Mmewahi kukumbana na uchawi wa kusahaulishwa

Mmewahi kukumbana na uchawi wa kusahaulishwa

Kuna dawa ya kesi unapewa unapaka makalioni...ukienda mahakamani na mashahidi wakija na kupewa muda wa kutoa maelezo... kabla hajaanza kuongea unabana makalio...wee ataanza kuongea pumba na issue tofauti na kesi,,haya akimaliza unalegeza makalio...hakimu anakupa nafasi ya kuuliza swali kwa shahidi..Basi unauliza swali ..kabla ya mtuhumiwa kujibu unakua ushabana makalio...Basi anaongea ujinga balaa. .mwisho wa siku kesi inaisha unakutwa huna hatia
. Inaitwaje hyo mkuu
 
Kuna bosi wetu mhindi alikua ana mtindo wa kuturudisha kwa gari hadi Victoria tulikua tunapita Kkoo almost daily.

Kuna siku gari ikapata pancha tukiwa hapo Kkoo. Tukasogeza gari pembeni kwenye uwanja wa nyumba ambayo wamiliki ni waarabu au wazenji.

Tukatoka kwenda kutafuta mtu wa pancha. Tumefika mbele bosi akasema tuwahi ofisini turudi baadaye, baadaye akasema kesho. Kesho akasema kesho.

Ikakata wiki.

Mkewe akatuhimiza tukamuonyeshe nyumba tukafunga safari, tumefika lile eneo mke akasema ngoja nikachukue vocha dukani, tulivyofika dukani akanunua soda tumekunywa tulivyomaliza akasema tuwahi nyumbani tutarudi kesho.

Mpaka naacha pale kazi ilikua miezi miwili lile gari halikufuatwa.

Miaka minne mbele work mate wangu ananiambia lile gari halikufuatwa. Ila mkipita Kkoo bosi atasema halafu pale niliacha gari langu, kesho nalifuata. Na hafuati.
Dadadeki bosi alikuwa spana za kizigua
 
Kuna dawa ya kesi unapewa unapaka makalioni...ukienda mahakamani na mashahidi wakija na kupewa muda wa kutoa maelezo... kabla hajaanza kuongea unabana makalio...wee ataanza kuongea pumba na issue tofauti na kesi,,haya akimaliza unalegeza makalio...hakimu anakupa nafasi ya kuuliza swali kwa shahidi..Basi unauliza swali ..kabla ya mtuhumiwa kujibu unakua ushabana makalio...Basi anaongea ujinga balaa. .mwisho wa siku kesi inaisha unakutwa huna hatia


Aisee.
 
Bro acha ubishi na ujuaji la sivyo utakuja kuomba Msaada humu uchawi upo ulikuepo na utakuepo
Nikupe dawa ya kudhibiti hali hiyo?.Wala haina gharama.Ni kumwini Mungu,kumtegemea yeye maana yake Usali sana kila wakati,Ondoa uoga,acha kuogopa vitu ambavyo havina nguvu,vipo sawa lkn havina nguvu yoyote,usiruhusu akili yako iogope uchawi.
 
Watu wa Bagamoyo siyo watu wazuri, unanunua kiwanja ama shamba halafu hurudi... ilitutokea mimi na rafiki yangu, tukanunua maeneo makurunge halafu hatukuwahi kurudi mpaka leo zaidi ya miaka 5, sidhani hata napakumbuka vizuri.
 
Mkuu Mimi nimeshuhudia na nina uhakika na hii kitu...basi ngja nigeneralize kwa kusema uchawi wa kizigua una uwezo wa kufuta form zote za ushahidi ikiwemo na hizo documents za upelelezi tena ikiwezekana kumsahaulisha kabisa mpelelezi wa kesi yako
Ni kweli ila sitasema details maana mtashangaa wote. Jamaa kesi yake aliponea Tanga. Aisee ni kiboko. Kuna siku watu wa DPP hawakutokea mahakamani kabisa. Kwenye ushahidi cross examination hawakuweza. Na aliyejiweka mbelembele sitaki kusema kilichotokea. Dunia nzito hii.
 
Nikupe dawa ya kudhibiti hali hiyo?.Wala haina gharama.Ni kumwini Mungu,kumtegemea yeye maana yake Usali sana kila wakati,Ondoa uoga,acha kuogopa vitu ambavyo havina nguvu,vipo sawa lkn havina nguvu yoyote,usiruhusu akili yako iogope uchawi.
Ahsante mkuu,nitajaribu kufanya hivo
 
Kuna jamaa alikuwa na biashara ya pamoja na rafikiye. Watu wa familia yake walikuwa wanajua hili. Siku jamaa alipokufa, ndugu mmoja akajaribu kuwashauri wenzake kuwa marehemu ana biashara na rafikiye. Hakika hakuna aliyekumbuka hadi leo rafiki wa marehemu alikuwa nani.

Sijasimuliwa, nilihusika kama mwanafamilia na tumepoteza mazima.
Nina nyumba yangu fulani Mbagala kwa Mbiku nilimpangisha mama mmoja sijawahi kuonana naye toka 2015,alikuwa analipa kwa kupitia njia ya simu ila mwaka juzi akanambia ameataafu,toka alipoingia sijawahi fika na toka alipostaafu hajalipa hata mia miezi kumi na sita na sijawahi enda.Inawezekana amanipiga muundo mbinu?
 
Back
Top Bottom