Mnaofurahia Mikopo, Sri Lanka pia iIianza kama sisi

Mnaofurahia Mikopo, Sri Lanka pia iIianza kama sisi

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,935
Huo ndio Ukweli mchungu kuumeza, lakini usiokwepeka.

Sio ujasiri wala ushujaa kwa viongozi kutembea mkifurahia mikopo na kujipiga kifua mbele ya wananchi majukwaani,kama vile ni jambo la kheri na kishujaa kukopa kopa bila Dira ya kitaifa.

Mnapaswa pia kutoa elimu kwa wananchi, juu ya madhara ya mikopo hiyo kwa uchumi wa nchi.
Ili wananchi waweze kujiandaa kisaikolojia huko mbeleni.

Kwa sababu nyinyi viongozi mnakwenda kukopa huko,lakini walipaji wakuu ni wananchi na vizazi vyao.

Kwa nchi iliyojaaliwa raslimali kama hii ya Tanzania.

Hatukupaswa na hatustahili kushinda mguu na njia kwenda kutembeza mabakuli huko Duniani,sambamba na nchi maskini wa kweli ambazo zipo Africa na kwingineko.

Wakati huo tukiziacha mali zetu zikichotwa kwa mkono mwingine na hao hao wakopeshaji,kwa msaada wa baadhi ya wenzetu wachache kwa manufaa binafsi.

Kwani mifano hai ya mikopo hiyo na madhara yake kwa ushamiri wa taifa tunao.

Mfano wa karibuni kabisa ni huu unaoendelea huko Sri Lanka [emoji1224].

Walikopa hadi wakanyanganywa Bandari yao kuu.

Na sasa wanaelekea kupoteza uhuru wao kama taifa.

Ni baada ya hao hao IMF watalapoitangaza Sri Lanka kama nchi iliyofilisika.

Bado mfano mwingine wa madhara ya mikopo uko Lebanon [emoji1146].

Kwa hiyo CCM wakati mkisifia ukopaji muelewe jinsi mnavyoelekea kulitumbukiza taifa hili tajiri la raslimali,mikononi mwa wakopeshaji.
View attachment 2297136
 
kitu unachopaswa kujua,
CCM ni just platform ambayo hata wewe unaweza kuitumia kufanya maono yako kuhusu Tanzania kwa vitendo... lawama haikusaidii
Wangapi wameitumia CCM kufanya maono yao na wakabaki salama?

Mfano mmoja ni Ndugai na kilichomkuta.
 
Ndivyo alivyofanyiwa Sri lanka!! Sasa mchina anataka amkopeshe Sri Lanka ili alipe deni !! Hayo ni maangamizi mengine !!
Mchina anachofanya ni kutotaka mkopeshaji mwingine tofauti na yeye aingie pale Sri Lanka maana tayari mpango wake unaendelea kufanikiwa.

Kwa hiyo hataki maslahi yake yaingiliwe au kutibuliwa.

Ingawa India [emoji1128] nayo inaonekana kutaka kujiingiza pale ili kuwaokoa ndugu zao.
 
Af kukopa hakuaaza rais huyu mbona ata baba wataifa alikuwa anakopa tatizo mliaminishwa hawamu iliopita ilikuwa haikopi wakati hualisia upo wazi kabisa ilikuwa inakopa kawwida acheni kufanya watu waonekane week haya at ukipewa ww nchi Leo huwezi ata kujitetea walio kutuma wambie bado tuna imani na samahia na 25 kapita bila ubishi
 
Af kukopa hakuaaza rais huyu mbona ata baba wataifa alikuwa anakopa tatizo mliaminishwa hawamu iliopita ilikuwa haikopi wakati hualisia upo wazi kabisa ilikuwa inakopa kawwida acheni kufanya watu waonekane week haya at ukipewa ww nchi Leo huwezi ata kujitetea walio kutuma wambie bado tuna imani na samahia na 25 kapita bila ubishi
"Af" "hawamu" "Samahia" "hualisia"

Kama hayo tu yanakutatiza kuandika basi huwezi jua ninachokimaanisha.
Wewe endelea kushikiwa akili.

Halafu kwako na wenzako mliozowea kutumwa mnadhani kila mtu humu ni mtumwa?

Change your Mindset Please!
 
Mchina anachofanya ni kutotaka mkopeshaji mwingine tofauti na yeye aingie pale Sri Lanka maana tayari mpango wake unaendelea kufanikiwa.

Kwa hiyo hataki maslahi yake yaingiliwe au kutibuliwa.

Ingawa India [emoji1128] nayo inaonekana kutaka kujiingiza pale ili kuwaokoa ndugu zao.
Kazi ipo !!
 
Tanzania sio Sri Lanka,Tanzania imekuwa ikikopa toka kabla ya Uhuru na Kuna kipindi tulikuwa na madeni mengi kuliko sasa hivi na tuliyalipa na mengine wahisani walitufutia.
 
"Af" "hawamu" "Samahia" "hualisia"

Kama hayo tu yanakutatiza kuandika basi huwezi jua ninachokimaanisha.
Wewe endelea kushikiwa akili.

Halafu kwako na wenzako mliozowea kutumwa mnadhani kila mtu humu ni mtumwa?

Change your Mindset Please!
Nijibu kwaza Kuna hawamu ambayo haijawai kukopa?
 
Tanzania sio Sri Lanka,Tanzania imekuwa ikikopa toka kabla ya Uhuru na Kuna kipindi tulikuwa na madeni mengi kuliko sasa hivi na tuliyalipa na mengine wahisani walitufutia..
Huo ni mujibu wa uelewa wako.
Huwezi kuishi kwa kutegemea historia.

Kumbuka kadri muda unavyokwenda na kadri kasi ya ukopaji inavyoongezeka.
Ndivyo tunausogelea ule mstari mwekundu.

Kuna kiwango maalumu ambacho tukifikia hata kesho tu.
Tayari tutakuwa tumepoteza imani kwa wakopehaji.

Ndipo hapo tutakapoanza kutakiwa kukopa kwa dhamana.

Wewe hilo hulielewi labda.
 
Back
Top Bottom