Mnaofanya mazoezi ya kukimbia kuna mambo mnadanganya

Mnaofanya mazoezi ya kukimbia kuna mambo mnadanganya

Mkuu toa location tuje tutoane upepo .

Sent from my CPH2349 using JamiiForums mobile app
Mkuu siko nchini halafu pia kwa sasa bado hali dhoofu mno. Kwa dakika 15 nimekimbia 2.25km tu. Hii ni hali mbaya sana. Lakini leo nimeona maendeleo kidogo kwasababi jana nilikimbia 2.19km kwa dakika 15. Nimejiwekea malengo ya kufikisha 3km kwa dakika 15 kisha nistaafu kwa heshima barabarani na kuhamia Gym.
 

Attachments

  • IMG-20230916-WA0023.jpg
    IMG-20230916-WA0023.jpg
    81.3 KB · Views: 7
Kulimbia ni swala jingine na kupungua kwasababu umekimbia ni jambo jingine.

Kuna level ya mwili ukifikia haupungui.

Yani kwenye ile minyama uzembe ukifanya zoezi itajikaza tu lakini usifikirie kuwa utakuwa slim.

By the way Sammo Hung namfuatilia sana
 
Kati ya vitu vinakata mwili uzembe ni kukimbia ndio maana wale Wakenya wanaochukua medali unaona mifupa tuu ila wakiacha mbio za medali mwili unakua kawaida ila wakimbiaji wengi hawa wa Road nawaona na Ubonge wao ni kama wanatafuta appetite tu ya kuendelea kula sana...
 
Kulimbia ni swala jingine na kupungua kwasababu umekimbia ni jambo jingine.

Kuna level ya mwili ukifikia haupungui.

Yani kwenye ile minyama uzembe ukifanya zoezi itajikaza tu lakini usifikirie kuwa utakuwa slim.

By the way Sammo Hung namfuatilia sana
Huyo sommo hung ni nani? Unamfwatilia kwa mtandao gani? Nami ni mdau wa mazoezi hasa kukimbia mkuu
 
Kuna jambo nimekuwa nikilifikiria na kubaki kushangaa sana. Ni hii tabia ya wafanya mazoezi ya kukimbia. Unakuta mtu anapost kaenda mazoezi ya kukimbia na kudai kamaliza labda 13km kwa kukimbia.

Kumaliza 13km sio tatizo kwa watu wenye mazoezi ila kukuta mtu kibonge na minyama ya kutosha kapost kumaliza 13km kwa kukimbia inaleta ukakasi sana.

Kwa msiojua ni kuwa mazoezi ya kukimbia sio kitu cha mchezo mchezo. Yaani hata kumaliza 1km bila kusimama wala kutembea inastahili pongezi.

Tuache kudanganyana kwenye mambo serious. Cha kushangaza wengi wanaojidanganya huwa hawapungui!

Inauma sana kuona unamaliza 2km huku roho ikikaribia kuacha mwili mara ghafla unaona kibonge kapost kamaliza 13km. Huu sio uungwana na kukatishana tamaa.
😳Jomoni yaani tangu kipindi bado hujasogea hata kufikasha km4😂 ? kwahiyo bado unaishia nusu km halafu roho inataka kukutoka.....
punguza ubonge bana, umezidi kuwa kibonge dah
 
Dont hate bro, be inspired. Mimi kwa wiki nina ratiba ya mazoezi siku 5 katika siku 7 ila mara nyingi huwa nafanya mazoezi mara 4 kwa wiki. Katika hizo 4 huwa nazigawa kwa siku mbili ni kukimbia (mostly 5~8kms) na kuruka kamba. Hizi siku 2 nyingine nafanya calisthenics.

Sasa mwanzo nilikua napata shida sana kumaliza hata km2 bila kupumzika ila baadae nikaanza kuzoea mpaka sasa naona kawaida tu.
 
Oyaa mi nakamua 4km, zamani ilikua dry mwanzo mwisho. Ila sasa utu uzima ushanijia nafanya run and walk ya hizohizo 4km. Yaani nakimbia nikiona roho inataka kuchomoka nawalk nikirecover na run tena.
Mazoezi sio vita fanya pumzi yako inapoishia. Usijedondoka barabarani buree.
 
Oyaa mi nakamua 4km, zamani ilikua dry mwanzo mwisho. Ila sasa utu uzima ushanijia nafanya run and walk ya hizohizo 4km. Yaani nakimbia nikiona roho inataka kuchomoka nawalk nikirecover na run tena.
Mazoezi sio vita fanya pumzi yako inapoishia. Usijedondoka barabarani buree.
Mkuu utu uzima ndiyo umri gani?
Maana kuna watu wako zaidi ya miaka 60 wanakimbia half marathon.
 
Back
Top Bottom