Mlevi aua Wanafunzi Watatu wa UDOM, Mama mjamzito na bodaboda wawili Dodoma

Nsoji go Nvaa

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2019
Posts
999
Reaction score
1,948
Mlevi mmoja akiendesha gari huku amelewa amewagonga na kuwaua Wanafunzi wa Tatu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Mama mjamzito na boda boda wawili maeneo ya Makulu opposite na ofisi za TISS na makutano ya Shoppers mkoani Dodoma, baada ya ajali wananchi nao walimshikisha adabu kidogo kwa kumpa kipondo kizito na kuharibu vibaya gari lake.


=================

Watu wawili inasemekana wamefariki dunia na wengine 10 wamejeruhiwa Jijini Dodoma, baada ya kugongwa mfululizo na gari aina ya RAVA 4 lenye namba za usajili T156 EJJ.

Dereva wa gari hilo anadaiwa kuanza kuwagonga watu hao kuanzia eneo la Makulu Majumba Sita mpaka Makulu Darajani majira ya saa mbili usiku wa Novemba 03, 2024.

Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema chanzo chake ni uzembe wa dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo huku akidaiwa amelewa.

Chanzo: TBC
 
RIP to Those who have lost their lives. Mwisho wa mwaka huu.
 
Asubh hii au usiku?
 
Kiongozi akiwa mbovu kila kitu huwa kinaharibika! Saizi maajali ya kizembe kama haya ni kawaida sheria hazina makali hamna wakuwafanya chochote.
 
Angeuawa na yeye kwa sababu vifo alivyosababisha ni mauaji ya makusudi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…