Mlioko Uingereza, msaidieni huyu mama kufahamu wanawe walipo

Ina mana hadi leo hawajawahi onana na mama yao hao watoto?
 
Wewe ni mke wa marehemu Abbas wa Bondeni Arusha....????

Huyo Msomali Mahmood kwao ni Ngarnaro .....???

Nauliza hivyo ili nasi tuanze kukusaidia kupitia ndugu na jamaa wa Mahmood
Mcheki kwa contacts zake wewe ni msaada mkubwa sana
 
Sio mda wa kumlaumu muhusika- mpotelewa watoto.. daah sema inafikirisha sana
 
Ina mana hadi leo hawajawahi onana na mama yao hao watoto?
Ndiyo, ninavyokujibu hapa mama wa Amina kanikumbusha nimsaidie kuangalia kama kuna yeyote amesema chochote kuhusiana na uwepo wa watoto hao.
 
Asante kwa elimu kiongozi👌
 
Where We Dare To Talk Openly

Mlioko Uingereza, msaidieni huyu mama kufahamu wanawe walipo​

MSAADA TUTANI: OMBI LA KUWASILIANA NA WATOTO WALIOPO UINGEREZA KWA ZAIDI YA MIAKA 22 SASA.


Picha za awali za wahusika wa waraka huu ikiwa ni pamoja na watoto Amina na Seleman Kichawela na Bw. Mahmud Hassan Mihile aliyewachukua miaka 22 iliyopita ili kuwasaidia masomo huko Uingereza.

Kutokana na kichwa cha habari hapo juu mimi AZAMA ABBASI KICHAWELE ambae kwa sasa ni mjane, mwenye namba ya simu +255 784 697319 na mkazi wa Majengo Arusha, Tanzania, na ambae ni mama wa nyumbani, nachukua nafasi hii kukutaarifu kama ifuatavyo.

Mume wangu kwa majina ABBASI ALLY KICHAWELE ambaye kwa sasa ni marehemu alikua na rafiki wake wa karibu kwa majina MAHMUD HASSAN MIHILE aliekuwa akitumia namba ya simu +441332270462 wakati huo mwenye asili ya Kisomali na uraia wa Uingereza na Tanzania walikubaliana awachukue watoto wetu ambao ni:

SELEMAN ABBASI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka kumi na AMINA JABIRI KICHAWELE aliekuwa na umri wa miaka saba aende nao Uingereza kwa ajili ya kuwasomesha.

Siku ya kuondoka watoto hawa ilikuwa ni mwaka 1994 na waliondoka na mke wa huyo Msomali kwa majina RAHMA MIHILE.

Mji wa kwanza walioshukia huko UINGEREZA unaitwa LEICESTER.

Baada ya hapo mawasiliano yaliendelea kuwepo kati ya mzazi wa kiume wa watoto na Msomali.

NB: Katika hawa watoto huyu wa kike, Amina Jabiri alikuwa ni wa mdogo wake mume wangu yaani shemeji yangu.

Kwa bahati mbaya mume wangu, aliugua maradhi ya cancer na ilipofika mwaka 1998, nikampoteza (alitangulia mbele ya haki).

Baada ya kifo cha mume wangu hakukua na mawasiliano yoyote kati yangu na huyu bwana aliyechukua watoto wangu.

Alikata mawasiliano kabisa na wala hakutaka watoto wajue kuwa baba yao hayupo tena Duniani.

Kwa bahati mbaya sikua na mtu mwingine mbadala wa kuweza kuniunganisha na huyu bwana ikizingatiwa pia mimi ni mama wa nyumbani sikuwa na PR kubwa. Leo hii ninapoandika barua hii, huu ni mwaka wa ishirini na mbili (22) toka nitengane na watoto wangu. Sisi pamoja na wanafamilia tutaendelea kutoa shukrani zetu kwa serikali ya Uingereza iwapo watoto hawa wapo salama na kwenye ajira zao. Kwetu hilo sio tatizo.

Jambo kubwa linaloniumiza ni kutokua na MAWASILIANO na watoto wangu kwa miaka ishirini na mbili sasa. Wakati mwingine najenga wasiwasi kwamba je, wako hai? Na hali hii nitaendelea nayo mpaka lini?

Huyu bwana Mahamudu (msomali) nini kimemsukuma kuwa na ujasiri wa kuwaficha watoto wangu hata nisiwe na mawasiliano nao? Ana dhamira gain?

Kutokana na maelezo mafupi hapo juu nimefikia hatua ya kuiomba ofisi yako tukufu kunisaidia kupata namna ya kuwasiliana na watoto wangu wapendwa huko waliko.

Jambo hili likifanikiwa litaleta faraja sana kwangu na kwa wana familia kwa ujumla.

Pia itakuwa ni fursa kwa watoto kutambua kuwa baba yao mpendwa alishafariki lakini mimi mama yao bado nipo hai, taarifa ambazo tuna hakika hawajazipata.

Naambatanisha picha za watoto ambazo walipigwa wakati wanakaribia kuondoka mwaka 1994.

Pia naambatinisha na picha ya Mahmud Hassan Mihile (Msomali) ya wakati huo aliyewachukua watoto kwa makubaliano na mume wangu.

NB: Kwa mawasiliano tumia namba hizi za barua pepe
hasatathuman@gmail.com
emfinanga4@gmail.com
Au Athuman Rashid Mfinanga
Box 2614, - Arusha Tanzania
Ph: 0754375602/0784375602/0689653424

Wako,
Katika ujenzi wa Taifa
Azama Abbasi Kichawele


Chanzo: Michuzi blog

============================
======================================
UPDATES kuhusu kupatikana kwa watoto
 
Umaskini Mbaya sana.
Hapa ukute watoto walishadhurika kisa njaa na umaskini wa akili na kipato kwa wazazi.
Nimeangalia picha mara kadhaa na kujawa na majonzi. Tunaona binadamu wakitumika kufanya makafara na matambiko tuombe Ndugu zetu na watoto wetu hawa wawe salama.

Lkn mpaka hapo mama alitakiwa awekwe chini ya ulinzi ahojiwe kwa kushindwa kuwalinda watoto wake.
 
kwa hiyo akishawekwa chini ya huo ulinzi ndo utasababisha watoto wapatikane.....
 
That was more than confidence. Nimpe mtu watoto wangu wa umri mdogo hivi aende Nao abroad. Inaonyesha Mume wako alikuwa na agenda ya Siri Kati yake na Rafiki yake. Isitoshe hata huyo Msomali hayuko hai
 
10 + 22 = 32yrs wa kike
7 + 22 = 29yrs wa kiume

Mama hapa anawataka watoto wake aishi nao au awaone tu ???maana kwa hiyo miaka hakuna chemistry(kama wakiwa hai) au mama kwa msoto wa maisha anataka ateljee kwa watoto wake.

Ujinga alishaufanya kuwatoa watoto waende wakakae mbali na mtu baki ilihali yupo hai
 
Amekutuma mwenyewe au? maana hiyo habari ni ya toka 2017.


Huyo Mahmood Mihile ukitaka kumpata ‘google search’ inaonyesha sio muda mrefu alishirikiana na taasisi moja ya maji kwenye charity ya mpira watakuwa na details zake.

Number ya 01332 hiyo ni area code ya Derby na sio mbali na Leicester ni miji jirani, hayo maeneo kuna wabongo wasomali kadhaa, ukimpata mwenyeji wa Derby anampata.

Sasa shutuma za wizi wa watoto (sio za mzaha uingereza) na watoto wenyewe ukute wamejipiga wasomali kama njia ya kupata makaratasi yao. Ukiingiza polisi na immigration usije kuharibia kila mtu na hao watoto wenyewe.

Ni ushauri tu vitu vya kuzingatia kabla kukurupuka. Halafu hao watoto sasa hivi watakuwa washakuwa wakubwa wanajitegemea. Huyo mama angetafuta mtu anaemfahamu U.K. mradi huyo Mahmood Mihile anatumia jina hilo hilo atakuwa tu kwenye data base za serikali na kupatikana kwa njia za mtaa.

Kuliko haya makelele akaenda wapelekea matatizo makubwa kwa njaa zake, utampaje mtu watoto wako kisa waende ulaya.
 
Inafikirisha sana😕
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…