Mliokutana na mauzauza katika ujenzi wa nyumba, naomba msaada wa hatua mlizochukua

Bado mdogo sana wewe kwenye haya mambo. Omba sana
 
Asante kiongozi
 
We utakua mchawi, kusalimia a kitu Gani Kila mtu kaja mjini kimpango wake. Kama unaona mtu kujenga makazi mazuri ni maringo Rudi huko kijijni kwenu ukaishi kwenye nyumba za nyasi.
Hamkomi mkiona mtu kajinyima kujenga kajumba kanapendeza kutwa maneno mara anaringa mara Hili full mawivu na michuki isiyo na mpango na ushirikina.
Mnapenda kupewa heshima ambayo hamna na hata mfanyiwe nini, majirani nuksi.
Yaani ni Raha sana kujenga mahala ambapo wengi wenu ni wakuja kuliko kujenga ambapo wenyeji nuksi ndo majirani
 
UCHAWI UPO NA UNAFANYA KAZI, CHUKUA HATUA.

MCHAWI NI WAKALA WA SHETANI ANAKUWANGIA BILA KOSA LOLOTE, HATA UJINYENYEKEZE VIPI ATAKUHARIBIA TU.

WEKA USOMI PEMBENI MPOKEE YESU KWA IMANI KABISA UWE UNAOMBEA ENEO LAKO NA FAMILIA YAKO. USIPOTEZE HELA KWA WAGANGA AU MANABII WA UONGO, SIMAMA KWA IMANI MWENYEWE HAWATAKUWEZA.
 
Hiyo ni message inatumwa kwako Mkuu, ila inaonekana wanakushindwa, sasa shikia IMANI ulonayo kwa usawasawa, zidisha.
Hakuna mtu atachinja Sungura na kufanya hayo mengine yote kwa nia ya kukutisha, huyo/hao wanamaanisha Mkuu, ni muhimu kupeleleza kumjua muhusika ni nani na anataka nini kuna watu hawaachagi kufatilia, ukahamia akaendelea kubadilisha akajifanya jirani mwema kumbe nia anaijua yeye. USIPUUZE.
 
Ulimfanyeje ndugu.
 
Ulianza ujenzi na mguu gani? Kama ulianza na Mungu tegemea ulinzi wa ki Mungu. Kama ulianza na zindiko la waganga, pambana mwana wane, mwenye kisu kikali ndiye alayr nyama
 
Mzee hapo hakuna uchawi,hizo zote zinaitwa poteza maboya,kama uchawi ungepata madhara toka mwanzo uliposhika sungura,ishu ya msingi jifanye nawe chizi nunua kuku alafu chinja jifanye unamwaga damu kuzunguka kiwanja chako chote,alafu uyo kuku nenda kapige supu,na kuhakikishia huyo anayejifanya ana mwaga uchawi kwako akiona hiyo damu atajaribu tena ujinga,ishu kama hizo nimekutana nazo sana huwa naziuwa kikatili hivyo
 
Ni rahisi tu kama una imani kwa Yesu. Fanya hivi: chukua maji kwenye chupa, sali ukisema, kuanzia sasa haya si maji tena bali ni DAMU YA YESU kwa Jina la Yesu. Wao si walimwaga damu ya wanyama? Basi wewe mwaga Damu ya Yesu mahali hapo huku ukisema; Damu ya Yesu inanena mema matupu juu yangu, rudia mara nyingi. Weka imani kwa Yesu, kazi imekwisha, endelea na ujenzi na fanya hivyo mara kwa mara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…