Mlenda wa unga unatokana na majani gani na yanapatikana wapi?

Mlenda wa unga unatokana na majani gani na yanapatikana wapi?

ndio ni majani ya maboga a.k.a msusa na yakifanywa hivyo unavyosema huitwa nswalu, pia huweza kupikwa yakiwa mabichi ila ili uwe mlenda lazima uweke bamia!.
Kuna mlenda na kuna bamia ,mlenda OG hautokani na majani ya maboga
 
Wana singida na dodoma...
Wanaita irende au nswalu kwa wanyamwezi,
Majani yake ni kama majani ya mmea wa ufuta...
Yaaani kama unavyouona mmea wa ufuta na huo mlenda uko hivyo hivyo unafanana 90%
Cha kufanya kama ukiuona chuma majani yake uloweke kwenye maji...utaona yana toa mlenda mwingi na mzito ukiushika tofauti na majani ya mmea wa ufuta.
Hayo majani membamba ndo huanikwa yakikauka yana sagwa au kutwangwa na kutoa poda line tyr kwa matumizi ya mboga.
Ni tamaduni za ukanda wa kati wao wanategemea mvua ya msimu wa masika tu kwa hivuo mboga mbichi hupatikana kwa wingi kipindi cha mvua kwa hivyo ili kuhifadhi mboga kwa msimu wa kiangazi.
Walikuwa wana kausha mboga mbali mbali ikiwemo
huo mlenda,majani ya kunde(nyafwe/safwe)Chipali,Chiwandagulu,mitanda( nyama)nk
bila kusahau nyanya mshenzi na matango n.k pia nayo yalikuwa yanakaushwa juani na kuhifadhiwa.
Ukanda Juu kusini na mikoa ya Pwani hawajui mambo hayo kwa sabb wao wanapata misimu miwili ya mvua..
Kwaivyo mbogamboga na viungo fresh hawaishiwi kabisa.
Kumbuka si hivyo tu mpk viazi vitamu humenywa na kuanikwa kwaajili ya kuhifadhi kwa matumizi ya kiangazi.
Huitwa Michembe,yakichemshwa na kuanikwa yanaitwa matoolwa(matoborwa)
Ni matunda pekee sijawahi ona yaliyohifadhiwa kwa kuanikwa kama yapo watasema wakongwe.
Asante mkuu,nimekuwa interested na matango,yanahifadhiwaje?
Hiyo michembe niliwahi kuila Mwanza
 
1735760523999.jpeg
 
Asante mkuu,nimekuwa interested na matango,yanahifadhiwaje?
Hiyo michembe niliwahi kuila Mwanza
Matango hasa ya kienyeji,yalikuwa yanamenywa na kukatwa vipande vipande kama vya kachumbali ila size itategemeana na mkataji.
vipande hivyo viliwekwa juani takribani siku 14 au chini ya hapo,baada ya hapo vitasinyaa.
Tyr kuhifadhiwa store ya vyakula.
Wkt wowote mwaka mzima utakapohitaji kutumia vipande vilitumika kama vile mpishi anavyoongeza vipande vya karoti,au hoho kwenye mboga ndivyo vipande vya tango viliwekwa kwenye mboga (tofauti na mlenda mfano nyama n.k)Wkt ikiandaliwa jikoni.

Kwenye kukausha hakukuishia hapo tu member mmoja akasema pia mihogo-makopa, pilipili, uyoga, nyanya na ngogwe zote hukaushwa.
Binafsi nimejionea Nyanya pia,pilipili&uyoga n.k
Karibu
 
Kuna ule mlenda huwa unapikwa kutokana na majani fulani yanayosagwa kama unga, unaitwa mlenda wa unga.
Haya majani yanayotengeneza huu mlenda wa unga yanapatikana wapi?
Yanauzwa sokoni kama mboga ?
Unaweza kuyapikia mlenda yakiwa mabichi(hayajakauka) kama mboga nyingine za majani?
Ule unga unaitwa mwage, waluguru ndio mboga zao
 
Unatokana na majani ya matango asili au mihogo.

Majani huwa yanachumwa mabichi yanakaushwa kwa jua kisha yanahifadhiwa kwa matumizi.

Pishi lake lazima lichanganywe na karanga kuleta ladha na uzito.

Kwa majani ya matango yanaweza kutengeneza mlenda yakiwa mabichi kwa kuchanganya na bamia au mlenda pori wasukuma wanaita twege, makonda au bhunani.
Duh, mkuu na wewe ni wa kwetu nini?
 
Kumbe hata huo wa unga huwa wanachanganya na majani ya maboga!
Hayo majani yako yenyewe tu.watu naona wanachanganya na mlenda wa bamia na majani ya maboga.Hayo uliyouliza ni majani ya size ya kati unayakausha unasaga.Ukitaka kupika unachemsha maji kidogo unachotea huo unga unakoroga. ukitafuna mabichi au kuyaloweka yana ukakasi na yanatoa uji mzito rangi ya maji unaovutika.sijawai kuyala mabichi ila nayafahamu vizuri.Kijijin tulikua tunayachuma vichakani sio kuyanunua sokoni.
 
ndio ni majani ya maboga a.k.a msusa na yakifanywa hivyo unavyosema huitwa nswalu, pia huweza kupikwa yakiwa mabichi ila ili uwe mlenda lazima uweke bamia!.
hujamwelewa mkuu ,kuna mmea flani unakaushwa then unasagwa sasa ule unga unaweka kwenye chungu chenye maji ya uvuguvugu jikoni then unaupekecha na mwiko na kuwa mlenda though unaweza kuchanganywa na majani ya maboga ila kwa kukaushwa sio ukiwa mbichi,bahati mbaya sina picha ya huo mmea
 
kuna ule unatokana na majani pori yana miba ,yanakaushwa kwa jua baada ya hapo unatwangwa kwa kinu au kusagwa mashineni unakuwa unga wa kijani , kwa watu wamkoa wa Kilimanjaro wanauita msele.
 
Matango hasa ya kienyeji,yalikuwa yanamenywa na kukatwa vipande vipande kama vya kachumbali ila size itategemeana na mkataji.
vipande hivyo viliwekwa juani takribani siku 14 au chini ya hapo,baada ya hapo vitasinyaa.
Tyr kuhifadhiwa store ya vyakula.
Wkt wowote mwaka mzima utakapohitaji kutumia vipande vilitumika kama vile mpishi anavyoongeza vipande vya karoti,au hoho kwenye mboga ndivyo vipande vya tango viliwekwa kwenye mboga (tofauti na mlenda mfano nyama n.k)Wkt ikiandaliwa jikoni.

Kwenye kukausha hakukuishia hapo tu member mmoja akasema pia mihogo-makopa, pilipili, uyoga, nyanya na ngogwe zote hukaushwa.
Binafsi nimejionea Nyanya pia,pilipili&uyoga n.k
Karibu
Asante Sana mkuu,nimepata somo hapo,kweli tunajifunza kila leo
 
  • Thanks
Reactions: 1gb
ndio ni majani ya maboga a.k.a msusa na yakifanywa hivyo unavyosema huitwa nswalu, pia huweza kupikwa yakiwa mabichi ila ili uwe mlenda lazima uweke bamia!.
Hahaha aisee kazi kwelikweli
 
Back
Top Bottom