Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Tarehe 3/14/2007

MWANANCHI HABARI
Polisi wamtetea Ditopile, mahabusu wazidi kugoma

Na Nora Damian

MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, ametaja sababu za kuharakishwa kwa upelelezi wa kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri.

Manumba alitoa maelezo hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya jeshi hilo kufuatia mgomo wa mahabusu unaoendelea katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha na Dodoma.

Mahabusu hao ambao mgomo wao unaonekana kuchochewa na kuachiwa kwa dhamana kwa Ditopile, wanadai upelelezi wa kesi zao unacheleweshwa kwa makusudi wakati ule unaohusu kesi za wakubwa kama Ditopile, unaharakishwa.

Akijibu maswali kuhusiana na madai ya Ditopile, kupendelewa na kuharakishiwa upelelezi, Manumba alisema katika kesi za namna hiyo ambapo mtuhumiwa anajisalimisha mwenyewe, inasaidia kuondoa ugumu wa upelelezi na hivyo kuwasadia polisi katika kukusanya ushahidi na hatimaye kesi hiyo kuharakishwa.

Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya mashahidi yaliyosomwa mahakamani Kisutu, Ditopile alijisalimisha kwa polisi na kuelezea tukio la mauaji lilivyotokea.

Manumba alipinga kuwa ucheleweshaji wa upelelezi katika baadhi ya kesi unategemea hadhi ya mtu.

Alisema mara nyingi ucheleweshaji au uharakishaji wa upelelezi, unategemea sana mazingira ya kosa lenyewe lilivyotendeka, upatikanaji wa haraka wa mtuhumiwa na vielelezo, vitu ambavyo alisema vinawarahisishia polisi kupata ushahidi wa kile kilichotokea.

Kwa mujibu wa Manumba, kesi inaweza kumalizika au kusikilizwa haraka au kuchelewa kutokana na mazingira ya jinsi kosa lilivyotendeka, tabia na mwenendo wa mshtakiwa kabla na baada ya kutenda kosa, mashahidi walioshuhudia kosa likitendeka na vielelezo vinavyohitajika kuthibitisha kosa.

Akizungumzia kuhusu baadhi ya mahabusu kupelekwa kwa makarandinga na baadhi yao kwenda kwa usafiri maalum, Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Alfred Tibaigana, aliyeambatana na Manumba, alisema kuwa suala hilo linatokana na uzito wa kesi husika na mshitakiwa mwenyewe.

“Mfano kesi ya Ditopile ile ina mvuto kwa jamii hivyo anapokwenda mahakamani lazima tuhakikishe yuko salama ili asije akadhuriwa kwa sababu akiwa mikononi mwetu, ikitokeo hilo, sisi tutakuwa hatuna kazi. Tulikuwa tunafanya vile kwa sababu ya usalama wake,” alisema Tibaigana.

DCI alikiri kuwa baadhi ya madai ya mahabusu ni ya kweli kwa kuwa Jeshi la Polisi lina udhaifu katika kushughulikia upelelezi wa baadhi ya kesi kutokana na matatizo ya uhaba wa vitendea kazi na upungufu wa taaluma ya upelelezi katika jeshi hilo.

“Mgomo huu wa mahabusu sisi kwa kweli umetusikitisha, matatizo ya upungufu wetu, nyenzo na taaluma ndani ya upelelezi yapo, hivyo kuna uwezekano mambo mengine pia yakachelewa, lakini si kwa kudhamiria,” alisema Manumba.

Alisema tayari wameshawaagiza makamanda wa polisi wa mikoa kwa kushirikiana na mahakimu wa mikoa, mawakili wa serikali walioko katika kanda na maafisa magereza, waende magerezani ili kusikiliza madai ya mahabusu nchi nzima ili yaweze kushughulikiwa.

Alisema wameagiza ucheleweshaji wa upelelezi unaotokana na sababu zisizo za msingi, uchukuliwe hatua na kwamba mahakimu wameagizwa watathmini uwekwaji wa watu ndani kulingana na taratibu za kisheria.

Aliwataka mahabusu waliopo katika mgomo kusitisha mgomo huo huku madai yao yakishughulikiwa ili kesi zao ziendelee kama kawaida.

“Tunaomba washitakiwa wetu watumie busara, waheshimu sheria za nchi na waendelee kuhudhuria mahakamani kwa sababu hiyo nayo ni haki yao na wajue kuwa kugoma ni njia nyingine ya kuendelea kuchelewesha kesi zao mahakamani,” alisema Manumba.

Wakati huo huo, mgomo wa mahabusu wa kupinga kucheleweshewa kesi zao, jana uliingia siku ya tatu katika mahakama zote za jijini Dar es Salaam, siku ya pili Arusha na ukasambaa zaidi hadi Dodoma.

Mahabusu hao waligoma kushuka katika makarandinga yaliyowapeleka katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mahakama za wilaya za Kinondoni, Temeke na Ilala wakishinikiza tamko la serikali kuhusiana na madai yao.

Walisema hawatamsikiliza kiongozi yoyote wala makamanda wa polisi wa wilaya na mikoa isipokuwa wanataka tamko hilo litolewe na Waziri Mkuu, Waziri wa Sheria na Katiba,Waziri wa Usalama wa Raia au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mjini Arusha, maafisa wa juu wa mahakama mkoa wa Arusha, wakiongozwa na Jaji mfawidhi na mahakimu na maafisa wa polisi jana, walikwenda kukutana na mahabusu waliopo katika gereza kuu la Mkoa wa Arusha ili kupata ufumbuzi kwa mgomo wao uliongia siku ya pili.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Matei Basilio, alithibitisha mahabusu hao kutokufikishwa
mahakamani jana na viongozi hao kuwafuata kuzungumza nao.

"Ni kweli leo mahabusu hawajafikishwa mahakamani, lakini kuna kikao cha kupata ufumbuzi kinachoendelea huko magereza kikiongozwa na Jaji Bwano mimi sikwenda ila maafisa wangu wapo huko,"alisema Kamanda Basilio bila kutaja kilichokubaliwa.

Mjini Dodoma nako iliripotiwa jana kuwa mahabusu waliopelekwa katika mahakama za Mwanzo, Wilaya na ile ya Hakimu Mkazi, nao waligoma kuteremka katika karandinga na kurejeshwa Gerezani la Isanga.

nb ,hii ndio ile hadithi ya kila siku fisi alipokuwa ana fuatia mkono wa binadamu akifikiri unakaribia kuanguka.wacha tuishi kwa matumaini
 
Huyu bwana Manumba kweli anatufanya watanzania wote ni wajinga; haishangazi kusikia kuwa Rasi Kikwete naye anaamini kuwa watanzania wote ni wajinga kiasi kuwa anatuombea wataalam toka Nrway.

Maelezo ya Bwana Kanumba kuhusu kuharakishwa kwa kesi ya Mheshimiwa Ditopile kweli hayana msingi wowote. Tukubali tu kuwa judicial system yetu inapendelea wenye uwezo fulani katika jamii kuliko raia wa kawaida, siyo impartial kama inavyotakiwa iwe. Kuna mahabusu kadhaa ambao walishikwa red-handed wakati wakifanya uhalifu wao lakini bado upelelezi wa kesi zao huchukua muda mrefu unaofikia mwaka au zaidi. Upelelezi wa kesi za wale jamaa waliomuua Imran Kombe ulichukua karibu mwaka mzima ingawa nao walijisalimisha na kusema walidhani kuwa Kombe alikuwa ni jambazi. Siku za nyuma kidogo niliwahi kutoa mfano wa Bwana Mwamwindi aliyemuua Dr. Kreluu na kuupeleka mwili wa victim moja kwa moja hadi kwenye kitu cha polisi ambako apofika akawekwa ndani. Huyu bwana alikaa ndani kwa miaka ipatayo mitatu na hatimaye akayongwa chini chini.
 
inasikitisha viongozi wetu wanavyotufanya sisi ni watoto. Kanumba anasema si kweli kesi ya dito imeharakishwa kwa kuwa ni maarufu. Anafikiri fikra za watanzania ni ndooooogo sana?? waandishi walikuwepo sana nafikiri hawakupewa nafasi ya kuuliza maswali.

Napenda kumuuliza bwn Kulikoni; Hatua gani zinachukuliwa dhidi ya ndugu za Dito ambao walisikika hadharani kweupeee wakisema,"nchi hii ya wakubwa, mlifikiri atasota mahabusu eeh au hamjui huyu ni best wa rais, waandishi mtaandika mpaka kalamu ziishe wino???"

Hizi zilikuwa ni insult kwa mahakama. Na mapolisi walikuwa pale vipi wasiwatie nguvuni?

pili; Kwa uelewa wangu kesi ya kuua, husikilizwa pande zote i.e mashahidi woooote hutoa shahidi zao na siku ya mwisho ya hukumu jaji kwa kuzingatia ushahidi na mazingira yote tangu awali ndio anasema, Kutokana na ushahidi mtuhumiwa anapatikana na hatia ya kuua bila kukusudia. Lakini tangu nizaliwe sijawahi kusikia kuwa original case ni MAUAJI halafu kabla ya mashahidi wote kusikilizwa, kesi hiyo hiyo inabadilishwa????? hapa naomba kulikoni anipe ufafanuzi.

tunaambiwa kuwa mshtakiwa ametoa ushirikiano kwa kujisalimisha. Well and Good. Pia akajiuzulu mwenyewe? hili hatulipigii kelele ila mazingira yote ya uendeshaji yanaleta wasiwasi.
Kulikoni watanzania hawashabikii tu pasi na sababu ni serikali yenyewe imeweka mazingira ya kuficha ficha mambo. na ndio tunakumbuka ule msemo bubu ukimchonoa sana husema................na ndio hayo yanayotokea hivi.
 
Manumba is the most corrupt person who care less about human life , the man who supports brutality , and all evils that you know . I have once dealt with him.Man the guy is kichaka hana muda nashangaa kaupataje u DCI .
 
As a government official there is only so much I am qualified to answer before overstepping the separation of powers.

Baadhi ya maswali uliouliza Mwanasiasa,mkjj na wengineo yanajibika vizuri iwapo mtampata jaji au member of judiciary awaelezeee.

I am curious to find out anyone who has been held for more than six yrs kwa kesi ya kuiba kuku kwa vile hii itamaanisha kwamba kamati tuliyounda ya CASE FLOW MANAGEMENT haipo perfect, it will help kama wadau humu mtatusaidia kwa details. Sometimes arguments zenu zinajibika na kueleweka kwa mifano.

Ila mkumbuke kama mtu ameshtakiwa kwa kuua kwa kukusudia [murder charge] basi itakuwa ni rumande tu whether amegoma au la atachezea mahabusu mpaka kesi/ushahidi ukamilike hata kama ni miaka kadhaa....hii ni the same ulimwenguni kote. Nionesheni mfano wa nchi ambayo ukiua kwa makusudi unapata dhamana....

Nadhani nikipata muda nitakuja kuweka hapa the current roles za DPP,MWANASHERIA MKUU MAJAJI, WIZARA YA SHERIA KWA UJUMLA NA SEKTA YA JUDICIARY itaweka mambo katika proper context na mtaelewa arguments za mtikila [ON DPP] na udhaifu wake....
 
As a government official there is only so much I am qualified to answer before overstepping the separation of powers.
...
Ila mkumbuke kama mtu ameshtakiwa kwa kuua kwa kukusudia [murder charge] basi itakuwa ni rumande tu whether amegoma au la atachezea mahabusu mpaka kesi/ushahidi ukamilike hata kama ni miaka kadhaa....hii ni the same ulimwenguni kote. Nionesheni mfano wa nchi ambayo ukiua kwa makusudi unapata dhamana....
....

Ningependa kujibu hili Kulikoni... kuna "kauwezekano" gani kwa hawa wengine ambao wamesota rumande kwa kuua kwa kukusudia kubadilishiwa mashtaka na kuyafanya yawe ya "kutokukusudia" ili na wenyewe nao wapate dhamana? Vigezo vilivyotumiwa na DPP kubadilisha mashtaka ya awali ya dhidi ya Dito na kufanya yawe ya "kutokukusudia" twaweza kuambiwa ni vipi na kuona kama vyaweza kutumiwa kwa washitakiwa wengine? Ni mara ngapi huko nyuma DPP alibadilisha mashtaka ya mauaji kuwa ya kutokukusudia? na mashtaka hayo yalimhusu mtu wa pori kama mimi....

Kwa maneno yako hapo umejenga hoja wazi ya kwanini mashtaka yalibadilishwa!!!!
 
MKJJ

Wasiliana na ofisi ya DPP, kwani huu uoga wa nini si unyanyue tu simu piga omba maelezo nk

Huu ni utawala wa uwazi na ukweli as we are committed to good governance you have right to access the information.

Mpigie Bwana Kaduri akupe maelezo unayotaka..

as to your accusation, mh mh nahene lolo kalagabaho!
 
As a government official there is only so much I am qualified to answer before overstepping the separation of powers.

Baadhi ya maswali uliouliza Mwanasiasa,mkjj na wengineo yanajibika vizuri iwapo mtampata jaji au member of judiciary awaelezeee.

I am curious to find out anyone who has been held for more than six yrs kwa kesi ya kuiba kuku kwa vile hii itamaanisha kwamba kamati tuliyounda ya CASE FLOW MANAGEMENT haipo perfect, it will help kama wadau humu mtatusaidia kwa details. Sometimes arguments zenu zinajibika na kueleweka kwa mifano.

Ila mkumbuke kama mtu ameshtakiwa kwa kuua kwa kukusudia [murder charge] basi itakuwa ni rumande tu whether amegoma au la atachezea mahabusu mpaka kesi/ushahidi ukamilike hata kama ni miaka kadhaa....hii ni the same ulimwenguni kote. Nionesheni mfano wa nchi ambayo ukiua kwa makusudi unapata dhamana....

Nadhani nikipata muda nitakuja kuweka hapa the current roles za DPP,MWANASHERIA MKUU MAJAJI, WIZARA YA SHERIA KWA UJUMLA NA SEKTA YA JUDICIARY itaweka mambo katika proper context na mtaelewa arguments za mtikila [ON DPP] na udhaifu wake....

Kwanza labda utuletee mifano ya watu wote waliowahi kutuhumiwa kuua halafu DPP akawafungulia kesi za kuua bila kukusudia hata kabla kesi zenyewe hazijaanza kusikilizwa mahakamani; nina hamu sana na mfano wa namna hiyo kwa sababu sijawahi kusikia mtu aliyetuhumiwa kuua akishitakiwa outright kwa kuua bila kukusudia. Ninafahamu kuwa mojawapo ya mbinu za kushitaki ni kujenga kesi kwa kupitia vipengele kadhaa vya sheria ili kusudi kipengele kimoja kikishindwa basi kingine kifanye kazi; ukishajiondolea alternatives za kisheria unakuwa unafanya kesi yako kuwa dhaifu, jambo ambalo ndilo DPP alilofanya labda kwa makusudi ili kudhoofisha kesi hii.
 
Mfanyabiashara akabiliwa na kesi ya mauaji
Na Mwandishi Wetu, Moshi

MKURUGENZI wa kampuni ya wakala wa utalii ya Akaro Tours, Renalda Akaro (30), ambaye wiki iliyopita alifikishwa kortini kwa kumpiga mfanyakazi wake,
sasa atakabiliwa na mashitaka ya mauaji.

Kubadilishwa huko kwa mashitaka kunatokana na mfanyakazi huyo,
Gabriel Amani, kufariki dunia juzi saa 7.00 mchana katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC alikopelekwa kwa matibabu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'hoboko, jana alilithibitishia Mwananchi kuwa mashitaka dhidi ya mwanamke huyo mashuhuri
mjini hapa, sasa yatabadilika na kuwa mauaji ya kukusudia.

Mwanamke huyo kwa sasa yuko mahabusu katika gereza kuu la Karanga mjini hapa, baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi, chini ya Hakimu Phares Mlay,
kukataa ombi la dhamana kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo mfanyakazi
huyo.

Suala zima la kipigo hicho awali lilifanywa ni siri na kijana huyo wa Kimasai alilazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi na kupatiwa
matibabu bila ya kuwa na fomu namba 3 (PF 3) kutoka polisi.

Marehemu alilazwa katika hospitali hiyo kuanzia Machi 7 hadi Machi 14 lakini hali yake ilibadilika na kuzidiwa na wauguzi wa Mawenzi wakakimbilia Polisi na kufichua kipigo hicho.

Baadaye polisi walitoa PF 3 na marehemu akakimbizwa Hospitali ya KCMC na wakati huo huo polisi wakimtia mbaroni Akaro. Kijana huyo alifariki
dunia juzi wakati madaktari wakijitahidi kuokoa maisha yake.

"Hakuna ubishi kwamba mashitaka hayo yatabadilishwa na kuwa ya mauaji," alisema Kamanda Ng'hoboko na kuongeza kuwa mashitaka hayo yatabadilishwa
wakati wowote baada ya taratibu za kisheria kukamilika.

Wiki iliyopita alipofikishwa kortini, mkurugenzi huyo wa Akaro Tours alisomewa shitaka la kumshambulia marehemu kwa kumpiga na fimbo kichwani
na sehemu mbalimbali za mwili wake.

Mwendesha Mashitaka, Inspekta Msaidizi Constantine, alidai
mtuhumiwa alitenda kosa hilo Machi 7 saa 12.00 jioni katika eneo la Soweto mjini hapa.

Mtuhumiwa alikana mashitaka hayo na kurudishwa rumande baada ya mwendesha mashitaka kupinga ombi la dhamana akisema kuwa hali ya mlalamikaji
ilikuwa ni mbaya,ombi lililokubaliwa na mahakama

nb kulikuwa na ile kesi ya dereva na konda wa daladalakule arusha ambayo wanatuhumiwa kumuua abiria sijui imefikia wapi,mwenye taarifa atujulishe
 
Mfanyabiashara akabiliwa na kesi ya mauaji
Na Mwandishi Wetu, Moshi

MKURUGENZI wa kampuni ya wakala wa utalii ya Akaro Tours, Renalda Akaro (30), ambaye wiki iliyopita alifikishwa kortini kwa kumpiga mfanyakazi wake,
sasa atakabiliwa na mashitaka ya mauaji.

Kubadilishwa huko kwa mashitaka kunatokana na mfanyakazi huyo,
Gabriel Amani, kufariki dunia juzi saa 7.00 mchana katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC alikopelekwa kwa matibabu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'hoboko, jana alilithibitishia Mwananchi kuwa mashitaka dhidi ya mwanamke huyo mashuhuri
mjini hapa, sasa yatabadilika na kuwa mauaji ya kukusudia.

Mwanamke huyo kwa sasa yuko mahabusu katika gereza kuu la Karanga mjini hapa, baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi, chini ya Hakimu Phares Mlay,
kukataa ombi la dhamana kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo mfanyakazi
huyo.

Suala zima la kipigo hicho awali lilifanywa ni siri na kijana huyo wa Kimasai alilazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi na kupatiwa
matibabu bila ya kuwa na fomu namba 3 (PF 3) kutoka polisi.

Marehemu alilazwa katika hospitali hiyo kuanzia Machi 7 hadi Machi 14 lakini hali yake ilibadilika na kuzidiwa na wauguzi wa Mawenzi wakakimbilia Polisi na kufichua kipigo hicho.

Baadaye polisi walitoa PF 3 na marehemu akakimbizwa Hospitali ya KCMC na wakati huo huo polisi wakimtia mbaroni Akaro. Kijana huyo alifariki
dunia juzi wakati madaktari wakijitahidi kuokoa maisha yake.

"Hakuna ubishi kwamba mashitaka hayo yatabadilishwa na kuwa ya mauaji," alisema Kamanda Ng'hoboko na kuongeza kuwa mashitaka hayo yatabadilishwa
wakati wowote baada ya taratibu za kisheria kukamilika.

Wiki iliyopita alipofikishwa kortini, mkurugenzi huyo wa Akaro Tours alisomewa shitaka la kumshambulia marehemu kwa kumpiga na fimbo kichwani
na sehemu mbalimbali za mwili wake.

Mwendesha Mashitaka, Inspekta Msaidizi Constantine, alidai
mtuhumiwa alitenda kosa hilo Machi 7 saa 12.00 jioni katika eneo la Soweto mjini hapa.

Mtuhumiwa alikana mashitaka hayo na kurudishwa rumande baada ya mwendesha mashitaka kupinga ombi la dhamana akisema kuwa hali ya mlalamikaji
ilikuwa ni mbaya,ombi lililokubaliwa na mahakama

nb kulikuwa na ile kesi ya dereva na konda wa daladalakule arusha ambayo wanatuhumiwa kumuua abiria sijui imefikia wapi,mwenye taarifa atujulishe


Hii hapa kweli ni kuua bila kukusidia. wakati marahemu anapigwa kwa fimbo, hakuwa anategemewa kufa. Hii ni tofauti na kumfyatulia mtu risasi halafu unasema hukuwa umemkusuida kumwua.
 
Tanzania ya magumu mengi inawezekana nalo tukasikia vinginevyo kunwa wakili Mwale hapo Arusha ni hodari naye abadilishe tuone ama ni kwa Ditto pekee ?
 
kichuguu,
nafikiri ujaisoma vizuri hii sentensi ya rpc l.nghoboko,amesema kuwa mashitaka sasa yatakuwa ya kuua kwa kukusudia.
 
Tanzania ya magumu mengi inawezekana nalo tukasikia vinginevyo kunwa wakili Mwale hapo Arusha ni hodari naye abadilishe tuone ama ni kwa Ditto pekee ?

Huyo wakili ni cha mtoto,Aweze wapi ?huoni katika utetezi wake hivi karibuni serikali walidai Kesi ya Ditto imeenda haraka kwasababu ya kuwa na mawakili wenye sifa.(Na hicho ndiyo walichomkokotea Nimrod Mkono pia, ili waje waongope baadae kama walivyofanya).Wasichokielewa watu waliliona kabla ya wao kutamka,waliyoyafanya ni marudio.
 
Nakukubali mkubwa mawazo yako . Tuliyasema haya ila Nimrod nitakutana naye Jimboni kwake nitamuuliza kulikoni katetea tajiri na kumwacha Mlalahoi analala kaburini na yeye akiwa Mbunge wa walala hoi kama anavyo jiita ?
 
Hii hapa kweli ni kuua bila kukusidia. wakati marahemu anapigwa kwa fimbo, hakuwa anategemewa kufa. Hii ni tofauti na kumfyatulia mtu risasi halafu unasema hukuwa umemkusuida kumwua.
Hakutegemea kufa na ilimchukua wiki mbili kufariki,Tukilitizama hivi basi kweli aliua bila ya kukusudia.Lakini maswali ya kisheria, alimpiga fimbo mara moja tu au laah?Alirudia tendo la kumpiga mara kadhaa au laah?Aliyekuwa anampiga marehemu ana akili timamu au laah?Je alijua au hapana kwamba kipigo kinaleta madhara?Alimpiga sehemu gani ya mwili? Je alijiandaa kutoa kipigo hicho kwa marehemu au laah?(yaani kulikuwa na kukamia ngoja huyu akirudi leo atanitambuan.k) Kulikuwa na provacation yeyote toka kwa marehemu iliyopelekea mhusika kumpiga marehemu...................!
 
Tukijibu maswali hayo machache hapo tutaelewa kama aliua kwa kusudia au hapana,Lakini haya yote tukiyasubiri kujibiwa bado mtuhumiwa atakuwa na kosa la kuua (mpaka baada ya miezi miwili au mitatu litakaporudi toka kwa DPP na kufutiwa shitaka la kuua kwa kukusudia na kuwa la kuua bila ya kukusudia). Hili mnalionaje? Tusubiri na msisahau na huyu ni mfanyabiashara...............Kama kweli.........Ila kama Mchuuzi....na amejiita mfanyabiashara ana kesi ya ziada....eh!
 
Kwa kweli mtu kama Kulikoni anapotetea uozo kama huu watu tunajiuliza mengi!Kulikoni.Askari wa Tanzania hasa wanaohusika na upelelezi hawafanyi kazi, wao wanapompeleka mtuhumiwa rumande humaliza kesi na huwa hawafanyi upelelezi hata kidogo.Kwa kesi ya Doto imekuwa tofauti kwa kuwa imepata msukumo toka juu.
 
Back
Top Bottom