Mlio Hamia nyumba zenu mpya, Majirani zenu Shwari au Vita?

Mlio Hamia nyumba zenu mpya, Majirani zenu Shwari au Vita?

Mimi alikuwa jamaa anahamia nyumba yake mitaa niliyopanga, sasa kufika mpaka lilipo geti lake kuna nyumba ipo barabarani na hio barabara ni ya huyo jamaa aliitoa tu watu wapite.
Siku ya kwanza ikapita kimya, after a week mke wa yule jamaa akamuambia mume wake, huyu mwanajeshi anapitisha gari lake.

Basi kesho asubuhi akamsubiri apite, alivyopita tu akamsimamisha akamwambia naomba hii njia ife sababu ni sehemu yangu halafu anaongea kwa nguvu. Yule mwanajeshi akasema haina shida ndugu alimjibu very humble.

Baada ya kama wiki kazaa yule mjeshi akamtuma mtu aongee na jamaa, yule mzee akagoma ikabidi mzee amfate kwake, akamwambia ndugu yangu naomba ninunue hii njia. Uwezi amini yule mjeshi alinunua ile njia kwa 2milion.
Na hakukataza mtu.

Baada ya muda yule mzee alikufa sababu alikuwa anakunywa sana pombe wanasema mapafu yalipata shida. Siku anazidiwa usiku wa manane walienda kumuomba usafiri yule mwanajeshi. Bila kinyongo jamaa alitoka usiku kumpeleka hosptali mpaka kwenye msiba jamaa alitoa maturubai yake.

Viumbe vzuri bado vipo duniani.

mmepata bahati kuwa na uyo jirani mjeshi,
 
Jirani yetu zamani alikua bibi mmoja wa kale kabisa.
Pale kwake alikua na ghorofa la wakoloni,si tumejenga hapo nyuma kwake na kuipata barabara lazima upite pale.
Sasa ye na mdingi walikua hawaelewani lugha.
Anampangia mdingi njia ya kupita na usafiri wake.
Mdingi afisa mipango miji yani anamletea mazereu ile kwamba "wewe nani nikitaka hapo kesho hata wewe unaondoka"
Kumbe ilikua sio utani,yule bibi onyo la kwanza,
Mzee kapita nalo palepale,kapiga mzinga mbele,onyo la pili mzee kasahau kapita tena palepale.kala mzinga mjini,onyo la tatu mzee kasahau kapita border yake ile ile kala mzinga kimoja.
Ndo kwaheri mpaka leo.
Cha ajabu mle kwa yule bibi nilikua nakatiza humo ndani sana tu,mapera yake naiba sana tu pale mbele kuna mwembe mkubwa mi naenda nachuma maembe yangu natoka baru mchana kweupe.
Hakunifanya lolote.
Ila kwa mzee ilikua tofauti.
Aise hii kali. kama nimekuelewa mzee kafariki kwa ajali au ni gari tu ilipiga mzinga?
 
Mi kuna mmoja mpemba ........yaani usinunue sehemu jirani yako akawa mpemba kumqmqmke hawa mbwa ni wasumbufu balaaa........mpaka alinuzia njia ndio roho yaake ikatulia na hata hakuchukua muda alifariki kifo kibaya .............ila huyu mpumbavu wacha afe tu .......alitaka kuniua bila sababu kisa ninampita kimaendeleo ........mana niliamia pakiwa pagala baadaya ya miaka kama miwili pakawa paradiso...
...sasa yeye hiko kitu hakukitaka kabisa yaani marehemu asemwi vibaya ila huyu gegedu aongezewe moto tu hamnaa namna alinirushia majini ..........nilikuwa napagawa balaa mara mbavu kama zitachomoka kichwa kinauma kama sio changu.......hata kazini siendi .......ila mwenyezi alijua kunisaidia kwa hili maana jinga lilianguka chooni kwake na kufia uko uko........na walivokuwa wajinga waliliacha huko chooni masaa 10 baada ya kulipereka hospital wakaenda nalo kwa mganga ndio wakaalibu zaidi.........yaani walitoa boko .........ila mbwa yule na mke wake wangeshaniua kama miaka mitatu nyuma sema mungu alipinga mpango wao.......asante yesu kwa uwezo wako nilishinda vita ile.....maana nilikuwa natumia gari mpaka na gari ilikufa kifo kibaya lilihalibika tu bila sababu
Dah. aisee kuna visa havi kwepeki ni Yesu tu aamue.. Embu I magine umejituma kwa jasho lako umejenga kwako jirani anaenda kwa mganga kuku tupia majin?? bora Yesu wako ali muwahi ..safi sana.. Pole pia kwa hicho kisa hatari sana
 
Tupeane Uzoefu wa Tabia za Wenyeji wako, ulizo kutana nazo kwa Jiran yako wa mpakani au mtaa ulio jenga na kuhamia au ulipo nunua kiwanja umepokelewaje? Vipi wenyeji wa pande zote za nyumba au eneo lako? Kuna kosekana wivu na gubu kwa jirana zako? au ndio ile ushazoea husemezani nao? Au umepata wenyeji wema sana?

Kuna Mada nimeziona mitandaon watu wakizungumzia uzoefu wa jinsi ya kuhami makazi mapya na jinsi wenyeji wenye hila walivyo wasumbua, wengine kuugua sana na uchumi kuharibika mazima, wengine kununiwa na wengine kujikuta wanatengwa bila sababu, wengine wana dai uchawi ulikuwa si wakawaida walikaribishwa kwakupimwa uwezo wao kama wana nguvu au lah.

Vipi wewe unauzoefu gani wa kushare na sisi??

Je! nikweli kabla ya kuhamia nyumba mpya anahitajika kiongozi wa kiroho aje kuomba na kama wewe ni wagiza lazima mganga aje kufanya mambo?

Tupeane visa na jinsi ulivyp kabiliana navyo maana kuna watu wanahitaji kujifunza wavuke vikwazo hivyo.. na wengine wametamani hata kuuza nyumba wahame.
Mi nilipo hamia Majilani wakajua mi ni Usalama. Badae nilikaa om wakati wa korona nikawamafanyia kazi nyumbani wakajua nimefukuzwa kazi. Wakafurahi mno. Badae nikatoa sapoti ya kujenga Barabara, wengine wakanuna na wengine wakachekelea. Majilani ni watu wagumu sana kuwaelewa.
 
Mimi alikuwa jamaa anahamia nyumba yake mitaa niliyopanga, sasa kufika mpaka lilipo geti lake kuna nyumba ipo barabarani na hio barabara ni ya huyo jamaa aliitoa tu watu wapite.
Siku ya kwanza ikapita kimya, after a week mke wa yule jamaa akamuambia mume wake, huyu mwanajeshi anapitisha gari lake.

Basi kesho asubuhi akamsubiri apite, alivyopita tu akamsimamisha akamwambia naomba hii njia ife sababu ni sehemu yangu halafu anaongea kwa nguvu. Yule mwanajeshi akasema haina shida ndugu alimjibu very humble.

Baada ya kama wiki kazaa yule mjeshi akamtuma mtu aongee na jamaa, yule mzee akagoma ikabidi mzee amfate kwake, akamwambia ndugu yangu naomba ninunue hii njia. Uwezi amini yule mjeshi alinunua ile njia kwa 2milion.
Na hakukataza mtu.

Baada ya muda yule mzee alikufa sababu alikuwa anakunywa sana pombe wanasema mapafu yalipata shida. Siku anazidiwa usiku wa manane walienda kumuomba usafiri yule mwanajeshi. Bila kinyongo jamaa alitoka usiku kumpeleka hosptali mpaka kwenye msiba jamaa alitoa maturubai yake.

Viumbe vzuri bado vipo duniani.
Bila shaka huyo bi mkubwa kajifunza kitu kama kweli zinachaji
 
Mie dadaangu mpaka leo nyumba yake hajaingia japokuwa ameshaimaliza yote na umeme ameweka sema ndo hvyo alimchukua jirani yake akamweka amlindie.

Mpaka leo kila anachogusa hamna kitu jirani kila akiambiwa mwez ujao ntahamia lazma itokee sababu ndug yang itayomfanya ahairishe leo nazungumzia mwaka wa 15 toka nyumba imalizwe jirani kagoma kutoka
 
Mie dadaangu mpaka leo nyumba yake hajaingia japokuwa ameshaimaliza yote na umeme ameweka sema ndo hvyo alimchukua jirani yake akamweka amlindie.

Mpaka leo kila anachogusa hamna kitu jirani kila akiambiwa mwez ujao ntahamia lazma itokee sababu ndug yang itayomfanya ahairishe leo nazungumzia mwaka wa 15 toka nyumba imalizwe jirani kagoma kutoka
Duh.. hii sasa hatari.. uchawi huo.. dada aende kwenye maombi apeleke Kiongoz wa kiroho haraka maana wana weza muondoa
 
Usiombe Upakane na Mhaya hawa watu wanatabu sana katika mipaka ,Kuna jamaa ni mhaya nimepakana naye aisee tumesumbuana sana mpaka nilipojenga ukuta ,ni watu wabinafsi wachoyo wa mimi na ukiwa legelege kila siku atakuwa anasogeza mpaka ,
Pia hawa wagogo nao sio waelewa kabisaaa ..Ila nilichojifunza ili kuishi kwa amani jitahidi ujenge fensi
 
Usiombe Upakane na Mhaya hawa watu wanatabu sana katika mipaka ,Kuna jamaa ni mhaya nimepakana naye aisee tumesumbuana sana mpaka nilipojenga ukuta ,ni watu wabinafsi wachoyo wa mimi na ukiwa legelege kila siku atakuwa anasogeza mpaka ,
Pia hawa wagogo nao sio waelewa kabisaaa ..Ila nilichojifunza ili kuishi kwa amani jitahidi ujenge fensi
Kweli kabisa!
 
Back
Top Bottom