Mmoja kati ya Watanzania waliokuwa hawajulikani walipo Nchini Israel, yabainika amefariki Dunia

Mmoja kati ya Watanzania waliokuwa hawajulikani walipo Nchini Israel, yabainika amefariki Dunia

Kwanini alitekwa , kwanini hawakumuachia baada ya kumuona anatoka nchi rafiki. Au hawaijui bongo . Sisi tunajipendekeza kwao.
Hayo maswali waulize Hamas mimi sijui kwanini waliteka watu , au nchi rafiki.
 
Mkuu Rudia Historia...Nchi iliitwa Palestine na Nani....Utawala wa Ottoman Empire uilipoangishwa na Waingereza.....walimuachia mplestine gani hapo?
Mimi naanzia nilipokuta ukitaka leo hii nikwambie Tanganyika mwaka 1200 ilikua chini ya nani nitakua muongo.
 
Pole kwa familia, watanzania tunalaani mauaji ya raia wasiokuwa na hatia awe myahudi au mpalestina
Wanatumika lugha ya kidiplomasia. Ila ukweli ni kwamba alikuwa mateka. Na mwili wake ulipatikana hapo hospitalini Shifa na majeshi ya Israel.
Waturudishie mwili wetu tuje kuzika, balozi wetu aufuate waulete hadi jeddah atcl ikauchukue, huyu ni shujaa wa tanzania kafa akipigania kuwaondoa watanzania kwenye njaa na umasikini
 
Mkuu Rudia Historia...Nchi iliitwa Palestine na Nani....Utawala wa Ottoman Empire uilipoangishwa na Waingereza.....walimuachia mplestine gani hapo?
Unajua hata Egypt imekalia Gaza toka 1949 to 1956....Halafu 1957 to 1966.......Mbona hamkuita ni occupation...? Rudia historia mkuu....
 
Mchi kama israel tupeleke mabalozi wajeda, hapo brigedia general Gaguti angeufata
 
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa masikitiko na huzuni imetangaza kifo cha Clemence Felix Mtenga, Kijana Mtanzania ambaye ni miongoni mwa Watanzania wawili ambao pamoja na raia wa Mataifa mengine walikuwa hawajulikani walipo tangu yaliyopotokea mapigano October 07, 2023 nchini Israel na katika maeneo ya Wapalestina hususani Gaza.

Taarifa iliyotolewa na Wizara haijasema chanzo cha kifo chake na Mji ambao amefia lakini imesema Clemence alikuwa ni miongoni mwa Vijana wa Kitanzania wapatao 260 waliokwenda nchini Israel kushiriki mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa vitendo chini ya Mpango wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Israel.

Tayari Wizara imechukua hatua stahiki ikiwemo kuijulisha Familia na inaendelea kuwasiliana na Serikali ya Israel kuhakikisha kwamba taratibu za kurejesha mwili wa marehemu nchini kwa ajili ya mazishi zinakamilika kwa wakati.

Wizara imesema inaendelea kufuatilia taarifa za Mtanzania mwingine Joshua Mollel ambaye bado hajulikani alipo tangu yalipotokea mashambulizi hayo “Wizara inatoa pole kwa Familia, Ndugu, Jamaa na Marafiki pamoja na Watanzania kwa ujumla kwa msiba huu

View attachment 2816839
Pole sana kwa wafiwa,naomba timu Hamas mje na utetezi wenu.
 
Pole kwa familia, watanzania tunalaani mauaji ya raia wasiokuwa na hatia awe myahudi au mpalestina

Waturudishie mwili wetu tuje kuzika, balozi wetu aufuate waulete hadi jeddah atcl ikauchukue, huyu ni shujaa wa tanzania kafa akipigania kuwaondoa watanzania kwenye njaa na umasikini

Kijana alikwenda kutafuta maisha......akajikuta kwenye kimbunga....wako wengi, toka Nepal, Thailand.....Kinachoniumiza ni kuwa Hamas lazima walifanya interrogations baada ya kuwachukua.....Kwa nini haikuwachia wasio husika....
 
Mimi naanzia nilipokuta ukitaka leo hii nikwambie Tanganyika mwaka 1200 ilikua chini ya nani nitakua muongo.
Kuna mtu kaikuta Tanzania CCM ilipozaliwa, hivyo hawezi kujua kulikua na TAA, TANU nk......ndio maana kna watu wanasema CCM inawenyewe usiwapuuze...
 
Israel ilaaniwe Kwa kusababisha Kijana Wetu kupoteza maisha.
Timu Hamas mlivyoenda kuishambulia Israel kwa sababu zenu za kishamba hamkujua kuwa kuna Raia wa Tanzania huko wasiokuwa na hatia?Na bado mmetuulia kijana wetu na bado unatoa laana kwa mtu ambaye hakuhusika pumbavu.
 
Inshaalah ustaaz
Hapo umesema...Allah....sio Jehovah....ni deity tofauti kabisa....matokeo yake positive and negative tunaona pande zote...Ukisoma Charter ya Hamas....unajua wanapigania nini.....Allah kawapa command ya kuichukua Palestine.....lazima watimize matakwa ya Allah...
 
Mkuu umefuatilizia Historia......? Nini kilitokea 1948.......Au kuanguaka/kushindwa kwa Ottoman Empire kualichaje Hapo mahali panapoitwa Palestine.....? Labda Uwe na kusema kwa kufuatia Historia....wala si hii brainwashing iliyofanywa na Waarabu...na kuwazuga akili wengi.....Je Umesoma Charter ya kuangishwa Hamas inasema nini.....In short is more religion than land...
Haijalishi lakini kumfanya binadamu mwenzako kuwa daraja la pili kama Israel inavyo wachulia wapalestina katika dunia ya sasa ni uovu ulio vuka mipaka.
 
Hivi wakati Yaser Arafat akiwa Kiongozi wa Palestine,Hamas walikuwa wanamuunga mkono au hapana?

Nauliza hivi Kwa sababu Nina hakika Serikali yetu ingepitia Iran ambako tuna mahusiano mazuri wao Iran wangewatafuta Washirika wao Hammas wangeqaachia Vijana Wetu.
Wazo zuri sana ila watu wetu wa Diplomasia hawana akili kama zako. Wengi wanaenda kwenye Diplomasia sababu ya safari za nje tu. Inasikitisha mnoo
 
Hapo umesema...Allah....sio Jehovah....ni deity tofauti kabisa....matokeo yake positive and negative tunaona pande zote...Ukisoma Charter ya Hamas....unajua wanapigania nini.....Allah kawapa command ya kuichukua Palestine.....lazima watimize matakwa ya Allah...
Kwani kuna tatizo? Si ardhi yao
 
Haijalishi lakini kumfanya binadamu mwenzako kuwa daraja la pili kama Israel inavyo wachulia wapalestina katika dunia ya sasa ni uovu ulio vuka mipaka.
Ndiyo muue Raia wa Kitanzania wasiokuwa na hatia kisa Israel?
 
Mkuu huyo dogo ali kuwa hajatekwa bali alikuwa amepotea siku ya shambulizi ndo akadhaniwa ame tekwa, wenda aliuawa siku ya shambulizi au vinginevyo na mbaya zaidi huyo mtoa taarifa hakutoa maelezo yanayo eleweka.
Kama alipotea machoni Kwa WA Israeli, mbona hakuwasiliana na Tz , ktk kipindi hicho. Hapo tungesema hajatekwa, lakini kulikuwa hakuna Mawasiliano , sababu ya Hamas
 
Back
Top Bottom