Mliokutana na mauzauza katika ujenzi wa nyumba, naomba msaada wa hatua mlizochukua

Ulimfanyaje?
 
Jifanye kama hauoni vile... Endelea na ujenzi wala usimwambie jirani yoyote, hapo unatishwa. Ukijichanganya kwenda kwa mganga ndiyo utajichanganya kabisa na hiyo nyumba hautamaliza..
Wenzio tulikuta jeneza chini ya mchanga na ujenzi ukaendelea afu wewe unasema kisu chenye Damu au ngozi, piga kazi bra
 
Sawa ila ukiwa unaenda weka unafki kwa majirani kidogo, unajua sisi weusi nuksi sana, yaani unapiga hatua kimaendeleo majirani wanavimba hasira so kuepusha wape hi kidogo, jifanye unawasikiliza ushauri wao nk yaani fast mauza uza yanaisha
Jirani mmj alinijibu utumbo nilimtafakari Sana. Ilikuwa katika kujadil changamoto za mtaa, akaongea povu Moja nikaona huyu ni gele tu. Wivu na shombo yaani usimuamini MTU katika maisha yako
 
Mmh jeneza? Asante kiongozi
 
Nashukuru sana kwa matumaini nimefarijika nilikuwa nimekataa tamaa
 
Mmmh hii hatari ushauri wako nitaufanyia kazi
 
Mbona unanitisha hivyo
 
Huyo aliyekuuzia ndio anafanya hayo, yalinitokeaga Mimi mwaka 2001 kwenye eneo langu, yule jamaa kaniuzia halafu kumbe akawa anaparoga nipasahau, nilienda kwa babu pemba, nikachukua mchanga katika eneo langu akausomea Sana, halafu akaniambia kautupe pale kwenye eneo lako, aisee yule jamaa alikuja kuumwa Hadi nilimuonea huruma,sijui alienda kujariba tena ujinga wake, miguu ilikuwa inampata Moto Sana ,kazunguka Hadi muhimbili wapi,

Sasaivi ni majirani tunaheshimiana na umri ushaenda
 
Mbona unanitisha hivyo
Mkuu mim sikutishi mchawi akimbiwi ......Fanya maombi kwa ajili ya nyumba Yako kwa Imani Yako...... unaweza pia ita masheikh au wachungaji waombe wakiwa hapo hapo
Damu ni kafara kwa hyo kua makini inaweza kua ni mambo ya chuma ulete ndio imetengenezwa hapo au mauti.....haya mambo sio mazuri.. ....kwa hyo lazima nikwambie ukweli
 
Mkuu ukiishi kwa kuogopa ogopa hutasonga... ishi kwa kumwamini Mungu wako as long as hela unayotumia kujenga hiyo nyumba ni jasho lako.
 
Kumbe we huwajui waswahili
 
Mambo ya kutekenywa tena, ila nikipata mteja ninauza kuishi na walughalugha inahitaji uvumilivu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…