Mlenda wa unga unatokana na majani gani na yanapatikana wapi?

Mlenda wa unga unatokana na majani gani na yanapatikana wapi?

Kwa jinsi ninavyoupenda Mlenda, kuna Mwaka nilisafiri nje nililazimika kuubeba kwenda nao

Ni mboga ya faster, unachemsha Maji kisha unauweka baada ya kuweka chumvi

Unaweza kuongeza Ladha kwa kuunga na Karanga za kusagwa.
 
Asee hii nchi kweli ni kubwa...
Maana ya mlenda ni KITU chochote kinachoteleza... (Utajua mwenyewe)
Nilivyomwelewa mtoa mada faster nilijua anazungumzia mboga maarufu kwa sisi wenyeji wa Iringa na Njombe, maarufu kama MKUNUNGU...
Hii mboga haichanganywi chochote wakati wa kuandaa, na ni mboga pori, inaota kama vichaka kwenye udongo wa mfinyanzi, mashina yake Hadi majani Yana miba, haikui kuwa miti mikubwa sana hapana. Ni kama ilivyo mimea ya ndula.
Majani yake yakiwa mabichi Yana aroma kama ya Limau hivi, na haiandaliwi Toka kwenye majani mabichi, isipokuwa yaliyokaushwa kwenye kivuli na kusagwa. UNGA wake hubaki na ule ukijani wake wa ASILI.
MBOGA HII HAICHAGUI MAPISHI WALA KIUNGO... NA INA MATCH NA KILA CHAKULA, AROMA YAKE YA CITRUS IKIWA NI APPETIZER MUJARABU KABISA.
-kamwene mbemuli-
 
Wana singida na dodoma...
Wanaita irende au nswalu kwa wanyamwezi,
Majani yake ni kama majani ya mmea wa ufuta...
Yaaani kama unavyouona mmea wa ufuta na huo mlenda uko hivyo hivyo unafanana 90%
Cha kufanya kama ukiuona chuma majani yake uloweke kwenye maji...utaona yana toa mlenda mwingi na mzito ukiushika tofauti na majani ya mmea wa ufuta.
Hayo majani membamba ndo huanikwa yakikauka yana sagwa au kutwangwa na kutoa poda line tyr kwa matumizi ya mboga.
Ni tamaduni za ukanda wa kati wao wanategemea mvua ya msimu wa masika tu kwa hivuo mboga mbichi hupatikana kwa wingi kipindi cha mvua kwa hivyo ili kuhifadhi mboga kwa msimu wa kiangazi.
Walikuwa wana kausha mboga mbali mbali ikiwemo
huo mlenda,majani ya kunde(nyafwe/safwe)Chipali,Chiwandagulu,mitanda( nyama)nk
bila kusahau nyanya mshenzi na matango n.k pia nayo yalikuwa yanakaushwa juani na kuhifadhiwa.
Ukanda Juu kusini na mikoa ya Pwani hawajui mambo hayo kwa sabb wao wanapata misimu miwili ya mvua..
Kwaivyo mbogamboga na viungo fresh hawaishiwi kabisa.
Kumbuka si hivyo tu mpk viazi vitamu humenywa na kuanikwa kwaajili ya kuhifadhi kwa matumizi ya kiangazi.
Huitwa Michembe,yakichemshwa na kuanikwa yanaitwa matoolwa(matoborwa)
Ni matunda pekee sijawahi ona yaliyohifadhiwa kwa kuanikwa kama yapo watasema wakongwe.
 
Wana singida na dodoma...
Wanaita irende au nswalu kwa wanyamwezi,
Majani yake ni kama majani ya mmea wa ufuta...
Yaaani kama unavyouona mmea wa ufuta na huo mlenda uko hivyo hivyo unafanana 90%
Cha kufanya kama ukiuona chuma majani yake uloweke kwenye maji...utaona yana toa mlenda mwingi na mzito ukiushika tofauti na majani ya mmea wa ufuta.
Hayo majani membamba ndo huanikwa yakikauka yana sagwa au kutwangwa na kutoa poda line tyr kwa matumizi ya mboga.
Ni tamaduni za ukanda wa kati wao wanategemea mvua ya msimu wa masika tu kwa hivuo mboga mbichi hupatikana kwa wingi kipindi cha mvua kwa hivyo ili kuhifadhi mboga kwa msimu wa kiangazi.
Walikuwa wana kausha mboga mbali mbali ikiwemo
huo mlenda,majani ya kunde(nyafwe/safwe)Chipali,Chiwandagulu,mitanda( nyama)nk
bila kusahau nyanya mshenzi na matango n.k pia nayo yalikuwa yanakaushwa juani na kuhifadhiwa.
Ukanda Juu kusini na mikoa ya Pwani hawajui mambo hayo kwa sabb wao wanapata misimu miwili ya mvua..
Kwaivyo mbogamboga na viungo fresh hawaishiwi kabisa.
Kumbuka si hivyo tu mpk viazi vitamu humenywa na kuanikwa kwaajili ya kuhifadhi kwa matumizi ya kiangazi.
Huitwa Michembe,yakichemshwa na kuanikwa yanaitwa matoolwa(matoborwa)
Ni matunda pekee sijawahi ona yaliyohifadhiwa kwa kuanikwa kama yapo watasema wakongwe.
😂😂😂😂😂 Wewe ni mgogo kabisa eti irende,safwe,chipali,chiwandagulu,nyamhuzha,nyapembe.
 
Niliukuta Mombo cku nikwa naenda kaskazini,uliweka maharage meupe sijui yanaitwaje lakini ni meupe nilikula samaki na huo mlenda duh ulikua mtamu sana,mjini yale maharage sijawahi yaona
Mlenda na maharage mixer au sijaelewa.
 
Kuna ule mlenda huwa unapikwa kutokana na majani fulani yanayosagwa kama unga, unaitwa mlenda wa unga.
Haya majani yanayotengeneza huu mlenda wa unga yanapatikana wapi?
Yanauzwa sokoni kama mboga ?
Unaweza kuyapikia mlenda yakiwa mabichi(hayajakauka) kama mboga nyingine za majani?
Hawa wachina watatuua....mlenda wa unga?
 
Wana singida na dodoma...
Wanaita irende au nswalu kwa wanyamwezi,
Majani yake ni kama majani ya mmea wa ufuta...
Yaaani kama unavyouona mmea wa ufuta na huo mlenda uko hivyo hivyo unafanana 90%
Cha kufanya kama ukiuona chuma majani yake uloweke kwenye maji...utaona yana toa mlenda mwingi na mzito ukiushika tofauti na majani ya mmea wa ufuta.
Hayo majani membamba ndo huanikwa yakikauka yana sagwa au kutwangwa na kutoa poda line tyr kwa matumizi ya mboga.
Ni tamaduni za ukanda wa kati wao wanategemea mvua ya msimu wa masika tu kwa hivuo mboga mbichi hupatikana kwa wingi kipindi cha mvua kwa hivyo ili kuhifadhi mboga kwa msimu wa kiangazi.
Walikuwa wana kausha mboga mbali mbali ikiwemo
huo mlenda,majani ya kunde(nyafwe/safwe)Chipali,Chiwandagulu,mitanda( nyama)nk
bila kusahau nyanya mshenzi na matango n.k pia nayo yalikuwa yanakaushwa juani na kuhifadhiwa.
Ukanda Juu kusini na mikoa ya Pwani hawajui mambo hayo kwa sabb wao wanapata misimu miwili ya mvua..
Kwaivyo mbogamboga na viungo fresh hawaishiwi kabisa.
Kumbuka si hivyo tu mpk viazi vitamu humenywa na kuanikwa kwaajili ya kuhifadhi kwa matumizi ya kiangazi.
Huitwa Michembe,yakichemshwa na kuanikwa yanaitwa matoolwa(matoborwa)
Ni matunda pekee sijawahi ona yaliyohifadhiwa kwa kuanikwa kama yapo watasema wakongwe.
Nyanya mshenzi ndo zile ndogo? Ila umeongea ukweli mtupu. Mihogo-makopa, pilipili, uyoga, nyanya na ngogwe zote hukaushwa.
 
Kuna ule mlenda huwa unapikwa kutokana na majani fulani yanayosagwa kama unga, unaitwa mlenda wa unga.
Haya majani yanayotengeneza huu mlenda wa unga yanapatikana wapi?
Yanauzwa sokoni kama mboga ?
Unaweza kuyapikia mlenda yakiwa mabichi(hayajakauka) kama mboga nyingine za majani?
Maswali YOTE jibu NI Ndiyo.
Yanapatikana Kwa wingi DODOMA.
 
Back
Top Bottom