Mliokuwa 'mkimdhihaki ' Rais Dr. Magufuli juu ya Ununuaji wa Ndege Kubwa pateni mfano huu Kuntu wa Kenya

Mliokuwa 'mkimdhihaki ' Rais Dr. Magufuli juu ya Ununuaji wa Ndege Kubwa pateni mfano huu Kuntu wa Kenya

Swala la ununuzi wa ndege linajadiliwa kisiasa tu. Uelekeo wa mijadala yetu unategemea mno misimamo ya kisiasa na si uhalisia.

Hata humu JF kila mjadala hoja kuwa positive au negative angalia IDs maarufu utaona zile hoja zao zinakinzana kutokana na misimamo yao kisiasa.
Kweli kabisa. Kwa mfano MWALLA yeye kila akiona mchango wangu lazima atapinga tu (hata kama hajausoma), eti kwa sababu yeye yuko upande ulee.
 
Tanzania ndo nchi ya kwanza duniani kuongozwa na kichaa na wananchi kumkubali awaongoze cjui nao ni vichaa wa ngazi za chini yake
 
Watu 7000 wameshakata ticket, lakini Tanzania idadi haitajwi kwasababu za kibiashara...bado huoni tatizo
 
Kweli kabisa. Kwa mfano MWALLA yeye kila akiona mchango wangu lazima atapinga tu (hata kama hajausoma), eti kwa sababu yeye yuko upande ulee.
Kwasababu wewe ni mgonjwa mtambuka unasapoti mgonjwa wa akili unafikiri matokeo yake ni nini??
 
Kosa vyote Duniani lakini usikose akili,wewe huna akili kabisa,nitajie taifa lolote Duniani lenye mfumo usiofuata sheria kisha likaendelea,Eti " Go JPM" yes let him go to hell,kazungukwa na wajinga Kama wewe unadhani nchi itaendelea wapi?
We LOFA umeacha kipaumbele cha kununua meli na vivuko umehamia huku?
Sheria ni moja ya vitu vilivyoturudisha nyuma sana nchi hii.
Sheria imekuwa ni kichaka kwa mafisadi kutupiga kama taifa.
Watu wamepiga madili makubwa makubwa kwa sababu ya sheria.
Akina Chenge hawakamatiki kwa sababu walifuata sheria.
Kuna MAFISADI hayashitakiki kwa sababu yalifuata sheria.
Nchi hii kuna mijizi mingi tu ukiisema inakwambia twende mahakani. - We LOFA Unajua ni kwa nini wanakwambia nipeleke mahakamani?
Kwa sababu yaliiba kwa kufuata sheria, na yanajua sheria itawaachia huru.
Nchi hii hakuna sheria inaiumiza serikali kama sheria ya manunuzi.
Kalamu ya 200/= sokoni inaweza kununuliwa kwa 1000/= ukifuata sheria.
Darasa linaloweza kujengwa kwa million 20 ukifuata sheria linajengwa kwa Milioni 100.
Unakumbuka akina Chenge walinunua Rada kwa Billioni ngapi? Hadi Bunge la Uingereza likashtuka?
Hao ndo walikuwa wanafuata sheria kama hujui we ZUZU.
Ni heri JPM tunalalamika sheria (Huku tukipanda ndege zetu) kuliko tulipokuwa tukilalamika kuibiwa ni mijizi iliyokuwa inafuata sheria.
Ni upunguani kulalamika eti sheria sheria wakati miradi tunaona SGR inajengwa na hatujapigwa na wazee wa madili,
Ndege zinanunuliwa na tunazipanda,
Dodoma inajengwa na tunaiona ikijengwa,
Umeme wa Stieglers George watu wapo site.
Very proud of JPM!!! GO JPM Goooo!
Hizi kelele za MALOFA hata Nyerere alizitabili. Usigeuke Nyuma SONGA MBELE kwa sababu nchi hii tumecheleweshwa saana na MAZUZU na MALOFA.
 
Kichwa cha habari na maelezo tofauti! Ni kama umevurugwa hivi au ni kichaa kichaa?!
 
Naona mleta mada amejawa na mahaba kwa jpm mpaka anashindwa kuelewa hoja ya msingi ya upinzani [emoji23][emoji23]
Anamwita mwanaume wake wa shoka[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Kuna muda huwa nawashangaa sana kama siyo mno Watanzania kwamba ni kwanini hawataki Kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwapa ' Zawadi ' ya Rais ambaye ana ' maono ' makubwa sana ya Kimaendeleo kama aliyonayo Rais wetu Mpendwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli a.k.a Mwanamume wa Shoka.

Kwa wale Ndugu zangu ambao mmekuwa mkipiga Kelele juu ya Ununuaji wake wa Ndege ili kuweza kuzidisha Kasi ya Utalii nchini nadhani kwa hili alilolifanya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta sasa mtakuwa na la Kujifunza na ikibidi bado hamjachelewa kumuomba radhi Mheshimiwa Rais JPM au Kutengua ' Kauli ' zenu kwani kiukweli Rais JPM yupo sahihi kwa 100% na hizi Ndege anazozinunua zitaongeza mno Ukuaji wa Uchumi na hasa Sekta nzima ya Utalii kwa nchi ya Tanzania.

Ni kwamba Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amezindua rasmi Safari ya Ndege ya moja kwa moja kutoka Nairobi ( Kenya ) hadi New York ( Marekani / USA ) ambayo itaanza rasmi tarehe 29, October 2018 na mpaka hivi sasa tayari Watu 7000 wameshakata ' Tiketi ' zao ili kuwemo katika hiyo Safari ya Kwanza.

Kwa mujibu wa Rais Kenyatta amesema kwamba uzinduzi huu wa hii Safari ya moja kwa moja kati ya Kenya na Marekani ( USA ) kutaongeza maradufu ' mapato ' katika Sekta nzima ya Utalii ya nchini Kenya na pia Uchumi wa nchi yake utakuwa kwa haraka kwakuwa Kenya imekuwa na ' Vivutio ' vingi ambavyo Wamarekani wengi hupenda kuvitembelea mara kwa mara.

Bado nitasema na leo nasema tena bila ' Unafiki ' kwamba kama kuna ' Zawadi ' ambayo Mwenyezi Mungu ametupa Watanzania basi ni kwa kutupatia Rais mwenye maono ya kweli, yenye tija na uhakika wa Kimaendeleo kwa nchi hii Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli a.k.a Mwanamume wa Shoka.

Hakuna Rais ninayempenda na kumkubali kama JPM na Mwenyezi Mungu ambariki sana azidi kutuletea Maendeleo Watanzania.

Source: Daily Monitor

Nawasilisha.
Hahahaha... Kwa hiyo unajiamini kwa Kuwa Kenyatta kasema???? Tunakoseaga sana na muda mwingi tunaishia kuhaha katika mipango mingi isiyo ya kudumu kwa kuiga nchi nyingine zinavyojikwamua kiuchumi. Mazingira ya nchi na nchi hayafanani mkuu..., Tanzania tunahitaji strategies zetu zinazotufaa sisi kwa mazingira yetu na ukomavu wetu wa kimaendeleo. Hushangai ni kwanini kuanzia uhuru tumekuwa na frameworks, strategies na reforms nyingi pasipo mafanikio? Tunapenda kugusagusa kila sehemu, pasipo kufikiri kama tunachokigusa kinaendana na hali yetu.

Ndege hazijawahi Kuwa kipaumbele Tanzania, ndo maana hata katika ilani ya chama tawala ndege haikuwa katika scale of preference.

Ni vizuri muda mwingine ukija na statistics uwekezaji wa ndege umetusaidiaje, siyo mifano dhaifu kiasi hiki.

Nawakilisha Pia
 
Mleta mada fuatilia utaratibu waliofuata Kenya kununua hizo ndege. kwanza ni joint venture pia sio kwa cash kama sie. na ni mpango wa taifa lao kununua ndege hawajakurupuka na taratibu za manunuzi walizingatia.
 
Kuna muda huwa nawashangaa sana kama siyo mno Watanzania kwamba ni kwanini hawataki Kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwapa ' Zawadi ' ya Rais ambaye ana ' maono ' makubwa sana ya Kimaendeleo kama aliyonayo Rais wetu Mpendwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli a.k.a Mwanamume wa Shoka.

Kwa wale Ndugu zangu ambao mmekuwa mkipiga Kelele juu ya Ununuaji wake wa Ndege ili kuweza kuzidisha Kasi ya Utalii nchini nadhani kwa hili alilolifanya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta sasa mtakuwa na la Kujifunza na ikibidi bado hamjachelewa kumuomba radhi Mheshimiwa Rais JPM au Kutengua ' Kauli ' zenu kwani kiukweli Rais JPM yupo sahihi kwa 100% na hizi Ndege anazozinunua zitaongeza mno Ukuaji wa Uchumi na hasa Sekta nzima ya Utalii kwa nchi ya Tanzania.

Ni kwamba Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amezindua rasmi Safari ya Ndege ya moja kwa moja kutoka Nairobi ( Kenya ) hadi New York ( Marekani / USA ) ambayo itaanza rasmi tarehe 29, October 2018 na mpaka hivi sasa tayari Watu 7000 wameshakata ' Tiketi ' zao ili kuwemo katika hiyo Safari ya Kwanza.

Kwa mujibu wa Rais Kenyatta amesema kwamba uzinduzi huu wa hii Safari ya moja kwa moja kati ya Kenya na Marekani ( USA ) kutaongeza maradufu ' mapato ' katika Sekta nzima ya Utalii ya nchini Kenya na pia Uchumi wa nchi yake utakuwa kwa haraka kwakuwa Kenya imekuwa na ' Vivutio ' vingi ambavyo Wamarekani wengi hupenda kuvitembelea mara kwa mara.

Bado nitasema na leo nasema tena bila ' Unafiki ' kwamba kama kuna ' Zawadi ' ambayo Mwenyezi Mungu ametupa Watanzania basi ni kwa kutupatia Rais mwenye maono ya kweli, yenye tija na uhakika wa Kimaendeleo kwa nchi hii Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli a.k.a Mwanamume wa Shoka.

Hakuna Rais ninayempenda na kumkubali kama JPM na Mwenyezi Mungu ambariki sana azidi kutuletea Maendeleo Watanzania.

Source: Daily Monitor

Nawasilisha.
maandishi mabovu, hayasomeki
 
Mkuu skuhz umekua ukianzisha Thread za kipuuz mno l.

So sad
 
Kwa watanzania kila kitu haiwezekani kwa wakenya kila kitu kinawezekana na kinafanyika. JPM anayo hiyo spirit kama ya majirani zetu ndio maana huwa wanamsema vibaya. Ngosha haogopi kujaribu, ndio maana mabeberu wanamchukia.

Wakoloni wanapenda sana kiongozi wetu akiwa mbele yao basi awe kama mbwa koko mkia urudi tumboni. Aina ya huyu tuliyenaye huwa hawapendwi na wajuaji haswa waliogawana bara letu mwaka 1884 kule Berlin.
 
Back
Top Bottom