Mliofanikiwa kwenye Network Marketing tunawaomba mtoe Ushuhuda hapa

Mliofanikiwa kwenye Network Marketing tunawaomba mtoe Ushuhuda hapa

Me nawaza kuanza kuuza maharage kuna mtu anakuja kukwambia biashara za kuwa bilionea ghafla..ingekuwa hivyo kila mtu angekuwa bilionnea...no pain no gain....tujitume hakuna shortcut
 
Wiki 4 zilizopita aliyekuwa classmate wangu alinisumbja sana, alinambia kuna ishu ya investment inaweza kuniingizia mamilion, mimi nikadhan ni true investment, maybe ana project proposal ambayo tunaweza kuingiza pesa tukapata pesa hv

Au maybe kuna kampuni unadhamin mikopo hivi, nikamwuliza ni ishu gani? Akasema haitoshi kuongea kwenye smu maana ni ishu pana.... dah nikatafakari... nikamwuliza, ni forever living? Akasema No, nikamwuliza ni Alliance? Akasena NO... doh.... nikamwambia nidokeze, akasema tuonane....

Sasa kwa kuwa nina miaka sjaonana naye tangu tulivyomaliza chuo, ikanbd niwapigie watu wake wa karibu, mmoja akasema alisikia anafanya kaz kampuni ya mikopo... nikasema oh bas huenda kuna mikopo huku, na kwa kuwa mimi siogopi mikopo na nina shida na pesa za kuingiza kwenye miradi... nikasema ngoja niende..........


Sku imefika, nikachukua usafiri.... fuuuuuuuu mpaka mwege...

Lahaula, kufika kule ananambia hii ishu inaweza kukuingizia had m. 15 kwa mwezi na hata kwa siku

Ishu gani mama???? Q_Net...... mimi lohhhhhh ehz inakuwaje.... oh unanunua bidhA hata moja, unajiunga, na ww unatafuta watu wanajiunga.... aseh, nikafanyiwa semina na watu karibu wanne..... mara kuoneshwa mapicha sjui nini

Dahhhh nilimwangalia classmate wangu nikamhurumia sana, nikawatazama wale vijana wengne wanaosema unapata hata m. 15 kwa wiki, mavazi yao hayafanani hata kidogo, ni watu wanaoonekana bado wanahangaika na kufungwa kifikra......

Sikutaka kuwaudhi, nikawaambia mimi nafanya miradi binafsi.. hata hvyo, nitawasiliana nanyi kesho...... ikawa kimoja

SHIME VIJANA, TUACHE SHORTCUT, PESA ZIPO KAMA TUTAJIINGIZA KTK MIRAD HALISI, KUTHUBUTU PASIPO KUJATA TAMAA. HAKUNA SLOPE KTK KUTAFUTA PESA, TUKUMBUKE MUDA UNAKWENDA

ni heri ukakodi shamba upande mpunga, uvune uuze
 
Wiki 4 zilizopita aliyekuwa classmate wangu alinisumbja sana, alinambia kuna ishu ya investment inaweza kuniingizia mamilion, mimi nikadhan ni true investment, maybe ana project proposal ambayo tunaweza kuingiza pesa tukapata pesa hv

Au maybe kuna kampuni unadhamin mikopo hivi, nikamwuliza ni ishu gani? Akasema haitoshi kuongea kwenye smu maana ni ishu pana.... dah nikatafakari... nikamwuliza, ni forever living? Akasema No, nikamwuliza ni Alliance? Akasena NO... doh.... nikamwambia nidokeze, akasema tuonane....

Sasa kwa kuwa nina miaka sjaonana naye tangu tulivyomaliza chuo, ikanbd niwapigie watu wake wa karibu, mmoja akasema alisikia anafanya kaz kampuni ya mikopo... nikasema oh bas huenda kuna mikopo huku, na kwa kuwa mimi siogopi mikopo na nina shida na pesa za kuingiza kwenye miradi... nikasema ngoja niende..........


Sku imefika, nikachukua usafiri.... fuuuuuuuu mpaka mwege...

Lahaula, kufika kule ananambia hii ishu inaweza kukuingizia had m. 15 kwa mwezi na hata kwa siku

Ishu gani mama???? Q_Net...... mimi lohhhhhh ehz inakuwaje.... oh unanunua bidhA hata moja, unajiunga, na ww unatafuta watu wanajiunga.... aseh, nikafanyiwa semina na watu karibu wanne..... mara kuoneshwa mapicha sjui nini

Dahhhh nilimwangalia classmate wangu nikamhurumia sana, nikawatazama wale vijana wengne wanaosema unapata hata m. 15 kwa wiki, mavazi yao hayafanani hata kidogo, ni watu wanaoonekana bado wanahangaika na kufungwa kifikra......

Sikutaka kuwaudhi, nikawaambia mimi nafanya miradi binafsi.. hata hvyo, nitawasiliana nanyi kesho...... ikawa kimoja

SHIME VIJANA, TUACHE SHORTCUT, PESA ZIPO KAMA TUTAJIINGIZA KTK MIRAD HALISI, KUTHUBUTU PASIPO KUJATA TAMAA. HAKUNA SLOPE KTK KUTAFUTA PESA, TUKUMBUKE MUDA UNAKWENDA

ni heri ukakodi shamba upande mpunga, uvune uuze
Hahahahaha Story yako inachekesha na kufundisha
 
Me nawaza kuanza kuuza maharage kuna mtu anakuja kukwambia biashara za kuwa bilionea ghafla..ingekuwa hivyo kila mtu angekuwa bilionnea...no pain no gain....tujitume hakuna shortcut
Yaah kwakweli. Asee!!
 
Kuna mtu mimi namfahamu aliuza gari yake na kujiunga QNET, ana zaidi ya mwaka sasa hajapata hata mtu mmoja wa kumuunganisha anajutia tu sasaivi.
Hao jamaa ni matapeli aisee. Mimi kuna ndugu yangu alinialika kwenye izo presentation zao, nikamwambia hiyo pesa milioni tano hata mkinikopesha siitaji kujiunga na huu upuuzi.
Damn!!!
 
Hii upuuzi inachukua sana wale vijana ambao ndio wamemaliza chuo na wako desperate na ajira,

Mzazi mkanye mwanao, utapeli umeingia mjini
 
...
idrissultan-20190511-0001.jpeg
 
Kuna moja hiyo rafiki yangu alinipeleka huko, ofisi zao zilikuwa pale kinondoni sijui sasa kama bado wapo! maana ilikuwa 2yrs ago.
Ile kuingia tu kwa ofisi naona kila mtu ananisalimia GOOD MORNING na wakati huo ni jioni ya saa tisa, Duh walinipotezea muda wale watu siku ile, na ndicho walichofanikiwa kunipotozea muda, ila kwa kifupi sikuwahi kurudi tena, na huyo rafiki yangu urafiki ulikufa imebaki kujuana tu sababu alikuwa anajua kabisa yale ni masinema ila alitupoint watu ambao angalau tulikuwa na chochote kitu ili yeye apate fungu lake,
Kifupi hakuna pesa ya mtelemko.
 
Wacha kuita watu waongo wakati akili zako ni finyu. Umeshindwa hata kufahamu comment yangu.
Sasa nimekupata ucjali mkuu! Lkn na mm nilihudhuria semina zote ukihitaji full data nitakupa. Ila sijajiunga kila siku wananipigia simu nikakope benki au niuze kiwanja
 
Habri zenu ,,wakuu ,, mwenye uelewa na kampuni ya forever living naomba kunijuza ,,ijihusiayo na online marketing
 
Adi September sijaona shuhuda dah

Mm ndo shuhuda wao sasa,

hizi kampuni za network marketing sijui, forever, Alliance, q net, Bf suma, n.k nikajua zipo kwa wizi Tanzania kumbe zimesajiliwa adi BRELA , TRA, kama distributor tu wa diet supplement, vitu vya urembo ndo saa, mikufu ( q net) na kuuuza na sio kutoa utajili wa bure kwa watu wanyonge


Ila kinachofanyika ndo tofauti na makubaliano ya leseni zao, wao wanatakiwa kusambaza diet supplement mfano forever living, alliance, ndo wanaziuza ila wao wanadanganya watu kuwa zinatibu magonjwa kama vile cancer, stroke, nk.


Wale walio na elimu kidogo ya madawa ya binadamu wanajua diet supplement ni tofauti na dawa za hospital ambazo MSD inasambaza kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa vimelea vya mwilini.


Sasa ukifika pale kila mtu ni MD, na mphamacist kwa hizi kampuni utambiwa inatibu ichi mara ichi ila ukisoma leaflet (Ingredient ya dawa) wanasema tofauti not for therapeutic it's diet supplement.


Unachokipata kwa hawa watu ni commission kama M pesa tu baada ya kuuza na kuingiza watu hamna mujiza wa bilion wala nn.


Watu wanao jiunga sana ni watoto wa vyuo wengi sana wanakuta wametoka maporini wakitimba tu mjini wanambiwa utajili uko hapa unauziwa supplement na risiti juu ya efd, ukauze mwenyewe.


Nimeona watu wamejiunga kama 6 ivi mmoja ana miaka 3, wengine 2.5. Maskini tu adi leo wanaomba nauli ya dala dala hamna pesa rahisi kupata duniani na shortcut.


Ukiona mtu kafanikiwa uko ni wale chambo wa kwanza ili wavutie samaki wengine wavuliwe kisawa sawa,.

N.B Tanzania ukiitiwa fursa ujue ww ndo fursa kwao
 
Good morning!!(changa la macho la kwanza)
Ukipigwa hiyo salamu unawehushwa kwanza jeshini tunasema wiki sita za kutolewa uraia kuingizwa jeshini pili unapigwa speech kali wakimrefer Bill Gates na kitabi cha poor dad rich dad cha kiyosaki cjui ukimalizwa hapo unapewa mda uje presentation ya pili hiyo ucipoenda hata home kwako watakutimbia utaonyeshwa kitabu kina saa mikufu na vifaa vingne vya nyumbani unaambiwa bei ya chini ni dola 2000 cjui saa ya golden rose limited edisheni(edition) ***** zao ukiwa naela ukiweka umeumia ukisema sina unapigwa sound uza hata kiwanja within one year utapiga pesa ndefu unaweza nunua nyumba posta kundindiku so usijali hako kakiwanja mda huo washaidharaulisha ajira yako yaan unalipwa laki saba kazi ilivyongumu ile achana nayo anatoa mfano wa.kisenge nlikuwa mhasibu anakitajia likampuni nlikuwa nalipwa milioni 2 ila nimeacha kazi baada ya hapa qnet kufanya vzr maisha yangu duuuh usipoingia kama mm ww ni Genius
Duhhj nomaa
 
Mimi mdada aliyekuja kunipanga nijunge nao aliniambia wanaimiliki timu ya man city... Nikamuuliza unaijua hata timu yenyewe na unamfahamu shehe Mansoor alibaki kutoa macho nikamfukuza.
Kakosea hakukariri vizuri, ila hawa wanatia huruma wakikujia ama kukualika ofisini kwao, wanatumia nguvu nyingi kupindukia kufanya ushawishi ili ujiunge, na istoshe ukiwatazama miongoni mwao utawakuta wamo partners ambao wameingizwa chaka na wenzao na wanajuta hadi kufikia kuumiza mioyo yao, hata sura zao utaziona wakati wanatoa ushuhuda wa mafanikio huwa wanalazimisha tabasamu, ila wengine hapohapo utagundua kuwa hawakubaliani na hiyo mikitu, ila basi tuu wamebakia ili kurejesha mitaji yao. Mm leo hii ndio narudi kupigwa shule ili nijiunge. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
That is true, I don't like to hear these kind of business. They managed to convince my son and he kept crying to do that business and I ended up giving my precious $1750. Kept going everywhere trying to build the pyramid until he ended up getting kwashakoo
Oh hell no sio poa kabisa haki tena😂😂
 
Kakosea hakukariri vizuri, ila hawa wanatia huruma wakikujia ama kukualika ofisini kwao, wanatumia nguvu nyingi kupindukia kufanya ushawishi ili ujiunge, na istoshe ukiwatazama miongoni mwao utawakuta wamo partners ambao wameingizwa chaka na wenzao na wanajuta hadi kufikia kuumiza mioyo yao, hata sura zao utaziona wakati wanatoa ushuhuda wa mafanikio huwa wanalazimisha tabasamu, ila wengine hapohapo utagundua kuwa hawakubaliani na hiyo mikitu, ila basi tuu wamebakia ili kurejesha mitaji yao. Mm leo hii ndio narudi kupigwa shule ili nijiunge. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hahaaaa. Umejiunga au bado fursa hiyo
 
Huku mwanza wanjiunga kwa dollar 2200 sawa na milion 5 ,hyo milion tano unachagua bidhaa moja lkn ili ww upate hela wanakuambia uwe na partners share yaani utafute watu ili utengeneze chain sasa najiuliza kama ww masikini umejiunga nao utaenda kutafuta wapi wa kutoa milion 5 wakti na ww marafiki zako ni walewale wenye kipato kama cha kwako
Kuna msela moja hapa tunamsubiria apige hela nitawaletea mrejesho,alijiunga january sasa anasubiria mwezi wa 6
Kwa mwanza wapo pale pasiasi kuna rafiki yangu aliacha kazi kaenda kujiunga kwenye huu ujinga paka namuonea huruma
 
Back
Top Bottom