Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Matatizo yapo kotekote, Polisi na Mahakama pia,

tuangalie tusije tukaingia ktk kesi ya kuku na yai ya kwamba kipi kilianza.

Jamani lets give JK credit where he deserves, kateua majaji na muundo wa polisi unaendelea kubadilishwa, tusubiri matokeo yake maybe another year or two.

Kuharakishwa kwa kesi ya braza Ditto, wakati kuna kesi nyingi on queue ni UONEVU WA HALI YA JUU kwa wanaosota rumande na ndugu zao.

Mwendapole
hebu tumegee kidogo haya mambo yanakuwaje kuwaje
 
Jamani lets give JK credit where he deserves, kateua majaji na muundo wa polisi unaendelea kubadilishwa, tusubiri matokeo yake maybe another year or two.

Kuharakishwa kwa kesi ya braza Ditto, wakati kuna kesi nyingi on queue ni UONEVU WA HALI YA JUU kwa wanaosota rumande na ndugu zao.

Mwendapole
hebu tumegee kidogo haya mambo yanakuwaje kuwaje

Ogah sasa unaleta majibu rahisi kwa maswali magumu. Hivi Marais waliopita walikuwa wanashindwa nini kuteua judges wakati wa vipindi vyao? Tatizo kulikuwa hakuna wenye sifa nyakati hizo? Au tatizo lilikuwa resources? Au hakukuwa na kesi nyingi wakati huo? Baada ya uteuzi huo ni kanda ngapi za mahakama kuu zimeongezwa au kuundwa au wote wameendelea kuwa Dar? Lakini zaidi tatizo letu lipo kwa idadi ya ma-judge? Yale yale ya kujenga vyumba vya madarasa nakudai mafanikio katika sekta ya elimu.
Kuhusu hilo la polisi muundo wake kubadilishwa hebu tupe mfano wake maana hapo sasa naona unakuja na hekaya zile zile za watawala.
Suala la Dito kama kesi imeharakishwa well and good, bila shaka hilo si tatizo hapa, suala ni mashtaka yake. Hiyo kesi ilitakiwa kuanza kuunguruma ndani ya mwezi mmoja na wala siyo miezi minne kama ilivyo sasa.
 
Ogah sasa unaleta majibu rahisi kwa maswali magumu

Lets not complicate some issues ambazo ziko soo obvious and simple!!

Hivi Marais waliopita walikuwa wanashindwa nini kuteua judges wakati wa vipindi vyao? Tatizo kulikuwa hakuna wenye sifa nyakati hizo? Au tatizo lilikuwa resources? Au hakukuwa na kesi nyingi wakati huo?

Good questions........ningefurahi sana kama ningekuwa na uwezo wa kujibu hayo maswali hapo juu.

Sasa baada ya kujiuliza hayo maswali, sasa pata picha; kaja JK kateua majaji...........

Baada ya uteuzi huo ni kanda ngapi za mahakama kuu zimeongezwa au kuundwa au wote wameendelea kuwa Dar?

kuongeza kanda its a next step after uteuzi huo, ingechekesha ikiwa angeanzisha kanda bila ya kuwa na Judges

Lakini zaidi tatizo letu lipo kwa idadi ya ma-judge?

to some extent, Ndio, hivyo kukawa na umuhimu wa kuteua majaji, pia kuna msongamano wa kesi nyingi mahakama kuu

Yale yale ya kujenga vyumba vya madarasa nakudai mafanikio katika sekta ya elimu.

Nafikiri hapo ni kinyume chake kwani JK kateua halafu "nina Imani" kanda "madarasa" zitaongezwa kinyume cha hapo ninaweza kuuita uamuzi huo "NONSENSE"

Kuhusu hilo la polisi muundo wake kubadilishwa hebu tupe mfano wake maana hapo sasa naona unakuja na hekaya zile zile za watawala.

Kama utakumbuka....Mzee Mwanakijiji.....nafikiri ilikuwa kule BCS alipendekeza muundo maalumu wa utendaji kwa jeshi letu la polisi, na tumeshuhudia juhudi za forum kama hii kuzaa matunda hayo ambayo tumeyaona yameanza kufanyiwa kazi "Kanda ya Dar es salaam" kamanda ni Tibaigana.

Suala la Dito kama kesi imeharakishwa well and good, bila shaka hilo si tatizo hapa,

Ndugu yangu.......... ni 'well and good kwa Ditto!!! however, HILI NI TATIZO kwetu sisi wananchi tulio na ndugu zetu wenye kesi za "kuku" wanaosota bila kujua hatma za kesi zao miaka nenda miaka rudi. Ninachoweza kusema ni kuwa kama walitaka kumsaidia 'mwenzao" basi wangeharakisha kufanya uchunguzi wa kesi zilizo mbele ya hiyo ya Ditto ili nayo ifanyiwe maamuzi kwa wakti wake. May be FIFO doesn't apply in LAW.....Mwendapole hebu tuelimishe hapo!!

suala ni mashtaka yake (Ditto).

Nakubaliana na wewe only if una maanisha kubadilishwa kwa Kosa kuwa "Kuua bila kukusudia" ya kwamba si haki!!
Huu mimi nauita UHUNI!! na ni DHAMBI KUBWA Mbele ya MOLA WETU. Mzee Kichuguu alitoa mfano mzuri saana wa Kleruu, nafikir kilichompata muuwaji wake ndicho kilichotakiwa kumpata huyu Ditto

Hiyo kesi ilitakiwa kuanza kuunguruma ndani ya mwezi mmoja na wala siyo miezi minne kama ilivyo sasa.

NO!!, nafikir ilitakiwa iungurume kama zilivyo za wengine wanaosota rumande hadi leo miaka nenda miaka rudi.
Hata hivyo NAFARIJIKA YA KWAMBA DITTO IS NO BODY MBELE YA MOLA WETU NA ATAKULA HAKI YAKE TU HIYO SIKU

 
Mgomo wa mahabusi wasambaa Dar

Na Waandishi Wetu

MGOMO wa mahabusu wa kupinga kucheleweshewa kesi zao ulioanza katika Mahakama ya Kisutu juzi, umeendelea jana na kusambaa katika mahakama nyingine jijini Dar es Salaam na mjini Arusha.

Jijini Dar es Salaam, mahabusu hao waligoma kwa mara ya pili kushuka katika karandinga, wakishinikiza Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Mary Nagu, atoe tamko juu ya kesi zao ambazo wanadai zimechukua muda mrefu bila ya upelelezi wake kukamilika.

Mgomo huo uliingia siku ya pili jana, baada ya juzi mahabusu hao kukataa kushuka katika karandinga kwa ajili ya kusikiliza kesi zao, wakishinikiza upelelezi wa kesi zao ufanywe haraka kama ilivyokuwa kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, anayekabiliwa na kesi ya kuua bila ya kukusudia.

Mgomo huo ambao unaonekana kuishika pabaya serikali, uliendelea tena jana kwa nyakati tofauti katika mahakama ya Kisutu na mahakama za wilaya za Ilala na Temeke ambako mahabusu waligoma kushuka huku wakisisitiza kuwa hawatafanya hivyo hadi hapo serikali itakapotoa tamko kuhusiana na madai yao.

Wakiwa ndani ya makarandinga ya polisi katika mahakama hizo, mahabusu hao waliendelea na staili yao ya kuimba nyimbo za kudai haki na kuishutumu serikali kuwa inafanya upendeleo katika kushughulikia kesi za vigogo na walalahoi.

Walimtaka Dk Nagu na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) watoe tamko litakalofafanua muda ambao mtuhumiwa wa mauaji anastahili kukaa mahabusu wakati upelelezi wa kesi yake ukiendelea kwa kile walichoeleza kuwa upo upendeleo wa dhahiri katika kushughulikia kesi hizo.

Walisema tatizo zaidi linakuwa katika kesi zinazohusisha vigogo wa serikali na watu maarufu, huku zile zinazowahusu walalahoi zikipuuzwa na upelelezi wake ukichukua muda mrefu na kuwaacha wakiteseka gerezani bila ya kupatiwa haki za msingi.

Pia walimtaka Waziri Nagu, atembelee magereza aweze kujionea mwenyewe hali halisi, ili ajue kuwa kuchelewesha kesi hizo ni kuwaumiza na kuwapa mateso makubwa mahabusu.

Katika Mahakama ya Kisutu, jana, karandinga la kwanza lililochukua mahabusu kutoka Gereza la Keko lilifika saa 3.30 asubuhi na kama ilivyokuwa juzi, waligoma kushuka na baada ya muda mfupi walirudishwa gerezani.

Karandinga la pili lilifika saa 4.38 asubuhi, likiongozwa na gari la polisi namba T 220 AMV Land Rover, lakini mahabusu waliokuwamo pia waligoma kushuka na kurudishwa mahabusu.

Katika mahakama za wilaya za Ilala na Temeke, kesi zote zinazohusu mahabusu waliotoka katika magereza ya Keko na Segerea, ziliahirishwa jana baada ya mahabusu kugoma kushuka kwenye karandinga wakidai kucheleweshwa kwa upelelezi wa kesi zao.

Kutokana na hali hiyo, baadhi ya mahabusu waliokuwa wakitarajia dhamana, waliangua kilio baada ya kuwaona ndugu zao waliofika mahakamani hapo kwa ajili ya kuwawekea dhamana.

Katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, waliobahatika kushuka kwenye karandinga ni mahabusu wanawake kutokana na wao kuwekwa katika chumba tofauti na wanaume ndani ya gari lililowafikisha mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Joyce Minde, alisema kuwa amewasiliana na polisi ili wafuatilie suala hilo.

Mjini Arusha, mahabusu wanaokabiliwa na kesi mbalimbali nao waligoma kushuka katika karandinga katika viwanja vya Mahakamani Kuu wakitaka kuonana na Rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwa jirani na mahakama hiyo, ilipo Ikulu ndogo wakilalamikia kucheleweshwa kesi zao.

Mahabusu hao wanaokaridiwa kufikia 70, walipaza sauti wakilalamikia kuachiwa kwa dhamana kwa Ditopile huku wao wakiachwa wateseke gerezani.

Mahabusu hao baadaye walianza kuimba kwa sauti kubwa "polisi wanataka nini...wanataka rushwa na Ditopile kawapa nini, kawapa rushwa" hatua ambayo ilizuwa tafrani kubwa mahakamani hapo na kwa maafisa wa usalama ambao walikuwa viwanja vya Ikulu.

Tukio hilo lilianzaa majira ya saa 3.30 mara baada ya mahabusu hao kuwasili katika gari lao lenye namba za usajili STG 9266 na lilidumu hadi saa 4.11 pale maafisa kadhaa wa polisi walipowasili na kuamuru mahabusu hao kurejeshwa magerezani.

Maafisa wa polisi wakiwa katika gari lenye namba za usajili T638AJR na polisi wengine wa kutuliza ghasia wakiwa katika gari lenye namba za usajiri T 447 APF waliwaondoa mahabusu hao kupitia njia tofauti na ambayo hutumika, hivyo kukwepa Rais Kikwete asisikia kelele hizo.

Awali, mahabusu hao huku wakipiga mayowe, walikuwa wakilalamikia polisi kuchelewesha kesi zao na hasa upelelezi, hatua ambayo inachangia kukaa muda mrefu magerezani.

Hata hivyo, hakuna hakimu ambaye alikuwa tayari jana kuongelea tukio hilo kwa maelezo kuwa wanaolalamikiwa ni polisi na sio wao.

Katika mgomo wa juzi katika mahakama ya Kisutu, Mahabusu wanaokadiriwa kuwa kati ya 250 hadi 300 wakitokea katika magereza ya Keko na Segera, waligoma kushuka ndani ya magari ya polisi STH 3058 na STJ 903 wakilalamikia ucheleweshwaji wa upelelezi wa kesi zao.



kazi kwelikweli.........
 
Mgomo wa mahabusi wasambaa Dar

Na Waandishi Wetu

MGOMO wa mahabusu wa kupinga kucheleweshewa kesi zao ulioanza katika Mahakama ya Kisutu juzi, umeendelea jana na kusambaa katika mahakama nyingine jijini Dar es Salaam na mjini Arusha.

Jijini Dar es Salaam, mahabusu hao waligoma kwa mara ya pili kushuka katika karandinga, wakishinikiza Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Mary Nagu, atoe tamko juu ya kesi zao ambazo wanadai zimechukua muda mrefu bila ya upelelezi wake kukamilika.

Mgomo huo uliingia siku ya pili jana, baada ya juzi mahabusu hao kukataa kushuka katika karandinga kwa ajili ya kusikiliza kesi zao, wakishinikiza upelelezi wa kesi zao ufanywe haraka kama ilivyokuwa kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, anayekabiliwa na kesi ya kuua bila ya kukusudia.

Mgomo huo ambao unaonekana kuishika pabaya serikali, uliendelea tena jana kwa nyakati tofauti katika mahakama ya Kisutu na mahakama za wilaya za Ilala na Temeke ambako mahabusu waligoma kushuka huku wakisisitiza kuwa hawatafanya hivyo hadi hapo serikali itakapotoa tamko kuhusiana na madai yao.

Wakiwa ndani ya makarandinga ya polisi katika mahakama hizo, mahabusu hao waliendelea na staili yao ya kuimba nyimbo za kudai haki na kuishutumu serikali kuwa inafanya upendeleo katika kushughulikia kesi za vigogo na walalahoi.

Walimtaka Dk Nagu na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) watoe tamko litakalofafanua muda ambao mtuhumiwa wa mauaji anastahili kukaa mahabusu wakati upelelezi wa kesi yake ukiendelea kwa kile walichoeleza kuwa upo upendeleo wa dhahiri katika kushughulikia kesi hizo.

Walisema tatizo zaidi linakuwa katika kesi zinazohusisha vigogo wa serikali na watu maarufu, huku zile zinazowahusu walalahoi zikipuuzwa na upelelezi wake ukichukua muda mrefu na kuwaacha wakiteseka gerezani bila ya kupatiwa haki za msingi.

Pia walimtaka Waziri Nagu, atembelee magereza aweze kujionea mwenyewe hali halisi, ili ajue kuwa kuchelewesha kesi hizo ni kuwaumiza na kuwapa mateso makubwa mahabusu.

Katika Mahakama ya Kisutu, jana, karandinga la kwanza lililochukua mahabusu kutoka Gereza la Keko lilifika saa 3.30 asubuhi na kama ilivyokuwa juzi, waligoma kushuka na baada ya muda mfupi walirudishwa gerezani.

Karandinga la pili lilifika saa 4.38 asubuhi, likiongozwa na gari la polisi namba T 220 AMV Land Rover, lakini mahabusu waliokuwamo pia waligoma kushuka na kurudishwa mahabusu.

Katika mahakama za wilaya za Ilala na Temeke, kesi zote zinazohusu mahabusu waliotoka katika magereza ya Keko na Segerea, ziliahirishwa jana baada ya mahabusu kugoma kushuka kwenye karandinga wakidai kucheleweshwa kwa upelelezi wa kesi zao.

Kutokana na hali hiyo, baadhi ya mahabusu waliokuwa wakitarajia dhamana, waliangua kilio baada ya kuwaona ndugu zao waliofika mahakamani hapo kwa ajili ya kuwawekea dhamana.

Katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, waliobahatika kushuka kwenye karandinga ni mahabusu wanawake kutokana na wao kuwekwa katika chumba tofauti na wanaume ndani ya gari lililowafikisha mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Joyce Minde, alisema kuwa amewasiliana na polisi ili wafuatilie suala hilo.

Mjini Arusha, mahabusu wanaokabiliwa na kesi mbalimbali nao waligoma kushuka katika karandinga katika viwanja vya Mahakamani Kuu wakitaka kuonana na Rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwa jirani na mahakama hiyo, ilipo Ikulu ndogo wakilalamikia kucheleweshwa kesi zao.

Mahabusu hao wanaokaridiwa kufikia 70, walipaza sauti wakilalamikia kuachiwa kwa dhamana kwa Ditopile huku wao wakiachwa wateseke gerezani.

Mahabusu hao baadaye walianza kuimba kwa sauti kubwa "polisi wanataka nini...wanataka rushwa na Ditopile kawapa nini, kawapa rushwa" hatua ambayo ilizuwa tafrani kubwa mahakamani hapo na kwa maafisa wa usalama ambao walikuwa viwanja vya Ikulu.

Tukio hilo lilianzaa majira ya saa 3.30 mara baada ya mahabusu hao kuwasili katika gari lao lenye namba za usajili STG 9266 na lilidumu hadi saa 4.11 pale maafisa kadhaa wa polisi walipowasili na kuamuru mahabusu hao kurejeshwa magerezani.

Maafisa wa polisi wakiwa katika gari lenye namba za usajili T638AJR na polisi wengine wa kutuliza ghasia wakiwa katika gari lenye namba za usajiri T 447 APF waliwaondoa mahabusu hao kupitia njia tofauti na ambayo hutumika, hivyo kukwepa Rais Kikwete asisikia kelele hizo.

Awali, mahabusu hao huku wakipiga mayowe, walikuwa wakilalamikia polisi kuchelewesha kesi zao na hasa upelelezi, hatua ambayo inachangia kukaa muda mrefu magerezani.

Hata hivyo, hakuna hakimu ambaye alikuwa tayari jana kuongelea tukio hilo kwa maelezo kuwa wanaolalamikiwa ni polisi na sio wao.

Katika mgomo wa juzi katika mahakama ya Kisutu, Mahabusu wanaokadiriwa kuwa kati ya 250 hadi 300 wakitokea katika magereza ya Keko na Segera, waligoma kushuka ndani ya magari ya polisi STH 3058 na STJ 903 wakilalamikia ucheleweshwaji wa upelelezi wa kesi zao.



kazi kwelikweli.........
 
Majaji wangapi walioteuliwa na wangapai waliostaafu ama kufa? Je, hilo siyo suala la kata mti. panda mti?
 
Message sent kwa wapelelezi
Siku zote wakazi wa Dar huyaogopa makarandiga ya Polisi yakiwa yamebeba wafungwa kutokana na mitusi ya nguvu wanayoporomosha, ila jana walikuwa wanawashangilia na kuwapungia mikono.

Mabadiliko hayo ya mioyo ni hatua ya kuwaunga mkono kwa uamuzi wao wa kugoma kushuka katika Mahakama ya Kisutu kusikiliza kesi zao.

Wakati mgomo huo ukiendelea raia waliojazana Mahakama ya Kisutu waliungana na watuhumiwa hao wa mauaji kuimba wimbo wa 'parapanda italia parapanda.....'

Kilichoibua mgomo ni hatua ya Mahakama kuharakisha uendeshaji wa kesi ya Dito kwa miezi mitatu na hadi kuachiwa kwa dhamana kwa kosa la kuua bila kukusudia.


Kibao kiligeuka na raia kushangilia mgomo wa wafungwa..


Malalamiko ya watuhumiwa hao ni kutokana na baadhi yao kukaa
lupango kwa miaka 10 na bado kesi zao hazijasikilizwa.

Kushindiliwa kwenye karandinga kupita kiasi hadi kufikia 170 kwa gari moja (lenye uwezo wa kubeba watu 30) huku wakidai kuwa huletwa mahakamani saa 12:00 asubuhi na kurejeshwa gerezani saa 11:00 jioni bila ya chakula wala maji ya kunywa.

Waliendelea kutema cheche kuwa hata ndugu zao huzuiwa kuonana nao na baadhi ya ndugu zao wa uraiani walishawekwa mahabusu kwa siku mbili kwa kisa cha kuwaletea chakula.

Mgomo huo ulidumu hadi saa 5:00 asubuhi hadi Hakimu Mwangesi
alipoamua warejeshwe magerezani huku message ikiwa sent
 
habari, tatizo siyo mahakama..! kesi imeharakishwa na DPP na maafisa wa polisi.. Mahakama husikiliza kesi baada ya ushahidi kukamilika....
 
Serikali yatoa tamko sakata la Ditopile
Nduguze kuchukuliwa hatua za kisheria

Nasra Abdallah, Safina Tibanyendela na Amana Nyembo

HATIMAYE serikali imetoa tamko kuhusu vurugu zilizofanywa katikati ya wiki iliyopita na ndugu na jamaa wa Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, ndani na nje ya jengo la Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam. Mbali ya hilo, serikali pia imeeleza kuguswa na matukio ya jana na juzi, ya mahabusu walio katika magereza mbalimbali nchini, kugoma kushuka katika makarandinga wakipinga kuchelewa kusikilizwa kwa kesi zao.

Tamko hilo la serikali lilitolewa na Waziri wa Usalama wa Raia, Harith Bakari Mwapachu, ambaye aliwataka ndugu na jamaa hao wa Ditopile-Mzuzuri na watu wengine walioshiriki katika vurugu zilizotokea Mahakama Kuu siku Ditopile alipoachiwa kwa dhamana, kukaa chonjo. Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mwapachu alisema wizara yake haiwezi kukaa kimya na kuliacha suala hilo, ambalo ni ukiukwaji mkubwa wa sheria, lipite hivihivi.

Alisema ofisi yake bado inalifuatilia suala hilo kwa karibu na hatua zaidi zinatarajiwa kuchukuliwa pale Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema, atakaporejea kutoka Afrika Kusini. Kuhusu waandishi waliopigwa na kuharibiwa vifaa vyao vya kazi, Mwapachu alisema uongozi wa polisi unasubiri taarifa ya mahakama kabla kuchukua hatua kwa wote watakaobainika kukiuka sheria, kanuni na taratibu. Alisema hivi sasa, uchunguzi unafanyika kwa nia ya kubaini kilichotokea na kuwatambua wote waliohusika ili sheria ichukue mkondo wake.

Mwapachu ametoa kauli hiyo wakati mgomo ulioanzishwa na mahabusu wanaosikiliza kesi zao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kutokana na mwenendo wa kesi ya Ditopile, ukisambaa mikoani. Kuhusu mgomo huo, alisema tayari ameshaliagiza Jeshi la Polisi na taasisi nyingine kwenda katika mahabusu zote zilizoathirika na kuzungumza na mahabusu waliogoma.

Waziri Mwapachu alisema amewataka polisi watakaoifanya kazi hiyo, kuhakikisha wanapitia kila jalada la kesi ya mahabusu mwenye matatizo kwa lengo la kubainisha imechukua muda gani. Mwapachu alitaka kupewa taarifa kuhusu agizo hilo mwishoni mwa mwezi huu. Aidha, alisema katika taarifa hiyo, polisi hao wanapaswa kuongeza maelezo kuhusu mahusiano kati ya mahabusu, wafungwa na askari magereza.

"Nimeagiza ripoti hii iandaliwe kwa ushirikiano kati ya wanasheria, majaji, mahakama na polisi," alisema Mwapachu ambaye ameongeza kuwa, lengo litakuwa ni kuhakikisha kesi ndogo ndogo zote zinashughulikiwa haraka kwa nia ya kupunguza msongamano katika mahabusu na magereza. Kuhusu Ditopile kupata dhamana haraka wakati mahabusu wengine wanasota kwa miaka mingi, Mwapachu alisema hiyo inatokana na uwezo wa Ditopile kuweka mawakili wazuri kumtetea.

"Watu wenye uwezo wa kufuatilia mambo yao, kesi zao huenda haraka kutokana na kuweka mawakili wazuri kitaaluma, ambao wana uwezo mkubwa wa kufuatilia kesi hizo," alisema na kukiri kutokuwepo kwa usawa kati ya watu wenye uwezo na wasio na uwezo, akibainisha kuwa hilo ni jambo la kawaida popote duniani.

Alisema suala la Ditopile kutoka haraka si la serikali wala mahakama, kwani ametolewa kwa mujibu wa sheria zilizopo. Wakati huo huo, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Sivangilwa Mwangezi, amedai kuwa mgomo wa mahabusu hao hauwezi kuathiri utendaji kazi wa mahakama hiyo.

Alidai kuwa, kazi kubwa ya mahakama ni kusikiliza mashauri yanayoletwa mbele yake iwapo mahabusu watakuwepo mahakamani. Kwa kuwa mahabusu hao wamegoma, alisema kuwa mahakama haitakuwa na cha kufanya mpaka pale watakapoamua kurejea ili kesi zao ziendelee. "Kama wao hawashuki, sisi tunaendelea kusikiliza kesi za washitakiwa ambao wako nje kwa dhamana… mimi si kazi yangu kufuatilia mgomo kwa sababu hiyo ni kazi ya ofisa wa makosa ya jinai kanda ya Dar es Salaam na kama wataamua waende gerezani wakawaombe ili waje kuendelea kusikiliza kesi zao," alisema.

Mgomo huo, ulioanzishwa juzi na mahabusu katika Mahakama ya Kisutu, jana ulisambaa katika mahakama zingine Dar es Salaam na Arusha. Jana, mgomo huo ulianzia katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala majira ya saa 3:10 asubuhi baada ya gari la kubeba mahabusu lilipowasili kutoka gereza la Keko. Mahabusu waligoma kuteremka wakidai haki itendeke kupitia nyimbo walizokuwa wanaimba na vikaratasi walivyoviandika na kuvipenyeza kwa waandishi wa habari.

Katika vikaratasi hivyo, mahabusu hao walitaka viongozi kadhaa wa juu wa Jeshi la Polisi kujiuzulu wakiwatuhumu kwa uzembe, upendeleo na rushwa, na kwamba utendaji wao umedhihirisha kuwa hawaiwezi kasi mpya. Karandinga hilo lililokuwa na namba za usajili STH 3058 liliondoka kuelekea Mahakama ya Kisutu na liliwasili saa 3:30, lakini mahabusu hao walishikilia msimamo wao na kumtaka Waziri wa Sheria na Katiba, Mary Nagu, kutoa tamko.

"Hatushuki humu ndani labda mtuue humuhumu, waendesha mashtaka wanachelewesha kesi zetu, ndio chanzo kikubwa cha sisi kuendelea kujazana huku magerezani wakati kuna magonjwa mengi… mahakimu wanaendesha kesi kwa kuwasikiliza waendesha mashitaka tu, sisi hatusikilizwi," walidai. Alimtaka Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) naye awaeleze upelelezi wa kesi unachukua muda gani wakati wengine wamekaa mahabusu zaidi ya miaka kumi.

Ilipofika saa 3:47 asubuhi mahabusu walirudishwa Keko na karandinga la pili kutoka Gereza la Segerea lenye namba za usajili STJ 903 liliwasili Mahakama ya Kisutu saa 4:23 asubuhi likiwa limeongozana na gari moja la polisi lenye namba za usajili T 220 AMV na FFU lenye namba PT 0892. Mahabusu hao wapatao 150, nao walishikilia msimamo wa kutoshuka katika gari hilo wakiomba upelelezi wa kesi zao uharakishwe.

Baada ya mahabusu hao kugoma kuteremka, gari hilo liliondoka mahakamani hapo kuwarudisha Segerea majira ya saa 4:36 asubuhi huku wakiimba wimbo maarufu wa "Parapanda italia." Naye mkuu wa waendesha mashtaka mahakamani hapo, Germanus Mhume, alisema hawawezi kutumia nguvu kuwalazimisha mahabusu hao wateremke kwenye gari. Alisema wataendelea kusubiri mpaka siku watakayoamua kushuka kusikiliza kesi zao.

Kutoka Arusha, Ramadhani Siwayombe na David Frank wanaripoti kuwa, sakata la mahabusu kugoma baada ya kuachiwa kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, limechukua sura mpya mara baada ya mahabusu jijini Arusha jana nao kuamua kugoma kushuka katika karandinga kwa madai ya upelelezi wa kesi zao kucheleweshwa.

Sakata hilo lilianza majira ya saa nne asubuhi, baada ya mahabusu hao kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi na kutakiwa kushuka baada ya askari kufungua mlango, lakini wao wakaanza kuimba nyimbo mbalimbali za kuashiria mgomo.

Mahabusu hao walianza kupiga kelele wakidai waambiwe Ditopile katoa nini ili nao watoe, ili kesi zao zisikilizwe haraka. Walisema bila ya kupatiwa maelezo yanayoridhisha, hawatashuka katika gari hilo lenye namba za usajili STG 5699 aina ya Scania. Baada ya kufunguliwa kwa mlango wa karandinga hilo, askari walishuhudia mahabusu mmoja tu mwanamke, akishuka katika karandinga hilo huku mahabusu wote waliobaki wakigoma na kusababisha shughuli mahakamani hapo kusimama.

Hatua hiyo ya mahabusu kugoma kushuka na kuanza kuimba nyimbo na kupiga kelele, ilizua mtafaruku mwingine, kwani mahakama hiyo ipo jirani na Ikulu ndogo ambayo Rais Jakaya Kikwete, ambaye yupo mjini hapa kwa ziara ya kikazi, amefikia.

Kelele hizo ziliwalazimisha askari waliokuwepo katika Ikulu hiyo, kwenda mahakamani hapo kwa ajili ya kuimarisha usalama. Hata hivyo, kuwasili kwa askari hao waliokuwa katika magari manne aina ya Land Rover Defender na pikipiki, kuliamsha ari ya mahabusu hao, ambao waliongeza kelele za kutaka waambiwe kiini cha kesi zao kuchelewa kusikilizwa.

"Tunaomba tuelezwe sababu ya kesi zetu kuchelewa kusikilizwa kwa madai ya uchunguzi kutokamilika, huku kesi za anayetajwa kuwa mwana mtandao kusikilizwa kwa haraka na kuachiwa kwa dhamana huku sisi tukiendelea kuteseka jela," walisema.

Kufuatia kelele hizo kuzidi, Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) mkoani hapa, Kamanda Shilogile, alifika mahakamani hapo na kuwabembeleza mahabusu hao kushuka, lakini juhudi zake ziligonga mwamba. Baada ya kujadiliana na wahusika wengine kwa muda, aliamuru mahabusu hao warejeshwe magereza Lisongo.

Akizungumza na gazeti hili baada ya mgomo huo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Basilio Matei, alisema umetokana na mgomo uliotokea jijini Dar es Salaam na madai yao hayana tofauti na yale yaliyotolewa na mahabusu wa Dar es Salaam. Kamanda Matei alisema, hivi sasa anafanya utaratibu wa kuwasiliana na mamlaka zinazohusika na masuala ya kesi hizo ili kuangalia hatua gani za kufanya kutatua tatizo hilo linalolalamikiwa na mahabusu hao.

Hii ni mara ya pili kutokea kwa tukio kama hilo mkoani Arusha. Miaka miwili iliyopita, mahabusu wa kesi kubwa za jinai na mauaji waligoma wakilalamika kucheweshwa kwa kesi zao.

Kutoka Mwanza, Mwandishi Wetu, anaripoti kuwa, baadhi ya mahabusu katika gereza kuu la Butimba, wametishia kugoma kuteremka kutoka katika karandinga siku ya kupelekwa mahakamani kutokana na madai ya kesi zao kucheleweshwa kutolewa maamuzi, huku za vigogo na wale wenye uwezo kutolewa maamuzi haraka haraka.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa, baadhi ya mahabusu wamekuwa wakisubiri kusikilizwa kwa kesi zao kwa zaidi ya miaka mitano sasa. Walidai kuwa wapo tayari kuungana na wenzao wa Dar es Salaam ambao jana na juzi waligoma kushuka katika magari wakitaka kuelezwa sababu zinazochelewesha kesi zao.


MWANAKIJIJI JE MWAPACHU AMEKUCONVINCE AU NI YALEYALE

juu
 
http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/3/14/makala7.php

Kikwete usikubali kuwa shahidi wa uovu kulinda urafiki wa Dito
Mwandishi Wetu

MACHI 12 mwaka huu, kwa mara nyingine Tanzania ilishuhudia mwamko mpya wa watu kujua haki zao. Tanzania ilizaliwa upya. Hii ni baada ya siku tano kabla heshima ya mahakama kuchafuliwa na kuifanya ionekane kama si chochote si lolote. Haki kwa mara ya kwanza ilidaiwa na wanyonge, tena wafungwa. Nimekuwa nikisema mara nyingi kuwa unaweza kuufunga mwili lakini si ubongo.

Unaweza kuumiza mwili hata kuua lakini huwezi kuua mawazo. Kilichofanyika Machi 12 ni mapinduzi makubwa. Tumezidiwa akili na wafungwa kiasi cha kutufundisha jinsi ya kuiangalia na kuitenda haki! Tumekuwa wanafiki na dhulumati kiasi cha kushangilia uovu na dhuluma mchana kweupe! Yaani hatujali hata thamani ya damu ya mwenzetu! Mbona inatisha na kusikitisha sana!

‘Vox populi vox dei' Walatini husema, yaani sauti ya wengi ni sauti ya Mungu. Ukiipuuza unampuuza Mungu na ukiisikiliza unamsikiliza Mungu. Maana ni hao hao wengi wanaoiweka na kuiondoa mamlakani serikali. Tuwe wazi. Kitendawili kilichosababisha hadi wafungwa wakagoma kushuka kwenye makarandinga ni kutokana na kesi tata ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ditopile Mzuzuri.

Sitataka kuingia kwenye undani wa suala ambalo ni ‘Sub Judice' yaani lipo mahakamani. Ila kitu kinachoiacha nchi yetu njia panda na uchi, watu na mamlaka zake zote ni ile hisia kuwa kumbe kuna watu miongoni mwetu wana haki kuliko wengine na wana umuhimu kuliko wengine.

Hii ni kinyume cha taratibu, sheria na imani yetu kwa mifumo yetu yote inayohimiza usawa bila kujali jinsia, cheo, mbari, kujuana na kadhalika. Ukiwaondoa mahabusu walioamua kuiondolea uvivu tabia hii chafu, waandishi wa habari na Mchungaji Christopher Mtikila waliojitokeza na kupinga wazi wazi uchafu huu, wananchi waliobaki wamekuwa wanafiki na dhulumati kutaka kubariki jinai.

Kisa? Kwa sababu mhusika kama walivyokaririwa ndugu zake hivi karibuni ni rafiki eti wa rais! Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali (DPP) si mahakama. Inaweza ikajadiliwa hata kukosolewa. Inaanza kutuchezea na kuchezea uhuru wa nchi hii. Pamoja na kwamba lengo la darasa hili si kupinga madaraka ya DPP, hatuwezi kuachia matumizi ya ovyo ya ofisi hii yapite bila kujadiliwa. Kimsingi ofisi hii tuliirithi kutoka kwa mkoloni ambaye aliianzisha kuokoa watawala wa kikoloni wasifungwe wanapovunja sheria.

Kimsingi lengo la kuundwa kwa ofisi hii na mkoloni ilikuwa ni kutoa haki kwa mkono wa kulia na kuichukua haki hiyo hiyo kwa mkono wa kushoto. Kwa bahati mbaya, watawala wetu baada ya kupata uhuru wa bendera waliiacha hivyo hivyo kwa makusudi. Maana kilichoitwa uhuru kwa nchi nyingi ilikuwa ni kubadilisha mkoloni mweupe kuingiza mweusi.

Kuna walioiacha hivyo hivyo kutokana na tabia ya kudhani kuwa kila anachofanya mkoloni ni chema. Na wengine waliiacha ili waitumie kikoloni kama ambavyo imetumika siku za karibuni hadi kuzua malalamiko makubwa. Ukisoma sheria inayohalalisha ofisi ya DPP, inasema wazi kuwa DPP anaweza kuingilia kesi yoyote, kuifuta au kuamua anavyoona bila kuhitajika kutoa maelezo kisheria isipokuwa kwa rais (gavana) peke yake.

Hii maana yake ni kwamba ofisi ya DPP si ya umma kama tunavyoaminishwa bali ya DPP mwenyewe na bosi wake, yaani rais. Haya. Kuthibitisha maana hii na hali hii, kilichoelezwa na ndugu wa mtuhumiwa Mzuzuri tusikilaani, bali tufurahi kuwa kimetufungua macho kuwa ofisi hii si chochote bali kichaka cha dhuluma na unafiki.

Ukirejea kilichotokea Machi 8 mwaka huu wakati ndugu yao akipewa dhamana, na kutafakari kauli zao kuwa ndugu yao ni rafiki mkubwa wa rais, unapata maana na umuhimu wa ofisi hii kuwa ni mali ya rais. Hii maana yake ni kwamba hawa watu si wendawazimu. Wana sababu, tena za maana.

Wanajua kuwa nyuma ya pazia kuna rais anayeshinikiza rafiki yake kipenzi aachiwe bila kujali haki ya marehemu wala sheria. Hakuna anayebisha, akiwamo hata rais na ofisi yake. Kwa nini rais hakukanusha wala kuwakemea wahuni hawa kama wanavyoitwa? Hivi tunapelekwa wapi? Polisi ambao waliapa kupambana na uhalifu wanapoamua kuulinda uhalifu usidhani ni bure.

Lazima kuna mtu au watu wazito wenye mamlaka wanaowaambia kufanya hivi. Maana polisi wetu si vichaa wala mazoba na mabunga ya kufanya vitu kama hivi. Ila ieleweke kuwa ulevi wa madaraka kama huu huwa na mwisho mbaya. Rejea Rais mstaafu Benjamin Mkapa, anavyosukasukwa hadi kuhitaji na kuridhia kutetewa na Rais Kikwete. Aibu.

Hivi ni jinai na kufuru kiasi gani mhalifu kugeuzwa jaji hadi kupitishwa kwenye mlango rasmi na pekee kwa ajili ya majaji? Laiti nchi hii ingekuwa na watu makini, sina shaka siku hiyo hiyo wangejaa mitaani na kuhakikisha hawaondoki hadi Jaji Mkuu, Inspekta Mkuu wa Polisi (IGP), hata Rais aliyetajwa wazi wazi, wanaondoka kwenye ofisi za umma. Ajabu hawa wanaoitwa wahuni waliofanya yote haya, bado wako mitaani wakitanua!

Nani atawakamata iwapo walikuwa wanamtetea rafiki wa mwenye dola? Aibu. Ila wajue ukuu wa dola si umiliki wa dola. Hata mtu akijidanganya kuwa anamiliki dola ni kwa muda tu. Hata kama upuuzi huu unafanywa na wakubwa, hili ni jambo la hatari kwa nchi yetu. Uswahiba, ushoga, kujuana na uovyo huu, vitahatarisha usalama wa nchi hii. Kama hatua madhumuni hazitachukuliwa, umma utapoteza imani na serikali yao kiasi cha kujichukulia sheria mkononi.

Ndiyo. Watu baada ya kuona mahakama dhalili na polisi wanaoweza kumlinda mhalifu na wapambe wake, vikitumika kwa manufaa ya kikundi kidogo cha watu, tena wasio waadilifu, lazima watajichukulia sheria mkononi. Matokeo ya hali hii Mungu pisha mbali hayatakuwa mazuri. Tusutane. Dola haiendeshwi kimdundiko. Leo tumekuwa mashahidi wa uovu ili kulinda urafiki! Tumekuwa woga na wa ovyo kiasi hiki kushindwa hata kusema kuwa hivyo sivyo!

Nchi hii si mali ya chama, serikali wala klabu ya urafiki, hata kama ni wa rais. Nchi hii ni mali ya Watanzania wote kwa usawa. Huu ndiyo msingi aliuoweka Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Hiki ndicho mababu zetu walichopigania. Hii ndiyo heshima ya nchi yetu. Anayeichezea hata awe mkubwa kiasi gani anatuchokoza. Hii ni nchi, si kipande cha nchi cha kufanyia majaribio wala kulipia fadhila.

Hatuwezi kukaa kimya wakati nchi yetu inachezewa na watu wachache kwa kusingizia mamlaka.
Kitendo cha wananchi kushuku kuwa haki inadhulumiwa na sheria zinapindwa ni rufaa ya umma. Wahusika wasijidanganye kuwa wananchi wataendelea kugeuzwa punda au kondoo na kuku. Hii ni rufaa ya umma na ya aina yake.

Maana inafanyika hata kabla ya kesi husika haijasikilizwa wala kutolewa uamuzi. Je, haki itatendeka? Na ieleweke hapa kuwa hatuingilii mahakama wala kuishutumu bali tunachojua kuwa haina lawama maana mahakama si ‘ambulance chaser'. Yaani haiwezi kuingilia mambo yaliyoletwa mbele yake. Maana huwa haiendi mitaani yanakofanyika hayo yaliyoletwa kwake.

Hii ndiyo maana hakimu hawezi kutoa ushahidi kwenye kesi anayoisikiliza. Leo mtu anaua kwa hasira na ujinga wake, kesho unaambiwa aliua bila kukusudia! sheria gani hii?

Kwani dhamira ya kuua inatowekaje iwapo mtu anachomoa bastola au kisu mfukoni ili avifanyie nini? Alie ugali! Kama lengo si kuua, kwanini mhusika asichomoe lau mkanda wa suruali au hata kalamu? Hapa ndipo Mchungaji Christopher Mtikila anapowazidi wengi akili.

Hapa ndipo hatari ya uwepo wa ofisi ya DPP unapojidhihirisha. Hapa ndipo jeuri ya madaraka, ushoga na urafiki inapochipuka hata kama si kweli.

Hapa ndipo zilipo tambo za ndugu wa mtuhumiwa. Ndipo ilipo chemchemi ya dharau na vitendo vya fujo kwetu sisi wana habari na mahakama.

Wito kwa Mtikila. Kama atatimiza azima yake ya kufungua kesi upya atakuwa amepigania heshima ya nchi na mahakama zetu kuliko mtu yeyote mwingine. Tumpongeze kwani si mara yake ya kwanza kuona watu wengine wanachokifumbia macho.

Kuna haja ya wahusika kuacha kufanyia mzaha, uhuni, utoto na upuuzi mambo ya umma.
Nchi nyingi zimejikuta shakani kutokana na uchafu wa aina hii. Rwanda walifikia kuchinjana kwa mamilioni baada ya kabila moja kujikuta likitendewa kama si raia wa nchi hii na kabila jingine.

Leo nchini kuna makabila makubwa mawili, wenye pesa na madaraka na makapuku.

Uzuri ni kwamba makapuku ni wengi. Wakiamua kuondoa uvivu, hao wenye pesa na madaraka ambao ni wachache hawawezi kula pesa yao vizuri.

Wito kwa Rais Jakaya Kikwete. Tunataka kusikia kauli yake juu ya madai yaliyotolewa na ndugu wa Ditopile kuwa yeye ni rafiki yake mkubwa, hivyo rais hawezi kuona rafiki yake anatesekea gerezani wakati wao wana madaraka.
 
Mimi kinachonisikitisha ni kuwa wakati Mtikila anataka kufunguwa kesi ya ditopile upya ndugu na jamaa wa marehemu wapo kimya kabisaa kama hawapo. Hata mashtaka yalipobadilishwa kutoka kuua kwa kukusudia kuwa kuua bila kukusudia pia walikuwa kimya. Au kimya chenyewe kinatokana na ziara za viongozi wetu zilizo wazi na zisizo wazi pamoja na rambi rambi walizopewa? Hivi kumbe siku hizi roho inaweza nunuliwa bei rahisi hivyo.
 
joo wane karibu tukate ishu na tuendeshe nchi...

mimi ninao ushauri mmoja kwa muheshimiwa rais..katika juhudi za kurudisha hadhi ya idara ya mahakama kwa ajili ya rafiki yake ditto ...kitendo ambacho forum hii ilikijua tangu anakamatwa hasa BAADA ya rambi rambi yake na zilizofuatia kwenye msiba wa mbonde..werevu walishajua kuwa pale UHAI ULISHANUNULIWA...

Muungwana anatakiwa achukue hatua za haraka kuhakikisha wale nduggu zake ditto waliopiga waandishi mahakamani wanafikishwa mahakamani na kushitakiwa...

anatakiwa yeye binafsi alikemee hili suala....

hatua ya haraka ichukuliwe kuhakikisha suluhisho la kudumu la PP na CID na ikiwezekana hivi vitengo vipewe bajeti zaidi na vitendea kazi..

hii agalau itarudisha imani iliyopotea...
 
Mimi kinachonisikitisha ni kuwa wakati Mtikila anataka kufunguwa kesi ya ditopile upya ndugu na jamaa wa marehemu wapo kimya kabisaa kama hawapo. Hata mashtaka yalipobadilishwa kutoka kuua kwa kukusudia kuwa kuua bila kukusudia pia walikuwa kimya. Au kimya chenyewe kinatokana na ziara za viongozi wetu zilizo wazi na zisizo wazi pamoja na rambi rambi walizopewa? Hivi kumbe siku hizi roho inaweza nunuliwa bei rahisi hivyo.


Hapo ndipo wakati mwingine huwa nakubaliana na wakenya kuwa sisi watanzania ni watu wa aina yake! Hii kesi ingechukua sura ingine kabisa kama ndugu wangeonesha kidogo tu kujali roho ya ndugu yao. Lakini hawa wamethamini sana zile ziara za wakubwa wa hapa duniani.

Inabidi turejee tena zile safari tujiulize hivi hawa walikuwa wanaenda kufanya nini kule Kawe kwa ndugu wa marehemu? Ni kutoa pole tu kweli? Kama ni pole tu mbona athari zake zimekuwa kubwa namna hii kwa ubinadamu wa hawa ndugu?
 
Kweli wadanganyika tupo tupo tu. Hivi hizo "ngo" za haki za binadamu zipo wapi zinashindwa hata kuaandaa maandamano ya amani kupinga dhamana hiyo na jinsi mazingira ya kesi ilivyoendeshwa ukizingatia kuna watuhumiwa wamekaa miaka 15 ndani. Si huwa nasikia kuna "ngo" za kwasaidia watuhumiwa/wafungwa au ndio zile zile za kuwasaidia waliozianzisha? Mpaka watuhumiwa/wafungwa wanagoma ndio watu tulio nje tunashtuka na kujitia tunawasapoti. Jamani wanadanganyika wenzangu tuamke tupiganie haki za wafungwa/watuhumiwa kwani magereza yapo kwa ajili ya binadamu wote huwezi kujua ni siku gani unaweza kuteleza ukajikuta upo ndani ya gereza
 
Joo wane
nakubaliana nawe kabisa . NGO zikijitokeza watakiona cha moto kama kile cha Hakielimu .

Lakini bado we need them to out.
 
hata kama ndugu wa marehemu watakaa kimya, tusife moyo, hii yaweza kusabiswa na uelewa mdogo wa mswala ya kisheria au sababu nyingine....

kesi inayomkabili dito haijafunguliwa na ndungu wa marehu bali ni Jamuhuri ya muungano vs Dito jamuhuri ni wewe na mimi.

jambo la msingi ni kuumuunga mkono Mtikila ili mashitaka yabadilishwe, ili dito kesi yake iwe ni kuua kwa kusudia
 
Joo wane,

Hata mimi nakusupport mzee, hizi NGO zinafanya kazi gani??

Mtu unakaa unasubiri kesi yako kwa muda wa miaka 15? duh!!! this is too much - wana haki ya kugoma
 
hivi mnajua ni kiasi gani serikali imekuwa karibu na familia ya Marehemu Mbonde? mtashangaa!!
 
Chakusikitisha baada ya miaka 15 ya kukaa mahabusu na miaka 4 ya kesi unaambiwa na jaji huna makosa upo huru. Duu umetumikia kifungo cha miaka 19 bila kosa uuuuuh ndio Tanzania hiyo nchi ya domokrasia na waumiani ( sorry demokrasia na amani)
 
Back
Top Bottom