usalama wake au umaarufu wake?
Umaarufu na si usalama,usalama ni karandika chini ya ulinzi wa defender tatu siku hizi na hata wakati ule wa kosa la watuhumiwa wa kupindua serikali ya Mwl. karandika ,pikipiki za kuongozea magari,landrover na FFU na kikosi cha farasi.
 
Ila jana amepelekwa na watuhumiwa wengine... (si dhamana inanukia?)

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameamua kubadili mashtaka yanayomkabili Bw. Ditopile Mzuzuri anayetuhumiwa kumuua kijana Hassan Mbonde kwa kumlipua na risasi akiwa ndani ya daradara alilokuwa akiendesha. Mashtaka ya sasa ni yale ya "kuua bila kukusudia". Mwendesha mashtaka ameda kuwa Watanzania hawaelewi sheria ila yeye peke yake!! Mimi sikubaliani naye na ninazijibu hoja alizozitoa hadharani kuhusu kwanini mashtaka sasa ni yale ya "kutokukusudia". Sizungumzii hatia ya mtuhumiwa kwani hiyo ni kazi ya mahakama.

http://mwanakijiji.podomatic.com
 
kama asemavyo Tabasamu.....................only possible in Tanzania!!
 
"...Kaduma alisema alifikia uamuzi wa kubadili shitaka kwa kuwa mashahidi wote walitoa ushahidi unaofanana, kwa maelezo kulikuwa na malumbano kati ya Ditopile na dereva na pia Ditopile alitukanwa.
Alisema anashangazwa na baadhi ya watu kuhoji uamuzi wa kubadili shitaka na kwamba hafanyi kazi kwa shinikizo au kusikiliza maneno ya watu, bali anachofuata ni sheria..."
Kaduma alisema upelelezi unaonyesha Ditopile alitukanwa na katika hali ya kawaida ya kibinaadamu, hakuna mtu ambaye anapenda kutukanwa hivyo alipandwa na hasira na kupelekea kufanya kosa hilo.
"Unajua watu hawajui sheria, kama angeamka na kutembea na bastola kuanzia asubuhi na kusema lazima auwe hapo sawa. Hiyo moja kwa moja ni shitaka la mauaji, lakini yule siyo 'chizi' atoe bastola na 'kushuti', kulikuwa na majibizano, alitukanwa akapandisha hasira, na kwa misingi ya kisheria hakukusudia kwa sababu hakupanga kufanya hivyo, "alisema Kaduma.


Bila kuathiri mwenendo wa sheria; naomba kutoa mchango wangu kama ifuatavyo:
Kaduma Kuongea na waandishi wa habari
Huu ni ukiukwaji wa sheria na taratibu za mahakama. It is a known principle kwamba wakati shauri liko mahakamani hakuna chombo au mamlaka yoyote yanaruhusiwa kulizungumzia nje ya mahakama.
Kitendo cha Kaduma kutolea ufafanuzi uamuzi wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu kubadili shtaka si utaratibu kabisa; hakuwa na sababu ya kufanya hivyo..it was uncalled for, and worst of all, an interference with the due process of the court.
Sina hakika kama katika taarifa iliyotolewa imeonyeshwa ni kwa misingi gani Kaduma aliamua kuongea na waandishi wa habari..ni nani aliitisha kikao hicho, and for whose benefit.
Sio kawaida kabisa kwa ofisi ya mwanasheria mkuu kutolea ufafanuzi maamuzi yake yanayohusu masuala yaliyoko mahakamani.
Hili linaashiria jinsi ambavyo suala hili limevuka mipaka ya kisheria na kuingia katika siasa!

Kuua bila Kukusudia
Pamoja na kwamba sio vema kujadili suala lililoko mbele ya mahakama; ni vema pia tukaangalia vipengele vinavyoangaliwa katika suala kama hili.
Kwanza, nijuavyo mimi, and I stand to be corected, ili mtu aonekane ameua bila kukusudia; ni lazima ithibitike kuwa:
-alikuwa na motive
-alikuwa amejiandaa kufanya mauaji hayo
-alikuwa na nia ovu (malice aforethought)
-alitumia nguvu iliyopita kiasi katika mazingira husika

Ni juu yetu kuangalia kama mazingira ya kaka Ditto yanakidhi vipengele hivyo
Hata hivyo;
Ili aonekane kuwa hakukusudia, the opposite of the above applies, plus;
-alikuwa amechokozwa...mahakama inaangalia kama kuchokozwa huko kungeweza kumfanya mtu makini ( a reasonable person) katika mazingira hayo hayo, ku-react kama alivyofanya Ditto.
nk nk

Sasa tu-narrow down to Ditto na tujiulize:
-Je, silaha hiyo aliibeba makusudi kumpiga huyo victim? did he even know him before?
-Je, alimpiga risasi wakati gani; mara tu alipomuona, au baada ya muda gani, na baada ya nini kutokea?
-je, mara baada ya kitendo hicho, what was his reaction?
- Je, mashahidi wanasemaje?

Kaduma may be right, and I think he is in some aspect, shida yake ni ile kuelezea umma kwanini mabadiliko yamefanyika..hayo hutokea kila kukicha katika kesi za mauaji and no one questions..it is a procedure for the DPP to charge the accused with the lesser offence(manslaughter instead of murder) when the evidence collected proves so..na hata kama asingefanya hivyo at this stage, ni lazima at some stage ingerudi kuwa manslaughter

Nimeweka hili kwa jinsi nijuavyo ili kuondoa hisia ambazo zaweza kuwa potofu..
however much we dislike this govt we should not outdo our criticisms...
In this case Kaduma has erred in procedure but he is right in content if what he says is the evidence is true

Yeah...having a press conference on an issue thats pending before a court of law can only happen in Tz..but amending the charge to conform to the evidence on record is perfectly legal and it happens everywhere..be it common law or civil law systems
 
Back
Top Bottom