voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,545
- 11,935
Huo ndio Ukweli mchungu kuumeza, lakini usiokwepeka.
Sio ujasiri wala ushujaa kwa viongozi kutembea mkifurahia mikopo na kujipiga kifua mbele ya wananchi majukwaani,kama vile ni jambo la kheri na kishujaa kukopa kopa bila Dira ya kitaifa.
Mnapaswa pia kutoa elimu kwa wananchi, juu ya madhara ya mikopo hiyo kwa uchumi wa nchi.
Ili wananchi waweze kujiandaa kisaikolojia huko mbeleni.
Kwa sababu nyinyi viongozi mnakwenda kukopa huko,lakini walipaji wakuu ni wananchi na vizazi vyao.
Kwa nchi iliyojaaliwa raslimali kama hii ya Tanzania.
Hatukupaswa na hatustahili kushinda mguu na njia kwenda kutembeza mabakuli huko Duniani,sambamba na nchi maskini wa kweli ambazo zipo Africa na kwingineko.
Wakati huo tukiziacha mali zetu zikichotwa kwa mkono mwingine na hao hao wakopeshaji,kwa msaada wa baadhi ya wenzetu wachache kwa manufaa binafsi.
Kwani mifano hai ya mikopo hiyo na madhara yake kwa ushamiri wa taifa tunao.
Mfano wa karibuni kabisa ni huu unaoendelea huko Sri Lanka [emoji1224].
Walikopa hadi wakanyanganywa Bandari yao kuu.
Na sasa wanaelekea kupoteza uhuru wao kama taifa.
Ni baada ya hao hao IMF watalapoitangaza Sri Lanka kama nchi iliyofilisika.
Bado mfano mwingine wa madhara ya mikopo uko Lebanon [emoji1146].
Kwa hiyo CCM wakati mkisifia ukopaji muelewe jinsi mnavyoelekea kulitumbukiza taifa hili tajiri la raslimali,mikononi mwa wakopeshaji.
View attachment 2297136
Sio ujasiri wala ushujaa kwa viongozi kutembea mkifurahia mikopo na kujipiga kifua mbele ya wananchi majukwaani,kama vile ni jambo la kheri na kishujaa kukopa kopa bila Dira ya kitaifa.
Mnapaswa pia kutoa elimu kwa wananchi, juu ya madhara ya mikopo hiyo kwa uchumi wa nchi.
Ili wananchi waweze kujiandaa kisaikolojia huko mbeleni.
Kwa sababu nyinyi viongozi mnakwenda kukopa huko,lakini walipaji wakuu ni wananchi na vizazi vyao.
Kwa nchi iliyojaaliwa raslimali kama hii ya Tanzania.
Hatukupaswa na hatustahili kushinda mguu na njia kwenda kutembeza mabakuli huko Duniani,sambamba na nchi maskini wa kweli ambazo zipo Africa na kwingineko.
Wakati huo tukiziacha mali zetu zikichotwa kwa mkono mwingine na hao hao wakopeshaji,kwa msaada wa baadhi ya wenzetu wachache kwa manufaa binafsi.
Kwani mifano hai ya mikopo hiyo na madhara yake kwa ushamiri wa taifa tunao.
Mfano wa karibuni kabisa ni huu unaoendelea huko Sri Lanka [emoji1224].
Walikopa hadi wakanyanganywa Bandari yao kuu.
Na sasa wanaelekea kupoteza uhuru wao kama taifa.
Ni baada ya hao hao IMF watalapoitangaza Sri Lanka kama nchi iliyofilisika.
Bado mfano mwingine wa madhara ya mikopo uko Lebanon [emoji1146].
Kwa hiyo CCM wakati mkisifia ukopaji muelewe jinsi mnavyoelekea kulitumbukiza taifa hili tajiri la raslimali,mikononi mwa wakopeshaji.
View attachment 2297136